Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 7/1 uku. 7
  • Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Thawabu ya Kufuata Haki
  • Vijana Katika Italia Wanafanyiza Nafasi za Kutoa Ushuhuda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kufuata Yaliyo ya Haki Hupendekeza Huduma Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Msaada kwa ‘Wenye Kiu’ Katika Urusi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Uwe Mnyofu Katika Mambo Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 7/1 uku. 7

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

◻ ULE “mnyanyaso mkubwa” dhidi ya kundi la mapema la Kikristo ulitumika kutawanya wanafunzi wengi wa Kristo. (Matendo 8:1) Hata hivyo, mnyanyaso huo ulitokeza kinyume cha yaliyotazamiwa kwa sababu wale waliotawanywa “walienda wakipita katika bara lile wakijulisha wazi habari njema za lile neno.” (Matendo 8:4, NW) Filipo aliendelea kuhubiri, na “kwa upatani mmoja umati ulikuwa ukitoa uangalifu.” (Matendo 8:6, NW) Kama vile mnyanyaso ulivyotokeza kinyume cha yaliyotazamiwa katika karne ya kwanza, ndivyo ulivyofanya katika kijiji kimoja kaskazini mwa Thailand.

Painia wa pekee wa Mashahidi wa Yehova alianza kuhubiri katika kijiji hicho, lakini kwanza wanakijiji wakawa hawataki kusikiliza. Hata hivyo, alipoongea na mhubiri wa hapo watu walikusanyika kuwazunguka ili wasikilize. Baadhi yao wakapata kung’amua kwamba Shahidi huyu aliijua Biblia vizuri kuliko mhudumu wao, kwa hiyo wakaanza kujifunza Biblia pamoja na painia huyo hata ingawa wengine waliwasumbua-sumbua. Baadhi ya mabata wao waliuawa, uhai wa painia ukatishwa, na nyumba ya mwanamume mmoja mwenye kupendezwa ikateketezwa. Mwanamume huyo alisema hivi: “Wao waweza kuteketeza nyumba yangu, lakini hawawezi kuteketeza moyo wangu.” Wale wenye kujifunza na Shahidi huyo walisafiri mbali kwa baiskeli ili kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme. Wanne kati yao walibatizwa, na sita wengine wangali wakihudhuria mikutano pamoja nao.

Thawabu ya Kufuata Haki

◻ Akina ndugu katika Zambia wamesitawisha sifa njema ya ufuataji haki, na hiyo imewatokezea mibaraka, na pia ikasaidia wengine kuutambua ukweli. Mzee mmoja, aliye painia wa kawaida, alikuwa akisafiri katika basi moja akamsikia kwa mbali kidogo Shahidi mmoja katika basi akiongea na wengine juu ya ufufuo. Abiria mmoja alimwuliza hivi Shahidi huyo wa kike: “Kwa nini nyinyi Mashahidi hudai kwamba dini yenu tu ndiyo ya kweli?” Yule ndugu akajiunga katika maongezi na kuambia abiria huyo kwamba Yehova atathawabisha Mashahidi kwa sababu wao hufundisha ukweli kutokana na Biblia.

Baada ya usiku-kati kufika wakiwa katika safari ndefu hii, basi lilifika kwenye kizuia-magari barabarani. Mvua ilikuwa nyingi. Askari-jeshi akaingia ndani ya basi na kuuliza kama humo ndani mlikuwa na yeyote wa Mashahidi wa Yehova. Walikuwamo watatu. Halafu akasema: “Haya basi, Mashahidi bakini mkiwa mmeketi, wale wengine tokeni na mifuko yenu.” Wengine wote wakaenda nje kwenye mvua, na baada ya ukaguzi, wakarudi mizigo na nguo zao zikiwa zimelowana.

Aliporudi ndani ya basi, askari akasema: “Sababu iliyofanya niwaache Mashahidi wabaki ni kwamba wao ni watu wafuataji haki. Sisi tumejionea mengi tukakuta kwamba wao tu ndio wafuataji haki; tuulizapo mifuko yao ina nini, wao hutuambia ukweli.” Basi lilipoendelea na mwendo, ndugu yule aliuliza hivi: “Ni ipi dini ya kweli?” Mtu mmoja akajibu: “Ni ile isiyolowana katika mvua.”

Ndiyo, ufuataji haki husaidia kuitambulisha dini ya kweli, na kwa uhakika una thawabu zao!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki