Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 9/15 kur. 10-15
  • Wazee Ilindeni Amana Yenu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wazee Ilindeni Amana Yenu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Nyinyi Mmekabidhiwa Amana?
  • Jinsi ya Kulinda Amana Yako
  • Epuka Mitego
  • “Toeni Uangalifu kwa Nyinyi Wenyewe”
  • Shangwe Inatokana na Kuilinda Amana Yako
  • “Wakumbukeni Wale Wanaoongoza Kati Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Uangalizi Wenye Upendo Hujenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Wanaume Wenye Hekima, Akili na Ujuzi wa Kuongoza Watu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Wachungaji, Waigeni Wale Wachungaji Wakuu Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 9/15 kur. 10-15

Wazee Ilindeni Amana Yenu

“Toeni uangalifu kwa nyinyi wenyewe na kundi lote la kondoo, ambalo miongoni mwalo roho takatifu imeweka nyinyi kuwa waangalizi, kuchunga kutano la Mungu, ambalo yeye alinunua kwa damu ya Mwanaye mwenyewe.”—MATENDO 20:28, NW.

1. Amana ya Kikristo inatia nini ndani?

YEHOVA MUNGU amewapa amana ya ajabu wale walio katika tengenezo lake la kidunia. Lakini amana ni nini? Ni kitu fulani chenye thamani ambacho hupewa mtu ambaye lazima atoe hesabu. Amana ya Kikristo inatia ndani “kigezo cha maneno yenye afya,” ukweli unaotolewa kupitia Maandiko na kugawanywa na “mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu” ukiwa ‘chakula kwa wakati unaofaa.’ (2 Timotheo 1:13, 14; Mathayo 24:45-47, NW) Amana hii inatia ndani huduma inayohusiana na ukweli, ambao ni lazima uhubiriwe ndani na nje ya kundi. (2 Timotheo 4:15) Wapiga mbiu ya Ufalme, kutia na wazee wapakwa-mafuta kwa roho, wanapaswa kustahi amana hii yenye thamani ya juu sana.

2. Wazee wana amana gani zaidi, na Petro alisema nini juu yayo?

2 Wazee Wakristo wana amana zaidi—daraka la kuchunga kundi la Mungu. Kwa habari hii, mtume Petro aliandika hivi: “Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye; lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi. Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka.”—1 Petro 5:14.

3. Ni lazima wazee Wakristo wawe vyanzo vya nini?

3 Wazee Wakristo ‘lazima wawe kama mahali pa kujificha kutokana na upepo na mahali pa ficho kutokana na tufani ya mvua, kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji, kama kivuli cha jabali zito katika nchi isiyo na kitu.’ (Isaya 32:1, 2, AW) Hii inamaanisha kwamba wazee wanapaswa kuwa vyanzo vya usalama, amani, na uthabiti kwa kundi la watumishi wa Mungu walio kama kondoo. ‘Mengi zaidi’ yanatakwa kwa wazee, au wachungaji-wa-chini wa kundi la kondoo, kwa sababu ‘wamewekewa amana vitu vingi.’ (Luka 12:48) Na kwa kweli wana amana yenye thamani ambayo lazima ilindwe.

Kwa Nini Nyinyi Mmekabidhiwa Amana?

4. Kwa nini wazee wengi sana wanahitajiwa?

4 Kuwapo kwa makundi zaidi ya 60,000 ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kunahitaji maelfu mengi ya wanaume wenye sifa za kiroho watunze kundi la kondoo za Mungu. Kuna wazee wengi katika kila nchi, na hii ni sababu ya shangwe. Ulimwenguni pote kuna wastani wa wapiga mbiu ya UfaIme 60 katika kila kundi. Kwa sababu hiyo, kuna kazi nyingi ya kufanywa na wazee. — 1 Wakorintho 15:58.

5. Pendeleo la kutumikia kuwa mzee hunyooshewa mwanamume kwa msingi gani?

5 Ikiwa wewe ni mzee, kwa nini ulinyooshewa pendeleo hili lenye baraka? Kwa sababu umefanya mambo fulani, nawe una sifa za kiroho. Kwa kielelezo, lazima uwe umejifunza Neno la Mungu kwa bidii ya uendelevu. (Yoshua 1:7, 8) Lazima uwe umeshiriki huduma ya shambani kwa juhudi, pia umewasaidia wengine wawe wapiga mbiu ya Ufalme. Ukiwa ‘umejaribiwa juu ya kufaa kwanza,’ ulitumika kwa uaminifu ukiwa mtumishi wa huduma. ‘Ulijitahidi kufikia,’ au ulitaka kustahili, kuwa mzee, ukithamini kwamba kuwa mwangalizi ni “kazi nzuri.” (1 Timotheo 3:1, 10, NW) Kama Timotheo, ‘ulishuhudiwa vema na ndugu.’ (Matendo 16:2) Ulipopendekezwa kuwa mzee, yaelekea ulikuwa katika umri wa miaka ya mwishomwisho ya 20 au umri mkubwa zaidi na ulikuwa umejionea mengi maishani. Kundi lilikuwa limepata kukustahi kuwa ndugu aliyekomaa kiroho, mwenye kufikika na mwenye uwezo wa kutoa shauri la Kimaandiko lenye matokeo na kudumisha usiri.—Mithali 25:9, 10.

Jinsi ya Kulinda Amana Yako

6, 7. Timotheo wa kwanza 4:13-15 inaandaa shauri gani ili kumsaidia mwanamume alinde amana yake akiwa mzee?

6 Ndiyo, ikiwa wewe ni mzee, ulikabidhiwa amana ya uangalizi wa Kikristo kwa sababu zinazofaa. Nawe umehisi ukiwa mwenye pendeleo kama nini! Lakini unaweza kuilindaje amana yako?

7 Njia moja ya kulinda amana yako ukiwa mzee ni kuwa mwenye mtazamo mzuri na mwenye bidii katika kutunza kazi zako. Sisi sote tuna migawo ya madaraka mbalimbali katika tengenezo la Yehova. Basi, kaa mahali pako, na uridhike ‘kuwa mdogo.’ (Luka 9:46-48; linganisha Waamuzi 7:21.) Tunza mapendeleo yako, na ‘usitende mambo kwa mkono mlegevu’ kamwe. (Mithali 10:4) Usisimame zizima, lakini kwa msaada wa Yehova, fanya maendeleo pande zote za huduma. Kweli kweli, fuata shauri hili ambalo Paulo alimpa Timotheo: “Ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha. Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee. Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote.”—1 Timotheo 4:13-15.

8. Ni nini kitamsaidia mzee atoe shauri timamu na kutoa kitu fulani chenye kutajirisha kiroho kwenye mikutano?

8 Hakikisha unadumisha ratiba nzuri, yenye matokeo ya funzo la kibinafsi. Ukiwa mzee, unatazamiwa kwa kufaa utoe shauri timamu la Kimaandiko. Ili ujiandae kwa daraka hili, je! wewe umesoma Biblia nzima na kuitafakari, labda mara nyingi? (Mithali 15:28) Namna gani migawo yako ya jukwaani? Itayarishe vizuri, ukiomba msaada wa Yehova katika sala ili uweze kutoa kitu fulani chenye kuwatajirisha kiroho wale walio kwenye mikutano yetu. Wazee hasa wanapaswa ‘waseme yaliyo mema na kujenga, ili yawape neema wanaosikia.’—Waefeso 4:29; Warumi 1:11.

9. Kulingana na 2 Timotheo 4:2, ni lazima mzee afanye nini?

9 Ukiwa mzee, tii shauri la Paulo: “Lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.” (2 Timotheo 4:2) Paulo alihangaishwa na uasi-imani kwa sababu watu fulani katika kundi ‘walishindana kuhusu maneno,’ wakajitia katika “maswali ya upumbavu,” na ‘walishindana na ukweli.’ (2 Timotheo 2:14-18, 23-25; 3:8-13; 4:3, 4) Kundi liwe lilikuwa katika majira yenye taabu au majira yanayofaa, Timotheo alipaswa ‘kulihubiri neno.’ Hili lingeimarisha waamini wenzi wapinge uasi-imani. Vivyo hivyo leo, ni lazima wazee wahubiri Neno, au ujumbe wa Mungu wenye kupenya ndani, unaofikia moyo na kutia moyo kushika viwango vya Yehova.—Waebrania 4:12.

10. Kwa nini mzee anapaswa afanye kazi kwa ukawaida katika huduma ya shambani pamoja na washiriki wa jamaa yake na wengine?

10 Ili aseme kwa mamlaka, ni lazima mzee aishi kupatana na Neno la Mungu. Lakini yeye halindi amana yake kikamili ikiwa ‘analihubiri neno’ kwenye jukwaa tu ndani ya kundi. Katika mistari ile ile inayozunguka, Paulo alimhimiza Timotheo hivi: “Fanya kazi ya mhubiri wa Injili.” Ili ‘utimilize huduma yako’ ukiwa mzee, ni lazima uhubiri Neno la Mungu “waziwazi, na nyumba kwa nyumba.” (2 Timotheo 4:5; Matendo 20:20, 21) Basi, fanya kazi katika huduma ya shambani pamoja na washiriki wa jamaa yako. Hii inaweza kuchangia kifungo cha kiroho kati yako na mke wako na kitanufaisha sana watoto wako. Tumia wakati fulani, pia, ukishiriki kazi ya kuhubiri pamoja na washiriki wengine wa kundi. Hii inaimarisha vifungo vya kiroho na kuongeza upendo wa kidugu. (Yohana 13:34, 35) Bila shaka, ni lazima mzee ajitahidi kuwa mwenye usawaziko katika kugawanya wakati wenye thamani kati ya jamaa yake na kundi. Kutumia utambuzi kutamwepusha asitumie wakati mwingi katika jambo moja, huku akiachilia na kuharibu jambo jingine.

11. Kwa nini mzee anapaswa afanye kazi kwa bidii ili aongeze uwezo wake wa kuwa mwalimu?

11 Ili kulinda amana yako ukiwa mzee, pia fanya kazi kwa bidii ili uongeze uwezo wako wa kuwa mwalimu. ‘Mwenye kufundisha, awemo katika kufundisha kwake,’ akasema Paulo, au ‘mwenye kuonya, katika kuonya kwake.’ (Warumi 12:7, 8) Kwa kuwa mwalimu anasimama mbele ya wengine akiwa mkufunzi, wao wana haki ya kutazamia mengi kutoka kwake. Mzee akikosea sana katika kufundisha kwake na jambo hili lisababishe matatizo kwa waamini wenzi, anaingia katika uelekeo wa kuhukumiwa na Mungu. Ndiyo, walimu ‘watapata hukumu kubwa zaidi.’ (Yakobo 3:1, 2; Mathayo 12:36, 37) Kwa hiyo wazee wanapaswa kuwa wanafunzi wazito wa Neno la Mungu na ni lazima walitumie katika maisha. Ndipo kufundisha kwao Kimaandiko, kukiwa kunategemezwa na matumizi ya kibinafsi, kutathaminiwa sana na waamini wenzi. Pia kutalinda kundi na mavutano yasiyoleta hali njema, kutia na uasi-imani.

Epuka Mitego

12. Ni shauri gani lililotangazwa kwa chapa wakati mmoja katika jarida hili ambalo litasaidia mzee aepuke kutumia vibaya ulimi?

12 Linda amana yako ukiwa mzee, kwa kuepuka mitego pia. Mmojapo ni kutumia vibaya ulimi ukiwa mwalimu. Uhitaji wa hadhari katika jambo hili umekaziwa kwa muda mrefu na tengenezo la Yehova. Kwa kielelezo, katika toleo la Mei 15, 1897, jarida hili lilizungumzia Yakobo 3:1-13 na kusema hivi kuhusu wazee hasa: “Wakiwa na ulimi wenye ufasaha unaweza kuwa mfereji wa kuleta baraka kubwa, ukigeuza hesabu kubwa za watu wamwelekee Bwana, ukweli na njia ya uadilifu; au, kwa upande mwingine, ukiwa umechafuliwa kwa kutiwa makosa, ulimi unaweza kuleta madhara yasiyoweza kuelezeka—kuumiza imani, maadili, kazi zilizo njema. Hakika ni kweli kwamba, yeyote anayejizoeza kipawa cha kufundisha anajifunua wazi kwenye daraka zaidi machoni pa Mungu na wanadamu. . . .Yeyote ambaye angekuwa chemchemi ambayo kutoka kwayo Neno la kimungu lingetoka, akileta baraka na burudisho na imara, yapasa ahakikishe kwamba maji machungu, mafundisho bandia ambayo yangeweza kusababisha laana, au umizo—kutomheshimu Mungu na kupotosha Neno lake—hayapasi kupata mfereji wa kutokea ili yatamkwe. Katika kuchagua viongozi wa mikutano sifa ya ‘ulimi’ kama ilivyoonyeshwa hapa haipasi kusahauliwa. Walio na ulimi moto hawapasi kuchaguliwa, bali ni wale tu walio wasikivu, wenye kiasi zaidi, ‘wanaotia lijamu’ katika ndimi zao na kujitahidi kwa uangalifu ‘kunena kama waneni wenye kuwakilisha Mungu.’” Ni jambo la maana kama nini mzee atumie ulimi wake kwa njia halali!

13. Wazee wanapaswa kujihadhari namna gani kuhusu tafrija?

13 Tafrija yenye kupita kiasi ni mtego wa kuepuka pia. Tafrija yapasa iburudishe na kujenga, si kuchosha na kumkengeusha Mkristo. Zaidi ya hilo, ni lazima waangalizi wawe ‘wenye kiasi katika mazoea.’ (1 Timotheo 3:2, NW) Ikiwa kiasi kinaongoza yale unayofanya kuhusiana na tafrija, hili litakulinda wewe na jamaa yako na litaandaa kielelezo kizuri kwa kundi. Huwezi kuwa unaweka kielelezo chema ikiwa unaenda nje mara nyingi ukafanye tafrija katika miisho-juma na huku waamini wenzako wakijihusisha katika huduma ya shambani kwa bidii-endelevu. Ni lazima habari njema zihubiriwe, na wazee wanapaswa watoe uongozi katika kazi hii wakiwa wapiga mbiu wenye bidii wa Ufalme.—Marko 13:10; Tito 2:14.

14. (a) Ni vielelezo gani vya Kimaandiko vinavyokazia uhitaji wa wazee kujilinda dhidi ya ukosefu wa adili katika ngono? (b) Wazee hawapaswi kupuuza shauri gani lililorudiwa-rudiwa kuhusu kusaidia dada za kiroho?

14 Ukosefu wa adili katika ngono ni mtego mwingine wa kuepuka. Hali ya adili yenye kuharibika ya ulimwengu inaweza hata kumvuta mzee ikiwa hakinzi vishawishi vinavyotumiwa na Shetani katika jitihada zake za kuvunja ukamilifu wa watu wa Mungu. (Linganisha Mathayo 4:1-11; 6:9, 13.) Kumbuka kwamba nabii Balaamu, kwa kutofanikiwa katika majaribio yake ya kulaani Israeli, alisababu kwamba Yehova mwenyewe angewalaani ikiwa wangeshawishwa wajiingize katika ibada ya ngono. Kwa hiyo Balaamu alimfundisha mfalme Mmoabu Balaki ‘aweke kikwazo mbele ya wana wa Israeli, kula vitu vilivyodhabihiwa kwa sanamu na kufanya uasherati.” Je! waliepuka mtego huo? La, kwa maana Waisraeli 24,000 walikufa katika pigo lililotoka kwa Yehova kwa sababu walifanya ngono zisizo za adili pamoja na wanawake Wamoabu na wakasujudu mbele ya miungu yao. (Ufunuo 2:14; Hesabu 25:1-9) Pia, kumbuka kwamba hata Daudi, ‘mtu aupendezaye moyo wa Mungu,’ alijikwaa akaingia katika mtego wa kukosa adili katika ngono. (1 Samweli 13:14; 2 Samweli 11:24) Basi, ukiwa mzee, tii shauri linalorudiwarudiwa na “wakili mwaminifu” la kutosaidia kamwe dada wa kiroho mkiwa peke yenu faraghani, bali mzee mwingine awepo unaposhughulikia daraka hili.—Luka 12:42.

15. Jamaa ya mzee inaweza kumsaidiaje aepuke mtego wa kufuatia vitu vya kimwili?

15 Ufuatiaji wa vitu vya kimwili ni mtego mwingine wa kuepukwa na wazee. Ridhika na vitu vinavyohitajiwa, ukijua kwamba Yehova atatoa uandalizi wa kutosha. (Mathayo 6:25-33; Waebrania 13:5) Zoeza jamaa yako wawe wawekevu, kwa kuwa kuharibu-haribu vitu ni mwizi wa wakati na mali ambazo zingeweza kutumiwa kusaidia jamaa, na pia kujihusisha katika huduma ya shambani, kuimarisha kundi, na kuendeleza masilahi ya Ufalme. Mzee ananufaika na ushirikiano wa jamaa yake katika jambo hili na anashukuru kwamba hawamkazi-kazi awape vitu ambavyo havihitajiwi kikweli. Kwa kweli, “kuwa na mali chache pamoja na kumcha BwANA [kumwogopa Yehova, NW]; ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.”—Mithali 15:16.

“Toeni Uangalifu kwa Nyinyi Wenyewe”

16. Ni shauri gani ambalo Paulo aliwapa waangalizi wa Efeso?

16 Ikiwa wazee watalinda amana yao, ni lazima watumie shauri la Paulo kwa waangalizi wa Efeso. Yeye aliwaambia hivi: “Toeni uangalifu kwa nyinyi wenyewe na kundi lote la kondoo, ambalo miongoni mwalo roho takatifu imeweka nyinyi kuwa waangalizi, kuchunga kutano la Mungu, ambalo yeye alinunua kwa damu ya Mwanaye mwenyewe. Mimi ninajua kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwamwitu wenye kuonea wataingia miongoni mwenu nyinyi nao hawatalitendea kundi kwa wororo, na kutoka miongoni mwenu nyinyi wenyewe watu watainuka na kusema mambo yaliyopotoka na kuvuta mbali wanafunzi baada yao wenyewe. Basi endeleeni kukesha, na kukumbuka kwamba kwa miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kuwaonya kwa bidii kila mmoja kwa machozi.” —Matendo 20:28-31, NW.

17, 18. Ni shauri gani lililotangazwa kwa chapa katika gazeti hili miaka 80 hivi iliyopita ambalo bado linatumika kwa wazee Wakristo?

17 Zaidi ya miaka 80 iliyopita, Mnara wa Mlinzi (Machi 1, 1909, kwa Kiingereza) ilinukuu shauri la Paulo linalotangulia kwa wazee wenzi na kueleza hivi: “Wazee walio kila mahali wanahitaji kutii kwa njia ya pekee; kwa sababu katika kila jaribu wale wanaopendelewa sana na walio mashuhuri sana wanashambuliwa na kutahiniwa vikali. Kwa sababu hiyo [Yakobo] anasihi hivi, ‘Wengi wenu msiwe walimu, akina ndugu, mkijua ya kwamba mtu atapokea mtihani mkali zaidi.’ Sisi, vilevile, tunawasihi Wazee wote ambao wana moyo wenye kutakata, usio na ubinafsi, kwamba wasiwe na jambo lolote isipokuwa upendo na kuwatakia mema aina yote ya binadamu, na kwamba wajazwe zaidi na zaidi na matunda na neema za Roho takatifu, wakilitii kundi pia. Kumbukeni kwamba, kundi ni la Bwana na kwamba nyinyi mna daraka kwa Bwana, na pia kwao. Kumbukeni kwamba, nyinyi mnapaswa kuangalia nafsi (masilahi) zao kama wale ambao lazima watoe hesabu kwa Mchungaji Mkubwa aliye Mkuu. Kumbukeni kwamba, jambo kuu ni Upendo, katika yote; na, huku mkiwa hamwachilii mafundisho, uangalieni kwa njia ya pekee ukuzi wa Roho wa Bwana miongoni mwa washiriki mbalimbali wa Mwili wake, ili kwamba waweze ‘kupata urithi wa watakatifu katika nuru,’ na, kulingana na penzi la Kimungu, wasiteseke kwa kujikwaa katika siku hii mbovu, bali, wakiwa wamekwisha kufanya yote, wasimame wakiwa kamili katika Kristo, Mwili wake, Washiriki wake, Watoa-Dhabihu-Waungani wake, Warithi-Waungani wake.”

18 Maneno hayo yalielekezwa kwa wazee wapakwa-mafuta na waamini wenzao kupatana na uelewevu na hali za tengenezo la Yehova siku hizo za mapema. Hata hivyo, shauri hilo latumika vizuri kama nini leo! Matumaini yao yawe ni ya kimbingu au kidunia, ni lazima wazee Wakristo watoe uangalifu kwao wenyewe, walinde amana yao, na kutunza kwa upendo masilahi ya kundi la kondoo za Mungu.

Shangwe Inatokana na Kuilinda Amana Yako

19, 20. Kwa nini inaweza kusemwa kwamba shangwe inatokea wakati wazee wanapoilinda amana yao?

19 Furaha—kwa kweli, shangwe yenye kuhisiwa moyoni—inatokana na kuilinda amana yako ukiwa mzee Mkristo. Kuna furaha katika kutimiza daraka zito kwa njia nzuri. j(wa hiyo uwe mwenye hadhari, mwenye kusali, mwenye bidii ya uendelevu. Ilinde amana yako ukiwa mzee na kutazamia wakati ambapo unaweza kusema, kama alivyosema yule mwanamume mwenye kidau cha wino cha mwandishi: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.”—Ezekieli 9:3, 4, 11.

20 Ndiyo, fanya kazi kwa ushikamanifu ukiwa mzee ili iweze kusemwa juu yako kama ilivyosemwa juu ya Noa: “Hivyo hasa ndivyo alivyofanya.” (Mwanzo 6:22, JW) Kundi linanufaika kwa njia nyingi na utumishi wenye juhudi kama huo. Zaidi ya yote, Yehova anaheshimiwa na makundi yenye imara na utendaji ambayo yanatumikiwa na wazee waaminifu wanaoilinda amana yao. Lakini mengi yanahitajiwa ikiwa, kwa kweli, utaambiwa: “Vema, mtumwa mwema.” (Luka 19:17) Ukiwa mzee, lazima pia ulitendee kundi la Mungu kwa wororo.

Wewe Ungesema Nini?

◻ Wazee Wakristo wana amana gani zaidi?

◻ Ni hatua gani nzuri ambazo mzee anaweza kuchukua ili ailinde amana yake?

◻ Ili ailinde amana yake, m lazima mzee aepuke mitego gani?

◻ Kwa nini shangwe inatokea wakati wazee wanapoilinda amana yao?

[Picha katika ukurasa wa 10]

Wazee Wakristo ni ‘lazima wawe kama mahali pa kujificha kutokana na upepo, na mahali pa kujisitiri kutokana na dhoruba’

[Picha katika ukurasa wa 12]

Ukiwa mzee, shiriki huduma ya shambani kwa ukawaida pamoja na washirika wa jamaa yako na wengine

[Picha katika ukurasa wa 13]

Ukiilinda amana yako ukiwa mzee, kundi litanufaika katika njia nyingi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki