Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 9/15 uku. 30
  • Muono-Ndani Juu ya Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Muono-Ndani Juu ya Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uvutano wa Kishetani
  • “Isiyoweza Kudhibitiwa”
  • Vijana wa Leo—Je, Ni Windo Rahisi kwa Ushetani?
    Amkeni!—1994
  • Ibada ya Shetani Katika Wakati Wetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kuna Hatari Gani Kujihusisha Kidogo Tu na Mambo ya Mizungu?
    Amkeni!—2002
  • Usumbufu Hatari Unaoongezeka
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 9/15 uku. 30

Muono-Ndani Juu ya Habari

Uvutano wa Kishetani

Baada ya kufanya uchunguzi kuhusu uvutano wa ibada ya Shetani katika muziki wa roki na roki yenye kutumia vyombo vyenye madini mazito, mchangiaji habari za safu ya karatasi-habari ya Toronto Tom Harpur aandika katika The Sunday Star: “Lazima mimi nitoe onyo kali sana iwezekanavyo kuhusu linalotukia. . . . Sijapata kamwe kuona kitu chochote chenye kupotoka hivyo. Nyimbo zimejawa na mambo yenye kupotosha akili, kupagawa, roho waovu, damu, laana, jeuri ya aina yote, kutia na kulala kinguvu, kujikata viungo, uuaji, na kujiua. Kifo na uharibifu, unabii wa maangamizi, kukataa yote yaliyo mema na kukubali yote yenye kuchukiza sana na yaliyo maovu—hivi ndivyo vichwa [vya nyimbo].”

Linalopatana na kuzidi kwa muziki wa kishetani ni ongezeko la utendaji wa madhehebu ya kishetani katika United States na Kanada. Ikiripoti juu ya semina ya polisi ya hivi majuzi katika Ontario, The Globe and Mail, karatasi-habari ya Kanada, inasema kwamba madhehebu ya kishetani “yanahusishwa katika kudhabihu wanyama, kunajisi makaburi na sherehe za kuwatenda watoto vibaya.” James Bradley wa Washington, D.C., ambaye ni mpelelezi, alihusianisha mamia ya visa vya kuwatenda watoto vibaya na uhalifu kisherehe wa ibada ya Shetani. Kama ilivyonukuliwa katika The Globe and Mail, Mpelelezi Bradley anaongezea kwamba zaidi ya miaka mitano iliyopita, ripoti zilizotolewa kuhusu sherehe za kuwatenda watoto vibaya zimetoka kwa “mamia ya watoto, mamia ya wafanya kazi wa jamii ya watu na walimu.”

Akielekeza kwenye “siku za mwisho” za mfumo huu mbovu wa mambo, mtume Yohana aliandika: “Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.” (2 Timotheo 3:1; Ufunuo 12:12) Uvutano wa Shetani, “mtawala wa mamlaka ya hewa,” unaenea hata katika muziki wa ulimwengu huu unaopendwa sana. (Waefeso 2:2, NW) Hiyo ndiyo sababu mtume Paulo aliwasihi Wakristo wenzake ‘waweze kusimama imara kushindana na hila za Ibilisi.’—Waefeso 6:11, NW.

“Isiyoweza Kudhibitiwa”

Wakati mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 28 aliyekuwa akikimbia polepole kuzoeza viungo vya mwili alipopigwa na kulalwa kinguvu katika Bustani ya Kati ya Jiji la New York, mamilioni ya watu waligutuka na kufadhaika. Sababu ilikuwa nini? Shambulio hilo lenye ukatili na la kinyama lilitendwa na genge la matineja ambao “majivuno yao machafu ya matokeo na kutojali kwao mteseko uliopasishwa ni yenye kutia hofu kweli kweli,” inaripoti New York Post. Baadhi ya vijana waliohusika katika uhalifu huo mbaya sana waliripotiwa kuwa wenye umri mchanga wa miaka 14. Akishangazwa na shambulio hilo, mwandikaji mmoja wa Post alikiri kwamba ulimwengu umekuwa “jamii isiyotiwa nidhamu, inayojitia sana katika anasa, iliyojawa na dawa za kulevya, yenye kutamani sana ngono, yenye jamaa zilizovunjika, yenye kupenda sana jeuri” yaani “isiyoweza kudhibitiwa na swali ni: kwa nini?”

Kwa kweli, kizazi hiki chenye jeuri isiyolinganika ndicho kile hasa kilichotabiriwa na mtume Paulo kwenye 2 Timotheo 3:1-5. Humo yeye alieleza kwamba “siku za mwisho” zingetiwa alama na watu ambao ni wenye “ubinafsi, wenye pupa, wenye kujigamba, na wenye kichwa kikubwa.” Zaidi ya hayo, “wao wangekuwa wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, na wasioshika dini; wao watakuwa wasio na fadhili, huruma, wachongezi, wajeuri, na wakali; wao watachukia yaliyo mema; wao watakuwa wenye hila, bila hadhari, na wenye kujaa majivuno; wao watapenda raha badala ya Mungu.” (Today’s English Version) Je! ulimwengu huu wenye jeuri utabaki ukiwa ‘usioweza kudhibitiwa’ kwa wakati usio dhahiri? Hapana! Yesu alisema: “Mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”—Luka 21:28.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki