Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 2/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Wakati Wazee Watakapokuwa Vijana Tena
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Yehova Alimponya Maumivu Yake
    Igeni Imani Yao
  • Thawabu ya Ayubu—Chanzo cha Tumaini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Mtu Aliye Mfano Bora Ambaye Alikubali Kusahihishwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 2/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Ayubu 33:24 yasema juu ya “ukombozi” kuwa ukipatikana kwa ajili ya Ayubu, ukimruhusu aepuke kufa. Ni nani angekuwa ukombozi huo kwa ajili ya Ayubu?

Hakukuwa na dhabihu yoyote ya kibinadamu iliyotolewa kwa ajili ya Ayubu kule nyuma, lakini Mungu alifunika, au akasamehe, kosa la Ayubu.

Shetani alisababishia Ayubu matata mengi, kutia na “majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.” Hali ya Ayubu ilikuwa mbaya sana hivi kwamba mke wake akamhimiza ‘amkufuru Mungu, akafe.’ Hata Ayubu aliwazia-wazia kama kifo kilikuwa bora kuliko mateso ya jinsi hiyo.—Ayubu 2:7-9; 3:11.

Ilipoonekana kwamba Ayubu angeweza kufa, Elihu alikadiria hali yake hatari na kuuweka msingi kwa ajili ya tumaini, akisema hivi: “Nyama ya mwili wake huliwa, isionekane . . . Na uhai wake unakaribia waangamizi. Kwamba akiwapo malaika [mjumbe, NW] pamoja naye, mkalimani [mnenaji, NW], mmoja katika elfu, ili kumwonyesha binadamu hayo yampasayo; ndipo amwoneapo rehema, na kusema, mwokoe asishuke shimoni; mimi nimeuona ukombozi. Nyama ya mwili wake itakuwa laini kuliko ya mtoto.”—Ayubu 33:21-25.

Twajua kwamba Yesu Kristo alitoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu uwe ukombozi unaolingana kwa ajili ya wanadamu wasio wakamilifu. Dhabihu yake ilisawazisha kile ambacho Adamu alipoteza, ikilipa bei iliyohitajiwa kuleta ufungulio wa kutoka kwenye dhambi. (Warumi 5:12-19; 1 Timotheo 2:5, 6) Hata hivyo, huu sio utumizi pekee wa “ukombozi” katika Biblia. Neno la Kiebrania lipatikanalo kwenye Ayubu 33:24 humaanisha kwa msingi “kifuniko.” (Kutoka 25:17, NW) Mungu alipokuwa akishughulika na Israeli wa kale, alikuwa na mpango wa kufunika, au kufanyia upatanisho, dhambi—dhabihu zilizofunika dhambi, zikinyoosha mambo kati ya wanadamu na Mungu.—Kutoka 29:36; Walawi 16:11, 15, 16; 17:11.

Ingawa hivyo, mapema kidogo Mungu alikuwa amekuwa mwenye nia ya kukubali dhabihu ziwe maonyesho ya shukrani au ya maombi ya msamaha na kibali. (Mwanzo 4:3, 4; 8:20, 21; 12:7; 31:54) Ayubu alielewa thamani ya dhabihu hizo. Twasoma hivi: “Akarauka na mapema asubuhi, na kusongeza sadaka za kuteketezwa kama hesabu [ya wana wake wote] wote ilivyokuwa; kwani Ayubu alisema, Humkini kwamba hawa wanaangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu mioyoni mwao. Ndivyo alivyofanya Ayubu sikuzote.” (Ayubu 1:5) Kwa kuwa alijaribu kumpendeza Mungu na kwa wazi alikuwa na roho yenye kusikitikia makosa, dhabihu zake zilikuwa zenye thamani machoni pa Mungu.—Zaburi 32:1, 2; 51:17.

Lakini baadaye Ayubu alipatwa na ugonjwa ulioelekea kutisha uhai wake. Pia alikuwa na maoni yenye makosa juu ya uadilifu wake, hivyo basi alihitaji sahihisho, ambalo Elihu alimtolea halafu. (Ayubu 32:6; 33:8-12; 35:2-4) Elihu alisema kwamba Ayubu hakuhitaji kuendelea kuwa katika hali yake ya huzuni moja kwa moja mpaka kwenye kifo na shimo (Sheoli, au kaburi la kawaida). Kama Ayubu angetubu, “ukombozi” ungeweza kupatikana.—Ayubu 33:24-28.

Hatuhitaji kufikiri kwamba kwa kusema “ukombozi” Elihu alimaanisha binadamu fulani kule nyuma ambaye angekufa kwa ajili ya Ayubu. Kwa sababu ya dhabihu ambazo waabudu wa kweli walikuwa wamezoea kutoa, namna ya ukombozi ambao Elihu alikuwa akidokeza katika kisa cha Ayubu ingaliweza kuwa ni dhabihu ya mnyama. Kwa kupendeza, baadaye Mungu aliwaambia hivi waandamani watatu wachambuzi wa Ayubu: “Mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi.” (Ayubu 42:8) Hata ukombozi huo uwe ulikuwa wa namna gani, wazo kuu la Elihu lilikuwa kwamba Ayubu angeweza kulipiwa kosa lake na apate manufaa zenye kutokana na jambo hilo.

Ilitendeka hivyo. Ayubu ‘alitubu katika mavumbi na majivu.’ Halafu? “BWANA [Yehova, NW] akaugeuza uteka wa Ayubu . . . Basi hivyo BWANA [Yehova, NW] akaubarikia huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake . . . Kisha baada ya mambo hayo Ayubu akaishi miaka mia na arobaini, naye akawaona wanawe, na wana wa wanawe, hata vizazi vinne.” Yakubalika kwamba ukombozi huo haukumweka Ayubu huru kutoka dhambi, hivyo basi baada ya muda alikufa. Hata hivyo, kurefushwa kwa uhai wake kwathibitisha kwamba, kwa matokeo ya kustaajabisha, ‘nyama ya mwili wake ilipata kuwa laini kuliko ya mtoto, akazirudia siku za ujana wake.’—Ayubu 33:25; 42:6, 10-17.

Baraka hizo zilizokuja kutokana na kutumia ukombozi wenye mipaka kuelekea Ayubu zatumika kuwa mwono wa kimbele wa baraka nyingi ambazo katika ulimwengu mpya zitawajia ainabinadamu wanaoamini. Wakati huo, manufaa kamili ya dhabihu ya ukombozi ya Yesu itapatikana, ikiondoa milele matokeo yenye msiba ya dhambi na kutokamilika. Lo, sisi tutakuwa na sababu iliyoje ya “kupaaza sauti kwa shangwe,” kama vile Elihu alivyotaja!—Ayubu 33:26, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki