Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 2/15 uku. 25
  • Burudisha Watu wa Ukoo Wako kwa Maji ya Ukweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Burudisha Watu wa Ukoo Wako kwa Maji ya Ukweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Kuwatilia Maji” Watu wa Ukoo
  • Uwe “Kisima cha Hekima”
  • Acha Mwenendo Mwema Uhubiri
  • Usiliache Tumaini!
  • Vipi Jamaa Zako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kuifikia Mioyo ya Watu wa Ukoo Wasio Waamini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Tunawezaje Kuwahubiria Watu wa Jamaa Zetu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Kweli Huleta, “Si Amani, Bali Upanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 2/15 uku. 25

Burudisha Watu wa Ukoo Wako kwa Maji ya Ukweli

“KAMA vile maji baridi juu ya nafsi iliyochoka, ndivyo ilivyo ripoti njema kutoka bara la mbali,” Sulemani akasema. (Mithali 25:25, NW) Ni ono lenye kusisimua kama nini kwa nafsi iliyochoka kusikiliza ripoti yako njema kuhusu uhai wa milele katika Paradiso inayokuja! Kwa njia hii, kinywa chako huwa “chemchemi ya uzima.”—Mithali 10:11; Isaya 52:7.

Maji hulowesha kabisa udongo na kusababisha ukuzi, hali furiko laweza kuleta msiba. Pia, maji kwa namna ya kinywaji kilichotiwa baridi huburudisha, lakini ni nani apenda kunaswa katika upepo wenye manyunyu ya theluji au dhoruba yenye mawe ya mvua? Kwa kuwa kile ambacho hububujika kutoka kwenye kinywa chetu kimelinganishwa na maji, yahitajiwa kabisa kuelekeza uangalifu wa karibu kwenye fundisho letu. (1 Timotheo 4:16) Hasa ni lazima tuwe na fahamu za kutambua athari tofauti za “maji” haya wakati tuwahubiripo watu wa ukoo wetu.

“Kuwatilia Maji” Watu wa Ukoo

Katika nyakati za kale, Rahabu alifungua njia ya kuokoka kwa jamaa yake, na Kornelio alitoa ushahidi mbele ya watu wa ukoo wake. (Yoshua 2:13; 6:23; Matendo 10:24, 30-33) Andrea ndugu ya Petro alimsaidia awe mwanafunzi wa Yesu. (Yohana 1:40-42) Na leo wengi wa Mashahidi wa Yehova huacha ukweli wa Biblia ububujike na kufikia watu wa ukoo wao. Mithali 11:25, NW, yaahidi hivi: “Yeye anayetilia wengine maji kiuhuru yeye mwenyewe atatiliwa maji kiuhuru pia.”

Mwanamke mmoja katika Ulaya alitamani kushiriki imani yake mpya pamoja na wazazi, ndugu, na dada zake wanaoishi katika Ufilipino. Yeye aripoti hivi: “Nilifanya hivyo katika kila barua niliyowaandikia. Kabla ya ubatizo wangu, niliwapelekea vitabu pia na kuwauliza kama walitaka kufanyiwa ziara na Mashahidi wa Yehova.” Aliona shangwe kubwa walipokubali kufanyiwa ziara, na sasa wanane kati yao wamwabudu Yehova. Mashahidi fulani wameona matokeo mema kwa kupeleka maandikisho-zawadi ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa watu wa ukoo wao.

Lakini namna gani ikiwa washiriki wa jamaa hawaonyeshi upendezi wowote? Yesu alikabili hali hii, kwa maana wakati mmoja “ndugu zake walikuwa, kwa uhakika, hawajizoezi imani katika yeye.” Hata hivyo, baadaye, walidumu katika sala “kwa kauli moja” pamoja na mitume. (Yohana 7:5; Matendo 1: 14, NW) Kwa nini badiliko hilo la moyo? Yaonekana wazi kwamba Yesu aliwapa watu wa ukoo wake usaidizi kabla hajapaa mbinguni. Jinsi gani? Aliwasaidia kujipatia imani kwa kuonekana kwa Yakobo ndugu-nusu yake. (1 Wakorintho 15:7) Hivyo, usiache kujaribu kusaidia watu wa ukoo wako. Mashahidi wengi wameweza kuongea kuhusu ukweli wa Biblia pamoja na watu wa ukoo wasioitikadi baada ya kungojea wapate wasaa ufaao.

