Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 9/1 kur. 4-7
  • Ibada ya Shetani Katika Wakati Wetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ibada ya Shetani Katika Wakati Wetu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uchawi, Kuwasiliana na Roho Waovu, na Ulozi
  • Ushetani na Muziki
  • Si Mtindo Tu
  • Uvutano wa Ibilisi Katika Ulimwengu Wenye Kujaa Chuki
  • Vijana wa Leo—Je, Ni Windo Rahisi kwa Ushetani?
    Amkeni!—1994
  • Shetani Kavaa Kificha-Sura
    Amkeni!—1990
  • Inuko na Anguko la Ushetani
    Amkeni!—1994
  • Usumbufu Hatari Unaoongezeka
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 9/1 kur. 4-7

Ibada ya Shetani Katika Wakati Wetu

HAKUNA shaka kwamba Shetani anataka kuabudiwa. Alipokuwa akimjaribu Yesu, yeye alifanya toleo la kumpa thawabu kubwa sana kwa sharti moja tu: “Ikiwa wewe utaanguka chini na kutenda kitendo kimoja cha ibada kwa mimi.” (Mathayo 4:9, NW) Bila shaka, Yesu alikataa, lakini si kila mmoja ambaye amefuata kielelezo chake. Ibada ya Shetani imeenea kote kote katika ulimwengu wetu wa ki-siku-hizi.

Mathalani, katika Kanada The Calgary Herald ilichapisha mfululizo wa makala zikiwa chini ya kichwa “Wanafunzi wa Ibilisi.” Karatasi-habari hiyo ilinukuu ripoti moja ya mpelelezi wa polisi, ikisema hivi: “Kupitia mahoji mimi nimejifunza kwamba Ushetani hauachi nje kikundi cho chote kile katika jamii ya watu. Habari za upelelezi zilizokusanywa na Polisi wa Calgary na Polisi Wapanda-Farasi wa Kanada unafunua kwamba katika Calgary pekee kuna watu 5,000 wanaosemwa kuwa ni wazoeaji wa Ushetani.”

Ripoti nyinginezo za magazetini zinaonyesha kwamba kidhehebu cha Shetani, kikiwa cha namna tofauti-tofauti, kinatokeza-tokeza pande zote za United States na Ulaya. Hata polisi wanaonyesha upendezi katika Ushetani. Kwa nini? Kwa sababu katika visa vingi wao wanapata uhusiano fulani kati ya matendo ya uhalifu na vidhehebu vya kishetani. Hivi majuzi tu, mjasusi mmoja wa polisi alinukuliwa kuwa akisema: “Jambo ambalo sisi tunashughulika nalo ni dini na watu wanaoitikadi katika dini hiyo kama vile wengine wanavyoitikadi katika Ukristo, dini ya Kiyahudi au ya Kiislamu. Matendo ya uhalifu unayoona yakitendwa hayatendwi kwa ajili ya kufanya uhalifu tu, bali matendo hayo ya uhalifu yanafanywa kwa ajili ya dini.”

Kielelezo kimoja cha kutokeza kilikuwa yale mauaji yaliyofanywa na mbari ya Manson katika Kalifornia kule nyuma katika 1969. Kulingana na profesa wa historia Jeffrey Russell, “Manson alidai kuwa ndiye Kristo na ndiye Shetani pia. . . . Wakati Tex Watson mfuasi wa Manson alipokuja kuua Sharon Tate, alitangaza kwamba ‘Mimi ndiye ibilisi; mimi nipo hapa kufanya kazi ya ibilisi. ‘ “Lakini Ushetani haufanywi waziwazi hivyo sikuzote.

Uchawi, Kuwasiliana na Roho Waovu, na Ulozi

Kweli kweli, ibada ya Shetani haihusu kumwabudu Shetani moja kwa moja kwa jina lake tu. Mtume Paulo alionya hivi: “Vitu ambavyo mataifa wanadhabihu wanadhabihu kwa roho wabaya.” (1 Wakorintho 10:20, NW) Na ibada ya roho wabaya kwa kweli ni sawa na ibada ya Shetani, kwa kuwa Shetani anaitwa “mtawala wa roho wabaya.” (Marko 3:22, NW) Ni mazoea gani ya “mataifa” yanayoweza kutambulishwa kuwa ibada ya roho wabaya, au ibada ya Shetani? Maneno ya Mungu kwa Israeli yanatupa sisi vielelezo fulani: “Hapaswi kupatikana ndani yako wewe . . . ye yote ambaye hutumia uaguzi, mzoea mizungu au ye yote ambaye hutafuta ishara au mlozi, au mmoja ambaye hutafuta shauri kwa chombo cha kuwasiliana na ulimwengu wa roho au mtabiri kikazi wa matukio au ye yote ambaye huulizia habari za wafu. Kwa maana kila mtu anayefanya mambo haya ni kitu fulani chenye kukirihika kwa Yehova.”​—Kumbukumbu 18:10-12, NW.

Hivyo, sisi tunaonywa dhidi ya ile dhabihu ya damu na ushirika-roho unaozoewa na makuhani wa dini ya uchawi-vuuduu katika Brazili au na makuhani wahounga na wamambo wa Haiti. Na sisi tunaonywa dhidi ya mazoea yale yale ya Santeria, yanayoadhimishwa na Wakyuba fulani wa uhamisho walio katika United States. Tunaonywa, pia, dhidi wa walozi wanaodai kuwa wanawasiliana pamoja na nafsi zilizokufa ili kuvuvia hofu katika walio hai.​—Linganisha 1 Samweli 28:3-20.

Uchawi umeenea sana katika sehemu tofauti-tofauti za Afrika. Mathalani, katika Afrika Kusini, waganga wa kiuchawi wana umashuhuri mwingi, na watu wanawachukua kwa uzito sana. Visa vya hivi majuzi vilivyoripotiwa katika magazeti vilihusu vikundi vya watu wenye ghasia vilivyowachoma kwa moto wakiwa hai watu ambao walishtakiwa kusababisha umeme wa mvua upige wanakijiji wenzao! Waganga wa kiuchawi wa mahali hapo walishtaki watu wasio na hatia juu ya vitendo hivyo “visivyo vya kiasili” na ndipo wakawafunga kwenye mti ili wachomwe kwa moto. Itikadi kama hiyo katika ulozi au mizungu ni ibada ya roho wabaya vilevile.

Hata hivyo, uchawi haumo Afrika tu. Katika 1985, Herbert D. Dettmer, akitumikia kifungo cha gereza kwenye kitovu kimoja cha kurekebishia tabia katika Virginia, U.S.A., alipewa haki na Mahakama ya Wilaya ya Mashariki ya Virginia awe na ruhusa ya kuchukua nguo na vitu fulani-fulani ili yeye aweze kuzoea dini yake gerezani. Na dini yake ilikuwa nini? Kulingana na maandishi ya kumbukumbu ya mahakama, yeye alikuwa mshiriki wa “Kanisa la Wicca (ambao kwa kawaida huitwa uchawi).” Basi, Dettmer aliipata haki ya kisheria kutumia katika ibada yake kiberiti, chumvi ya baharini, au chumvi isiyotiwa ayodini; mishumaa; uvumba; saa yenye kengele; na kanzu nyeupe.

Ndiyo, kulingana na vile dalili zinavyoonyesha, uchawi umeenea kote kote katika Magharibi. Karatasi-habari ya Uingereza Manchester Guardian Weekly iliripoti hivi: “Miaka mitano iliyopita, ilifikiriwa kuna wachawi-kike wapatao 60,000 katika Uingereza: leo [1985] hesabu hiyo inakadiriwa na wachawi-kike fulani kuwa imeongezeka kufikia 80,000. Prediction, lile gazeti la kila mwezi la unajimu na mafumbo ulimwengu wa roho, lina mwenezo wa [nakala] 32,000.”

Ushetani na Muziki

Profesa Russell, katika kitabu chake Mephistopheles​—The Devil in the Modern World, anavuta fikira zetu kwenye njia nyingine ambayo katika hiyo makusudi ya Shetani yanaendelezwa mbele. Yeye anaandika hivi: “Ushetani wenye kufanywa waziwazi ulififia kwa haraka sana baada ya ile miaka ya 70, lakini vishemu vya Ushetani wa kitamaduni viliendelea vikaingia katika miaka ya 1980 katika muziki wa roki wenye mdundo mkubwa-mkubwa, ambao pindi kwa pindi huitia Ibilisi na kustahi sana viwango vya Kishetani vya ukatili, dawa za kulevya, kuwa na sura mbaya, kushuka moyo, kujiingiza mno katika anasa, jeuri, kelele na mvurugo, na kutokuwa na shangwe.”​—Italiki ni zetu.

Labda wanamuziki walioingiza mawazo ya Ushetani katika muziki wao hawakuwa wakichukua jambo hilo kwa uzito. Huenda ikawa walikuwa wakijaribu tu kugutusha watu au kuonekana kuwa wa kiajabu-ajabu. Hata hivyo, watu mmoja mmoja wenye kuvutwa hisia kwa urahisi waliathiriwa sana. Profesa Russell anaandika kwamba zile “propaganda za wakati wote zinazohusu uovu ambazo zinafanywa bila kuchukua mambo kwa uzito sana zimekuwa na matokeo ya kuharibu akili zenye ujinga na unyonge. Tokeo moja limekuwa mvuvumko wa uhalifu mbaya zaidi wenye kugutusha, kutia na kunajisi watoto na kukata-kata viungo vya wanyama.”

Kisa kimoja cha hivi majuzi kiligutusha wakaaji wa New York. Kulingana na ripoti moja ya karatasi-habari, mvulana wa miaka 14, “mwenye kushikwa sana na Ushetani,” alimdunga kisu mama yake na kumwua halafu akajiua mwenyewe. Kama ilivyoripotiwa katika gazeti Maclean’s, mshauri mmoja wa jamaa Kanada alitaarifu kwamba hesabu inayoongezeka ya vijana-matineja wenye kufadhaika waliungama kuwa wanazoea “ushetani, mara nyingi hiyo ikiwa ni pamoja na kutumia dawa za kulevya na zile namna za kukandamiza zaidi za muziki wenye mdundo mkubwa-mkubwa wa roki.”

Si Mtindo Tu

Mtindo mmoja ambao unakumba sehemu zote za United States sasa hivi unaitwa kutafuta kipitio (channeling). Mara nyingi watu wanalipa mamia kadhaa ya dola ili washiriki katika vipindi ambamo “kipitio” fulani, yaani mwanamke aliye chombo kipitiwa (kwa kawaida vipitio ni wanawake), anadai kuwa anajitia katika uwasiliano pamoja na roho ya mtu aliyekufa zamani. Magazeti yaliripoti kwamba, katika kisa cha kipitio kimoja, vipindi “hupelekwa pindi kwa pindi kwa maelfu ya watu kwa safari moja katika majiji sita kwa kutumia kamba zilizounganishwa kwa matumizi ya setilaiti ya televisheni.” Elekeo hili ni udhihirisho wa kutotii shauri la Biblia la kuepuka vyombo vinavyopitiwa kwa kuwasiliana na ulimwengu wa roho na watabiri kikazi wa matukio. Hivyo, ibada hiyo ni ya namna ambayo inaweza kutambulishwa na ibada ya roho wabaya. Na kama vile uwasilianaji wote pamoja na ulimwengu wa roho, hiyo inategemea ule msingi wa uwongo wa kishetani kwamba nafsi ya kibinadamu haifi.​—Mhubiri 9:5; Ezekieli 18:4, 20.

Uvutano wa Ibilisi Katika Ulimwengu Wenye Kujaa Chuki

Hali ya kuogopesha ya aina ya binadamu katika karne hii ya 20 inatufanya tujiulize kama uvutano wa Shetani haufiki hata zaidi ya hapo. Profesa Russell anagusia jambo hili wakati anapotaarifu hivi: “Kwa sasa, mabohari ya silaha za nyukilia yakiwa yanakadiriwa kuwa mara sabini ya wingi unaohitajiwa ili kuua kila kiumbe hai aliye na uti wa mgongo duniani, sisi tunafanya kwa shingo ngumu matayarisho ya vita ambayo haitafaidi mtu yeyote, taifa lolote, au wazo lolote bali itashutumu maelfu ya mamilioni ya watu kwenye kifo kibaya sana. Ni kani gani inayotuhimiza tuteremke kwenye kijia kinachozidi kuwa hatari kila siku? Uharibifu wa sayari hii kwa utumizi wa nyukilia utakuwa kwa faida ya nani? Ni kwa faida tu ya kani ile ambayo tangu hapo mwanzo imenuia uharibifu wa kosmosi [ulimwengu] ikiwa na ukatili na uhabithi usio na kikomo.”

Ni nani au ni nini kani hiyo? Profesa huyo anatoa jibu lake mwenyewe kwa maneno haya: “Ibilisi amefafanuliwa kuwa yule roho anayetafuta kukanusha na kuharibu kosmosi ya Mungu kwa nguvu zake zote. Je! haiwezi kuwa kwamba ile kani inayotuhimiza tueneze silaha za nyukilia ndiyo kani ile ile ambayo sikuzote imejitahidi kukanusha kwamba siyo yenyewe inayofanya hivyo? Katika hatari hii iliyo kubwa kupita zote ya sayari yetu, hatuwezi kupuuza uwezekano huo.” Kwa uhakika Wakristo hawapuuzi uwezekano huo! Yesu mwenyewe alionyesha uvutano mkuu ambao Shetani anao juu ya ulimwengu huu wakati Yeye alipomwita “mtawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31, NW) Kikisimulia mwelekeo wa akili ya Shetani leo, kitabu cha Ufunuo kinasema kwamba yeye ana “kasirani kubwa, akijua yeye ana kipindi cha wakati kifupi.” (Ufunuo 12:12, NW) Kikirejeza kwenye jambo ambalo Shetani anajaribu kutimiza katika wakati wetu, kitabu icho hicho kinasema kwamba yeye anatumia propaganda za roho wabaya kukusanya watawala wa ulimwengu huu pamoja “kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.” (Ufunuo 16:14) Hapana, sisi hatuwezi kukataa kwamba Shetani Ibilisi hana uvutano wakati tunapojaribu kuelewa sababu ya aina ya binadamu kufuata mwendo ule wa kujiharibu yenyewe kwa kichaa.

Mtume Paulo aliita Shetani “mtawala wa mamlaka ya hewa, roho ile inayotenda kazi sasa katika wana wa kutokutii,” na “mungu wa huu mfumo wa mambo.” (Waefeso 2:2; 2 Wakorintho 4:4, NW) Basi si ajabu sana kwamba watu wengi wanauliza kama yale matendo ya kinyama ya kizazi hiki cha kisayansi ‘chenye nuru ya kielimu’​—vita vya ulimwengu viwili, mauaji-jumla ya watu wenye asili moja ya kitaifa katika Ulaya na Kampuchea, njaa yenye kusababishwa na siasa katika Afrika, migawanyiko ya kidini na kirangi yenye kina kirefu ulimwenguni pote, chuki, uuaji, kuumiza vikali miili ya watu kwa kufuata mbinu za utesaji-tesaji, uhalifu wa kupindua fikira za aina ya binadamu kwa kutumia dawa za kulevya, kutaja machache tu​—hayangeweza kuwa yanafuata mbinu kubwa zaidi ya kani fulani mbovu yenye nguvu nyingi, ambayo imeazimia kusukuma aina ya binadamu iende mbali na Mungu na labda hata ijiue duniani pote.

Basi, Shetani ni nani? Lengo lake kwa kweli ni nini? Sisi tunaweza kufanya nini tukiwa watu mmoja mmoja? Sisi tunakualika wewe ufikirie zungumzo la maswali haya katika makala mbili zinazofuata.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Wakiepuka muziki wa kishetani, watu wa Mungu wanatafuta vitumbuizo vinavyofaa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki