Maswali Kutoka kwa Wasomaji
◼ Je! watu mmoja mmoja walio wagonjwa na viwete waliponywa kikweli katika yale maji ya Bethzatha yenye kutibuliwa, kama vile Yohana 5:2-7 inavyodokeza? na ikiwa ndivyo, miujiza hiyo ilitukia kwa nguvu gani?
Kwa kweli, ule usimulizi kwenye Yohana 5:2-9 hauonyeshi kwa imara kama hesabu fulani ya maponyo ya kimwujiza yalitukia kwenye kidimbwi kimoja katika Yerusalemu wa kale, Mwujiza mmoja tu ambao sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba ulitukia hapo ni ule uliofanywa na Yesu Kristo alipoponya mwanamume mmoja aliyekuwa amekuwa mgonjwa kwa miaka 38. Sisi tunaweza kukubali mwujiza huo, kwa maana ripoti inayouhusu imo katika Maandiko yaliyovuviwa. (2 Timotheo 3 16) Lakini wengi katika Yerusalemu wakati wa kule nyuma waliitikadi kwamba miujiza mingine ilikuwa imetukia mahali hapo, hata kama vile wengi leo wanavyoitikadi kwamba maponyo ya kimwujiza hutukia kwenye sehemu zinazoheshimiwa kuwa takatifu.
Angalia yale ambayo Biblia inasema. na yale ambayo kwa kweli haisemi: “Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano [nguzo tano za mfululizo, NW] Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu, viwete, nao waliopooza.———Na hapa palikuwa na mtu, ambaye amekuwa hawezi muda wa miaka thelathini na minane. Yesu alipomwona huyu amelala, naye akijua ya kuwa amekuwa hali hiyo siku nyingi, alimwambia, Wataka kuwa mzima? Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu. Yesu akamwambia, Simama, jitwike godoro lako, uende. Mara yule mtu akawa mzima, akajitwika godoro lake, akaenda.”—Yohana 5:2-9.
Birika linalorejezewa lilikuwa karibu na “mlango wa kondoo,” ambao kwa wazi ulikuwa katika Yerusalemu ya kaskazini-mashariki karibu na mpandio wa hekalu. (Nehemia 3:1, 12:39) Machimbuzi ya hivi majuzi yamefukua vitu vyenye kuthibitisha kwamba kulikuwa na mabirika mawili ya kale, yakiwa na vipande-vipande vya nguzo na misingi ya chini ya kuzishikilia ambazo zinaonyesha kwamba hapo palikuwa na jengo lenye nguzo za mfululizo katika nyakati za Herode, kama vile Yohana 5:2 inavyosema. Lakini watu wa huko nyuma walifikiri ni jambo gani lingetukia hapo?
Angalia kile kistari-chali kilicho katika nukuu lililo juu la Yohana 5:2-9. Biblia fulani zinatia ndani kifungu cha ziada kinachohesabiwa kuwa Yohana 5:4. Ziada hiyo inasema jambo kama hili “Kwa maana kuna wakati ambapo malaika hushuka, akaingia katika ile birika, akayatibua maji. Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, akapona ugonjwa wote uliokuwa umempata.”
Hata hivyo, hesabu fulani ya Biblia za ki-siku-hizi, kutia na New World Translation of the Holy Scriptures, zinaacha nje kifungu hicho. Kwa nini? Kwa sababu yamkini kabisa kifungu hicho hakikuwa katika Gospeli ya Yohana. Maelezo mamoja ya chini katika The Jerusalem Bible yanaonelea kwamba “mashahidi walio bora zaidi” huondoa nje kifungu hicho. “Mashahidi walio bora zaidi” wanaomaamshwa na hati za mkononi za Kigiriki za kale, kama vile Codex Sinaiticus na Vatican 1209 (zote mbili zikiwa ni za karne ya 4 W.K.), na fasiri za mapema katika Kisiriaki na Kilatini Baada ya kutaja ‘kutokuwapo kwa mstari wa 4 katika maandishi ya hati za mkononi zilizo bora zaidi,’ The Expositor’s Bible Commentary inaongezea hivi: “Kwa ujumla hilo linachukuliwa kuwa maelezo la ziada lililoongezewa ili kueleza kusukwa-sukwa kwa maji mara kwa mara, jambo ambalo halaiki ya watu ililichukua kwamba lingeweza kuwa chanzo cha kuponywa.”
Kwa hiyo Biblia haisemi kwa kweli kwamba malaika kutoka kwa Mungu alifanya miujiza kwenye birika la Bethzatha. Basi, je! maponyo ya kimwujiza yalitukia wakati maji yalipotibuliwa? Hakuna mmoja leo anayeweza kusema kwa uhakika. Huenda ikawa pokeo fulani halisitawi kwamba watu wagonjwa sana au walio viwete walikuwa wameponyewa hapo. Hadithi za wenye kusemwa kuwa waliponywa zilipoenea, huenda ikawa watu wenye shida sana walianza kukutana hapo kwa makundi wakitumainia kuponywa. Sisi tunajua kwamba jambo hilo limetukia kwenye sehemu mbalimbali katika wakati wetu, hata wakati ambapo hapana uthibitisho thabiti juu ya maponyo ya kimungu.
Ingawa hivyo, haitupasi kudhania-dhania mambo kuhusu ponyo ambalo Mwana wa Mungu alifanya kwenye lile birika la Bethzatha. Kwani, bila hata kuingia ndani ya maji hayo, mtu huyo aliponywa dakika hiyo hiyo na yule Tabibu Mkuu. Uwezo wake wenye uthibitisho thabiti wa kufanya hivyo unapasa kutupa sisi sababu ya kutazama mbele kwenye maponyo atakayofanya wakati wa Mileani inayokaribia. Yeye ataponya na kusaidia wanadamu waamimfu warudie ukamilifu.—Ufunuo21:4, 5, 22.1,2.
[Picha Credit Line katika ukurasa wa 31]
Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.