Ripoti Sahihi ya Shahidi Aliyeona kwa Macho!
Andishi la Kiugariti (KTU 1.161) la hivi majuzi linathibitisha utegemeko wa 2 Wafalme 10:19, 20. Ili kuharibu waabudu wa Baali, Mfalme Yehu aliamuru hivi: “Takaseni kusanyiko la dini [kusanyiko la mambo mazito, NW] kwa Baali.” (Huyo alikuwa mungu bandia, ambaye yawezekana ndiye anayewakilishwa na sanamu ndogo iliyopo kushoto.) Kulingana na Vetus Testamentum, gazeti linalotangazwa kwa chapa katika Uholanzi, usemi huo ni “Mkanaani halisi” na unamaanisha “‘mzingo usiopasa kuingiwa na mtu wa nje’: mtu yeyote wa kutoka nje angeweza kuadhibiwa kwa laana.” “Sasa sisi tunafahamu kwamba mwandikaji wa kifungu hicho katika 2 Wafalme anaonekana kuwa alijua vizuri maneno ya kidini yaliyotumiwa na Wakanaani,” inaeleza Vetus Testamentum.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 25]
Jumba la Vitu vya Makumbuaho la Louvre, Paris