‘Hatuoni Aibu Kuhusu Habari Njema’
“Mimi sioni aibu kuhusu habari njema; kwa uhakika, hizo ni nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu kwa kila mmoja aliye na imani.”—WARUMI 1:16, NW.
1. Kwa kawaida habari njema hupokewaje, lakini walimwengu wasio na imani wangezionaje habari njema za Ufalme wa Mungu?
ZILE zionekanazo kwa mtu mmoja kuwa habari njema huenda zisionwe na mwingine kuwa habari njema. Kwa kawaida, mpelekaji wa habari njema hupokewa kwa ukaribishaji wa moyo mchangamfu, na mtu mwenye hamu ya kusikia habari hizo angemgeuzia sikio lake. Hata hivyo, Biblia ilitabiri kwamba walimwengu wasio na imani hawangekuwa na maoni ya kuzifurahia sana habari njema za Ufalme wa Mungu na ujumbe wazo.—Linganisha 2 Wakorintho 2:15, 16.
2. Mtume Paulo alisema nini kuhusu habari njema alizojulisha wazi, na kwa nini ujumbe aliojulisha wazi ungali habari njema leo?
2 Mtume Paulo ni mmoja aliyetumwa kupelekea halaiki ya watu habari njema. Yeye alihisije juu ya utume wake? Alisema hivi: “Kuna hamu nyingi kwa upande wangu kuwajulisha habari njema nyinyi pia huko katika Roma. Kwa maana mimi sioni aibu kuhusu habari njema.” (Warumi 1:15, 16, NW) Ili habari ziwe zingali njema leo, karibu miaka 2,000 baada ya mtume Paulo kuandikia Wakristo huko nyuma katika Roma, zingepasa kuwa habari njema zenye kudumu kwa muda mrefu kweli kweli. Kwa uhakika, hizo ni “habari njema za milele.”—Ufunuo 14:6, NW.
3, 4. Kwa nini mtume Paulo alisema kwamba hakuona aibu kuhusu habari njema?
3 Kwa nini mtume Paulo alisema kwamba yeye hakuona aibu kuhusu habari njema? Kwa nini angaliweza kuzionea aibu? Kwa sababu huo haukuwa ujumbe wenye kupendwa na wengi, kwa maana ulihusu mwanamume aliyekuwa ametundikwa juu ya mti wa mateso kwa namna ya mhalifu mwenye kudharauliwa, jambo hilo likimpa sifa mbaya sana kwa wenye maoni ya kutazama sura ya nje-nje. Kwa miaka mitatu na nusu, mwanamume huyu alikuwa ameitembea miinuko na miteremko ya eneo la Palestina akiwa na habari njema na akawa amekutana na upinzani mkali kutoka kwa Wayahudi, hasa viongozi wa kidini. Na sasa Paulo alikuwa akikabili uhasama wa jinsi iyo hiyo, kwa kupeleka jina la mwanamume huyo mwenye kudharauliwa sana.—Mathayo 9:35; Yohana 11:46-48, 53; Matendo 9:15, 20, 23.
4 Kwa sababu ya upinzani huo, huenda ikawa Paulo na wanafunzi wenzake wa Yesu Kristo walionwa kuwa wenye kuwa na kitu cha kuonewa aibu. Kweli kweli, sasa Paulo alifuata sana kitu ambacho hapo kwanza yeye mwenyewe alikiona kuwa cha aibu. Alikuwa ameshiriki kibinafsi kurundika suto juu ya wafuasi wa Yesu Kristo. (Matendo 26:9-11) Lakini alikuwa ameacha kufuata mwendo huo. Tokeo ni kwamba yeye, pamoja na wengine waliokuja kuwa Wakristo, walipatwa na mnyanyaso wenye jeuri.—Matendo 11:26.
5. Paulo alielezaje juu ya taarifa yake kuhusu kutokuona aibu kuhusu habari njema?
5 Kama mtu angejiruhusu ahisi aibu juu ya kuwa mfuasi wa Yesu Kristo, angekuwa akifuata maoni ya kibinadamu kuhusu mambo. Mtume Paulo hakuwa hivyo. Bali, akieleza kwamba yeye hakuona aibu kuhusu habari njema alizohubiri, alisema hivi: “Kwa uhakika, hizo ni nguvu ya Mungu kwa ajili ya Nguvu ya Mungu si kisababishi cha kuonea aibu ikiwa yatenda kazi kupitia mwanafunzi wa Yesu ili kutimiza kusudi lenye kustahiki sifa la yule Mungu mtukufu ambaye Yesu Kristo mwenyewe alikuwa mwabudu na msifaji wake.—Linganisha 1 Wakorintho 1:18; 9:22, 23.
Habari Njema Zapigiwa Mbiu Ulimwenguni Pote
6, 7. (a) Ni daraka gani kuhusu habari njema ambalo Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kuishi kulingana nalo, na kwa tokeo gani? (b) Ingawa hatutaki kamwe kuacha hofu ituzuie kutoa ushahidi, ni jambo gani huenda likahitajiwa kabisa nyakati fulani? (Ona kielezichini.)
6 Kama Paulo, Mashahidi wa Yehova leo ni wanafunzi wa Mwana Wake aliyetukuzwa, Yesu Kristo. Yehova amewaaminisha Mashahidi hawa wake hazina hii ya “zile habari njema tukufu.” (1 Timotheo 1:11) Mashahidi wa Yehova hawakushindwa kuishi kulingana na daraka zito hili, nao wahimizwa wasilionee aibu. (2 Timotheo 1:8) Ni muhimu kutoacha kamwe hofu wala woga utuzuie kutoa ushahidi na kujitambulisha wenyewe kuwa Mashahidi wa Yehova.a
7 Kutoa ushahidi jinsi hiyo kwa ujasiri na bila hofu kumekuwa na tokeo la kufanya jina la Mungu Aliye Juu Zaidi lipigiwe mbiu sehemu zote za dunia na kukafanya habari njema za Ufalme wake zihubiriwe ulimwenguni pote. Mwana wa Mungu alisema: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa kwa ajili ya ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja,” na utabiri wake haungeweza kamwe kuruhusiwa ushindwe kutimia. (Mathayo 24:14, NW) Sasa habari njema zinahubiriwa katika mabara zaidi ya 210, na mwisho wa kazi hii ya kuhubiri haujafikiwa bado. Bila kuona aibu kuhusu habari njema na tukiwa tunakabiliana na wakati ujao kwa moyo mkuu, sisi twasali kama wanafunzi wa mapema wa Yesu Kristo: “Basi sasa, Bwana [Yehova, NW], . . . ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote.”—Matendo 4:29.
8. Kwa nini haiwapasi Mashahidi wa Yehova kuvunjwa moyo na upinzani katika mataifa yote ya dunia?
8 Ingawa ni kweli kwamba Mashahidi wa Yehova wachukiwa na kupingwa katika mataifa yote ya dunia, jambo hilo ni utimizo wa yaliyotabiriwa kuwa alama yenye kutambulisha waabudu halisi wa yule Mungu mmoja wa kweli aliye hai. (Yohana 15:20, 21; 2 Timotheo 3:12) Kwa hiyo badala ya kulegea na kuvunjika moyo kwa sababu ya hilo, wapiga mbiu ya habari njema wahakikishiwa kwamba wana kibali cha kimungu na wao ni wa lile tengenezo lenye kukubaliwa la Mwenye Enzi Kuu wa Ulimwengu Wote Mzima, Yehova.
9. Kwa nini si kitu kwamba ulimwengu mzima uko dhidi yetu?
9 Usisahau kamwe hivi: Sisi tuna tegemezo la Mungu Aliye Juu Zaidi wa ulimwengu wote mzima. Kwa hiyo, kuna nini hata ikiwa ulimwengu pamoja na madhehebu zao zote za kidini na vyama vya kisiasa uko dhidi yetu? Mwana mzaliwa pekee wa Mungu alikabiliwa na ulimwengu mzima ukiwa dhidi yake, nasi hatuoni aibu kupatikana tukiwa katika hali iyo hiyo. Kama vile yeye alivyoambia mitume wake: “Ulimwengu ukiwachukia nyinyi, mjue kwamba umenichukia mimi kabla ya kuwachukia nyinyi. Kama mngalikuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungalikipenda kilicho chao wenyewe. Sasa kwa sababu nyinyi si sehemu ya ulimwengu, bali mimi nimewachagua kutoka katika ulimwengu, kwa sababu hii ulimwengu unawachukia nyinyi.”—Yohana 15:18, 19, NW.
10. Kadiri kubwa ya mnyanyaso wa Mashahidi umetoka kwenye chanzo gani, na kwa nini wao hawaoni aibu juu ya hilo?
10 Hivyo Mashahidi wa Yehova wamevumilia mnyanyaso sehemu zote za kuzunguka ulimwengu lakini hasa sana katika mataifa yale yenye kufanyiza ile iitwayo Jumuiya ya Wakristo eti. Mnyanyaso huo wenye kufanywa na Jumuiya ya Wakristo hauwathibitishi Mashahidi kuwa si Wakristo. Bali, wathibitisha dai lao la kwamba wao ni Wakristo wa kweli, Mashahidi wa Mungu na Baba ya Yesu Kristo, yaani, Yehova. Kwa sababu wao ni Mashahidi wa Mungu, wao hawaoni aibu wapatwapo na mnyanyaso kwa sababu hizo za kidini. Kwa hiyo, shauri la mtume Paulo kwa Wakristo wa karne ya kwanza kutoona aibu latumika kwa kuwafaa sana Mashahidi wa Yehova sasa.—Ona Wafilipi 1:27-29.
Habari Bora Zaidi Ambazo Zingeweza Kupigiwa Mbiu
11. Kwa kuchukua jina Mashahidi wa Yehova, kwa nini sisi hatuachi kuwa wafuasi wa Yesu Kristo?
11 Mashahidi wa Yehova wamelikubali jina lao kwa moyo mkuu katika kutimiza ahadi ambayo Yehova aliwapa watu wake wa agano kwenye Isaya 43:10. Hata hivyo, hii haimaanishi kwamba wao hawamfuati tena Yesu Kristo. Yesu ndiye Kiongozi wao, ambaye wao hufuata kigezo chake. Yeye mwenyewe ni mmoja wa mashahidi wa Yehova. Kwa uhakika, yeye ndiye mwenye kuongoza katika kuwa Shahidi wa Yehova.—1 Timotheo 6:13; Ufunuo 1:5.
12. Ni habari za aina gani ambazo Mashahidi wa Yehova huhubiri ulimwenguni pote, na kwa nini?
12 Ujumbe ambao wahubiriwa na hawa Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote ndizo habari bora zaidi ambazo zingeweza kupigiwa mbiu. Hakuna serikali ambayo ingeweza kuwa bora kwa ajili ya aina ya binadamu kuliko Ufalme wa Kimesiya ambao Yehova amesimamisha ili utawale juu ya ulimwengu wa aina ya kibinadamu, ambao kwa ajili yao alimtuma Mwana wake mzaliwa wa pekee aufidie. (Isaya 9:6, 7) Wakaaji wa dunia wenye kuhubiriwa habari njema za Ufalme wanapewa fursa ya kuzikubali na kuthibitisha wana ustahiki wa kupata zawadi ya uhai wa milele katika ukamilifu wa kibinadamu katika dunia-paradiso.
13. Kwa nini twaweza kuwa na hakika kwamba serikali ya Ufalme wa Kimesiya itakuwa bora kupita zote, na Mashahidi wapendekeza nini bila kuona aibu?
13 Kwa uhakika, ikiwa Yesu alikuwa na nia ya kupatwa na kifo chenye ukatili ili afidie wale ambao wangekuwa raia zake, hakika yeye angewapa serikali ile iliyo bora kupita zote. Sisi twapendekeza hivi kwa kila kiumbe binadamu aliye duniani: Uwe raia mwenye imani na utii wa serikali hiyo. Sisi hatuoni aibu kuhusu serikali ambayo twapendekezea aina ya binadamu yote tukiwa na moyo mweupe. Sisi hatujikunyati tusihubiri Ufalme, ingawa huenda mwendo huo ukatuletea mnyanyaso. Kama mtume Paulo, kila mmoja wetu asema hivi: “Mimi sioni aibu kuhusu zile habari njema.”
14. Kulingana na Yesu, kuhubiriwa kwa Ufalme kungeenea kadiri gani katika siku yetu?
14 Yesu alitabiri kwamba habari njema za Ufalme zingehubiriwa ulimwenguni pote, na unabii huu wenye kuhusisha mambo mengi kwa mapana uliufaa ujumbe wa jinsi hiyo. (Marko 13:10) Yeye hakukosa nia ya kutabiri kuhubiriwa kwa Ufalme wa Yehova mpaka ncha iliyo mbali zaidi—ndiyo, kwenye miisho ya dunia. (Matendo 1:8) Yesu alijua kwamba mahali popote ambapo watu wangeweza kupatikana, wafuasi wake wenye imani wangefanya jitihada ya moyo mweupe kuwafikia wakiwa na habari njema za Ufalme.
15, 16. (a) Ni nani ambao wastahili kufikiwa kwa habari njema? (b) Kwa nini kazi ya kuhubiri itatimizwa kujapokuwa na mnyanyaso wenye kufanywa na tengenezo la Ibilisi?
15 Leo hesabu ya wakaaji wa dunia ni maelfu ya mamilioni na wamesambaa katika kontinenti zote na visiwa vikubwa-vikubwa vya zile bahari kuu. Hata hivyo, hakuna sehemu yoyote ya dunia yenye kukaliwa imekuwa mbali mno kufanya Mashahidi wa Yehova wasijitahidi kuifikia wakiwa na habari njema. Dunia yote yenye kukaliwa ni kibago cha kitamathali cha kuwekea nyayo za Yehova Mungu. (Isaya 66:1) Viumbe wanadamu wenye kukaa katika sehemu yoyote ya kibago cha kuwekea nyayo zake wastahili kufikiwa na ujumbe huu wa wokovu.
16 Leo habari njema ni habari zenye kufurahisha kuhusu serikali ya kifalme iliyo na uaminifu-mshikamanifu, ambayo tayari imesimamishwa imara ikiwa mikononi mwa Mesiya. Yesu alijua kwamba tengenezo la Ibilisi lijapofanya mnyanyaso ulio mkali kabisa, roho ya Mungu ingesukuma wafuasi wa kweli wa Mesiya waende kwenye ncha ya mwisho kabisa ili “habari njema hizi za ufalme” uliosimamishwa kihakika ziweze ‘kuhubiriwa katika dunia yote inayokaliwa.’—Mathayo 24:14, NW.
Hatuoni Aibu Kuhusu Yesu Kristo na Yehova
17. (a) Waabudu wa kweli hawaoni aibu kuhusu nini? (b) Ni kawaida gani ya mwongozo ambayo Yesu alionyesha wazi kwenye Marko 8:38, nao una umaana gani?
17 Mungu Aliye Juu Zaidi hakukosa nia ya kujipa mwenyewe jina, Yehova; wala waabudu wake wenye imani hawapaswi kuona aibu kuhusu jina hilo. Waabudu wa kweli wana furaha kujulikana na kutambuliwa kuwa wale ambao humpa yeye ibada na utii usiogawanyika. Kwa habari yake mwenyewe, kwenye Marko 8:38, NW, Yesu aliweka wazi kawaida, au kanuni, ipasayo kufuatwa: “Mtu yeyote yule awaye mwenye aibu kuhusu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki chenye uzinzi na dhambi, Mwana wa binadamu atakuwa mwenye aibu pia kuhusu huyo wakati yeye awasilipo katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.” Vivyo hivyo, mtu yeyote yule ambaye angekuwa mwenye aibu kuhusu Mungu na Baba ya Bwana Yesu Kristo, ingekuwa halali Yehova aone aibu kuhusu mtu huyo. Na kiumbe yeyote ambaye Yehova angemwonea aibu kwa sababu ya mwendo wake usio wa imani hangestahili kuona shangwe ya kuwamo katika sehemu yoyote ya makao ya Mungu mbinguni au duniani.—Luka 9:26.
18. (a) Kwa nini maneno ya Yesu kwenye Mathayo 10:32, 33 yapasa kukazwa kabisa katika mioyo na akili zetu? (b) Ni nini huwapata wale ambao hukana Yesu na Yehova kwa sababu ya kuhofu wanadamu? (Toa vielelezo vyenye kutegemea msingi wa kielezichini.)
18 Acheni maneno yanayofuata ya Yesu Kristo yakazike kabisa katika mioyo na akili zetu: “Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.” (Mathayo 10:32, 33; Luka 12:8, 9) Kwa msingi uo huo, yeyote yule ambaye angemkana Mungu na Baba ya Bwana Yesu Kristo angekanwa Naye. Hangehesabiwa kuwa astahiki kuwa mshirika wa watu wa nyumba ambayo Yesu Kristo ndiye Mwana mkuu. Kwa hiyo angeharibiwa wakati wa Mungu uliowekwa.b
19, 20. (a) Kwa nini wale ambao wamesali ili jina la Yehova litakaswe hawana chochote cha kuonea aibu? (b) Wapiga mbiu ya Ufalme wasio na hofu wametimiza nini, na wakiwa na tegemezo gani?
19 Sala ya kiolezo ambayo Yesu alifundisha wanafunzi wake itajibiwa: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Hilo litukiapo, wanafunzi wa Yesu wenye upendo hawatakuwa na chochote cha kuonea aibu. Jina la Yehova litapewa kicho, litakaswe, si na mamilioni walio hai sasa tu ambao hawahitaji kamwe kufa bali pia na maelfu ya mamilioni ya aina ya kibinadamu ambao yeye atawaita watoke katika makaburi yao wakati wa utawala wake wa Ufalme wa miaka elfu. Watakuwa na fursa ya kuishi milele juu ya dunia-paradiso.
20 Bila aibu, wapiga mbiu hawa wasio na hofu wa habari njema za Ufalme wameweza kufanya ushahidi wa duniani pote kujapokuwako upinzani wa ulimwenguni pote kwa sababu wana tegemezo la nguvu izidiyo ile ya kibinadamu—tegemezo la malaika za kimbingu. Kwa sababu hiyo, Mashahidi wa Yehova ‘huhofu Mungu na kumpa yeye utukufu.’—Ufunuo 14:6, 7, NW.
Hatuoni Aibu Kuhofu Mungu na Kumpa Yeye Utukufu
21. Mashahidi wa Yehova wamekuwa hawaoni aibu kufanya nini, na tokeo likawa nini?
21 Mashahidi wa Yehova wamejithibitisha wenyewe kuwa hawaoni aibu kuhofu Mungu na kumpa yeye utukufu, hata kutumia jina lake mwenyewe la kibinafsi, Yehova. Wamepata baraka zisizoelezeka kutokana na kufanya hivyo. Baraka hizi zimekuja kwa utimizo mwaminifu wa ahadi za Mungu Aliye Juu Zaidi. Hiyo imemtetea kama nini kuwa ndiye Mungu mmoja wa kweli aliye hai, yule Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima!
22. Kwa nini Mashahidi wa Yehova watakabili mnyanyaso mkali, lakini watakuwa na shangwe gani?
22 Wakati ulio usoni, serikali za kilimwengu zitageuka dhidi ya tawala za kidini na kuzifutilia mbali zote—kutia na Jumuiya ya Wakristo—zitokomee. (Ufunuo 17:16, 17) Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova watakabili kipindi cha kunyanyaswa vikali na viasili vya kilimwengu. Wao hawangeweza kuvumilia na kubaki hai kama yule Mungu wa milele hangekuwa pamoja nao. Lakini yeye yu pamoja nao, na kwa hiyo watakuwa na shangwe ya kuona yule Mungu ambaye Mashahidi hao humwabudu bila kuyumba-yumba akifutilia mbali adui wote hao walio dhidi ya Ukristo na dhidi ya Yehova ili watokomee. Wao hawatapatwa na aibu ya kufichuliwa wazi na kuharibiwa kuwa adui za theokrasi ya kweli bali watapata shangwe isiyoelezeka ya kumwimbia Yehova hivi: “Tangu milele hata milele ndiwe Mungu.”—Zaburi 90:2.
23. Kwa nini Mashahidi wa Yehova hawana chochote cha kuonea aibu, na tokeo litakuwa nini?
23 Wao watamwonea fahari Mungu, yule Baba ya Yesu Kristo, ambaye kwa njia yake jamaa ya kibinadamu yafidiwa ione shangwe ya uhai wa milele katika ukamilifu wa kibinadamu na furaha katika dunia-paradiso. Lo, Yehova Mungu amejionyesha kuwa Mungu mwenye nguvu kama nini kwa njia ya Kristo Yesu! Lo, Yehova amejionyesha kwa uzuri ulioje kuwa ni mtumizi mwenye hekima na upendo, si mtumizi mbaya, wa nguvu zake za uweza yote! Kwa hiyo, sisi hatuna chochote cha kuonea aibu kuhusiana naye wala kuhusiana na Mwana wake mzaliwa pekee, Yesu Kristo. Sisi hatuoni aibu kuwa wapiga mbiu wa zile habari njema tukufu, ambazo huonyesha wazi zile nguvu za Yehova Mungu ambazo huyashinda mambo yote kwa njia ya Kristo Yesu, aliyesema hivi katika saa za kumalizia maisha yake ya kidunia: “Jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.” (Yohana 16:33) Katika kufuata mwendo huu, acheni sikuzote tufuate kielelezo cha mtume Paulo, ambaye hakuona aibu kamwe kuhusu habari njema. Tukifanya hivyo, Mungu Mweza Yote hataona aibu kuhusu sisi.
[Maelezo ya Chini]
a Ingawa hatutaki kuona aibu kuukubali wazi uhakika wa kwamba sisi ni Mashahidi, kuna nyakati ambapo ni lazima ‘tuwe na tahadhari kama nyoka.’ (Mathayo 10:16, NW) Mashahidi katika Ujeremani ya Nazi walijua kwamba kulikuwako wakati wa kujitambulisha wenyewe na wakati wa kutofanya hivyo.—Linganisha Matendo 9:23-25.
b Tena na tena, wale waliokana Yesu na Yehova kwa kuhofu wanadamu hawakupata upendeleo wowote kutoka kwenye ulimwengu. Kwa kielelezo, ona Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1989, ukurasa 12; 1982 Yearbook, ukurasa 168; 1917 Yearbook, kurasa 174-6; 1974 Yearbook, kurasa 149-50, 177-8 (Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 1975 ukurasa 428 na Novemba 1, 1975, kurasa 503, 504). Kwa upande ule mwingine, hata wenye kuazimia kuwa wapinzani wa habari njema hutazamia kwamba Mashahidi hawatakana Yesu na Yehova. (1989 Yearbook, kurasa 116-18) Ona pia Mathayo 10:39 na Luka 12:4.
Maswali ya Muhtasari
◻ Kama mtume Paulo, ni mwelekeo gani ambao twapaswa kuwa nao kuhusu kujulisha wazi habari njema, na kwa nini?
◻ Kwa nini ujumbe ambao Mashahidi wa Yehova hupigia mbiu ndizo habari bora kupita zote?
◻ Ni onyo gani ambalo Yesu alitoa kuhusu mtu yeyote ambaye angeona aibu kuhusu yeye awasilipo katika utukufu wa Ufalme?
◻ Ni jambo gani huwapata wale ambao hukana Yesu na Yehova?
◻ Wapiga mbiu ya habari njema wameweza kutimiza nini bila aibu, na kwa nini?