Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 2/15 kur. 10-15
  • “Msiache Mioyo Yenu Ninyi Ifadhaike”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Msiache Mioyo Yenu Ninyi Ifadhaike”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Jinsi Gani Sisi Tunaweza Kushinda Sumbuko?
  • Shauri Ambalo Yesu Alitoa
  • Omba Dua kwa Yehova
  • Yehova Anajibu
  • ‘Tumia Kila Namna ya Sala na Kusihi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • “Maombi Yenu na Yajulishwe Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Jinsi Unavyoweza Kumkaribia Mungu
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Kumjia Msikiaji wa Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 2/15 kur. 10-15

“Msiache Mioyo Yenu Ninyi Ifadhaike”

“Msiache mioyo yenu ninyi ifadhaike. Jizoezeni imani katika Mungu, jizoezeni imani katika mimi pia.”​—YOHANA 14:1, NW.

1. Kwa sababu gani maneno ya Yesu kwenye Yohana 14:1 yalikuwa ya wakati unaofaa sana?

ILIKUWA Nisani 14 katika mwaka 33 W.K. Kikundi kidogo cha wanaume kilikuwa mkutanoni katika chumba kimoja cha juu katika Yerusalemu baada ya kuchwea kwa jua. Kiongozi wao alikuwa anawapa wao mashauri na kitia-moyo cha kuwaaga. Kwa sehemu yeye alisema: “Msiache mioyo yenu ninyi ifadhaike.” (Yohana 14:1, NW) Maneno yake yalikuwa ya wakati unaofaa sana, kwa maana matukio yenye kuvunja-vunja moyo yangetukia karibuni. Usiku huo yeye alikamatwa, akajaribiwa, na kushutumiwa kuuawa.

2. Kwa sababu gani siku hiyo ilikuwa ya maana sana, na ni jambo gani ambalo lilisaidia wale wanafunzi?

2 Wewe una sababu nzuri ya kuona siku hiyo kuwa iliyo ya maana zaidi ya zote katika historia, yenye kuathiri wakati ujao mzima wa aina ya binadamu. Kifo cha dhabihu cha yule Kiongozi, Yesu, kilitimiza maunabii mengi ya kale na kuandaa msingi wa uhai wa milele kwa wale ambao wanaitikadi katika yeye. (Isaya 53:5-7; Yohana 3:16) Lakini mitume walivurugika na kujawa na woga kwa wakati fulani, wakiwa wametiwa kimako kingi na kutatanishwa na matukio yaliyowashtua usiku huo. Petro hata alikana uenyeji wake na Yesu. (Mathayo 26:69-75) Hata hivyo, baada ya wale mitume waaminifu kupokea kile kisaidiaji ambacho kiliahidiwa, roho takatifu, wao wakawa wajasiri na wasiofadhaika. (Yohana 14:16, 17, NW) Hivyo, wakati Petro na Yohana walipopatwa na upinzani mgumu na kutiwa katika uzuizi, wao walipelekea Mungu sala ya kuomba msaada katika kusema neno lake “kwa ujasiri wote.” Sala yao ilijibiwa.​—Matendo 4:1-3; 29-31, NW.

3. Kwa sababu gani watu wengi sana wanafadhaika kwa kina kirefu leo?

3 Leo, sisi tunaishi katika ulimwengu ambao umefadhaika kwa kina kirefu. Mwisho wa huu mfumo wa kale wa mambo unakaribia kasi. (2 Timotheo 3:1-5) Mamilioni ya watu wanaathiriwa kibinafsi au wanavurugwa kwa kina kirefu na mvunjiko mkubwa katika maisha ya kijamaa na viwango vya kiadili, ongezeko la kugutusha katika magonjwa yasiyojulikana vizuri, ukosefu wa uthabiti wa kisiasa, ukosefu wa kazi ya kuajiriwa, mapungufu ya vyakula, uvamizi-haramu, na lile tisho la vita ya nyukilia. Mioyo mingi inafadhaika kwa woga inayokaa-kaa ndani yao juu ya wakati ujao. Kama vile Yesu alivyotabiri, kuna ‘huzuni kuu ya mataifa, huku wanadamu wakizimia kwa sababu ya woga na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa.’​—Luka 21:25, 26, NW.

4. Ni mambo gani ambayo yanaweza kusababisha Wakristo wataabishwe na mkazo?

4 Hata Wakristo wanaweza kuathiriwa kwa uzito na mambo hayo yenye kushusha moyo. Huenda wao pia wakaelekeana na mkazo kwa sababu ya maoni ya ubaguzi wa kidini kutoka kwa watu wa ukoo, majirani, wafanya kazi wenzi, wanashule wenzi, na mamlaka za kiserikali. (Mathayo 24:9) Kwa hiyo ni jinsi gani sisi tunaweza kuendelea kuwa watulivu, wasiofadhaika, katika nyakati hizi zenye magumu? Ni jinsi gani sisi tunaweza kudumisha amani ya akili wakati mwendo unapokuwa mgumu? Ni jinsi gani sisi tunaweza kukabiliana na wakati ujao tukiwa na uhakika? Ni nini ambacho kitatusaidia tushinde lile sumbuko la kina kirefu ambalo linaendelea kuwa kawaida ya watu wengi? Sisi tumo katika yale majira ambayo Yesu alitoa lile shauri kwenye Yohana 14:1, kwa hiyo acheni tulitazame kwa ukaribu.

Ni Jinsi Gani Sisi Tunaweza Kushinda Sumbuko?

5. Ni mihimizo gani yenye kutia moyo ambayo Maandiko yanatupa sisi?

5 Baada ya kutoa kitia-moyo cha upendo ‘wasiache mioyo yao ifadhaike,’ Yesu aliambia mitume wake: “Jizoezeni imani katika Mungu, jizoezeni imani katika mimi pia.” (Yohana 14:1, NW) Maandiko yaliyovuviwa na Mungu yanatupa sisi vihimizo vinavyofanana na hivyo: “Umtwike BWANA [Yehova, NW] mzigo wako naye atakutegemeza.” “Kunjua juu ya Yehova njia yako wewe, na tegemea juu yake, na yeye mwenyewe atafanya kitendo.” (Zaburi 55:22, UV; 37:5, NW) Paulo aliwapa Wafilipi shauri hili la maana sana: “Msisumbuke juu ya jambo lo lote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na utoaji-asante acheni maombi rasmi yenu yajulishwe kwa Mungu; na ile amani ya Mungu ambayo inapita mno fikira yote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za kiakili.”​—Wafilipi 4:6, 7.

6, 7. (a) Ni nini njia moja ya kupunguza mkazo? (b) Ni jinsi gani sisi tunaweza kusitawisha kifungo cha ukaribu pamoja na Yehova?

6 Sumbuko au hangaiko linalosababishwa na matatizo na daraka zito linaweza nyakati fulani kuathiri afya yetu na pia roho yetu. Hata hivyo, mstadi mmoja wa kitiba katika kile kitabu Don’t Panic, anaeleza hivi: “Ikiwa watu wanaweza kutokeza nje matatizo yao kwa kuambia mtu fulani ambaye wanamstahi . . . , mara nyingi ule mkazo unapunguzwa sana.” Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo kuhusu mbadilishano wa maoni pamoja na mwanadamu mwingine, msaada utazidi kuwa mkubwa kama nini kwa kumwambia Mungu. Ni nani ambaye sisi tungeweza kumpa staha kubwa kuliko Yehova?

7 Hiyo ndiyo sababu uhusiano wa kibinafsi wenye ukaribu pamoja naye ni wa muhimu sana kwa Wakristo leo. Watumishi wakomavu wa Yehova wanajua hilo vizuri, kwa hiyo wao wanakuwa waangalifu kuepuka namna ya ushirika pamoja na watu wa ulimwengu au namna ya nyakati za kupishwa ambayo ingeweza kudhoofisha uhusiano huo. (1 Wakorintho 15:33) Wao wanathamini pia jinsi lilivyo jambo la maana kusema na Yehova katika sala, si mara moja tu au mbili kwa siku, bali mara nyingi. Hasa Wakristo vijana au wapya wanahitaji kusitawisha kifungo hicho cha karibu pamoja na Yehova kwa funzo lenye ukawaida na utafakari wa Neno lake na kwa ushirika na utumishi wa Kikristo. Sisi tunahimizwa hivi: “Karibieni Mungu, na yeye atakaribia ninyi.”​—Yakobo 4:8, NW.

Shauri Ambalo Yesu Alitoa

8, 9. Sisi tunaweza kutumia shauri gani la mwelekeo chanya (positivu) juu ya matatizo ya kiuchumi?

8 Katika nchi nyingi, ukosefu wa kazi ya kuajiriwa na mshuko wa uchumi ni visababishi vikubwa vya wasiwasi. Yesu alitoa shauri lenye mwelekeo chanya (positivu) sana juu ya mahangaikio hayo: “Acheni kuwa wenye kusumbuka juu ya nafsi zenu ninyi kwa habari ya kile ambacho ninyi mtakula au kile ambacho ninyi mtakunywa, au juu ya miili yenu ninyi kwa habari ya kile ambacho ninyi mtavaa. Je! ile nafsi haimaanishi zaidi ya chakula na ule mwili zaidi ya mvao wa nguo?” (Mathayo 6:25, NW) Ndiyo, nafsi na mwili, au mtu kwa ujumla, ni vitu vya maana kwa kadiri kubwa kuliko chakula na mvao wa nguo. Watumishi wa Mungu wanaweza kuwa na uhakika kwamba yeye atawasaidia kupata mahitaji yao ya msingi. Yesu alitoa kielelezo hiki: “Waangalieni kwa kuwakazia macho ndege wa mbinguni, kwa sababu wao hawapandi mbegu wala hawavuni wala hawakusanyi ndani ya nyumba za akiba; na bado Baba yenu wa kimbingu anawalisha wao. Je! ninyi hamna ustahili mkubwa kuliko wao?” (Mathayo 6:26, NW) Ni jambo lisilofikirika kwamba Mungu angeandaa kwa ajili ya viumbe wa manyoya-manyoya lakini aachilie tu watumishi wake wa kibinadamu, ambao ni wenye thamani kubwa sana kwake na ambao Kristo alitoa uhai wake kwa ajili yao.

9 Ndipo Yesu alipoongeza kani katika katika jambo hilo kwa kurejeza kwenye maualili ya kondeni ambayo hayafanyi kazi ya kuchosha wala hayasokoti uzi, na bado “hata Sulemani katika utukufu wake wote hakuvikwa kwa mpangilio mzuri kama moja la hayo.” Utawala wa mfalme Sulemani ulijulikana sana kwa fahari yao. Ndipo Yesu alipouliza hivi kwa kufariji: “Je! si afadhali zaidi [Mungu] awavalishe ninyi nguo?”​—Mathayo 6:28-32; Wimbo Ulio Bora 3:9, 10, NW.

10. (a) Yale maneno ya Yesu yenye kufariji yameelekezwa kwa nani? (b) Ni shauri gani ambalo yeye anatoa juu ya wakati ujao?

10 Hata hivyo, Yesu anaendelea kuonyesha kwamba jambo hilo ni kwa wale tu ‘ambao wanatafuta kwanza Ufalme na uadilifu wake.’ Ulimwenguni pote, Wakristo hao wa kweli wanathamini Ufalme wa Mungu ni nini hasa na kuuweka kwanza katika maisha zao. Kwao, onyo la upole la Yesu linatumika: “Msisumbuke kamwe juu ya ile siku inayofuata, kwa maana ile siku inayofuata itakuwa na masumbuko yayo yenyewe. Wenye kutosha kwa kila siku ni ubaya wayo yenyewe.” (Mathayo 6:33, 34, NW) Ndiyo kusema, shughulika na kila tatizo kwa kadiri linavyoinuka, na usiwe na wasiwasi isivyofaa juu ya wakati ujao.

11, 12. Wakristo fulani wamehisi jinsi gani kwamba Yehova aliwasaidia wao kwa kujibu sala zao?

11 Ingawa hivyo, watu walio wengi wana mwinamio wa kindani wa kuwa na wasiwasi juu ya wakati ujao, hasa wakati mambo yanapoenda kombo. Lakini Wakristo wanaweza na wanapaswa kugeukia Yehova kwa imani. Fikiria kile kisa cha Eleanor. Mume wake alikuwa mgonjwa sana, na kwa mwaka mmoja mume huyo hakuweza kufanya kazi. Mke alikuwa na watoto wadogo wawili na baba mzee wa kutunza, kwa hiyo hangeweza kufanya kazi ya wakati wote na bado awatunze. Wao waliomba Yehova msaada. Asubuhi moja, muda mfupi baada ya hapo, wao walipata bahasha moja chini ya mlango. Ilikuwa na fungu kubwa la pesa—zenye kutosha kuwaendeleza mpaka mume yule alipoweza kufanya kazi tena. Wao walihisi wakiwa na shukrani za kina kirefu kwa msaada huo wa wakati unaofaa. Hakuna msingi wa Kibiblia kutazamia kwamba jambo kama hilo litatukia kwa kila Mkristo aliye katika uhitaji, lakini sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atasikia vilio vyetu na kwamba yeye ana uweza wa kutusaidia sisi katika njia mbalimbali.

12 Mjane-mwanamke wa Kikristo kusini mwa Afrika alilazimika kutafuta kazi ya kuwaandalia riziki watoto wake wawili wachanga. Lakini yeye alitamani sana kufanya kazi nusu-siku tu ili atumie wakati akiwa pamoja nao. Baada ya kupata kazi, yeye alishurutika kujiuzulu kazi hiyo wakati meneja alipoamua kwamba alihitaji mwandishi wa wakati wote. Akiwa bila kazi tena, dada huyo alisali kwa moyo kumwomba Yehova msaada. Majuma matatu baadaye, aliyekuwa meneja wake alimwomba yeye arudi awe akifanya kazi ya nusu-siku. Dada huyo alifurahi kama nini! Yeye alihisi kwamba Yehova alikuwa amejibu sala zake.

Omba Dua kwa Yehova

13. (a) Ni nini linalomaanishwa na “dua”? (b) Ni vielelezo gani vya Kimaandiko vya dua ambavyo sisi tunavyo?

13 Tafadhali angalia kwamba baada ya kushauri, “Msisumbuke juu ya jambo lo lote,” Paulo aI1aongeza, “bali katika kila jambo kwa sala na (na pamoja na utoaji-asante acheni maombi rasmi rasmi yenu yajulishwe kwa Mungu.” (Wafilipi 4:6, NW) Kwa sababu gani “dua” itajwe? Neno hilo linamaanisha “nasaha yenye kufanywa kwa moyo,” au ‘sala ya kusihi.’ Hiyo inatia ndani kuomba Mungu kwa moyo wenye haraka mwingi, kama katika wakati wa mkazo mkubwa au hatari. Wakati alipokuwa mfungwa-gereza, Paulo aliomba Wakristo wenzake wafanye dua kwa ajili yake ili kwamba yeye aweze kuhubiri pasipo woga “zile habari njema .  . . akiwa balozi katika minyororo.” (Waefeso 6:18-20, NW) Kornelio yule afisa-jeshi Mroma pia ‘aliendelea kuomba dua kwa Mungu.’ Lazima awe alisisimuka sana wakati malaika mmoja aliposema: “Sala zako wewe na zawadi za rehema zimepaa zikiwa kumbukumbu mbele za Mungu”! Na yeye alipendelewa kama nini kuwa miongoni mwa Wamataifa wa kwanza waliopakwa mafuta kwa roho takatifu!​—Matendo 10:1-4, 24, 44-48, NW.

14. Sisi tunaweza kujua jinsi gani kama Yehova anapaswa kusihiwa kwa moyo mara moja tu?

14 Inastahili kuangaliwa kwamba kwa kawaida ombi hilo la kumsihi Yehova kwa moyo halifanywi mara moja tu. Yesu alifundisha hivi katika Mahubiri ya Mlimani yake yanayojulikana sana: “Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kubisha, nanyi mtafunguliwa.” (Mathayo 7:7, NW) Fasiri nyingi za Biblia zinafasiri maneno hayo hivi: “Ombeni . . . tafuteni . . . bisheni.” Lakini kile Kigiriki cha asili kinatoa fikira ya kitendo chenye kuendelea.a

15. (a) Kwa sababu gani Nehemia alikuwa na uso wenye huzuni alipokuwa akimletea divai Mfalme Artashasta? (b) Ni jinsi gani Nehemia alikuwa amefanya jambo ambalo ni zaidi ya kutoa sala fupi tu?

15 Wakati Nehemia alipokuwa akitumikia yule mfalme Mwajemi Artashasta akiwa msimamiaji wa ugawaji divai, mfalme aliuliza ni kwa sababu gani yeye alikuwa na uso wenye huzuni sana. Nehemia alisema kwamba ilikuwa kwa sababu yeye alikuwa amepata habari kwamba Yerusalemu ulikuwa katika hali ya kuteketea. Ndipo mfalme yule akauliza: “Ni nini hiki ambacho wewe unatafuta kuwa nacho?” Mara hiyo Nehemia akaomba Yehova msaada, bila shaka kwa ufupi, kwa kimya. Ndipo yeye alipoomba takwa la kuruhusiwa kurudi Yerusalemu kulijenga upya jiji pendwa la nyumbani kwake. Alipewa takwa lake. (Nehemia 2:1-6) Hata hivyo, kabla ya hoji hilo la maana sana, Nehemia alikuwa ametumia siku kadha akimsihi Yehova, akimwomba dua apate msaada. (Nehemia 1:4-11) Je! wewe unaona somo lililo katika jambo hili kwa ajili yako wewe?

Yehova Anajibu

16. (a) Ni pendeleo gani la pekee ambalo Abrahamu alifurahia? (b) Sisi tuna misaada gani yenye nguvu nyingi ambayo inaweza kutiwa katika majibu kwa sala zetu?

16 Katika pindi fulani fulani, Abrahamu alifurahia lile pendeleo la kuwasiliana pamoja na Yehova kupitia kwao malaika. (Mwanzo 22:11-18; 18:1-33) Ingawa jambo hilo halitukii leo, sisi ni wabarikiwa kwa kuwa na misaada yenye nguvu nyingi ambayo Abrahamu hakuwa nayo. Mmoja ni Biblia kamili—chanzo ambacho hakiwezi kufilisika cha mwongozo na faraja. (Zaburi 119:105; Warumi 15:4) Mara nyingi sana, Biblia inaweza kutupa sisi mwongozo au kitia-moyo ambacho sisi tunahitaji, huku Yehova akitusaidia kukumbuka vifungu tunavyotamani. Mara kwa mara, konkodansi au kimoja cha vile vichapo vingi vya Kibiblia ambavyo Mungu ameandaa kupitia tengenezo lake kinaweza kutupa sisi jibu. Fahirisi kwa vichapo hivyo, ambayo ni yenye mafaa na mambo mengi, ni msaada mwingine wa thamani kubwa katika kupata habari zinazohitajiwa.

17. Ni katika njia gani nyinginezo huenda Yehova akajibu sala zetu, na Wakristo wenye fadhili na huruma wanaweza kusaidia jinsi gani?

17 Ikiwa sisi tunafadhaishwa na tatizo fulani au tunahisi sikitiko au kuvunjika moyo, majibu kwa sala zetu huenda yakaja katika njia nyinginezo pia. Mathalani, hotuba ya Biblia kwenye kundi au kwenye mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova huenda ikawa na “dawa” ambayo ndiyo ile tunahitaji hasa. Nyakati nyingine, kupiga domo pamoja na Mkristo mwingine kutatupa sisi jambo ambalo tunataka. Nyakati nyingi wazee wa kundi wanaweza kutoa kitia-moyo au shauri. Hata kule tu kujiondolea himila za mioyo yetu kwa kuambia Mkristo mkomavu, mwenye fadhili, na mwenye huruma ambaye ni msikilizaji mwema kunaweza mara nyingi kutufanya tuhisi vizuri. Iko hivyo hasa ikiwa rafiki huyo anatusaidia kuwaza tena juu ya fikira za Kibiblia. Mbadilishano huo wa maoni unaweza kuondoa mzigo mzito katika akili na moyo wetu.​—Mithali 12:25; 1 Wathesalonike 5:14.

18. Ni utendaji gani wa pekee ambao unaweza kusaidia Wakristo washinde vipindi vya kushuka moyo, na huo ulisaidia painia kijana jinsi gani?

18 Namna mbalimbali za hali za kushuka moyo ni za kawaida wakati wa hizi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1, NW) Watu wanakuwa wenye kuvunjika moyo na kuingiwa na majonzi kwa sababu za namna-namna. Huenda jambo hilo likatukia kwa Wakristo pia, na linaweza kuwa lisilo la kufurahisha hata kidogo. Ingawa hivyo, wengi wamepata kwamba kuhubiri zile habari njema kumewasaidia wajiondoe katika kipindi cha kushuka moyo kwa muda.b Je! wewe umejaribu hilo? Wakati unapohisi roho ikiwa imeenda chini kidogo, jaribu kushiriki katika na mna moja ya utumishi wa Ufalme. Kuambia; wengine juu ya Ufalme wa Mungu kutakusaidia wewe mara nyingi ubadili hali yako y akilini iache kuwa ya mwelekeo hasi (negativu) iwe ya mwelekeo chanya (positivu). Kusema juu ya Yehova na kutumia Neno lake kunaweza, kukupa furaha—tunda moja la roho yake—na kukufanya uhisi ukiwa tofauti. (Wagalatia 5:22) Painia mmoja aliye kijana wa kike alipata kwamba kuendelea kuwa mwenye shughuli nyingi katika kazi ya Ufalme kulifanya yeye ang’amue kwamba “kwa kulinganishwa na matatizo ya wengine, [yake] yalikuwa madogo sana na ya muda.”

19. Ni jinsi gani Mkristo mmoja aliye katika afya mbaya alishinda fikira za mwelekeo hasi (negativu)?

19 Nyakati fulani, hali fulani ya kushuka kimwili, labda ikichangamana na mawasiwasi au matatizo, inaweza kuongoza kwenye hali ya kushuka moyo. Hilo huenda likasababisha mmoja aamke usiku akiwa amefadhaika, kama ilivyotukia nyakati fulani kwa Mkristo mmoja wa makamo ambaye alikuwa na afya mbaya Lakini mwanamume huyo alipata kwamba sala yenye kutolewa kwa hisia za moyoni ilikuwa msaada halisi. Wakati yeye alipoamka akihisi ameshuka moyo, yeye alikuwa akipelekea Yehova sala kwa utulivu. Baada ya muda mfupi jambo hilo lilimfanya ahisi vizuri zaidi. Yeye alipata kwamba ni jambo la kuburudisha moyo pia kurudia kukariri vifungu vyenye kufariji vya Biblia, kama vile Zaburi 23. Bila kubadilika-badilika, roho ya Yehova, ambayo ilifanya kazi katika kujibu sala au kupitia katika Neno lake, ilikuwa ikisaidia kuweka hali ya furaha zaidi mahali pa zile fikira za kushuka moyo, Baadaye, mwanamume yule angeweza kufikiri juu ya matatizo yake akiwa na usawaziko na utulivu, akiona jinsi ya kushinda mambo hayo au akihisi amefanywa kama ngome aweze kuyahimili.

20. Kwa sababu gani huenda jibu kwa sala likaonekana kama kwamba limekawizwa nyakati fulani?

20 Hicho ni kielelezo cha jinsi sala inaweza kuleta jibu. Lakini nyakati fulani inaonekana kama kwamba kuna ukawivu katika kupata utatuzi. Kwa sababu gani? Labda lile jibu lazima lingojee wakati wa Mungu unaofaa. Inaonekana kwamba katika visa fulani Mungu anawaachia nafasi wale wanaotoa maombi rasmi waonyeshe kina cha hangaiko lao, kadiri ya azimio la tamaa yao, uhalisi wa bidii ya kujitoa kwao. Mmoja wa watunga zaburi alijionea mwenyewe jambo hilo!​—Zaburi 88:13, 14; linganisha 2 Wakorintho 12:7-10.

21. Kwa sababu gani ni pendeleo kubwa kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova leo, na ni jinsi gani sisi tunaweza kuonyesha uthamini?

21 Katika tukio lo lote, kuwasiliana pamoja na Mungu Mweza Yote katika sala ni jambo lenye kuimarisha imani ambalo linaweza kutuinua sisi tutoke katika mtamauko tuwe na uhakika. Inafariji kama nini kujua kwamba yeye anasikia na kujibu! Kama vile Paulo alivyoandikia lile kundi katika Filipi, inatupasa sisi tutoe sala na dua zetu “pamoja na utoaji-asante.” (Wafilipi 4:6, NW) Ndiyo, kila siku inatupasa sisi tufungue mioyo yetu katika kutoa shukrani kwa Yehova na ‘tutoe asante kuhusiana na kila kitu.’ (1 Wathesalonike 5:18, NW) Jambo hilo litachangia kifungo cha ukaribu na uchangamfu, na litatuletea amani. Makala inayofuata inaonyesha jinsi hilo ni jambo la maana kwa watumishi wa Yehova katika nyakati hizi zenye mfadhaiko, zilizo hatari.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa mwafaka pamoja na New World Translation of the Holy Scriptures katika utoaji wa maana iliyo sawasawa, Charles B. Williams anatafsiri hivi mstari huo: “Endeleeni kuomba . . . endeleeni kutafuta . . . endeleeni kubisha, na ninyi mtafunguliwa ule mlango.”—The New Testament: A Translation in the Language of the People.

b Hali ya sikitiko la muda ni tofauti na mshuko-moyo ulio mkali na wa muda mrefu, hiyo ikiwa ni hali ya kimoyo au ya kiakili iliyo na uzito na utatanishi mwingi zaidi. Ona Amkeni! (Kiingereza) la Oktoba 22, 1987, kurasa 3-16.

Wewe Ungejibu Jinsi Gani?

◻ Ni mambo gani ambayo huenda yakasababisha Wakristo wafadhaike?

◻ Ni jambo gani ambalo linaweza kutusaidia tushinde sumbuko?

◻ Kwa sababu gani Wakristo wanaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atawasaidia wao kwa mahitaji yao ya msingi?

◻ “Dua” inamaanisha nini, na ni jinsi gani vielelezo vya wakati uliopita vinaeleleza jinsi Yehova anajibu?

◻ Ni katika njia gani tofauti-tofauti huenda Yehova akajibu sala zetu?

[Picha katika ukurasa wa 12]

‘Baba yenu wa kimbingu analisha wale ndege. Je! ninyi hamna ustahili m wingi zaidi ya wao?’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki