Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/1 uku. 21
  • Vijana Katika Italia Wanafanyiza Nafasi za Kutoa Ushuhuda

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana Katika Italia Wanafanyiza Nafasi za Kutoa Ushuhuda
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Tunawafurahia Vijana Wanaotembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Hubiri Habari Njema Kila Mahali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Shule Yenye Mafanikio Ambayo Ni ya Ulimwenguni Pote
    Amkeni!—1995
  • Mahali pa Vijana Katika Jamii ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/1 uku. 21

Watangazaji wa Ufalme Waripoti

Vijana Katika Italia Wanafanyiza Nafasi za Kutoa Ushuhuda

WALE ambao wanathamini makusudi mazuri ajabu ya Mungu wanafurahi sana kusaidia wengine wajifunze juu ya lile tumaini la ajabu la Ufalme. Mara nyingi hiyo inatia ndani kutumia kwa faida nafasi ambazo zinatokea, kama vile ripoti inayofuata kutoka Sardinia inavyoonyesha.

◻ “Mhubiri mmoja wa miaka 12 alikuwa akisafiri kwa basi kurudi kutoka utumishi wa shambani. Katika basi hiyo walikuwamo pia wavulana wawili na msichana mmoja, wote wakiwa na umri wa karibu miaka 18. Mhubiri kijana yule aliketi karibu na msichana huyo na kuanza kusoma gazeti Amkeni!, akitumaini kuamsha udadisi wa msichana huyo. Msichana yule aliliona gazeti na kuuliza mvulana huyo mhubiri alikuwa akisoma nini. Yeye alieleza alikuwa akisoma makala moja yenye kuhusu utatuzi kwa matatizo ambayo vijana wanalazimika kuelekeana nayo. Mhubiri alisema kwamba yeye alikuwa amenufaika sana kutokana na habari hizo na kwamba zingeweza kusaidia msichana huyo pia. Msichana alikubali magazeti yale kwa furaha.

“Kwa kuwa walikuwa wamesikiliza maongezi yalipokuwa yakiendelea, vijana wawili wale wengine waliomba magazeti. Walipokuwa wakitoa mchango wao, dreva aliwaambia wasipoteze pesa zao juu ya vitu ambavyo ni ovyo tu. Vijana wale walijibu kwamba wao ni wenye uelewevu, na magazeti hayo yalikuwa ya kupendeza. Kusikia hivyo dreva yule aliondosha basi barabarani akalisimamisha kando, naye akataka kuona ni jambo gani lililokuwa la kupendeza sana katika magazeti hayo. Yeye pia alizikubali nakala.

“Yule Shahidi kijana ambaye alisimulia jambo hilo lililoonwa alisema: ‘Mimi nafurahi kweli kweli kwamba nilianza kutoa ushuhuda katika basi.’”

◻ Shahidi mwingine kijana alitumia kwa faida hali moja katika shule. Kijana huyo anasimulia hivi: “Mwalimu wetu wa shule alitufundisha njia ya kujifunza ambayo ilikuwa tofauti sana na ile ya kawaida. Baada ya kufikiria habari alizokuwa akitufundisha, sisi tulipaswa kutayarisha muhtasari wenye kutia ndani mambo makuu na mambo madogo-madogo na ndipo tutoe hotuba ya papo hapo juu ya habari ile.

‘Mimi nimezoea sana njia hiyo,’ akasema Shahidi yule. ‘Hiyo ndiyo ile inayodokezwa na Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.’ Baada ya muda mfupi mwalimu aliona kwamba ni mimi peke yangu niliyepata mafanikio kutumia njia hiyo. Mwalimu huyo mwanamume aliuliza kwa sababu gani kulikuwa na tofauti kubwa hivyo kati ya kazi yangu na ile ya wengine. Mimi nilieleza kwamba nilikuwa nimejifunza njia hiyo katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Yeye alifurahi sana na kunialika nitoe kielezi kwa darasa, nikiwa na Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Nilifanya hivyo.

“Nilipoenda nyumbani, nilieleza jamaa yetu jambo lililokuwa limetokea. Baba yangu, ambaye si Shahidi, sikuzote alikuwa amesema kwamba kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova kulikuwa kizuizi cha maendeleo shuleni, lakini baada ya kusikiliza jambo langu lililoonwa, yeye alilazimika kubadili akili yake.”

Ni pendeleo kubwa kama nini ambalo ninyi vijana mnalo, na pia ninyi mlio na umri mkubwa zaidi, kuliinua juu jina la Yehova na kulijulisha!—Zaburi 148:12, 13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki