Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 1/1 kur. 8-9
  • Kafichuliwa na Vielezi vya Shamba la Mizabibu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kafichuliwa na Vielezi vya Shamba la Mizabibu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Kufichuliwa na Vielezi vya Shamba la Mizabibu
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Mifano Miwili Kuhusu Mashamba ya Mizabibu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Mzabibu Unaotoa Divai Inayofurahisha Mungu na Mwanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 1/1 kur. 8-9

Maisha na Huduma ya Yesu

Kafichuliwa na Vielezi vya Shamba la Mizabibu

YESU yuko hekaluni. Sasa tu ndiyo ametoka kuvuruga viongozi wa kidini waliodai kujua yeye anafanya mambo kwa mamlaka ya nani. Kabla wao hawajatulia kutoka kwenye vurugu yao, Yesu auliza hivi: “Nyinyi mwafikiri nini?” Halafu kwa njia ya kielezi awaonyesha wao ni watu wa aina gani hasa.

“Mtu mmoja alikuwa na watoto wawili,” Yesu asimulia. “Akiendea yule wa kwanza, akasema, ‘Mtoto, enda ukafanye kazi leo katika shamba la mizabibu.’ Kwa kujibu huyu akasema, ‘Nitaenda, bwana,’ lakini hakwenda. Akikaribia yule wa pili, akasema ivyo hivyo. Kwa kujibu huyu akasema, ‘Mimi sitaenda.’ Baadaye akahisi majuto na kwenda. Ni yupi wa wale wawili aliyefanya penzi la baba yake?” Yesu auliza.

“Ni yule wa mwisho,” wapinzani wake wajibu.

Kwa hiyo Yesu aeleza hivi: “Kwa kweli mimi nasema kwa nyinyi kwamba wakusanya-kodi na makahaba wanaenda mbele ya nyinyi kuingia katika ufalme wa Mungu.” Kwa kweli, wakusanya-kodi na makahaba walikataa kutumikia Mungu hapo kwanza. Lakini ndipo, kama yule mtoto wa pili, wakatubu na kumtumikia. Kwa upande mwingine, viongozi wa kidini, kama yule mtoto wa kwanza, walijidai kuwa watumikia Mungu, hata hivyo, kama vile Yesu aarifuvyo: “Yohana [Mbatizaji] alijia nyinyi katika njia ya uadilifu, lakini nyinyi hamkumwamini. Hata hivyo, wakusanya-kodi na makahaba walimwamini, na nyinyi, ingawa mliona jambo hili, hamkuhisi majuto baadaye ili mmwamini.”

Ndipo Yesu aonyesha kwamba jambo ambalo limewashinda viongozi hawa wa kidini si kutojali tu kutumikia Mungu. Sivyo, bali kwa kweli wao ni watu waovu. “Kulikuwa na mtu mmoja, mwenye nyumba,” Yesu asimulia, “aliyepanda shamba la mizabibu na kuweka ugo kulizunguka na akachimba shinikizo-divai humo na kusimamisha mnara, na kulikodisha kwa walimaji, na kusafiri ng’ambo. Majira ya matunda yalipofika, yeye alipeleka watumwa wake kwa walimaji ili watwae matunda yake. Hata hivyo, walimaji walichukua watumwa wake, na mmoja wakampiga sana, mwingine wakaua, mwingine wakapiga kwa mawe. Tena yeye akapeleka watumwa wengine, wengi kuliko wale wa kwanza, lakini wakawafanya hawa ivyo hivyo.”

“Watumwa” hao ni manabii ambao “mwenye nyumba,” Yehova Mungu, aliwatuma kwa “walimaji” wa ‘shamba lake la mizabibu.’ Walimaji hawa ni wawakilishi wenye kuongoza wa taifa la Israeli, taifa ambalo Biblia yalitambulisha kuwa ‘shamba la Mungu la mizabibu.’

Kwa kuwa “walimaji” wawatenda vibaya na kuwaua “watumwa,” Yesu aeleza hivi: “Mwisho [mwenye shamba la mizabibu] aliwapelekea mwana wake, akisema, ‘Wao watastahi mwana wangu.’ Kwa kumwona mwana walimaji wakasema miongoni mwao wenyewe, ‘Huyu ndiye mrithi; njoni, acheni tumuue tupate urithi wake!’ Kwa hiyo wao wakamtwaa na kumtupa nje ya shamba la mizabibu na kumuua.”

Sasa, akiambia viongozi hao wa kidini, Yesu auliza hivi: “Wakati mwenye shamba la mizabibu ajapo, yeye atawafanya nini walimaji hao?”

“Kwa sababu ni waovu,” wao wajibu, “yeye ataleta uharibifu mwovu juu yao na atakodisha shamba la mizabibu kwa walimaji wengine, ambao watamtolea yeye matunda uwapo ni wakati wayo.”

Kwa njia hiyo viongozi hao wa kidini wapiga mbiu ya kujihukumu wenyewe, kwa maana wao pia ni miongoni mwa “walimaji” Waisraeli wa ‘shamba la Yehova la mizabibu’ ambalo ni taifa la Israeli. Tunda ambalo Yehova atarajia kutoka kwa walimaji hao ni imani katika Mwana wake, yule Mesiya wa kweli. Kwa sababu ya wao kushindwa kuandaa tunda hilo, Yesu aonya hivi: “Je! nyinyi hamjasoma kamwe katika Maandiko [kwenye Zaburi 118:22, 23], ‘Jiwe ambalo wajenzi walikataa ndilo lile ambalo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Jambo hili limetoka kwa Yehova, nalo ni zuri sana machoni petu’? Hii ndiyo sababu mimi nasema kwa nyinyi, Ufalme wa Mungu utachukuliwa kutoka kwa nyinyi na kupewa taifa linalotokeza matunda yalo. Pia, mtu anayeanguka juu ya jiwe hili atavunjika-vunjika kabisa. Kwa habari ya yeyote ambaye hilo laanguka juu yake, litamsaga-saga kabisa.”

Sasa waandishi na wakuu wa makuhani watambua kwamba Yesu ananena kuwahusu, nao wataka kumuua, yule “mrithi” halali. Kwa hiyo pendeleo la kuwa watawala katika Ufalme wa Mungu litachukuliwa kutoka kwao wakiwa taifa, na taifa jipya la ‘walimaji wa shamba la mizabibu’ litafanyizwa, moja ambalo litatokeza matunda yafaayo.

Kwa sababu viongozi wa kidini wahofu umati wa watu, ambao wamwona Yesu kuwa nabii, hawajaribu kumuua katika pindi hii. Mathayo 21:28-46; Marko 12:1-12; Luka 20:9-19; Isaya 5:1-7, NW.

◆ Wale watoto wawili katika kielezi cha Yesu cha kwanza wawakilisha nani?

◆ Ni nani wenye kuwakilishwa na “mwenye nyumba,” “shamba la mizabibu,” “walimaji,” “watumwa,” na “mrithi” katika kielezi cha pili?

◆ Itakuwaje kwa ‘walimaji wa shamba la mizabibu,’ na ni nani atachukua mahali pao?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki