Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 3/1 uku. 3
  • Jinsi ya Kutambua Wahudumu wa Kweli wa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kutambua Wahudumu wa Kweli wa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Matakwa kwa Wahudumu wa Kweli
  • Wahudumu wa Mungu Ni Akina Nani Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Ni Nani Walio Wahudumu wa Mungu Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Ni Lazima Wakristo wa Kweli Wote Wawe Wahudumu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Wahudumu wa Ufalme Wanaelekeana na Ubishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 3/1 uku. 3

Jinsi ya Kutambua Wahudumu wa Kweli wa Mungu

ILITUKIA katika 1948. Wahudumu wawili, Mashahidi wa Yehova, walikuwa wakisafiri katika basi bovu katika barabara yenye mashimo-shimo, wakitoka mji mmoja katika Hispania kaskazini kuelekea Milima ya Pyrenee. Walikuwa wakienda kuzuru mhudumu aliye peke yake. Basi lile lilipokuwa likisimama karibu zaidi na kijiji ambacho mhudumu huyo aliishi, walimwona akiwangojea akiwa na punda wake. Lakini pia wakaona kikundi cha watu wasio wa kikawaida hapo karibu​—Walinzi-Raia wanne wenye silaha za kutosha na padri mmoja! Wahudumu hao walipokuwa wakipanda kijia kilichoinuka sana cha kwenda kijijini, mmoja wa Walinzi alichomoa bastola yake na kupaaza sauti hivi, “Marion arriba!” (Mikono juu!) Wageni hao wakakamatwa. Kwa nini? Padri huyo alikuwa amewaambia Walinzi kwamba wageni hao walikuwa wavamizi-haramu​—uwongo gani huo! Tokeo ni kwamba, wahudumu wote watatu walitiwa gerezani.

Hiyo inathibitisha nini? Kwamba si wote wanaodai kuwa ni mapadri au wahudumu (maminista) ni wahudumu wa kweli wa Mungu. Kwa uhakika, mara nyingi kuna tofauti kubwa sana kati ya wahudumu wa kweli na walio wa bandia. Ni nini matakwa ya msingi kwa wahudumu wa kweli?

Matakwa kwa Wahudumu wa Kweli

Maana ya msingi ya “kuhudumu” ni “kutoa msaada au utumishi.” Ni lazima wahudumu Wakristo walio wa kweli wawe na itikadi imara kwamba Biblia ndilo Neno la Mungu lililovuviwa. (Yohana 17:17) Hata hivyo, takwa hilo la msingi halitoshi. Ni lazima pia wawe na maarifa na uelewevu wa kutosha juu ya Biblia. Lakini ni lazima wasitumie maarifa hayo kwa ubinafsi​—kwa manufaa yao wenyewe tu. Inapasa pia wawe wahubiri wenye bidii wa Gospeli​—zile habari njema juu ya Ufalme wa Mungu na tumaini la uhai wa milele juu ya dunia paradiso.​—Yohana 17:3; Zaburi 37:11, 29.

Kufuatana na hilo, uhakika wa kwamba Mashahidi wa Yehova wanahubiri habari njema za Ufalme si katika Hispania tu bali katika sehemu zote za ulimwengu unatimiza yale ambayo Yesu alitabiri kiunabii kwa ajili ya wakati wa mwisho wa huu mfumo mbovu wa kale wa mambo. Alisema: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.”​—Mathayo 24:14, 33, 34, NW.

Takwa jingine la msingi kwa wahudumu wa kweli ni kwamba, kama alivyosema Yesu, wanapaswa kuwa “si sehemu ya ulimwengu”; kwa sababu hiyo, inawapasa wakae nje ya siasa. (Yohana 15:19, NW) Inawapasa pia wawe wanyenyekevu sana, wenye upendo, na fadhili, sikuzote wakiwa tayari kusaidia wastahilivu wenye uhitaji.​—1 Wakorintho 13:1, 4; 1 Petro 5:6.

Hilo ni jambo zito sana. Kupambanua kati ya wahudumu wa kweli na walio wa bandia ni jambo linalohusu uhai na kifo. Ni jambo zito kadiri hiyo! Katika Mahubiri ya Mlimani yajulikanayo sana aliyoyatoa, Yesu alionya hivi: “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.”​—Mathayo 7:15.

Hata hivyo, si kwamba tu wahudumu wa kweli wa Mungu wana wajibu mbalimbali na matakwa ya kutimiza bali wana mapendeleo mengi pia. Kwa uhakika, wakiwa kikundi, wao ndicho kikundi chenye pendeleo kubwa zaidi, chenye mafanikio mengi zaidi, na chenye furaha kubwa zaidi duniani leo, kama utakavyoona katika makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki