Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 12/15 uku. 7
  • Kujua Yaliyo Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujua Yaliyo Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Nyumba Iliyogawanyika
  • Kutumia Fimbo
  • Je! Kucheza Kamari Si Dhambi?
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Uchezaji Kamari—Uraibu wa Miaka ya 1990
    Amkeni!—1995
  • Michezo ya Bahati Nasibu kwa Nini Inapendwa na Wengi?
    Amkeni!—1991
  • Kuna Ubaya Gani Kucheza Kamari?
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 12/15 uku. 7

Kujua Yaliyo Katika Habari

Nyumba Iliyogawanyika

Yesu alisema kwamba “nyumba ikifitinika [ikigawanyika, NW] juu ya nafsi yake,” haiwezi kusimama. (Marko 3:25) Hivyo ndivyo Kanisa United la Kanada, ambalo ndilo kanisa kubwa zaidi la Kiprotestanti katika taifa hilo, linajikuta likiwa kuhusiana na suala la ugoni-jinsia-moja na kuagizwa rasmi kwa wanaume na wanawake wenye kulawitiana.

Azimio moja lililopitishwa na Baraza Kuu la 32 la Kanisa United la Kanada linaruhusu wagoni-jinsia-moja wafanye kazi wakiwa makasisi. Kulingana na The Globe and Mail, ambayo ni karatasi-habari ya Kanada, azimio hilo linataarifu kwamba bila kujali elekeo lao la kingono, watu wowote “wanaodai kuwa wana imani katika Yesu Kristo na wana utii Kwake wanakaribishwa waendelee kuwa au wapate kuwa washiriki wa Kanisa,” na “washiriki wote wa Kanisa wanastahili kufikiriwa wawekwe kuwa wahudumu rasmi.” Ripoti moja ya Kanisa United yenye kurasa 125 inasema hivi: “Kuna namna mbalimbali za maelekeo ya ngono: ya kufanya ugoni-jinsia moja, ya kuchanganya ugoni-jinsia-moja pamoja na ngono kati ya watu wa jinsia tofauti, na pia ngono ya aina moja tu kati ya watu wa jinsia tofauti. Mazoea hayo ni sharti yaonwe kuwa ya kiasili na kuwa zawadi kutoka kwa Mungu.”

Ikitoa maelezo juu ya uamuzi wa kanisa kukubali wagoni-jinsia-moja wawe makasisi, Globe inaeleza kwamba “kuzuia mmaliziko wa kanisa ndilo suala kuu lililofikiriwa zaidi ya mengineyo.” Ripoti zinafunua kwamba, tangu 1972 kanisa limekuwa likipoteza-poteza washiriki na limo katika matata ya kifedha. Sababu ni nini? Kasisi John Tweedie anataja “mhamo wenye kuendelea wa watu wakiacha kanisa wanapoliona likipeperukia mbali kutoka kwenye vyanzo vyalo vya Kikristo.” “Kwa sababu hiyo,” inaripoti The Post ya Kanada, “kukubali kwao mambo kama vile ugoni-jinsia-moja, ngono nje ya kifungo cha ndoa, utoaji-mimba wa kujidaia, na ndoa zenye uwezekano wa kuvunjwa ni mwanzo wa kuleta mambo hayo kwenye kizazi cha vijana.”

Hata hivyo, je! kumtii Kristo kunaruhusu kuacha msimamo unaofaa kuhusu kanuni za Biblia? Kinyume cha hivyo, Neno la Mungu linasema wazi hivi: “Msijipumbaze wenyewe; watu walio wakosefu wa adili . . . wenye kupotosha tabia kwa ugoni-jinsia-moja . . . hakuna wowote wa hao watamiliki Ufalme wa Mungu.”​—1 Wakorintho 6:9, 10, Today’s English Version; linganisha Warumi 1:26, 27.

Kutumia Fimbo

“Ukose Kutumia Fimbo, Lakini Uyaone Matokeo” ndicho kilikuwa kichwa cha makala moja iliyotokea katika The Natal Mercury, karatasi-habari moja ya Afrika Kusini, ikiomboleza juu ya elekeo la ki-siku-hizi la kutowapa watoto adhabu ya kimwili wakiwa kwenye maskani yao na shuleni. Ni nani mwenye daraka la kulaumiwa kwa mwelekeo huu uliobadilika kuhusu kuchapa? Profesa Smythe, daktari wa watoto kwenye Chuo Kikuu cha Natal, Afrika Kusini, anaweka lawama moja kwa moja juu ya washauri wa jinsi ya kuongoza fikira za watoto. “Kwa kawaida mtu anapochimba ndani ya mizizi ya suala fulani lenye kutokeza matata,” Smythe anaeleza, “yeye hupata kwamba badiliko katika mwelekeo huanza na fundisho fulani la washauri wa jinsi ya kuongoza fikira. Kwanza namna yoyote ya adhabu ya kimwili inapingwa vikali sana, halafu matokeo ya kutokutoa nidhamu yanagutusha sana kutokana na itikadi ya kwamba mtoto hapasi kuvurugwa wala kuzuiwa kutokeza wazi hisia zake za ndani.”

Smythe anatetea kuwe na usawaziko. “Kuendekeza kupita kiasi ni kubaya sawasawa na kuadhibu kupita kiasi,” yeye anasema, “lakini uhakika wa kwamba kurekebisha hali ya mtoto anayetiwa nidhamu kupita kiasi ni rahisi kuliko kurekebisha ya anayetiwa nidhamu pungufu unafanya iwe afadhali kuegemea upande ule wa nidhamu wakati mtu anapokuwa na shaka.” Profesa huyo anakazia kwamba kusudio la kutoa adhabu ya kimwili linapasa liwe ni kuhangaikia kwa upendo masilahi ya mtoto ya sasa na ya wakati ujao.

Ushauri huo si mpya bali ni rudio la mwongozo huu wa Kibiblia usiokosea: “Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; bali yeye ampendaye humrudi mapema.”​—Mithali 13:24; ona pia Mithali 23:13, 14.

Je! Kucheza Kamari Si Dhambi?

Hivi majuzi mtaa mmoja wa kanisa la Katoliki ya Kiroma ulipata kuwa shirika la kwanza la kidini katika Wisconsin, U.S.A., kujaza ombi la kuruhusiwa kuuza tikiti za nasibu, ndivyo inavyoripoti The Sheboygan Press. Ingawa mauzo hayo yanaelezwa kuwa jitihada ya ‘kuongezea’ sadaka zinazokusanywa kila juma, Press inasema kwamba sababu kubwa ya uuzaji unaonuiwa wa tikiti za nasibu “ni kuongeza hudhurio kwenye michezo yalo ya karata.” Inaripotiwa kwamba tayari kanisa linaendesha michezo ya karata kwa kupata faida ambazo “ni kati ya dola 800 hadi dola 1,000” kwa usiku mmoja.

Alipoulizwa kama kweli kucheza kamari ni dhambi, Robert Fleishman aliye padri wa mtaa huo alijibu hivi: “Mimi sijui.” Ingawa alikubali kwamba kuendeleza kwa kanisa michezo ya karata na kuuzia washiriki tikiti za nasibu “labda ni kwenda nje kidogo kutoka kwenye wito wetu wote wa kiroho,” yeye aliongeza kwamba “wao wasipokuja hapa, wataenda mahali penginepo” kutumia pesa zao.

Je! kiongozi wa kidini anayedai kuwa mfuasi wa Kristo anapaswa kuendeleza uchezaji kamari? Hasha! Katika karne ya kwanza, wahudumu Wakristo waliamriwa wawe vielelezo kwa kundi la kondoo “katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.” (1 Timotheo 4:12) Kwa kiongozi wa dini leo kuamsha katika mioyo ya wengine tamaa ya kuwa matajiri kwa kuwatia moyo wafuate zoea la kucheza kamari ni zaidi ya “kwenda nje kidogo” kutoka kwenye ‘wito wake wa kiroho.’ Uchezaji kamari wa namna yoyote huvutia moja ya sifa zilizo mbaya zaidi katika wanadamu​—pupa. Wale wanaouendeleza wanatia watu moyo waitikadi kwamba inafaa kufaidika kutokana na mapotezo ya wengine. Hata hivyo, Neno la Mungu lililovuviwa linataarifu kinaganaga kabisa kwamba watu wenye pupa hawatarithi Ufalme wa Mungu.​—1 Wakorintho 6:9, 10, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki