Waeneza-Evanjeli Wavuna Mavuno ya Ulimwenguni Pote
“Wakati kishale cha saa kinapoendeiea kupita ta ta ta ta kwenda kwenye Har–Magedoni, Mashahidi wa Yehova wanaongeza mwendo wa utendaji wao mbalimbali ili wafanye wengi wetu iwezekanavyo waokolewe kutoka uharibifu huo unaohofiwa sana.”—Makala ya mhariri iliyoandikwa na lan Boyne katika “The Sunday Gleaner,” Machi 15, 1987, Kingston, Jamaika.
MWANDIKAJI wa makala ya mhariri aliyetajwa juu anasema jambo la kweli. Mashahidi wa Yehova wana itikadi ya kwamba Har–Magedoni, wakati ambapo Mungu ataharibu waovu iko karibu na kwamba wanadamu wanaishi katika wakati wa hukumu ya kimungu. (Ufunuo 14:6, 7) Kwa sababu hiyo, kuna uhitaji kwa watu kutii ule ujumbe wa habari njema. Yesu Kristo, yule mweneza-evanjeli wa kibinadamu aliye mkuu zaidi aliyepata kuwako, alianzisha mwendo wa tengenezo ambalo lilieneza evanjeli “kwenye miisho ya dunia” katika karne ya kwanza. (Matendo 1:8, New English Bible; Wakolosai 1:23) Yeye alitabiria siku yetu kazi kama hiyo ya kueneza evanjeli. (Mathayo 24:14) Sasa tengenezo ambalo linafanya jambo hilo limefanyizwa kutokana na Mashahidi wa Yehova, ambao kwa kuhisi uharaka wanahubiri zile habari njema za Ufalme wa Mungu katika nchi na maeneo 210.
Ingawa hivyo, Mashahidi wa Yehova ni zaidi ya tengenezo la kuhubiri tu. Wao ni tengenezo la kufundisha pia. Yesu aliwapa wafuasi wake utume wa ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . kuwafundisha kushika mambo yote ambayo mimi nimeamuru ninyi.’ (Mathayo 28:19, 20, NW) Sisi tungependa kukujulisha wewe kwa watu fulani mmoja mmoja ambao wamenufaika kutokana na kazi yao ya kuhubiri na kufundisha.
Meksiko
Huyu ni Virginia. Yeye ana umri wa miaka 110 na anataka kukuambia wewe kwamba “haiwi kamwe kuchelewa mno kuja kujua na kutumikia Yehova.” Alipokuwa mwanamke kijana, yeye alikuwa mwenye kujitoa sana kwamba kwa miaka minne yeye alijivika mwenyewe mavazi maalum ya kidini. “Lakini jambo fulani lilikuwa limekosekana” yeye anasema. Hakuna mahali ambako yeye angeweza kupata majibu ya kuridhisha kwa maswali yake ya Biblia. Mathalani, wakati yeye alipowauliza walimu katika kanisa lake, “Jina la Mungu ni nani?,” wao walijibu, “Jina la Mungu ni Mungu.”
Lakini mambo yalibadilika katika 1983 wakati mjukuu wake wa kike alipoanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Mjukuu wake wa kike alijibu swali la Virginia kwa kusema kwamba Yehova ndilo jina la Mungu. (Zaburi 83:18) Jambo hilo lilimsukuma Virginia awe na funzo lake mwenyewe la Biblia pamoja na Mashahidi. Miaka miwili baadaye, Juni 2, 1985, yeye alibatizwa akiwa na umri wa miaka 108.
“Mimi nakumbuka tarehe hiyo kwa shauku,” yeye anasema, “kwa sababu katika siku hiyo mimi nilianza kuishi. Nikiwa na umri nilio nao, mimi nahubiri muda wa saa 5 au 6 kwa mwezi na kutumia mkongojo ili unitegemeze katika kutembea. Mimi naona ni afadhali kutembea badala ya kupanda gari. Kwa njia hiyo ninaendelea kuwa katika hali njema ya kimwili.”
India
Mimi ndiye nilikuwa jamaa aliye ovyo kabisa na mwenye makelele-makelele katika mahali hapo,” anasema mwanamume mmoja ambaye alikuwa mfungwa kwa maovu mengi. “Mimi nilikuwa nikiingiza nchini kwa haramu dawa za kulevya, nikicheza mutka (kamari), na kuvuta sigareti za bure ambazo nilipewa kwa hamu nyingi na wateja wangu wa siri. Ilikuwako pia ile tabia ya kuzoelea vileo—yote hayo nilifanya ijapokuwa nilikuwa mshiriki mtendaji wa kanisa.” Lakini wakati mmoja wa Mashahidi wa Yehova alipotembelea nyumbani kwake na akaanza kujifunza Biblia na kutumia mashauri yayo, maisha yake yalibadilika. (Mithali 2:1-22; 2 Timotheo 3:16) Sasa yeye, mke wake, na binti wawili wanasaidia wengine kuwa huru kutoka maovu kama hayo.
Ubelgiji
Mume na mke vijana walianza kuona hasira ya uchungu mwingi kuhusu Mungu. Kwa sababu gani? Mtoto wao wa kwanza, binti, alikufa siku kumi baada ya kuzaliwa. Mtoto wao wa pili alizaliwa akiwa kilema. Na mtoto wao wa tatu, ambaye alionekana kama kwamba ni mwenye siha na afya, alikufa bila kutazamiwa baada ya miezi mitano. Yule mama hangeweza kuitikadi ya kwamba Mungu mwenye upendo angeruhusu tanzia kama hizo ziwapate wao hali watu wengi sana wanaoishi maisha ya ufasiki wana watoto wenye afya.
Muda mfupi baada ya hapo, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuwa akihubiri kutoka nyumba kwa nyumba katika ule ujirani na akatembelea makao yake. Wakati yule Shahidi alipokuwa akisema juu ya ahadi za Mungu za wakati ujao wenye furaha kwa ajili ya aina ya wanadamu, mwanamke huyo alikaidi dhidi ya wazo la kwamba kuna Mungu ambaye ni Baba wa kimbingu mwenye upendo. (Zaburi 37:10,11) Lakini yeye alikubali vitabu fulani vya Kibiblia. Polepole, baada ya ziara za kurudiwa-rudiwa na yule Shahidi, ujumbe wa Biblia wa habari njema, ulifanya moyo wake uwe mwororo na ukajenga uhakika wake katika Mungu. Sasa yeye na mume wake wana tumaini lenye nguvu si kwamba tu katika dunia-paradiso ya wakati ujao Yehova ataponya mvulana wao aliyelemaa bali Yeye atafufua pia watoto wao wengine wawili.—Yohana 5:28, 29; Ufunuo 21:1-4.
Ureno
Asubuhi moja ya Jumapili, bibi mmoja mwenye kubeba mfuko uliojaa vitu alivyonunua dukani alisimama kusema na mume mmoja na mkeye. Hiyo ilikuwa ndiyo mara ya kwanza lakini siyo ya mwisho ambayo wangekutana. Mume na mke huyo, ambao ni Mashahidi wa Yehova, walikuwa katika utendaji wa kueneza evanjeli. Wao walipongeza mnunuzi huyo kwa kutunza mahitaji ya kimwili ya jamaa yake. Lakini ni nani, wao wakauliza, angeweza kutosheleza mahitaji ya aina ya wanadamu? Walijibu swali hilo wao wenyewe kwa kusema kwamba Mungu angeweza. (Zaburi 107:8, 9; Isaya 33:24) “Je! yeye ana dawa kwa tatizo langu?” Bibi huyo akauliza kwa sauti kubwa akitaka kujua. Mashahidi wale walijibu ndivyo na wakaalikwa kwenye nyumba yake ambako funzo la Biblia lilianzwa. Mume wake, kwa kuona mabadiliko bora katika mwelekeo wa mke wake, alijiunga katika funzo lile la Biblia na katika muda mfupi yeye pia akafanya mabadiliko katika mtindo wa maisha yake.
Baadaye, yule bibi aliambia wale Mashahidi kwamba kabla ya yeye kusema nao asubuhi ile ya Jumapili, yeye alikuwa amejaribu mara mbili kujiua. Alikuwa ameudhika sana kwa sababu yeye na mume wake walikuwa wameamua kutengana. Ingawa hivyo, sasa yeye, mume wake, na watoto wao wanafanya maendeleo kwa umoja katika kujifunza juu ya zile habari njema.
Thailand
Kwa sehemu iliyo kubwa zaidi ya maisha yake, mwanamke mmoja anayeishi katika sehemu ya kaskazini ya nchi hii alisumbuliwa-sumbuliwa na mashetani. Wakati yeye alipokutana na mmoja wa Mashahidi wa Yehova katika kazi ya kueneza evanjeli, yeye alijipatia vitabu fulani vya Kibiblia na akakubali kuwa na funzo la nyumbani la Biblia. Baada ya miezi miwili ya kujifunza, yeye akaja kuthamini zile sababu za Kimaandiko za kuondoa kabisa katika nyumba yake vyombo vyote vya ibada ya bandia, kama vile sanamu, na kubomoa nyumba yake ya roho aliyoithamini sana ambayo alijenga ili kuipa jamaa yake himaya ya kutoumizwa na roho waovu. (Matendo 19:19; 1 Wakorintho 10:21; 1 Yohana 5:21) Sasa yeye hapati tena mashambulio ya mashetani na anaweza kukaza fikira juu ya kusaidia wengine wajifunze juu ya yule Mungu mmoja wa kweli, Yehova.
Kenya
Wakati kiongozi mmoja wa genge la wahalifu alipoambiwa kwamba yeye alionwa kuwa hatari sana hivi kwamba polisi walikuwa wamepewa maagizo ya kumpiga risasi wakimwona, yeye alitikisa mabega kwa kucheka tu. Hata hivyo, muda mfupi baada ya hapo, moja la mavamio la genge lake halikwenda kulingana na mpango. Yeye alijikuta mwenyewe peke yake, akiwa amezungukwa na kundi la watu wenye hasira kali wakiwa tayari kulipiza haki ya kiraia. Wakati ule, polisi walikuja kumwokoa, wakampokonya kwa watu hao, na kumfungia katika gereza angoje kujaribiwa mahakamani.
Mwanasheria wake alimshauri juu ya mbinu nbalimbali za kukana hatia. Lakini alipokuwa katika kile jumba cha jela, yeye alikumbuka zile ziara zilizofanywa na mmoja wa Mashahidi wa Yehova miaka kadha iliyopita. Yeye alianza kujuta juu ya njia zake za kuvunja sheria na akapelekea Mungu sala kuomba msaada. Kwa hakika, yeye alisali kwa Yehova kwa kutumia jina lake. (Linganisha Matendo 10:1, 2.) Kwa mshangao wa hakimu, mhalifu huyu alikiri hatia yake kwa mahakama. Kwa hiyo hakimu akafikiliza hukumu ambayo ni pole kwa kulinganishwa na hatia yake; badala ya kifo, hukumu yake ilikuwa miaka kumi katika gereza ya wahalifu wakuu.
Alipokuwa amefungiwa humo korokoroni, yeye alisoma vitabu vya Kibiblia kwa idili na akasali-sali kwa Mungu, akiomba kwamba, ikiwezekana, wakati wake katika gereza upunguzwe ili kwamba aweze kumtumikia Yeye. Bila kutazamia, yeye aliambiwa kwamba hukumu yake ilikuwa imepunguzwa kwa nusu. Hivyo, baada ya kuwa kifungoni kwa miaka mitano, yeye alifunguliwa na mara hiyo akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Muda mfupi baada ya hapo yeye alibatizwa, na sasa mradi wake ni kueneza evanjeli wakati wote.
Vilivyo juu ni vielelezo vichache tu vya jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyotimiza utume wao na wajibu wa kueneza evanjeli “kwenye miisho ya dunia.” Mambo yaliyoonwa haya yangeweza kuzidishwa mara elfu. Basi, je! wewe inatilia shaka kwamba Mashahidi wa Yehova idio waeneza-evanjeli walio wa kweli leo?