Hata hivyo, ‘kuwatilia maji’ watu wa ukoo hakumaanishi kuwafisha maji kwa maneno. Jozi moja (mume na mke) ya Wayugoslavi wasema hivi: “Sikuzote kuna hatari ya kuwahubiri kupita kiasi.” Mwangalizi-msafiri mmoja aeleza hivi: “Mara nyingi akina ndugu hufanya zaidi, wakionyesha bidii yenye kuongozwa vibaya.” Ludwig akumbuka wakati alipoanza kujifunza Biblia: “Ndipo nikamfafanulia mama yangu mambo chungu nzima niliyokuwa nimejifunza kutokana na Biblia, na mara nyingi hiyo ilitokeza mabishano, hasa na baba yangu.”

Uwe “Kisima cha Hekima”

Twasoma kwamba “ulimi wa wenye hekima hufanya mema kwa maarifa, lakini kinywa cha wajinga hububujika upumbavu,” na “moyo wa mwadilifu hutafakari ili kujibu.” (Mithali 15:2, 28, NW) Hivyo utimamu wa akili, hekima, na ufahamu huhitajiwa ili kuyapa maneno yetu ladha yenye kuburudisha na kujenga. Ni jambo la maana tufikirie twanena wakati gani, twanena mambo gani, na twanena kiasi gani.

Kwa kielelezo, siku yenye joto kikombe cha maji humburudisha kama nini mtu mwenye kiu! (Mathayo 10:42) Lakini hakuna mtu ambaye angeota juu ya kujimwagia kichwani ndoo iliyojaa maji! Mwangalizi wa mzunguko aliyetangulia kunukuliwa aeleza hivi: “Matokeo bora zaidi hupatikana na wale ambao huamsha udadisi katika watu wa ukoo wao kwa kuwatolea ushahidi wenye kiasi.” Mara nyingi mazungumzo ya Kibiblia yenye matunda hufuata wakati mtu wa ukoo mwenye kupinga aonapo kiu, na kuanza kuuliza maswali.

Huriye, Shahidi Mturuki, aliweza kupata matokeo hayo nyumbani kwa kuacha vichapo vya Biblia vikiwa wazi kwenye habari ambazo zingeweza kupendeza mume wake asiyeitikadi. Alisomea watoto hadithi za Biblia, na —ikiwa mume alikuwa anasikiliza—akatoa maelezo yenye kumnufaisha. Nyakati fulani mke aliuliza hivi tu: “Nilijifunza hivi na hivi katika funzo langu leo. Wewe waonaje?” Pia ataarifu juu ya kawaida za mwenendo ambazo alitunza akilini: “Fuliza kuwa mtulivu, na usichokozoke au kuudhika. Usiwe ndiwe mjua yote. Uwe mnyenyekevu tu na ukae bila kimbelembele.” Mwishowe mume wake alikubali ukweli wa Biblia na sasa atumikia akiwa mhudumu wa wakati wote.

Marijan alisaidia watu kadhaa wa ukoo waikubali imani yake. “Usilazimishe mambo bali ngojea wasaa ufaao,” ndivyo yeye ashauri. “Twapaswa kuonyesha staha wakati watuambiapo tusinene nao kuhusu ukweli. Ni lazima tuwe wenye saburi na upendo.” Watu wa ukoo wafanyapo upinzani ndipo Mhubiri 3:7 hufaa hasa. Husema kwamba kuna “wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena.” Hiyo yadokeza kuwa na nia ya kusikiliza kwa saburi, si kukatiza-katiza, na kustahi maoni ya wengine. “Si jambo la akili kuwaka kasirani wakati wa kuongea na watu wa ukoo,” ataarifu Petar, ambaye wakati mmoja alikuwa akipinga sana lakini akabadili msimamo wake.

Acha Mwenendo Mwema Uhubiri

Mume asiyeitikadi alisababisha matata kwa mke wake Mkristo muda wa miaka mingi, nyakati fulani akimfungia nje ya nyumba. Wakati mmoja alikasirika vikali hata akararua kitabu ambacho mke huyo alikuwa amesahau kukiondoa. Ni nini kilichobadili mtazamo wake? Yeye aeleza hivi: “Niliendelea kujiuliza kwa nini mke wangu alikuwa mthibitifu sana akiendelea kutegemea Yehova. Sikuweza kupata dosari kwake, kwa maana alitunza nyumba vizuri, na alikuwa mke na mama mwema kwa watoto wetu.” Siku moja mume alikuwa akitafuta mambo mema ya kuhutubu katika semina ya dakika tano, kwa hiyo mke wake akampa matoleo mawili ya Amkeni! aliyatupia jicho kwa kusita, akagutuka kupata habari yenye mafaa kuhusu utengenezaji wa kalamu za risasi. Kwa njia hii upendezi wake katika magazeti haya uliamshwa. Leo, jamaa hii imeungamana katika ibada ya Yehova.

Shauri la mtume Petro kwamba mke aweza kuvutia mume asiyeitikadi ‘bila neno kupitia mwenendo safi pamoja na staha ya kina kirefu’ latumika kwa wanafamilia wengine pia. (1 Petro 3:1, 2, NW) Jozi moja iliyooana walipoacha pokeo la zamani lisilo la Kibiblia na dini ya wazazi wao Waromania, familia zao zilipata kuwa wapinzani wakali sana. Mke hata alishambuliwa na mama-mkweye, aliyejaribu kumuua. “Sisi hatukuruhusu jambo hili lituvunje moyo au kutufanya tuchokozeke. Tulitupa wasiwasi wetu wote juu ya Yehova,” aripoti Nikolic. Miaka kumi na mmoja baadaye wazazi wake, dada zake wote wawili, na waume za dada zake ni Mashahidi waliobatizwa. Ni nini kilichovunja pingamizi hilo? “Kielelezo kizuri na mwenendo wa Kikristo. Yaani, sisi hatukutumia wakati mwingi tukiongea nao kuhusu ukweli. Bali, tulijaribu kuutenda.”

Usiliache Tumaini!

Ingawa husababisha mshangilio mkubwa kuona watu wa ukoo wakianza kuabudu Mungu wa kweli, namna gani baadhi yao wakiendelea kupinga? Wewe wapaswa utendeje kwa kuitikia? Yesu alitangulia kuona kwamba nyakati fulani ibada ya kweli ingeleta migawanyiko mikubwa miongoni mwa watu wa ukoo. (Mathayo 10:34-37) Marica aliachwa na wanafamilia wote alipopata kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Yeye hakuridhiana katika ibada, na bado alitambua “kwamba hata watu wa ukoo wana haki ya kuwa na maoni na rai zao wenyewe.” Mtazamo wake uliwasukuma kumstahi kama walivyokuwa wamefanya kabla ya hapo.

Ludwig aling’amua kwamba alikuwa na wajibu wa kupenda wazazi wake hata ingawa huenda wakachagua njia tofauti ya maisha. Alikumbuka-kumbuka vifungu vya Biblia vyenye kuhusiana na habari hiyo, kama vile: “Waheshimu baba yako na mama yako”; “maneno yenu yawe na neema sikuzote”; “mwe tayari sikuzote kumjibu kila mtu [kutetea, NW] . . . kwa upole na kwa hofu [staha ya kina kirefu, NW]”; na, “haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi.” (Waefeso 6:2; Wakolosai 4:6; 1 Petro 3:15; 2 Timotheo 2:24) “Wakati wowote nilipowapigia simu au kuzuru wazazi wangu, nilisali kwa Yehova nipate hekima, na kidato-kwa-kidato uhusiano wetu ukawa wenye kustarehesha zaidi, wenye urafiki zaidi,” ndivyo aripoti.

Usikate tumaini kwamba hatimaye mbegu za kweli hazitachanua katika mioyo ya watu wa ukoo wao. Mume mmoja aliyebatizwa kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova miaka 31 baada ya mke wake aeleza hivi: “Nitazamapo nyuma, ni lazima niungame kwamba mke wangu alinisubiri sana. Mimi nilijua sana kwamba mara nyingi yeye alisali kwa Yehova kwa ajili yangu.”

Maneno yenye kutoka katika kinywa chako na yawe yenye uchangamshi na yenye kumaliza kiu kama maji safi! Ndiyo, zishiriki “habari njema tukufu za Mungu mwenye furaha” pamoja na watu wote, kutia na watu wa ukoo wako. (1 Timotheo 1:11, NW; Ufunuo 22:17) Hapo ndipo maneno haya ya Yesu yatatumika: “Yeye ambaye atia imani katika mimi, sawa na vile Andiko limesema, ‘Kutoka kwenye sehemu yake ya ndani kabisa vijito vya maji yaliyo hai vitatiririka.’”—Yohana 7: 38, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki