Kujua Yaliyo Katika Habari
Mistari-mistari ya Punda-milia
“Mamilioni ya miaka ya mageuzi” yaliwapa punda-milia mistari mistari yao, linadai gazeti la Afrika Kusini World of Wildlife Sababu ni nini? Wanasayansi fulani-fulani wanasema kwamba mistari-mistari hiyo ilitokea kwa mageuzi kama kidanganya macho ili kuhami mnyama huyo kutokana na wanyama mwitu wakali. Linaloonekana kuwa linaongezea rai hii ustahilifu wa kusadikika ni uhakika wa kwamba mistari-mistari haionekani waziwazi inapoonwa kwa mbali. Hata hivyo, si wanaume wote wa sayansi wanaokubaliana na jambo hilo. Dakt. Gerrie de Graaff, mshauri wa kisayansi wa gazeti Custos linalohusu wanyama mwitu aliaandika hivi: “Hatuwezi kukisia kwamba wanyama wanaona vitu kama sisi tunavyoviona.” Kwa kueleza, de Graaff anaonyesha kwamba tabia ya punda-milia haipatani na nadhari ya kidanganya macho cha ukuzi wa mistari-mistari. Kwa nini? Kwa sababu punda-milia hawajaribu kujificha wenyewe kama wanavyofanya wanyama wanaotegemea kidaganya macho cha rangi. Wao ni wenye kelele na watendaji nao wanajionyesha kwa kula nyasi katika nyanda zilizo waziwazi.
Wanamageuzi wengine wanakisia kwamba mistari myeusi na myeupe inayoonekana wazi sana ya punda-milia inafanyiza mazingaombwe. Kulingana na de Graaff, shindano moja ni kwamba “simba wenye kushambulia hawawezi kuchagua mmoja kwa sababu anachangamana na wengine katika kundi,” hali “mwingine anadokeza kwamba simba anakosa kuona vizuri kwa sababu ya mng’ao unaotokana na mistari-mistari hiyo au anakosea wakati wa mruko wake wa mwisho wa kuwazia tu.” Lakini kama vile yeye anavyoonelea, “nadharia hizo zinadidimia kwa utumainifu ambao umeonekana ambao simba wanawaua punda-milia.”
Kwa kumalizia, de Graaff anakiri kwamba “kufikia hapa, hatujui kwa nini punda mlia ana mistari-mistari.” Hata hivyo, sababu ni wazi kwa wanafunzi wa Biblia. Kwenye Mwanzo 1:20-25 tunaambiwa kwamba viumbe vyote vya duniani viliumbwa na Mungu “kulingana na aina yao “Kama tokeo, njia ya asili ya kibayolojia ndiyo inayohusika kwa kutokea kwa mistari-mistari ya punda-mlia. Mistari-mistari hiyo ni sehemu ya aina mbalimbali ya ubuni wa ajabu katika uumbaji wa Mungu.
Ati Wahudumu Wanaofanya Kazi?
Viongozi fulani wa kidini wanatazamia kuona mabadiliko makubwa katika kazi yao wakati ujao ulio karibu. Hili ndilo lililokuwa hangaiko lililoelezwa na kasisi mmoja Mlutheri, Jean-Pierre Jornod, katika Reformiertes Forum, jarida la Kilutheri linalochapishiwa Switzerland. Yeye alitaarifu: “Mimi ninaweza kwenda mbali kutabiri kwamba kasisi wa mwaka 2000 kwa visa vingi atakuwa na kazi ya nusu siku kuongezea parishi yake.” Kwa nini? Yeye aliongezea: “Si kwa sababu za kifedha tu, lakini jambo la kwanza na lililo kuu ni kwa sababu jamii ya watu ina uhitaji unaoongezeka wa makasisi ambao wanafahamiana sana na maisha ya kila siku.”
Akieleza zaidi juu ya uhitaji huu, Jornod alisema: “Kasisi wa mwaka 2000 atakuwa mwanamume au mwanamke ambaye anajua sana kupashana habari. Sifanyi madai ya kwamba makanisa yatakuwa matupu wakati huo, lakini watu ambao kasisi anataka kuwafikia watajiweka mbali na kanisa, sawa na wanavyofanya leo kwa sehemu. Hivyo, ujumbe wake utapaswa uwe wa wazi, unaoeleweka zaidi, na wenye kugonga kichwa cha msumari.
Ni jambo linalostahili kukumbukwa kwamba wachungaji wanaolipwa hawakujulikana katika karne ya kwanza ya Ukristo. Mathalani, mtume Paulo alijiandalia mahitaji yake mwenyewe ya kimwili kupitia kwa kazi—kutengeneza hema. Jambo zaidi, yeye aliwafikia watu katika njia yenye matokeo sana, kwa kuwafundisha “waziwazi na nyumba kwa nyumba.” (Mdo. 18:3; 20:20, 21, 33, 34, NW) Tofauti na wahuduma wa siku hizi wanaolipwa, wazee, au wachungaji, miongoni mwa Mashahidi wa Yehova wangali wanafuata kigezo hiki cha Kimaandiko cha Wakristo wa karne ya kwanza.