Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 3/15 kur. 10-11
  • Insight on the Scriptures—Ensaiklopedia Mpya ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Insight on the Scriptures—Ensaiklopedia Mpya ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Vitabu vya Biblia
  • Marekebisho ya Kutakasa
  • Atlasi ya Ramani za Biblia
  • Mambo ya Pekee Katika Rangi Kamili
  • Ramani za Kutimiza Mahitaji Yako
    Amkeni!—1995
  • Usanifu-Ramani—Msingi wa Kuufahamu Ulimwengu
    Amkeni!—1998
  • Jinsi ya Kufanya Utafiti
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Tegemea Yehova Uwe na Muondo-Ndani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 3/15 kur. 10-11

Insight on the Scriptures​—Ensaiklopedia Mpya ya Biblia

KWENYE “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova, tangazo lilifanywa juu ya kutolewa kwa ensaiklopedia mpya ya Biblia yenye kichwa Insight on the Scriptures (Muono-Ndani Juu ya Maandiko). Hicho ni kichapo chenye mabuku mawili, chenye jumla ya kurasa 2,560, yote yakiwa na herufi zenye kuonekana wazi na zenye kusomeka. Kwa wakati uliopo inapatikana kwa Kiingereza tu, lakini tayari tafsiri inaendelea katika lugha kadhaa nyinginezo.

Insight on the Scriptures inatia ndani mengi ya mambo yaliyokuwa katika kitabu Aid to Bible Understanding na mengine zaidi. Iko tofauti katika mambo gani? Visehemu vingi vimesahihishwa na kulinganishwa na hali za kisasa. Pia katika Insight on the Scriptures mna makala nyingi mpya na mambo yaliyoongezwa.

Vitabu vya Biblia

Kila kitabu cha Biblia kimepewa fikira za pekee. Habari za thamani kubwa zimetolewa juu ya matukio yanayohusika nazo. Kuna mihtasari mipya-mipya ya vitabu vyote vya Biblia, kila mmoja ukivuta fikira kwenye sehemu zile kubwa-kubwa hasa za kitabu kinachohusika. Mihtasari hiyo inatoa maoni mafupi lakini yenye kuelewesha kikamili mambo yaliyo katika kitabu kinachohusika, kwa njia iliyo rahisi kueleweka. Kwa kielelezo, kuna masimulizi manne ya Gospeli juu ya maisha na huduma ya kidunia ya Yesu, kila moja likiwa na lengo tofauti. Wakati mihtasari mbalimbali inapotoa utangulizi wa zile Gospeli, inaeleza malengo hayo kwa njia hii: ‘Usimulizi wa mtume Mathayo juu ya maisha ya Yesu uliandikwa kwa kuwafikiria Wayahudi hasa. Gospeli hii inaonyesha kwamba Yesu ndiye Mfalme wa Kimesiya aliyetabiriwa.’ ‘Marko anatokeza wazi usimulizi mfupi, wenye kusonga mbele haraka kuhusu maisha ya Yesu, akimwonyesha kuwa Mwana wa Mungu mwenye kufanya miujiza.’ ‘Usimulizi wa Luka juu ya maisha ya Yesu uliandikwa ili kuthibitisha uhakika wa matukio yaliyozunguka maisha ya Kristo na kwa njia ambayo ingevutia watu wa mataifa yote.’ ‘Usimulizi wa mtume Yohana kuhusu maisha ya Yesu unakazia kichwa cha kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu, ambaye kupitia kwake uhai wa milele unawezekana.’ Baada ya maneno hayo ya utangulizi, mihtasari hiyo inatokeza mambo yaliyo katika vitabu hivyo yakiwa chini ya hesabu ndogo ya vichwa vikubwa-vikubwa. Hiyo inaweza kukusaidia ukumbuke mawazo makuu ambayo mwandikaji wa Biblia alisitawisha.

Marekebisho ya Kutakasa

Taarifa zimechanganuliwa kwa uangalifu katika kichapo hiki kwa kutegemea nuru ya maana ya maneno yaliyotumiwa katika lugha za awali za Biblia. Maelezo ya kirefu yametiwa ndani pia kuwezesha msomaji athamini jinsi maneno ya lugha ya awali yalivyo na maana pana ya Kibiblia. Kwa kuongezea, maana za majina ya Kibiblia zimefanyiwa marekebisho ya kuzitakasa kwa kutegemea nuru ya njia ambayo sehemu za msingi za majina hayo zimefasiriwa hasa katika New World Translation.

Jitihada ya bidii-endelevu imefanywa pia ili kufanya habari zilizo katika kichapo hiki zipatane na mambo ambayo yamechapishwa katika Mnara wa Mlinzi katika miaka ya majuzi. Kwa kielelezo, tumejifunza mengi juu ya moyo, kitabu cha uhai, kutangazwa kuwa waadilifu, na mambo mengine mengi. Habari hizo zimetiwa katika Insight on the Scriptures.

Maelezo ya kirefu ya historia ya kilimwengu yamechunguzwa dhidi ya vyanzo vile vya awali, ikiwa vilipatikana, badala ya kutegemea yale tu ambayo yamesemwa na waandikaji wengine juu ya mambo yaliyo katika vyanzo hivyo; mamia ya marejezo yametiwa ndani pia kuonyesha ni wapi habari hizo zinaweza kupatikana. Mambo ya kisayansi juu ya makala hizo yamelinganishwa na hali za kisasa. Mahali-mahali pa kujiografia pamechanganuliwa upya kabisa kwa kutegemea utafiti wa uchimbuzi wa vitu vya kale uliofanywa katika miaka ya majuzi.

Atlasi ya Ramani za Biblia

Insight on the Scriptures ni kutia ndani ramani kama 70, zikionyesha mamia ya mahali panapotajwa katika Biblia. Hivyo, kichapo hiki pia kina atlasi ya ramani za Biblia zenye kuelewesha mambo kikamili. Katika visa vingi, ramani moja inakaza fikira juu ya jambo moja tu la ufupi juu ya historia ya Kibiblia au ya kilimwengu. Kwa sababu hiyo, inavuta fikira kwenye mahali-mahali pa umaana wa pekee katika habari zinazohusika humo. Utapata ramani moja ikionyesha safari za Abrahamu, moja ikionyesha mahali ambapo Israeli walipitia wakitanga-tanga jangwani, nyingine ikihusu ushinde wa Bara la Ahadi, moja ikiwa ya maisha ya Daudi alipokuwa mtoro-mtoro na nyingine ya matukio yanayoshirikishwa na umaliki wake, mfululizo wa ramani zinazotoa muhtasari wa mahali-mahali ambapo Yesu alisafiri wakati wa huduma yake ya kidunia, na ramani kadhaa zikionyesha mambo kwa urefu kuhusu Yerusalemu wakati wa vipindi mbalimbali vya historia. Fahirisi ya ramani imeandaliwa kukusaidia ujue mahali zilipo ramani fulani za wazi zinazoandaa habari zenye msaada kuhusu mahali fulani-fulani.

Kuhusiana na nyingi za ramani hizo, pia kuna orodha ya majina ya mahali, pamoja na maandiko yanayoonyesha kwa nini mahali hapo ni pa maana katika habari hususa za kihistoria zinazozungumziwa. Katika kurasa zinazoelekeana na ramani hizo zimo picha za mahali-mahali palipoonyeshwa katika ramani. Mambo hayo yanaweza kukusaidia unufaike kikamili zaidi na masimulizi ya Biblia, unapoona uhusiano wa mahali pamoja na pengine, kusoma maelezo ya kirefu juu ya jambo lililotukia hapo, na kuona mahali hapo pana sura gani leo.

Mambo ya Pekee Katika Rangi Kamili

Katika kutayarisha kichapo hiki, majumba ya kuhifadhi vitu vya ukumbusho katika Amerika ya Kaskazini, Ulaya, na Mashariki ya Kati yalipekuliwa kweli kweli ili kupata vitu vyenye thamani kubwa kuhusiana na maandishi ya kumbukumbu la Biblia. Picha za vitu vilivyo na ustahiki mwingi zaidi zilichukuliwa. Kwa kuongezea, mikusanyo kadhaa ya picha za mahali-mahali panapotajwa katika Biblia ilichunguzwa upya, ili kuchagua ile ambayo ingesaidia zaidi. Matokeo ya jambo hilo yamefanyizwa kuwa nyongeza za kurasa 16 zenye rangi kamili za thamani yenye kutumika. Hayo ni mambo makuu ya kusisimua ambayo wewe utayaonea shangwe na uweze kuyatumia katika njia nyingi unapofundisha wengine.

Kwa kielelezo, kuna kisehemu chenye kichwa “Jinsi Sisi Tulivyoipata Biblia.” Kwa maelezo yenye kueleweka wazi, kinaonyesha hatua ambazo Biblia imezipitia ili itufikie sisi​—kuanzia maandishi ya awali kuteremka mpaka tafsiri za kisiku-hizi. Kinakazia picha za visehemu vya baadhi ya hatimkono za kale zaidi na ushuhuda unaoonekana kwa macho ambao unashuhudiza waandishi wa mapema walifanya uangalifu, hata kufikia hatua ya kuzihesabu herufi katika hati-mkono walizonakili.

Kisehemu kingine ni juu ya “Furiko la Siku ya Noa.” Kinazungumzia maswali kama vile, “Je! safina ingaliweza kuchukua wanyama wale wote?” na, “Maji ya furiko yalienda wapi?” Pia kinafanya uchanganuzi wa ngano za mapokeo zilizotoka kontinenti sita na visiwa vya bahari kuhusiana na Furiko hilo ili kuonyesha kwamba kumbukumbu zinazohusu Gharika ya siku ya Noa zinapatikana miongoni mwa watu wa tamaduni mbalimbali kote kote duniani.

Visehemu vingine vinashughulika na mambo ya kijiografia ya Bara la Ahadi, milki za kale ambazo utendaji wazo uliathiri Israeli, na safari moja ya kutumia picha ili kutalii mahali-mahali ambapo wenye kuzuru wanaweza kupaona leo ndani na kandokando ya Yerusalemu. Kwa ujumla, kuna vichwa vya mazungumzo 50 vya jinsi hiyo, vikiwa vimekuzwa kwa rangi kamili.

Habari zote hizi zimefanywa ziwe rahisi kupatikana kwa kutumia fahirisi zenye mambo mengi zilizo humu humu katika mabuku haya. Fahirisi hizi zinakuelekeza kwenye mazungumzo yaliyo bora zaidi ya maandiko yaliyotajwa bila maneno, na kwenye habari zilizoorodheshwa.

Kwa kutoa maoni ya ujumla juu ya kazi hiyo, maelezo haya ya utangulizi yanaonekana katika buku la kwanza: “Lengo la kichapo hiki ni kukusaidia wewe ujipatie muono-ndani juu ya Maandiko. Jambo hilo linafanywa jinsi gani? Kwa kukusanya pamoja kutoka sehemu zote za Biblia maelezo ya kirefu yanayohusiana na habari zinazozungumziwa. Kwa kuvuta fikira kwenye maneno ya lugha za awali na maana yayo halisi. Kwa kufikiria habari zinazohusiana kutokana na historia ya kilimwengu, utafiti wa uchimbuzi wa vitu vya kale, na nyanja nyingine za sayansi na kukadiria ubora wazo kwa kutegemea nuru ya Biblia. Kwa kuandaa misaada yenye kuonwa na macho. Kwa kukusaidia wewe utambue thamani ya kutenda kupatana na inayosema Biblia.” Kwa hiyo ndani ya kurasa za Insight on the Scriptures mna utajiri wa habari zenye thamani kweli kweli unazoweza kutumia kwa manufaa yako mwenyewe na ya wengine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki