Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 9/1 uku. 29
  • Msaada kwa ‘Wenye Kiu’ Katika Urusi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaada kwa ‘Wenye Kiu’ Katika Urusi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Uzee Si Kizuizi cha Kujifunza Kweli ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Matendo Mema Yamtukuzayo Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kondoo wa Yesu Husikiliza Sauti Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 9/1 uku. 29

Wapiga-mbiu wa Ufalme Waripoti

Msaada kwa ‘Wenye Kiu’ Katika Urusi

“HERI wenye njaa na kiu ya haki; maana hao watashibishwa,” alisema Yesu. (Mathayo 5:6) Mambo yaliyoonwa yafuatayo yatoa kielezi cha jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyosaidia kutosheleza kiu ya kiroho ya wengi katika Urusi, ambako uhuru wa kidini ulizuiwa kwa zaidi ya miaka 70.

▪ Mwanamke fulani aitwaye Valentina alikuwa na maswali mazito ya Biblia ambayo hayakujibiwa kwa miaka mingi. Kwa kielelezo, alijiuliza: ‘Yesu alisali kwa nani?’ Alisababu kwamba ni lazima iwe Yesu alikuwa akisali kwa mtu fulani aliyekuwa mkuu zaidi kuliko yeye mwenyewe na alitaka kujua kuhusu jina la Huyo.

Alizuru Kanisa Othodoksi la Urusi. Hata hivyo, hakuyapata majibu kwa maswali yake katika dini hiyo. Akiwa hajatosheka, alienda kwenye kanisa Protestanti lakini akakosa tena kupata majibu ya wazi. Akiwa hajui ni wapi kwingineko angeweza kwenda, Valentina alianza kuisoma Biblia, akijaribu kupata majibu mwenyewe—lakini hakufaulu. Alisali ili kupata msaada.

Wakati fulani baadaye Mashahidi wa Yehova walibisha kwenye mlango wake. Walimwonyesha kutoka Biblia kwamba jina la Mungu ni Yehova. Hatimaye, alijifunza ni nani Yesu alikuwa akisali kwake! Alianza kujifunza Biblia kwa ukawaida pamoja na Mashahidi. Mara nyingi alikesha kucha akisoma fasihi zilizotangazwa na Watch Tower Society na kuchunguza na kusoma maandiko ya Biblia. Upesi Valentina alifikia mkataa kwamba alikuwa ameipata kweli. Kabla ya miezi mitatu kwisha alianza kushiriki katika kazi ya kuhubiri, na miezi miwili baadaye, akabatizwa. Kutafuta kwake kweli kwa njia ya sala kulithawabishwa.

▪ Shahidi mmoja alisafiri kwa basi ili kuhubiri katika eneo la mbali. Katika safari yake aliongea na mwanamke kijana kuhusu ahadi za Biblia, lakini huyo mwanamke kijana hakupendezwa. Miezi miwili baadaye huyo Shahidi alifanya safari ya pili ya kwenda eneo lilo hilo ili kutoa hotuba ya watu wote. Baada ya hotuba alimwendea mgeni mmoja akamuuliza: “Je, mtu fulani tayari amesema nawe kuhusu habari njema kutoka Biblia?” Mwanamume huyo akajibu, “Ndiyo, wewe umesema nami.” Huyo Shahidi alifikiri kwamba mwanamume huyo alikuwa akimfanyia mzaha. Lakini huyo mwanamume kijana akaeleza kwamba miezi miwili mapema alikuwa amesikia bila kukusudia, mazungumzo kati ya huyo Shahidi na yule mwanamke kijana, katika ile safari ya basi. “Nilitaka kujua zaidi, lakini ukashuka katika basi, nami nikafikiri nisingewaona Mashahidi wa Yehova tena kamwe. Halafu kazini kwangu nilikutana na mwanamume anayejifunza Biblia pamoja na Mashahidi. Na basi nipo hapa!”

Huyo mwanamume na mke wake walianza kujifunza Biblia. Baada ya muda mfupi sana, aliweza kuona kwamba kazi yake ya kuajiriwa ilipingana na kanuni za Biblia. Akitaka kudumisha dhamiri njema mbele ya Mungu, alibadili kazi yake. Sasa yeye huwaambia wengine kuhusu Ufalme wa Mungu kwenye kila fursa. Mke wake anafanya maendeleo pia katika funzo lake la Biblia.

Mashahidi wa Yehova katika lile eneo kubwa sana la Urusi wanapendezwa kushiriki katika kuwaambia watu wote wenye mioyo myeupe: “Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.”—Ufunuo 22:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki