Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 3/1 kur. 4-7
  • Ni Nani kwa Kweli Walio Wahudumu wa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani kwa Kweli Walio Wahudumu wa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Itikadi Katika Biblia
  • Wahudumu wa Kweli na Maadili
  • Wahudumu wa Kweli Hufundisha Mafundisho ya Kweli
  • Matakwa ya Kimaandiko ya Wahudumu wa Kweli
  • Je! Wanawake Waagizwe Rasmi?
  • Yesu Kristo.​—Kielelezo Chenye Kung’aa
  • Kuwasaidia Maskini, Wagonjwa, na Wazee-Wazee
  • Kutimiza Unabii wa Biblia
  • Wahudumu wa Mungu Ni Akina Nani Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Ni Nani Walio Wahudumu wa Mungu Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Jinsi ya Kutambua Wahudumu wa Kweli wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Ni Lazima Wakristo wa Kweli Wote Wawe Wahudumu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 3/1 kur. 4-7

Ni Nani kwa Kweli Walio Wahudumu wa Mungu?

“KATIKA saa hii ya kukata maneno tunawashauri askari wetu Wakatoliki wafanye wajibu wao kwa kumtii Fuehrer [Hitler].”​—Maaskofu Wakatoliki wa Ujeremani, kama ilivyonukuliwa katika The New York Times, Septemba 25, 1939.

“Wajua, padri, katika ndege yetu mmoja wa wanausukani wetu ni Mkatoliki, nawe unambariki kabla hatujafunga safari ya tume zetu za kuangusha makombora juu ya Ujeremani. Sasa, dini ile ile ya Kikatoliki katika Ujeremani inabariki mshiriki Mkatoliki aliye mwanausukani wa ndege ya Ujeremani inayokuja na kuharibu majiji yetu. Hivyo basi swali langu ni hili, ‘Mungu yuko upande wa nani?’” Hivyo ndivyo alivyonena ofisa mrukaji Mwingereza, David Walker, katika maongezi aliyofanya pamoja na padri Mkatoliki wakati wa Vita ya Ulimwengu 2.

Tofauti na hivyo, maelfu ya Mashahidi wa Yehova walikaa miaka mingi katika kambi za mateso ya kutisha za Nazi kwa sababu ya kukataa kuisema shime ya heil Hitler (mwokozi ni Hitler) au kupigana katika majeshi yake. Katika nchi za Mataifa-Mafungamani, Mashahidi wengi walitiwa gerezani kwa kukataa utumishi wa kijeshi.

Wahudumu wa kweli wa Mungu ni akina nani, na ni matakwa gani ambayo lazima watimize?

Itikadi Katika Biblia

Ni wazi kwamba lazima mhudumu wa kweli wa Mungu awe na itikadi imara katika Biblia. Inampasa pia aijue vizuri kwa kadiri inayotosha kufundisha wengine. Lakini wengi wa makasisi wa Jumuiya ya Wakristo hawatimizi matakwa hayo ya msingi. Daktari mmoja katika Afrika Kusini alitaarifu kwamba wahudumu wa Kanisa Anglikana, alilokuwa mshiriki walo hapo kwanza, ‘walitumia kidogo sana’ Biblia, na mahubiri yalionekana kuwa kauli ya kibinafsi ya mhubiri. Pia alilalamika juu ya makasisi, kama Askofu Mkuu Tutu wa Cape Town, kwa sababu ya kujihusisha katika siasa.

Tofauti na hivyo, watumishi waaminifu wa Yehova wanaitikadi kwa imara katika Biblia na kutumia mwingi wa wakati wao wakijifunza yaliyomo na kuwaeleza wengine. Upendezi na upendo wao kwa Biblia una kina kirefu sana hivi kwamba wametokeza tafsiri iliyofanyiwa utafiti wa kweli kweli na iliyo sahihi sana inayoitwa New World Translation of the Holy Scriptures, inayotegemea hati-mkono za Biblia zenye mamlaka thabiti, za Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Katika Reference Edition (Chapa ya Marejezo) ya Biblia hiyo mna maelfu ya maandishi-pambizo na marejezo-mlinganisho kusaidia wasomaji waelewe Biblia vizuri zaidi na kuwawezesha waeleze wengine. Waaidha, tafsiri hiyo ya Biblia iliyo ya kutokeza imetafsiriwa, yote au kwa sehemu, katika lugha nyinginezo 10, na makumi ya mamilioni ya nakala zimegawanywa ulimwenguni pote.

Wahudumu wa Kweli na Maadili

Biblia hushutumu vikali namna zote za dhambi ya ngono​—kutia na uzinzi, uasherati, ugoni-jinsia-moja, na ugoni-wanyama. (Walawi 20:10-13; Warumi 1:26, 27; Wagalatia 5:19) Wahudumu wa kweli wa Kikristo huunga mkono kanuni za maadili ya Mungu kwa moyo mzima. Ndiyo, Mashahidi wa Yehova wanachukua sheria ya Mungu kwa uzito sana. Wanawatenga na ushirika wale wanaofanya dhambi za jinsi hiyo bila kutubu, huku wakiwarehemu wale wanaotubu kikweli juu ya vitendo vya kukosa adili na kusafisha maisha zao.​—1 Wakorintho 5:11-13; 2 Wakorintho 2:5-8.

Katika Afrika Kusini, Shemasi Mwanglikana wa Cape Town anaripotiwa kuwa alisema hivi: “Mahusiano fulani ya ngono za jinsia ile ile ni bora kuliko mahusiano ya ngono za jinsia tofauti na kwa sababu ya ule ubora wa mapenzi yenyewe, mimi nina hakika yanamfurahisha Mungu zaidi.” Ni kinyume kabisa. Mungu anachukizwa sana na mahusiano ya jinsi hiyo. ​—1 Wakorintho 6:9, 10.

Wahudumu wa Kweli Hufundisha Mafundisho ya Kweli

Wahudumu wa kweli hufundisha mafundisho yaliyoimarishwa juu ya msingi wa Neno la Mungu. Wahudumu wa bandia hufundisha mafundisho yasiyo na utegemezo au msingi katika Biblia. Mathalani, fikiria fundisho la Utatu. Kama inavyotaarifu The Encyclopaedia Britannica (Chapa ya 15): “Wala neno Utatu wala fundisho lenyewe hasa halionekani katika Agano Jipya, wala Yesu na wafuasi wake hawakuwa na madhumuni ya kuipinganisha Shema katika Agano la Kale: ‘Sikia, O Israeli: Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja’ (Kum. 6:4).” Utatu halikuja kuwa fundisho rasmi la kanisa mpaka karne ya nne W.K. katika siku za Mmaliki Mroma Konstantino. Kwa uhakika, sababu iliyofanya fundisho hilo la bandia likubaliwe na Baraza la Nikaya katika 325 W.K. ilikuwa kwa sehemu ni fahari na umashuhuri wa mmaliki huyo.

Fundisho la Utatu limesababisha washiriki wengi wa kanisa, wenye kutafuta ukweli kwa kufuata haki, wapoteze uhakika katika wahudumu wao. Ndivyo ilivyokuwa kwa mwanamke kijana katika Afrika Kusini ambaye hangeweza kuitikadi kwamba dini yake, Kanisa Dutch Reformed, ilifundisha itikadi hiyo ya Utatu yenye kuvuruga sana fikira, mpaka mmoja wa Mashahidi wa Yehova alipomtolea uthibitisho wa kimaandishi kwamba ndivyo mambo yalivyo! Mwanasheria mmoja mzeemzee aliyestaafu, wa Afrika Kusini pia, alijiuzulu kutoka kanisa lake kwa sababu “mafundisho mbalimbali yanayofundishwa katika makanisa kwa namna ile ile moja bila ubadilikano yanakosea kabisa na kutoa uongozi wenye makosa.”

Fundisho jingine bandia la Jumuiya ya Wakristo ni lile la moto wa mateso. Ingawa halihubiriwi kwa mapana wala haliitikadiwi kama hapo kwanza, lingali ndilo fundisho rasmi la makanisa yaliyo mengi. Yanadai kwamba kifo kitokeapo mwili hufa lakini nafsi, kwa kuwa haiwezi kufa, huendelea kuishi, na wale ambao wameendesha maisha maovu wanaumizwa-umizwa kwa umilele wote katika moto unaowaka. Je! wewe unaitikadi hivyo? Kwa umaana hata zaidi, je! hilo ni jambo la kweli? Si kulingana na Biblia, inayosema: “Nafsi inayofanya [dhambi], itakufa.” (Ezekieli 18:4, 20, ZSB) Waaidha, mtume Paulo aliyevuviwa aliandika hivi: “Mshahara wa dhambi ni mauti”​—si moto wa mateso!​—Warumi 6:23.

Acheni sasa tufikirie viwango ambavyo ni lazima wahudumu Wakristo watimize.

Matakwa ya Kimaandiko ya Wahudumu wa Kweli

Neno la Kiingereza “minista” (mhudumu) ni tafsiri ya neno la Kigiriki “di·aʹko·nos,” lisilojulikana asili yalo kwa uhakika. Linarejezea mtu anayetekeleza amri za mwingine, hasa za bwana-mkubwa. Kwa sababu hiyo, neno hilo katika Biblia huelekeza waziwazi kwa mtumishi. Utumizi wa neno hilo katika Biblia unaonyesha mtu asiyechoka na kuacha kutoa kwa unyenyekevu utumishi wa kikamili kwa ajili ya wengine. Yesu alikazia uhitaji wa utumishi huo wa unyenyekevu, kama vile kielelezo kinachofuata kinavyoonyesha.

Siku moja, muda mfupi kabla ya Yesu kufa juu ya mti wa mateso, mama ya Yakobo na Yohana alimfikia na kusema: “Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.” Wanafunzi wale wengine walighadhibishwa na jambo hilo. Ndipo Yesu akawafundisha kwa fadhili somo la maana. Aliwakusanya pamoja na kusema: “Mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi [mhudumu, NW] wenu; na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu.”​—Mathayo 20:20, 21, 24-27.

Katika moja ya hotuba zake zenye kujenga, zilizotiwa katika kumbukumbu la maandishi, Yesu alionya wasikilizaji wake juu ya waandishi na Mafarisayo. Pia alionyesha wazi baadhi ya kasoro za wazi sana za hao wahudumu wa bandia, wenye unafiki. Aliwaeleza kuwa wenye kiburi sana na wenye kudai mambo na kutaka umashuhuri sikuzote.​—Mathayo 23:1-7.

Leo, makasisi wengi, hasa mapadri wa Kanisa Katoliki na, katika visa fulani, Waanglikana, hudai kwamba waitwe “Baba.” Mathalani, padri mmoja wa Kanisa la Uingereza katika Msumbiji, alipoulizwa maswali miaka kadhaa iliyopita na mmoja wa Mashahidi wa Yehova juu ya sababu ya yeye kutumia cheo “Baba,” alijibu hivi: “Najivunia kufanya hivyo!” Na, bila shaka, inajulikana vizuri kwamba papa wa Roma huwa na upendezo wa kuitwa “Baba Mtakatifu”​—lijapokuwa agizo la Yesu kwa wanafunzi wake kwamba “msimwite mtu yeyote duniani baba yenu, kwa kuwa nyinyi mna Baba mmoja tu, na yeye yuko mbinguni.” Yesu aliongeza kanuni hii ya msingi: “Mtu yeyote ajikwezaye atanyenyekezwa.”​—Mathayo 23:9-12, The Jerusalem Bible.

Je! Wanawake Waagizwe Rasmi?

Hivi majuzi, kumekuwa na ongezeko la hesabu ya wanawake wanaoagizwa rasmi wawe makasisi. Lakini Paulo aliagiza Timotheo hivi: “Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume.” (1 Timotheo 2:12) Hata hivyo, hiyo haimaanishi kwamba mwanamke Mkristo hawezi kufundisha watoto wake au kufundisha miongoni mwa watu kwa ujumla, bali kwamba hapaswi kufundisha katika kundi.

Basi, je! wanawake hawapaswi kamwe kunena kwenye mikutano ya Kikristo? Mashahidi wa Yehova hujifunza gazeti hili, Mnara wa Mlinzi, kwenye mmoja wa mikutano yao ya kila juma, wakitumia makala zinazoongezewa maswali kuhusiana na mafungu. Mhudumu anayeongoza funzo hilo, ambaye sikuzote ni ndugu, huwatolea wito washiriki wa kundi, kutia na akina dada, wajibu maswali hayo. Lakini wanawake hao hawawi wakifundisha. Wao wanakuwa wakieleza kwa maneno yao wenyewe tu fikira zilizo katika makala ile. Hata watoto wanatiwa moyo washiriki kutoa majibu, na mara nyingi maelezo yao, ambayo kwa kawaida ni mafupi na rahisi, hugonga kichwa cha msumari sawasawa​—tukitumia usemi ujulikanao sana.

Paulo alisema taarifa hii pia kuhusu wanawake: “Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa [kundi, NW].” (1 Wakorintho 14:35) Hiyo inamaanisha kwamba ikiwa akina dada hawaelewi au wanafadhaishwa na taarifa fulani zilizosomwa au kusemwa nyakati za mikutano, hawapaswi kutokeza mawazo ya ushindani mbele ya kundi. Bali, inawapasa wawaombe waume zao kuwaelewesha mambo wakiwa nyumbani.

Hata hivyo, kuna pindi ambazo wanawake Wakristo wanaweza kuhubiria wanaume. Mashahidi wa Yehova hutumia wakati mwingi wakihubiri habari njema za Ufalme nyumba kwa nyumba. Wakati mhubiri mwanamke anapokuta mwanamume, je! ni lazima yeye aombe radhi na kwenda zake tu? Sivyo bila shaka. Katika kisa hicho, yeye hawi akihubiria kundi bali mtu mmoja ambaye huenda akawa si mwitikadi. Vilevile, mhudumu wa kike anaweza kujifunza Biblia pamoja na jamaa isiyo ya Kikristo hata ingawa baba wa hapo yupo.

Yesu Kristo.​—Kielelezo Chenye Kung’aa

Yesu alikuwa kielelezo chenye kung’aa ambacho ingetufaa tujaribu kukinakili! Alikuwa ndiye mwalimu bora zaidi, mhubiri mzuri zaidi, mfanya kazi mwenye bidii nyingi zaidi, na mshauri mwenye upendo mwingi zaidi aliyepata kuishi duniani. Kufuata katika hatua za nyayo zake ni pendeleo kubwa sana. Je! wewe unajaribu kufanya hivyo?

Mamilioni ya Mashahidi wa Yehova wanafanya yote wawezayo kumnakili​—ijapokuwa kwa njia isiyokamilika. Njia zake zilikuwa tofauti sana na zile za makasisi walio wengi leo. Yeye hakupiga kengele za kanisa na kungojea watu wamjie, ingawa wengi walikuja kwa kupenda kwao. Badala ya hivyo, aliwaendea watu na kuwafundisha katika nyumba zao, mahali peupe, juu ya milima, na katika ufuo wa Bahari ya Galilaya. Nyakati fulani alihutubia vikundi vyenye maelfu ya watu, kama inavyoonyeshwa chini katika kielezi. ​—Mathayo 9:35; 13:36; Luka 8:1.

Kuwasaidia Maskini, Wagonjwa, na Wazee-Wazee

Hao ni wangapi leo? Ni mamia ya mamilioni. Na hesabu yao inaongezeka kasi wakati hali za ulimwengu zinapozorota haraka sana na mfumo wa sasa wa mambo kukaribia mwisho wao kamili kwenye pigano la Har-Magedoni. (Ufunuo 16:16) Maafa ya kiasili, njaa kubwa, na magonjwa ya kipuku yanaongezea madhara na mteseko. Wakristo wa mapema pia walilazimika kushughulika na matatizo ya jinsi hiyo. Karibu na 46 W.K., Klaudio alipokuwa mmaliki wa Roma, ilikuwako njaa kubwa yenye kuenea kwa mapana. Hivyo basi, wanafunzi walifanya nini? ‘Waliazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi.’​—Matendo 11:27-30.

Katika nyakati za ki-siku-hizi, mara nyingi Mashahidi wa Yehova wamewagawia watesekaji au wahitaji msaada wa ukarimu. Hivi majuzi, Msumbiji ilipokumbwa vibaya na vita ya wenyewe kwa wenyewe​—matokeo yakiwa ni upungufu mbaya sana wa chakula, nguo, vifaa vya kitiba, na mahitaji mengine ya msingi​—Mashahidi wa Yehova katika Afrika ya Kusini iliyo jirani walisaidia ndugu zao katika taabu kubwa. Vyakula vingi, nguo, na vitu vinginevyo vilikusanywa na kupelekwa Maputo, jiji kuu, katika malori makubwa.

Kutimiza Unabii wa Biblia

Ndiyo, wahudumu wa kweli wa Mungu leo wana pendeleo zuri sana la kushiriki katika utimizo wa manabii ya Biblia. Jinsi gani? Katika ile pindi ya kihistoria ambapo wanafunzi waliuliza Yesu: “Mambo hayo yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” yeye alijibu kwamba katika wakati wa vita vya ulimwengu, njaa kubwa, matetemeko ya dunia, na kutotii sheria, “habari njema hizi za ufalme zi[nge]hubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa.” (Mathayo 24:3, 14, NW) Paulo aliwawekea kielelezo wahudumu wote wa kweli kwa kuhubiri “nyumba kwa nyumba.”​—Matendo 20:20, NW.

Mashahidi wa Yehova wanajulikana ulimwenguni pote kwa bidii yao katika kazi hii ya kuhubiri. Labda wao wamekutembelea nyumbani nyakati fulani. Je! wewe umewahi kuwapa usikivu mwema? Ikiwa sivyo, kwa nini usifanye hivyo wakati ule mwingine wakikutembelea? Huenda ukapata mshangao mzuri!

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 4]

Inategemea picha ya Jeshi la United States

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki