Haki ya Kimungu—Kisababishi cha Kushangilia!
“NJOONI mwimbe nasi . . . ‘Yehova atawala; dunia ishangilie.’” Maneno hayo yalikuwa sehemu ya wimbo uliokuwa midomoni mwa wajumbe wa Kiarabu, Kigiriki, Kiitalia, Kireno na Kihispania wapatao 9,000 kwenye “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya katika Montreal, Kanada. Wakusanyikaji walimiminika kuingia uwanjani ndani kwenye Olympic Stadium kwa ajili ya dakika za kumalizia mkusanyiko huu wa siku nne ili kujiunga katika wimbo pamoja na wajumbe 36,900 waliokuwa tayari katika stediamu hiyo.
Vikundi vya lugha zile nyingine vilikuwa vimekuwapo kwa ajili ya programu iyo hiyo ya mkusanyiko katika arena na oditoriamu za hapo wa haki ya kweli, Yehova. Kwa sababu ya ukosefu wa haki ulioenea sana katika ulimwengu wa ki-siku-hizi, kichwa cha mkusanyiko—“Haki ya Kimungu”—kilikuwa cha wakati unaofaa kweli kweli. Kwa kuhusishwa-husishwa katika sehemu zote za programu, kichwa hicho kiliongezea uthamini wetu kwa sifa hiyo kuu ya Yehova Mungu.
Wenye Furaha Ni Wale Wanaoshika Haki”
Hicho kilikuwa ndicho kichwa cha siku ya kwanza ya mkusanyiko. (Zaburi 106:3, NW) Hotuba ya mwenyekiti ya ukaribishaji ilielewesha wazi kwamba haki ya kimungu si ule utumizi baridi tu wa sheria yenye kufikilizwa na mahakama. Badala ya hivyo, ni udumisho wa linalofaa kwa njia sawa na isiyo na upendeleo yenye kulingana na viwango vya Mungu. Yehova ndiye huweka viwango vilivyo vya juu zaidi naye ni mkamilifu katika haki kwa sababu yeye hufuatilia sana viwango hivyo. Kwa sababu hiyo, inaweza kusemwa kwamba “njia zake zote ni haki.”—Kumbukumbu 32:4.
Jambo hilo lilikaziwa zaidi katika hotuba ya msingi, yenye kichwa “Haki Hutia Alama Njia Zote za Mungu.” Yehova hajapata kamwe kukengeuka kutoka kwenye viwango vyake vya uadilifu bali ametumia njia zile zile moja za haki katika kushughulika pamoja na aina ya binadamu isiyokamilika. (Malaki 3:6) Ingawa huenda watu fulani wakashtaki Mungu kwa ubandia juu ya kuwa asiye haki kwa sababu wanaona ukosefu mwingi sana wa haki katika jamii ya kibinadamu, yeye siye wa kulaumiwa kwa upotovu wa aina ya binadamu yenye ufisadi.
Kwa kuwa Yehova ni mpenda haki, yeye anatutarajia tujizoeze sifa hii kwa kufanya yaliyo sawa na yenye kufaa. Ni lazima sisi tufanye hivyo kuelekea mwanadamu mwenzetu na jamaa zetu, ndani ya kundi, na katika pande zote za ibada yetu. Hiyo inaleta baraka nyingi, kama vile inavyoweza kuonwa kutokana na mambo yaliyotokezwa katika programu wakati wa siku tatu zilizobaki za “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya.
“Pokea Nidhamu Inayotoa Muono-Ndani”
Siku ya pili ya mkusanyiko ilikuwa na kichwa hicho kilichotangulia, msingi wacho ukiwa ni Mithali 1:3, NW. Tulichagizwa ya kwamba “Kubali Nidhamu na Kuwa Mwenye Hekima,” hicho kikiwa ndicho kichwa cha sehemu fulani ya mapema katika programu. Nidhamu kutoka kwa Yehova hutia alama njia ya maisha inayotia ndani kutakatisha nguvu zetu za kiakili na umbo letu la kiadili. Ni wonyesho pia wa upendo wa Mungu kwetu. (Waebrania 12:4-11) Nidhamu hiyo hutufanya tuwe na hisia yenye wepesi wa kujali viwango vya juu zaidi vya haki—haki ya kimungu.
Maneno hayo ya mwelekeo chanya yalifuatwa na hotuba “Uwe Safi Katika Akili na Mwili.” Nayo iliamsha mawazo kwa njia iliyoje! Ilitukazia uhitaji wa kujitoa wenyewe kwa Mungu tukiwa watu wenye kutakata, walio safi, na watakatifu. Kwa nini? Kwa sababu Yehova ni safi na mtakatifu kwa kadiri ya juu kupita wote—hiyo ikiwa ni hali ambayo inamtenganisha na miungu yote yenye kinyaa ya mataifa. Kwa kuwaza-waza juu ya hotuba hiyo, ndugu mmoja kijana alieleza hivi: “Kila jambo kuhusiana na usafi wetu wa kiakili, wa kimwili, na wa kiroho lilichunguzwa. Mavazi yetu, kujipamba, maskani, gari, na utu, yote yalielekezewa fikira.” Mzee mmoja alionelea hivi: “Kufuata mashauri hayo katika mazoea kutafanya ndugu zetu watokeze wazi zaidi ya wakati mwingine wowote kwa kutofautiana na watu wanaowazunguka, na kutaandaa kipimo fulani cha afya isiyojulikana na ulimwengu kwa ujumla.”
Ile drama ya ki-siku-hizi “Watiwa Alama kwa Ajili ya Kuokoka” iliongezea hisia ya uharaka kwenye programu, kwa maana ni lazima karibuni haki ya kimungu itoshelezwe. Utoaji huo wenye kugusa moyo ulionyesha kwa udhihirifu mwingi kwamba ni jambo la haraka wote wafungue macho waone umaana wa nyakati zetu. Kweli kweli, kabla dini bandia haijapigishwa chini, ni lazima sisi tukimbie kwenda mahali pa kimbilio na kutiwa alama ya kuokokea iliyo wazi kabisa.
Alasiri, mfululizo wa wanenaji walishuhudiza uhitaji wa “Kutoa Nidhamu kwa Uadilifu Katika Jamaa.” Waume na akina baba walionywa kwa upole wawe na programu ya kiroho katika maskani, wakichukua uongozi katika sala, funzo, na utumishi mtakatifu. Sifa za baba za kimwanamume na jinsi yeye anavyoshughulikia ukichwa wake zinakuwa na athari yenye kuonyesha sana rai ambayo mtoto atakuwa nayo juu ya mamlaka, ya kimungu na ya kibinadamu pia. Kwa hiyo, ni lazima baba Wakristo wafuate kanuni na upatani usio na ugeugeu katika nidhamu yao. Wanahitaji kuonyesha hisia-mwenzi na uchangamfu, hivyo wakiendeleza njia za mawasiliano pamoja na watoto wao zikiwa zimefunguka wazi.
Wazazi walitiwa moyo warekebishe maagizo yao yalingane na watoto. Ni jambo la maana kuwapa watoto muono-ndani kwa kufikiria jinsi ya kufundisha na mambo ya kufundisha ili kufikia mioyo yao. Lengo ni kufanya ukweli utie uvutano katika jamaa nzima kwa njia yenye mafaa.
Mnenaji wa mwisho wa mfululizo huu alitoa usihi mchangamfu kwamba watoto wafanye yale ambayo Yehova anatarajia wafanye ndani ya mpango wa jamaa. Vijana walichagizwa waepuke roho ya uasi ya jamii ya leo yenye uendekevu na kushangilia katika nidhamu inayotoa muono-ndani.
Katika maelezo yenye msingi wa Mithali 2:1-9, wakusanyikaji walitiwa moyo ya kwamba “Endelea Kutafuta-tafuta kama Kutafuta Hazina Zilizofichika.” Kielezi kilitolewa kwamba vito vya kiroho vinaweza kupatikana kupitia funzo la bidii-endelevu na utafiti. Akinena juu ya habari “Tegemea Yehova Uwe na Muono-Ndani,” mnenaji aliyefuata alieleza kwamba muono-ndani ni uwezo wa kuona ndani ya hali fulani, kutazama ng’ambo ya mambo yenye kuonekana wazi na kupata maana ya jambo fulani. (Mathayo 13:13-15; Warumi 3:11; Waefeso 5:17) Halafu siku hiyo ya kusisimua ikafikia upeo wakati Olympic Stadium ilipounganishwa kwa kamba ya simu pamoja na majiji mengine katika Kanada na United States. Ule mfululizo wenye sehemu mbili, “Tegemea Yehova Uwe na Muono-Ndani,” ulitiliwa mkazo kwa kutolewa kwa kichapo chenye mabuku mawili Insight on the Scriptures, cha kurasa zaidi ya 2,500 zilizo na makala zenye kuarifu na vielezi ambavyo vitaongezea kina uthamini wetu wa mambo ya kiroho.
“Hukumu Zake Ni za Kweli na za Uadilifu”
Siku ya tatu, iliyokuwa na kichwa hicho chenye msingi wa Ufunuo 19:2, kulikuwa na mengi ya kufanya tushangilie. Hotuba “Usafi wa Kiadili Ndio Uzuri wa Ujana” iliwasihi sana vijana. Wao walichagizwa wathamini sana uzuri unaoshirikishwa na kudumisha viwango vya Mungu vya usafi wa kimwili, wa kiadili, na wa kiroho. Nyimbo zenye kutokeza wazi mambo ya ngono, programu za televisheni zenye ukosefu wa adili, sinema na fasihi ya kipornografia, na mbano unaotokana na marika huwapiga kwa wingi vijana Wakristo. Kulingana na chanzo kimoja, kijana wa hali tofauti kabisa ndiye huwa hajafanya ngono kabla ya ndoa kufikia umri wa miaka 19. Lakini hadhirina ilipiga makofi kwa uchangamfu wakati mnenaji alipopongeza maelfu ya vijana Mashahidi wanaojionyesha kuwa wa hali tofauti kabisa kwa kudumisha kiwango cha juu cha uadilifu. Ndoa za mapema zinaambatana na matatizo, na ilionyeshwa kwamba maneno ya Paulo juu ya kufunga ndoa kwa sababu ya ‘kuwaka harara’ yameelekezwa si kwa matineja bali kwa wale ‘waliopita ukamilifu wa ujana.’—1 Wakorintho 7:9, 36, NW.
“Msijifunge Nira Wenyewe na Wasioitikadi” ikawa ndiyo mada iliyofuata. Kutii amri ya Mungu kufunga ndoa “katika Bwana tu” hutuepusha sisi na matokeo yenye maumivu. (1 Wakorintho 7:39) Waaidha, hakuna kitu chenye kuimarisha ndoa kuliko bidii yenye kushirikiwa pamoja katika kujitolea Yehova na kufuatilia viwango vyake vya uadilifu. Ndipo sisi tuliposaidiwa kuona jinsi tunavyopaswa kuwa katika “Kutenda kwa Staha na Hofu ya Kimungu.”
Ndipo ilipokuja sehemu ya kusisimua sana—ile hotuba “Ubatizo Unaoongoza Kwenye Hukumu Yenye Kupendeleka,” ikifuatwa na uzamisho wa watu waliojiweka wakfu karibuni. Ilikaziwa kwamba mengi zaidi yalitarajiwa kwao kuliko kuondolea mbali tu kinyaa (uchafu) cha mnofu. Toba, uongofu, na utumishi mtakatifu wa muda wote wa maisha lazima vishirikishwe na wakfu na ubatizo wao ndipo waone shangwe ya kupata hukumu inayopendeleka kutoka kwa Yehova.
Hakika programu ya alasiri ilikuwa ya kukumbukika. Tena kupitia muunganisho wa kamba ya simu, washiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova walisisimua sana hadhirina za watu upande mmoja hadi mwingine wa Amerika ya Kaskazini kwa utoaji wenye kuchochea wa ule mfululizo “Wakati Uliowekwa U Karibu.” Kwa miongo ya miaka, mashahidi wapakwa-mafuta wa Yehova wamepiga mbiu ya jumbe za hukumu ya kimungu dhidi ya Babuloni Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini bandia. Hata hivyo, kwenye mkusanyiko huu jumbe hizo ziliimarika zaidi. Babuloni Mkuu amekuwa na hatia ya kuvunja amri adilifu za Yehova. Yeye anastahili uharibifu, kwa maana “madhambi yake yametungamana pamoja moja kwa moja hadi kwenye mbingu, na Mungu ameita akilini matendo yake yasiyo ya haki.” Hivyo, kama vile malaika wa Yehova anavyotangaza, “katika siku moja tauni zake zitakuja, kifo na ombolezo na njaa kuu, na yeye atachomwa kabisa kwa moto, kwa sababu Yehova Mungu, ambaye alihukumu yeye, ni imara sana.”—Ufunuo 18:5, 8, NW.
Akinena juu ya habari “‘Kahaba’ Mwenye Sifa Mbaya Sana—Anguko na Uharibifu Wake,” mnenaji wa mwisho wa mfululizo huu alivuta fikira kwenye upeo mtukufu wa Ufunuo. Upeo huo unafikiwa kwa ndoa ya Mwana-Kondoo, ambaye anaungamana pamoja na bibi-arusi wake, lile jiji takatifu, katika kubariki aina ya binadamu kwa uhai wa milele. Jina la Yehova linatakaswa! Mfululizo huo ulimalizia kwa taarifa yenye kusukuma kwenye kitendo kwamba wakati uliowekwa u karibu kuliko vile ambavyo huenda sisi tukafikiri! Kweli kweli, upeo mtukufu wa Ufunuo u karibu!
Hadhirina ilipokuwa ingali ikipiga makofi, kikatolewa kitabu kipya cha kurasa 320 Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Lo, kilikuwa kisababishi kilichoje cha kushangilia! Kichapo hicho hakika kitakuwa njia yenye athari nzuri ya kutangaza kwamba Babuloni Mkuu amehukumiwa maangamizi, kwamba sasa mataifa yanaelekeana usoni na Har-Magedoni, na kwamba Yehova yuko karibu kufikiliza hukumu. Acheni wote wenye uthamini wajibu mwaliko wa “roho na bibi-arusi” unaosema “njoo” kwenye maji ya uhai. (Ufunuo 21:2, 9; 22:17, NW) Kitolewaji hicho cha kusisimua kilichopigwa chapa kilifuatwa na kisababishi kingine cha kushangilia. Kwa usadikisho wenye shangwe, hadhirina za mkusanyiko zilipitisha kwa nia moja azimio lenye kueleweka vizuri sana na la wazi likitaarifu karaha yetu juu ya Babuloni Mkuu.
“Haki—Haki Wewe Umepaswa Ufuatie”
Kikiwa juu ya msingi wa Kumbukumbu 16:20, hicho kilikuwa ndicho kichwa cha siku ya mwisho. Wanenaji wa asubuhi walikazia uhakika wa kwamba ili kunufaika kutokana na haki ya kimungu, ni lazima sisi tuwe tofauti na ulimwengu. Fikiria ile hotuba “Kudumisha Afya ya Kiroho Katika Ulimwengu Mgonjwa.” Ilionyesha jinsi sisi tunavyoweza kuepuka kuchafuliwa na ulimwengu wenye afya mbaya kiroho kwa kujilinda dhidi ya udhaifu mbali-mbali wa kimnofu, uvutano wa kilimwengu, na “hila za Ibilisi.” (Waefeso 6:11, 12, NW; Warumi 7:21-25; 1 Yohana 2:15-17) Hotuba “Je! Imani Yako Inashutumu Ulimwengu?” ilionyesha kwamba ikiwa sisi tuna imani kama ile ya Noa, tutatokeza wazi kuwa tofauti na ulimwengu. Katika siku ya Noa, kulikuwa na tofauti ya wazi kati ya waokokaji wa Gharika na wale walioangamia. Ndivyo ilivyo na leo.
Wazo hilo la maana lilikaziwa katika drama ya Biblia “Hukumu za Yehova Dhidi ya Watu Wanaokaidi Sheria.” Ililinganisha kwa udhihirifu mwingi watu wenye kukaidi sheria katika siku za Noa na Loti pamoja na wale wanaoishi katika wakati wetu. Noa na Loti walitokeza wazi kuwa tofauti sana, na imani yao ilishutumu marika wao. Je! sisi binafsi hutokeza wazi kuwa tofauti na watu wa leo wenye kushughulikia zaidi vitu vya kimwili na wenye kupenda mabaya?
Hotuba ya watu wote, “Haki kwa Ajili ya Wote Kupitia Hakimu Mwekwa wa Mungu,” ilikuwa mchanganuo wenye kuvuta sana fikira juu ya hotuba ya mtume Paulo kwa watu wa Athene juu ya Areopago, au Kilima cha Mars. Kwa kuwa sisi tumezungukwa na matendo mabaya sana ya kukosa haki na dini bandia, maneno ya mtume yana maana kubwa kwetu. Hasa sisi tuna sababu ya kushangilia kwa sababu tunaishi wakati wa maana sana wa hukumu ambapo sisi tunaweza kuchukua hatua ya kupata kibali cha Mungu. Ndiyo, kama vile Paulo alivyosema, Yehova anakusudia “kuhukumu dunia inayokaliwa na watu katika uadilifu kwa mwanamume [Yesu Kristo] ambaye yeye ameweka, na yeye ametoa uhakikisho kamili kwa watu wote kwa sababu yeye amefufua huyo kutoka kwa wafu.”—Matendo 17:31, NW.
Programu ilipokuwa ikaribia mwisho, tulichagizwa ya kwamba “Endelea Kufuatia Haki Upeo Unapokaribia.” Mkusanyiko huo wa siku nne ulio wa kupendeza sana ulitujaza hali ya kupiga moyo konde tufanye hivyo. Programu ilitukazia pia kadiri ya mweneo wa udugu wetu wa kimataifa. Mathalani, ilikuwa shangwe iliyoje kusikia kutoka kwa wamisionari wenye kuzuru waliokuwa wamekuwa wakitumikia kwa uaminifu katika migawo yao kwa miaka mingi!
Sisi tulitoka kwenye mkusanyiko tukiwa na hali iliyofanywa upya ya kupiga moyo konde tubaki tukiwa tumejitenga na ulimwengu huu na kuendelea kuwa safi kiroho, kiadili, kiakili, na kimwili. Tulipokuwa tukijiunga katika wimbo wa kumalizia, tuliterema kuimbia Yehova sifa, tukiwa na shukrani kwamba haki ya kimungu inatupatia kisababishi kikubwa cha kushangilia.
Kwenye mikusanyiko zaidi ya 125 katika United States na Kanada pekee, watu 1,440,932 walikuwako na 19,878 walibatizwa
[Picha katika ukurasa wa 26]
1, 2. Vichapo Insight on the Scriptures na Revelation—Its Grand Climax At Hand! vikitolewa Yankee Stadium, Jiji la New York, na washiriki wa Baraza Linaloongoza, J. E. Barr na W. L. Barry
3, 4. Tamasha kutoka drama ya Biblia “Hukumu za Yehova Dhidi ya Watu Wanaokaidi Sheria
5. Maelfu walibatizwa kwa ufananisho wa wakfu wao kwa Yehova Mungu
6. Tamasha kutoka drama ya ki-siku-hizi “Watiwa Alama kwa Ajili ya Kuokoka”
7. Wamisionari wenye kuzuru, kama vile John Cutforth wa Papua New Guinea, walishiriki maono yao pamoja na wakusanyikaji