Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 1/15 uku. 21
  • Je! Wakati Mmoja Wewe Ulishirikiana na Tengenezo la Yehova?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakati Mmoja Wewe Ulishirikiana na Tengenezo la Yehova?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wewe Umekwazwa?
  • Je! Wewe Ulikosa Kuwa na Mwafaka Juu ya Fundisho Fulani?
  • Rudi Sasa
  • Wasaidieni Warudi Haraka!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Wewe Umekwazwa na Mambo Yaliyofanywa na Wengine?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kupokea kwa Uchangamshi Wale Wanaorudi
    Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • “Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 1/15 uku. 21

Je! Wakati Mmoja Wewe Ulishirikiana na Tengenezo la Yehova?

YULE mwanamume kijana alihisi akiwa na aibu na mwenye majonzi sana. Mavazi yake, yakiwa yametatuka na kuraruka, yalikuwa na ishara za kwamba wakati mmoja yalikuwa yamekuwa mavazi ya mtindo wa wakati huo. Sasa hayo hayakuacha shaka lo lote kwamba yeye alikuwa ameangukia nyakati zenye magumu. Huku akili yake ikifikiri-fikiri juu ya mambo ya kule nyuma kwenye nchi ya mbali nyumbani kwao, yeye alianza kuhisi kwa kina kirefu mbadiliko mkubwa wa kutotaka yale maisha ya ufasiki ambayo yeye alikuwa amekuwa anaishi na ile njia ambayo yeye alikuwa ametapanya urithi ambao alikuwa amesisitiza sana apewe kabla ya wakati unaofaa. Tumbo lake tupu liliongezea shida yake, na yeye alihisi akitaka sana kuwa nyumbani. Kwani, hata watumishi wa baba yake kule nyumbani walikuwa katika hali nzuri zaidi ya vile yeye alivyokuwa! Jamani, yeye angependa kama nini kuwa katika hali kama hiyo yao!

Lakini ni upokezi wa namna gani ambao angeweza kutazamia kutoka kwa baba yake kama angerudi sasa? Ingeweza kuwa vigumu kwake kutazamia kusalimiwa kwa uchangamfu au hata kuruhusiwa aingie ndani ya nyumba ile baada ya kuwa ametumia vibaya kwa njia ya aibu sana fadhili za baba yake. Hata hivyo, hisia ya kina kirefu ilitawala akili na moyo wake: Lazima aende nyumbani.

Mwanamume kijana huyo kumbe hakuelewa vizuri sana hisia za baba yake kumhusu yeye! Ni kishtushi kikubwa kama nini kilichomngoja yeye alipokuwa akikaribia maskani yake ya zamani! Kwa kweli, “huku yeye akiwa bado umbali mrefu kutoka hapo, baba yake alipata kumwona na akasukumwa na sikitikio, na yeye akapiga mbio na kuanguka juu ya shingo yake na kumbusu yeye kwa wororo mwingi.”—Luka 15:20, NW.

Kama yule mwana mpotevu, je! wewe umeacha maskani yako ya kiroho? Je! wewe umepeperuka kutoka kwa Baba yako, Yehova, na tengenezo lake? Je! sasa pia unatamani ‘kuja nyumbani’?

Katika visa vilivyo vingi, wale ambao wamepeperuka kutoka tengenezo la Yehova hawakuwa wamefanana kabisa yule mwana mpotevu. Kwa habari ya wengi, ulikuwa mwendo wa kupeperuka pole kwa pole, ambao ni kama haukuhisiwa sana—kama mashua ndogo, inayopeperuka na kuelea-elea ikisonga polepole mbali zaidi na zaidi kutoka nchi kavu. Watu fulani wamelemewa sana na magumu ya kifedha au matatizo ya kijamaa, na magonjwa au hata na kutaka “kusonga mbele” katika ulimwengu, hivi kwamba mambo ya kiroho yamesongwa yakasukumwa nje. Watu fulani wamejiruhusu wenyewe wakwazwe na watu mmoja mmoja wenye kushirikiana na kundi la Kikristo au wameacha kwa sababu wao hawakufanya mwafaka na ufahamu fulani ambao tengenezo la Yehova lilikuwa nao juu ya jambo fulani la Kimaandiko. Wengine bado wamejiruhusu wenyewe wavunjike moyo na wakaenda zao wakati mfumo wa mambo uliopo haukukoma katika wakati ambao wao walitazamia.

Ikiwa wewe ni mmoja ambaye hashiriki tena kwa utendaji pamoja na tengenezo la Yehova, inaelekea kwamba mmoja au zaidi ya sababu hizo italingana na hali zako. Lakini hata kisababishi kiwe nini, je! huu sio wakati wa kufikiria kurudi sasa?—Mathayo 18:12-14.

Je! Wewe Umekwazwa?

Kwa kufikiria ni kwa umbali gani aina ya wanadamu imeanguka kutoka ukamilifu, mmoja anaweza kutazamia kwamba migongano ya kiutu itatukia mara kwa mara. Jambo hilo limeongoza kwenye mkwazo wa watu fulani. Wengine wamekwazwa wakati mtu fulani ambaye wao waliheshimu kwa kina kirefu alipotenda kwa ghafula kwa njia fulani ya haraka-haraka bila kufikiri au kwa njia isiyo ya Kikristo au akahusika katika kufanya kosa.

Je! jambo hilo limekupata wewe? Hata kama ni jambo gani lilifanya wewe ukwazike, kwa uhakika si Yehova ambaye alisababisha mkwazo huo. (Linganisha Wagalatia 5:7, 8.) Kwa hiyo, je! kuna faida yo yote ya sisi kukata uhusiano wetu pamoja na yeye kwa sababu ya jambo ambalo mtu fulani mwingine amefanya? Badala ya hivyo, je! sisi hatupaswi kuendelea kumtumikia yeye kwa uaminifu, tukiwa na uhakika kwamba Yehova anajua jambo linaloendelea kutukia na atashughulika pamoja nasi kwa upendo?—Wakolosai 3:23-25.

Baada ya wakati kupita, watu fulani wamepata kwamba jambo ambalo hapo kwanza liliwakwaza wao halionekani kuwa la maana sana kama wakati huo au huenda hata lisiwepo tena. Au katika fikirio la utulivu juu ya jambo lile, huenda sasa wao hata wakakata shauri kwamba wao ndio kwa kweli waliokuwa katika kosa. Mara nyingi hivyo ndivyo inavyokuwa kweli wakati mtu amekosa kuwa na mwafaka na akakwazika juu ya shauri fulani au nidhamu aliyopewa. Katika kutazama nyuma, huenda yeye akang’amua kwamba nidhamu hiyo ilitolewa katika upendo wa kweli na kwa faida yake. (Waebrania 12:5-11) Basi, inafaa kama nini kutenda kwa kufuata shauri la mtume Paulo! Yeye aliandika: “Inyosheni mikono iliyolegea na magoti yaliyopooza, mkaifanyie miguu yenu njia za kunyoka ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali kiponywe.”—Waebrania 12:12, 13.

Je! Wewe Ulikosa Kuwa na Mwafaka Juu ya Fundisho Fulani?

Huenda ikawa kwamba wewe uliacha tengenezo la Yehova kwa sababu wewe ulikuwa na ufahamu tofauti juu ya jambo fulani la Kimaandiko. Kama vile Waisraeli walioponyolewa kutoka Misri walivyofanya haraka ‘kusahau [kazi za Mungu]’ zilizofanywa kwa ajili yao na ‘hawakungoja shauri lake,’ huenda ikawa wewe ulikata shauri haraka-haraka kwamba kwa kuwa tengenezo halikuunga mkono maoni ambayo wewe uliyafikiria kuwa sahihi, ungekata vifungo vyako pamoja nalo. (Zaburi 106:13, NW) Labda jambo hilo limeeleweshwa wazi tangu wakati huo, ama likibadilishwa au likithibitishwa na utafiti zaidi wa Kimaandiko chini ya mwelekezo wa roho ya Mungu. Je! isingalikuwa vizuri zaidi kama tu ungalibaki pamoja na tengenezo la Mungu ukimngojea Yehova?

Ni vizuri kukumbuka kwamba sikuzote Yehova amefanya kazi kupitia tengenezo moja tu. Katika siku yetu, “mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu” anatoa chakula cha kiroho “kwa wakati unaofaa.” Angalia kwamba mtumwa huyu alipaswa ‘kukutwa akifanya hivyo Bwana wake awasilipo.’ (Mathayo 24:45-47, NW) Kwa kweli, ni nani leo ambao wameng’amua kwamba Bwana huyo amekwisha kufika tayari? Na ni nani ambao wana shughuli nyingi ya kazi ile iliyoonyeshwa? Ni wale tu ambao wanashiriki pamoja na tengenezo la Yehova la Mashahidi wa Kikristo!

Wakati wengine walipomwacha Yesu, mtume Petro alisema: “Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.” Petro alijua kwa kadiri inayopita shaka lo lote kwamba Yesu alikuwa ndiye Mesiya. Kwa hiyo wakati wanafunzi wengi walipopata baadhi ya maneno ya Yesu kuwa ya kugutusha, Petro aling’amua kwamba halingekuwa jambo la hekima kuacha kile chanzo cha “maneno ya uzima wa milele.” Baada ya wakati, shaka lo lote au ufahamu usiofaa ungefanywa uonekane wazi. (Yohana 6:51-68; linganisha Luka 24:27, 32.) Ingali iko hivyo leo, kwa kuwa Yehova anatolea watumishi wake mwongozo wa hatua kwa hatua katika njia ya ukweli.—Mithali 4:18.

Rudi Sasa

“Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, na kumrudia BWANA [Yehova, NW] tena,” akalalamiza yule nabii Yeremia. (Maombolezo 3:40) Hata hivyo, huenda watu fulani bado wakasita-sita, labda wakiogopa kupata upokezi wa hali ya chini kutoka kwa wale walio katika kundi. Lakini je! itikio lilikuwa nini wakati yule mwana mpotevu aliporudi nyumbani? “Ilikuwa lazima tu sisi. . . tushangilie,” akaeleza yule baba, “kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa mfu na akaja kwenye uhai, na yeye alikuwa amepotea na alipatikana.” (Luka 15:32, NW) Karibisho changamfu kama hilo linangoja wale ambao ‘wanarudi kwa Yehova’ wakiwa na tamaa ya moyo mweupe kufanya mapenzi yake.—Linganisha Luka 15:7, NW.

Lakini kundi la Kikristo limekuwa haliketi tu likingojea kukaribisha watu hao ikiwa na iwapo wao wataamua ‘kuja nyumbani.’ Katika kielezi cha Yesu, yule baba alipiga mbio nje kulaki mwana wake wakati “yeye alipokuwa bado umbali mrefu kutoka hapo.” Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wanaufikiria kuwa wajibu wa kibinafsi kutafuta wale ambao wakati mmoja walishiriki, na kusaidia hao warudi ndani ya tengenezo la Yehova.

Lakini namna gani ikiwa mtu alikuja kuwa na hatia ya mwenendo mbaya ulio mzito alipokuwa ametenganika na tengenezo la Yehova? Au namna gani ikiwa ilikuwa lazima mtu fulani aondolewe katika ushirika pamoja na watu wa Mungu kwa sababu ya kufanya kosa zito lakini tangu wakati huo ameacha kujitia katika mwenendo usio wa Kikristo? Wazee watajua jinsi ya kusaidia huyo kwa njia yenye fadhili na upendo ili anyoshe mambo pamoja na Yehova. Kwa hiyo mmoja ye yote ambaye sasa ametamani kurudi na kuishi kupatana na mapenzi ya Mungu anapaswa kujulisha wazee tamaa hiyo. “‘Njoni, sasa, ninyi watu, na acheni sisi tunyoshe mambo kati yetu,’ anasema Yehova. ‘Ingawa zile dhambi za ninyi watu zithibitike kuwa kama wekundu-mwangavu, hizo zitafanywa nyeupe sawa kama vile theluji.’”—Isaya 1:18, NW.

Ni mwenye fadhili, mchangamfu, na mwenye upendo kama nini Baba yetu wa kimbingu! Na ni mwenye subira, na mwenye kupendezwa kama nini na kila mmoja wetu kibinafsi! Kwa uhakika, yeye hataki sisi tuangamizwe pamoja na huu mfumo mbovu wa mambo. (2 Petro 3:9) Ni Yehova ambaye alihimiza watu wake wa kale hivi: “Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi.” Mwaliko uo huo ungali upo leo.—Malaki 3:7.

Wakati unaisha, kwa hiyo usikawie. Ukiwa pamoja na watu wa Yehova, furahia tena ile ‘amani nyingi ambayo ni ya wale wanaopenda sheria ya Mungu.’ Hao “hawana la kuwakwaza,” akasema mtunga zaburi. (Zaburi 119:165) Katika urefu wa kina cha moyo wako, wewe unapenda sheria ya Yehova? Ikiwa wewe ni mtumishi aliyejitoa wakfu wa Mungu, hiyo ndiyo sababu ile ile yenyewe ambayo ilifanya wewe ujitoe wakfu kwake. Hakuna cho chote—naam, cho chote kabisa kabisa—kinachoweza kuwa cha maana zaidi ya kurudisha uhusiano wako na Yehova. Usimgeuzie yeye kisogo chako. Fikiri juu ya jambo hilo kwa uangalifu na kwa sala. Ikiwa wewe umekuwa ukikosa ule umoja na uchangamfu wa watu wa Yehova, haijawa kuchelewa mno kurudi kwenye tengenezo la Yehova. Fanya hivyo bila kukawia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki