Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 1/15 kur. 3-4
  • Je! Kweli Wao Wanasema na Wafu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kweli Wao Wanasema na Wafu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nini Lililotukia Katika Kisa cha Sauli?
  • Je! Kweli Inawezekana?
  • Lakini Chanzo Ni Nini?
  • Uhitaji wo Wote wa Kusema na Wafu?
  • Je! Wewe Unaweza Kusema na Wafu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je, Wafu Wanaweza Kuwasaidia Walio Hai?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Kuwasiliana na Pepo
    Amkeni!—2014
  • Je, Wafu Wanaweza Kuwasaidia Walio Hai?
    Amkeni!—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 1/15 kur. 3-4

Je! Kweli Wao Wanasema na Wafu?

TIMU za mpira katika Brazil nyakati nyingine hutafuta msaada kupitia vyombo vya kuwasiliana na ulimwengu wa roho. Kwa sababu gani? Ili kupata shauri kwa sababu ya kuogopa kwamba timu ya wapinzani huenda ikashinda. Kulingana na karatasi-habari moja, ile “fursa ya kuwasiliana moja kwa moja pamoja na nguvu zipitazo zile za kiasili katika utafiti wa utatuzi kwa namna zote za matatizo inatokeza kivutio chenye nguvu nyingi juu ya mamilioni ya watu.” Katika nchi fulani-fulani, wanasiasa wenye madaraja ya juu, wanasanaa, na wafanya-biashara wanaomba mashauri kwa kawaida kwa wale roho. Katika jitihada ya kutafuta ponyo au kutatua tatizo la kifedha, wengi wanajarihu kuomba mashauri kwa wafu, ambao wanaitikadiwa kuwa wenye nuru nyingi zaidi ya kujua mambo.

Lakini je! inafaa kujaribu kusema pamoja na wafu? Je! inawezekana kweli-kweli kufanya hivyo? Na je! kuna hatari zo zote zinazohusika? Huenda wewe ukashangazwa kuona mambo ambayo Biblia inasema.

Ni Nini Lililotukia Katika Kisa cha Sauli?

Fikiria tukio hili la kweli la maisha lililoandikwa katika Biblia: Akiwa amejawa na woga juu ya Wafilisti maadui, Mfalme Sauli wa Israeli wa kale alitafuta akapata mmoja aliyekuwa chombo cha kuwasiliana na ulimwengu wa roho katika Endori. Yeye aliomba mwanamke huyo apashane habari na nabii mfu Samweli. Aliposikia usimulizi wake juu ya mwanamume mmoja mzee mwenye koti lisilo na mikono, Sauli alijitwalia maoni ya kwamba mzuka huyo alikuwa Samweli. Na ujumbe ule ulikuwa gani? Israeli wangetiwa ndani ya mikono ya Wafilisti, na siku yenye kufuata Sauli na wana wake wangekuwa pamoja na “Samweli,” kuonyesha kwamba wangekufa huku wakipigana na wale Wafilisti. (1 Samweli 28:4-19) Je! hilo ndilo lililotokea?

Si hilo hasa. Sauli alijeruhiwa vibaya katika pigano pamoja na Wafilisti, lakini alikufa kifo cha kujiua. (1 Samweli 31:1-4) Na tofauti na lile bashiri lenye kudokeza kwamba wote kati ya wana wa Sauli wangekufa pamoja naye, Ishboshethi mwana wake alibaki hai baada ya yeye kufa.

Lakini je! ilifaa kuulizia habari juu ya wafu pale mwanzoni? Sivyo, haikufaa. Maandiko yanatuambia: “Sauli alikufa kwa ukosefu wake wa uaminifu . . . na pia kwa kuomba mmoja aliye chombo cha kuwasiliana na ulimwengu wa roho afanye ulizio-ulizio.” (1 Nyakati 10:13, NW) Je! sisi tunaweza kujifunza jambo fulani kutokana na hilo? Ndiyo. Sauli alikufa kwa kuomba aliye chombo cha kuwasiliana na ulimwengu wa roho aulizie-ulizie juu ya wafu. Kwa sababu gani? Kwa sababu katika kufanya hivyo, yeye alikosa kutii sheria iliyo wazi kabisa ya Mungu: “Hakupaswi kupatikana ndani yako wewe . . . ye yote ambaye hutafuta mashauri kwa chombo cha kuwasiliana na ulimwengu wa roho au mtabiri kikazi wa matukio au ye yote ambaye huulizia habari za wafu. Kwa maana kila mtu ambaye anafanya mambo haya ni kitu fulani chenye kukirihika kwa Yehova.” (Kumbukumbu 18:10-12, NW) Kwa sababu gani kuulizia-ulizia habari za wafu kunakirihika kwa Mungu? Kabla ya kujibu swali hilo, huenda sisi tukauliza:

Je! Kweli Inawezekana?

Ikiwa mmoja ye yote atasema pamoja na wafu, lazima wafu hao kwa kweli wawe wako hai. Lazima wao wawe wana nafsi ambazo haziwezi kufa. Hata hivyo Biblia inasema: “Yehova Mungu akaanza kufanya umbo la yule mwanamume kwa mavumbi ya kutoka kwenye ardhi na kupuliza ndani ya mianzi ya pua ya huyo mwanamume ile pumzi ya uhai, na yule mwanamume akaja kuwa nafsi inayoishi.” (Mwanzo 2:7, NW) Basi, yule mtu mwenyewe ni nafsi. Yeye hana nafsi isiyoweza kufa ambayo inaendelea kuishi baada ya kifo cha ule mwili. Kwa kweli, Maandiko yanasema: “Ile nafsi inayofanya dhambi—hiyo yenyewe ndiyo itakayokufa.” (Ezekieli 18:4, NW) Zaidi ya hilo, Neno la Mungu linasema: “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa: lakini wafu hawajui kitu . . . Hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima ndani ya kaburi [Sheoli, NW’ kaburi la ujumla la aina ya wanadamu.—Mhubiri 9:5, 10, ZSB.

Basi, mbali na kuwa na nuru ya kujua mambo, wafu hawajui kitu. Kwa hiyo haiwezekani kusema pamoja nao. Basi kwa kutenda kupatana na sheria ya Mungu dhidi ya kuulizia habari za wafu kunatupa sisi himaya tusidanganywe. Hata hivyo, inawezekana kupata ujumbe kutoka makao ya roho, kama vile tukio la Mfalme Sauli linavyoonyesha.

Lakini Chanzo Ni Nini?

Jambo moja ni kwamba, vitendo vya kupunja vinapatikana sana miongoni mwa wale wanaodai kuwa wanapashana habari na wafu. The World Book Encyclopedia inatujulisha hivi: “Imeonyeshwa kwamba vyombo vya kuwasiliana na ulimwengu wa roho vinapumbaza watu kwenye mikutano yao ili wawe na itikadi kwamba roho wanaweza kuwasiliana na walio hai. Wanasayansi wanatoa maelezo kwa mengi ya mambo ambayo hutukia kwenye mikutano ya wenye kuwasiliana na ulimwengu wa roho. Mathalani, watu fulani walio vyombo hivyo ni wastadi wa kujifanya ili ionekane kana kwamba sauti inatoka mahali pengine hali ni wao wenyewe wanaosema. Watu fulani wanatumia wasaidiaji na namna mbalimbali za vifaa vya kupumbaza watu. Wengine wanatumia usingizi wa mazingaombwe. Watu wengi ambao wanahudhuria mikutano ya wanaowasiliana na ulimwengu wa roho wana tamaa yenye nguvu ya kupashana habari na mpendwa mfu. Huenda tamaa hiyo ikafanya Wao wawe na itikadi kwamba ujumbe wo wote unaotolewa na yule mtu aliye chombo cha mawasiliano unatoka kwenye ulimwengu wa roho.”

Lakini je! inatupasa sisi tufikiri kwa njia hizo tu? Sivyo, kwa maana kushikilia uamuzi wa Mungu dhidi ya kuulizia habari za wafu kunatupa sisi himaya pia kwa njia fulani iliyo ya maana kubwa zaidi. Ujumbe unakuja kutoka makao ya roho, lakini chanzo chayo ni viumbe wenye nguvu nyingi wanaotafuta kuongoza vibaya aina ya wanadamu. Biblia inatambulisha hao kuwa “kani za roho zenye ovu.”—Shetani Ibilisi na malaika wasiotii wanaojulikana kuwa mashetani. (Waefeso 6:12, NW) Wakati Mfalme Sauli alipozuru yule chombo wa kuwasiliana na ulimwengu wa roho katika Endori, shetani mmoja ndiye aliyeji-fanya kuwa na utu wa nabii mfu Samweli.

Kama kilivyoonyeshwa kwa kielezi katika kisa cha Sauli, wale mashetani hawana jambo lo lote lenye manufaa kupitishia watu, na unaodhaniwa kuwa msaada kutoka kwao ni wa muda mfupi. Kama mtawala wao, yule Ibilisi, wao ni wawongo. (Marko 3:22; Yohana 8:44) Katika habari hii, Arthur Conan Doyle mtafiti Mwingereza wa mafumbo ya ulimwengu wa roho ambaye sasa amekufa aliandika hivi: “Jambo lisilo la kufurahisha ni kwamba, sisi tunalazimika kushughulika na uwongo unaosemwa kwa kutojali kabisa kwa upande wa watu wenye akili walio waovu au wakorofi. Kila mmoja ambaye amechunguza jambo hili, mimi nadhani, amekuta vielelezo vya udanganyifu wa kukusudia ambavyo pindi kwa pindi unachanganishwa na mawasiliano mema na ya kweli.” (The New Revelation, uku. 72) Bila shaka, wewe hutaki kudanganywa, au unataka?

Sasa, fikiria hili: Historia inatuambia sisi juu ya biashara ya kuuza na kununua watumwa na mateso yaliyohusika humo. Je! mmoja ye yote angekubali kwa nia kupatwa na magumu na unyenyekezo kama huo? Bila shaka hangekubali. Basi, kwa sababu gani sisi tujiruhusu wenyewe kuwa wenye kutumikishwa na roho waovu? Si kwamba wao wanasema uwongo tu bali wananyang’anya pia watu uhuru wao na huenda wakaongoza kwenye jeuri na uuaji. Mathalani, Jose wa Pernambuco, Brazili, mwenye umri wa miaka 29 alisema kwamba ‘roho mmoja aliingia ndani ya yeye, akilazimisha kuua binti yake mwenye umri wa mwaka mmoja.’ Ndivyo, kuhusika na roho waovu kunaweza kuongoza kwenye utumwa kama huo. Hivyo basi, sawa na vile watumwa wenye kihoro wa wakati uliopita walivyokuwa na hamu nyingi ya kupata uhuru, ndivyo wale ambao wametumikishwa na mashetani leo wanavyopasa kutaka kuwa huru. Njia moja ya kupata uhuru huo ni kujizuia kuwaomba mashauri walio vyombo vya kuwasiliana na ulimwengu wa roho na kutojaribu kusema pamoja na wafu. Ikiwa hivyo, je! kuna . . .

Uhitaji wo Wote wa Kusema na Wafu?

Sivyo, kwa sababu sisi hatuwi bila usaidizi. Kama vile watoto ambao wanaitibari baba yao, sisi tunaweza kuomba msaada kwa uhuru—kutoka kwa yule Baba wa kimbingu, ambaye anafurahia kusaidia wenye mioyo ya unyofu. (Luka 11:9-13) Isaya nabii wa Mungu aliandika: “Wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong’ona; je! haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? je! waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai? Na waende kwa sheria na ushuhuda”!—Isaya 8:19, 20.

Ndiyo, sisi tuna msingi imara kuwa na uhakika katika Yehova Mungu ikiwa sisi tunafanya mapenzi yake na kukataa kupashana habari ko kote pamoja na roho waovu. Yakobo mwanafunzi Mkristo aliandika: “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.” (Yakobo 4:7) Baada ya kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, mwanamume mmoja ambaye alikuwa akizoea kuwasiliana na ulimwengu wa roho kwa miaka 28 alisema: “Usiogope kamwe mambo ambayo Ibilisi huenda akawatenda wale ambao wanaachia mbali zoea la kuwasiliana na ulimwengu wa roho, bali, badala yake, uwe na itibari katika Yehova Mungu.”

Kujaza akili ule ukweli kutoka Neno la Mungu na kutenda kulingana na ukweli huo kutatuwezesha sisi ‘kuvaa suti ya silaha kamili [za kiroho] kutoka kwa Mungu’ ili tupate “kusimama imara kushindana na hila za Ibilisi” na kutotumikishwa na kani za roho zenye uovu. (Waefeso 6:11, NW) Zaidi ya hilo, kupelekea Yehova sala kwa ukawaida kutaandaa kinga yenye nguvu nyingi dhidi ya kusumbuliwa-sumbuliwa na mashetani.—Mithali 18:10.

Inafariji kama nini kujua ule ukweli juu ya hali ya wafu! Kifo ni kama usingizi mzito. (Yohana 11:11) Na Yesu Kristo alitoa uthibitisho kamili kwamba kungekuwa na ufufuo wa wafu—Yohana 5:28, 29.

Akiwa pamoja na mke na watoto wake, mwanamume mmoja ambaye alikuwa mwasilianaji na ulimwengu wa roho alijifunza kutokana na Maandiko kwamba hakuna mmoja anayehitaji kujaribu kusema pamoja na wafu au mtu fulani anayejifanya kuwa na utu wao. Wewe pia unaweza kufurahia uhuru wa kiroho kama jamaa hiyo na nyingine nyingi kuzunguka ulimwengu. (Yohana 8:32) Jifunze ule ukweli juu ya wafu na kusudi la Mungu kwa aina ya wanadamu. Ndipo wewe unapoweza kutazama mbele kwenye mfumo mpya wa Yehova, ambapo wewe unaweza kusema pamoja na wapendwa wafufuiiwa na kufurahia uhai wa milele chini ya hali zenye kujawa na amani.—Isaya 25:8.

[Picha katika ukurasa wa 4]

Ni nani ambaye alisema kwa kweli wakati Mfalme Sauli alipoomba ujumbe kutoka kwa Samweli nabii mfu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki