Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 3/15 uku. 3
  • Je! Sala Inastahili Jitihada?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Sala Inastahili Jitihada?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Inueni Mikono Yenye Uaminifu-Mshikamanifu Katika Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Uwe Imara Katika Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kumwomba Yehova Ili Usikiwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 3/15 uku. 3

Je! Sala Inastahili Jitihada?

SIKU ya Ijumaa, Mei 31, 1985, mfululizo wa vimbunga ulikumba sehemu ya kusini ya Ontario, Kanada. Kiongozi wa kidini anayeishi katika kijiji kidogo cha Grand Valley alitazama akiwa hoi, huku upepo huo wenye kuvuma kwa fujo uking’oa paa kutoka sehemu ya jengo anamokaa. Kama ilivyoripotiwa katika magazeti, yeye ‘aliona miujiza na misiba ikitukia kwa kuambatana-ambatana, huku yeye akishuhudia hasira-kisasi isiyozuiwa ya asili.’

Kwa uhakika, wapendwa na marafiki wa wale watu wawili waliouawa na vimbunga hivyo waliviona vimbunga hivyo kuwa msiba mbaya sana. Ndivyo na wale watu zaidi ya elfu moja walioachwa bila maskani na vivingirishi hivyo vya uharibifu. Kwa upande ule mwingine, wengi wa wale ambao waliponyoka kifo au umizo zito walieleza kuokoka kwao kuwa ni “muujiza.” Ron na mfanya kazi mwenzake walikuwa wawili wa hao. Wao walifika mahali salama pa sehemu imara zaidi ya afisi yao sekunde nne tu baada ya kupewa onyo. Baada ya kusimulia jinsi walivyoponyoka kifo kwa njia ya kustaajabisha, Ron alisema: “Ndiyo, kabla ya hapo mimi niliitikadi katika Mungu na kwa hakika hata sasa mimi naitikadi katika Mungu.”

Imesemwa kwamba katika dakika ya afa la ghafula, lisilotazamiwa, ‘ni watu wachache tu wanaokuwa hawaamini kwamba kuna Mungu, ikiwa kweli kunao.’ Na ikiwa kuna wakati wa kutosha katika pindi hizo, sala nyingi za juhudi zinatolewa kuomba himaya na uokokaji.

Siku ya Jumapili, Julai 21, 1985, wanaume, wanawake, na watoto zaidi ya mia moja walikutana kwa ajili ya ibada kwenye Jumba la Ufalme lao katika Sydney, Australia. Baada ya wimbo wa kusifu Mungu, sala ilitolewa kwa ajili ya kundi hilo. Wakati mhudumu mmoja alipokuwa amefika dakika 15 katika hotuba yake ya Biblia asubuhi hiyo ya Jumapili, kwa ghafula kombora lililipuka likavuruga kabisa amani hiyo, likamuumiza yeye vibaya sana, likaua mwanamume mmoja aliyeketi kule mbele ya jumba, na kufanya watu zaidi ya 40 walazwe hospitalini.

[Box/​Picture on page 3]

Je! Sala Inafanyiza Tofauti Yo Yote?

Matukio yote mawili ambayo yamesimuliwa sasa hivi​—⁠lile lililoelezwa kuwa “hasira-kisasi isiyozuiwa ya asili” na lile jingine lililoelezwa kuwa kitendo cha uhalifu​—⁠yanatokeza maswali juu ya thamani ya sala. Kusali kuna thamani gani? Je! sala inafanya kazi kweli kweli? Je! hiyo inaistahili ile jitihada ya kusali?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki