Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/15 kur. 3-4
  • Malaika—Wakati Uliopita na Wakati wa Sasa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaika—Wakati Uliopita na Wakati wa Sasa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Malaika Katika Dini Fulani Fulani
  • Je! Wewe Unaitikadi Katika Malaika?
  • Malaika Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Namna Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/15 kur. 3-4

Malaika—Wakati Uliopita na Wakati wa Sasa

“Wao wamefanyiwa vielelezo wakati wa Krismasi katika mapambo ambayo sisi tunaangika juu ya mti, au tunayoona katika kadi za Krismasi—vitoto-bandia vya dhahabu vyenye nyuso za kuvutia, vikipiga kinubi au kinanda cha kanisani au vikibeba mishumaa. Wao wana mabawa mafupi manene kama yale ya ndege wadogo. Kwa neno moja, wao wana sura za kupendeza.”—The Sunday Denver Post.

“MALAIKA kwa jumla wanaachwa bila kuzungumzwa katika shule za theolojia, wanapuuzwa katika shule ya Jumapili, na hata hawatajwi katika fahirisi ya ‘National Catechetical Directory,’ ambacho ndicho kitabu cha uongozi kwa elimu ya kidini ya Katoliki katika Amerika.”

Hivyo ndivyo alivyotangaza rasmi Charles W. Bell, mhariri wa kidini. Yeye aliandika kwamba wanatheolojia fulani, hasa kutoka makanisa makubwa-makubwa ya Kiprotestanti, wanahisi “wakiwa na hali ya kutotulia fikira na mashaka juu ya malaika.” New Catholic Encyclopedia kinaonelea kwamba watu fulani wa kisasa wenye kufikiri sana wanasema kwamba “itikadi yote ya kwamba kuna malaika inapasa ikataliwe katakata.”

Haikuwa hivyo sikuzote. Kwa mfano, katika karne ya 13, wanachuo ambao walijifunza lile tawi la theolojia linaloshughulika na malaika walisemwa kuwa walivutiwa na fikira zinazohusu “umbile, uelewevu, na nia” ya malaika. Kwa karne kadha, sala hata zilitolewa kuelekezwa kwa “malaika walinzi.” Lakini, kama ilivyosemwa juu, mielekeo imebadilika tangu wakati huu.

Kulingana na New Catholic Encyclopedia, “katika akili ya ki-siku-hizi malaika . . . wanaendelea zaidi na zaidi kusukumwa wawe wa kihadithi tu, wa hekaya za kizimwi, na ngano tu za kusisimua watoto.” Kwa kweli, kufikia katikati ya karne ya 19, katika akili za watu wengi malaika walikuwa wameacha zaidi kuhusianishwa na dini wakawa wakishirikishwa zaidi na mawazo ya kimahaba ya kilimwengu. Leo, watu wengi hata zaidi wanawafikiria wao kuwa kitu cha kuwaziwa tu; na kwa sababu hiyo, watu hawa wanakana kuwako kwa malaika.

Malaika Katika Dini Fulani Fulani

Hata hivyo, bado malaika wana mahali katika dini fulani fulani. Kwa mfano, Kanisa Katoliki la Kiroma “linawatia moyo waaminifu kupenda, kustahi, na kuwaomba msaada malaika.” Kwa hakika, Ukatoliki umekweza watatu ambao unawahesabu kuwa malaika—Mikaeli, Gabrieli, na Rafaeli—wawe na cheo cha watakatifu. Rafaeli anaonekana katika vitabu vya kiapokrifa tu na si katika orodha ya Biblia ya vitabu vilivyokubaliwa kuwa Maandiko Matakatifu.

Katika makanisa ya Orthodoksi ya Mashariki, malaika ni mashuhuri katika ile litani, namna ya sala ambamo maombi ya msaada au dua zinatolewa, huku kundi likiitikia-itikia. Malaika wana mahali pia katika Islamu, na itikadi katika malaika ni kimoja cha vifungu vya imani katika theolojia ya Kiislamu.

Hata hivyo, hakuna shaka kwamba katika siku yetu itikadi katika kuwako kwa malaika inafifia.

Je! Wewe Unaitikadi Katika Malaika?

Kuhusu itikadi katika malaika, New Catholic Encyclopedia inasema: “Pole kwa pole . . . katika kusonga mbele kwa ukuzaji na utakasaji wa muda mrefu . . . kupitia maelezo yaliyoongezewa mambo ya ziada kwa kukisia-kisia juu ya mawazo yaliyo katika Andiko Takatifu, kuliendelea kutokea nadharia ya malaika ambayo imekuwa ndilo fundisho la Kanisa, ikiwa na uhakika wa kadiri zinazotofautiana-tofautiana.” Wewe ungekuwa na itikadi iliyo imara jinsi gani katika malaika kama ungejua kwamba imani yako ilikuwa juu ya msingi wa “maelezo yaliyoongezewa mambo ya ziada kwa kukisia-kisia”?

Ajabu ni kwamba, migawanyiko ya fikira juu ya jambo hilo imo hata ndani ya Kanisa Katoliki. Kwa habari ya wakati ambapo malaika waliumbwa, Enciclopedia de la Religión Católica inasema: “Kwa maoni ya mababa wa Kigiriki, malaika waliumbwa kabla ya ulimwengu unaoonekana, lakini maoni ya ujumla ya mababa ya Kilatini ni kwamba wao waliumbwa baadaye. Hata hivyo, maoni ambayo yana wafuasi walio wengi zaidi ni kwamba wao waliumbwa wakati ule ule mmoja na ulimwengu.” Ukosefu huo wa uhakika unafanyiza mvurugo katika akili za watu na kusaidia kuongoza lile elekeo la kutokuwa na itikadi leo.

Mwanafalsafa Myahudi, Philo, alishikilia kwamba malaika walikuwa tu “midhihirisho na nguvu za ulimwengu wote mzima.” Katika muda wa miaka ambayo imepita, wanatheolojia wamefanya majadiliano juu ya masuala yasiyofaa kitu kuhusu umbile na vitabia vya malaika, kama lile swali la kupuuza, Ni malaika wangapi ambao wangeweza kusimama juu ya ncha ya sindano? Je! ni ajabu kwamba watu wengi katika kizazi chetu cha ki-siku-hizi wameona afadhali wasiwe na itikadi katika malaika?

Kwa sababu ya mawazo yote hayo yenye kutofautiana, kwa sababu gani tusichunguze mambo ambayo Biblia yenyewe inasema juu ya malaika? Hiyo itatusaidia tupate majibu imara juu ya maswali kama haya: Je! malaika ni halisi? Ikiwa ndivyo, je! wao wamepata wakati wo wote kujiingiza katika mambo ya wanadamu? Na, la maana zaidi, je! malaika wanaweza kuathiri maisha yako wewe?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki