Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 3/15 uku. 29
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Aliyeitunga Biblia?
    Amkeni!—2007
  • Mungu Aliipuliziaje Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Kweli Tunaweza Kujua Ni Nani Aliyeandika Biblia?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 3/15 uku. 29

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Ni mwandikaji gani wa Biblia aliyekuwa “jemadari,” jinsi inavyotajwa katika kitabu The Bible—God’s Word or Man’s?a

Kitabu hicho chenye kusaidia juu ya Neno la Mungu chasema hivi katika ukurasa wa 10: “Biblia pia ni ya namna ya peke yake kwa sababu ya dai la waandikaji wayo wengi. Watu wapatao 40 kutia ndani wafalme, wachungaji, wavuvi, watumishi wa serikali, makuhani, angalau jemadari mmoja, na tabibu, walishiriki katika kuandika sehemu tofauti-tofauti za Biblia. Lakini mara kwa mara, waandikaji walidai lile lile: kwamba walikuwa wakiandika si mawazo yao wenyewe bali ya Mungu.”

Wengine wameuliza ni waandikaji gani wa Biblia waliotambuliwa na kazi au utendaji huu mbalimbali. Kwa habari hiyo, tafadhali angalia yanayofuata:

Wafalme: Idadi fulani ya waandikaji wa Biblia walikuwa wafalme. Huenda Daudi na Sulemani wakakumbukwa kwa urahisi sana. (Zaburi 3, maandishi ya juu; Mithali 1:1; Mhubiri 1:1) Hata hivyo, wimbo ulio katika Isaya 38:10-20 uliandikwa na Hezekia. (Mstari 9) Wanachuo wengi huamini kwamba yeye alitunga pia Zaburi 119, labda kabla ya kuwa mfalme. Na Hezekia alishiriki katika kuunganisha Mithali sura za 25–29. (Mithali 25:1) Sura ya mwisho ya Mithali ilitayarishwa na “mfalme Lemueli.” Wengine humtambulisha kuwa mfalme Hezekia, ingawa wengine hudhani kwamba Lemueli alikuwa Mfalme Sulemani.—Mithali 31:1.

Wachungaji: Daudi na nabii Amosi walifanya kazi wakiwa wachungaji. (1 Samweli 16:11-13; 17:15, 28, 34; Amosi 1:1) Amosi aliandika kitabu cha Biblia chenye jina lake, na Daudi alitunga zaburi nyingi. Kwa uhakika Zaburi 23 iliyo maarufu inaonyesha ujuzi wa Daudi wa uchungaji.

Wavuvi: Miongoni mwa mitume wa Yesu waliokuwa wavuvi, Yohana na Petro baadaye waliongozwa kwa roho kuandika vitabu vya Biblia. (Mathayo 4:18-22) Chini ya uongozi wa roho ya Mungu Yohana aliandika usimulizi wa Gospeli na pia barua tatu na kitabu cha Ufunuo. Petro aliandika barua mbili zenye kupuliziwa roho.

Watumishi wa serikali: Danieli na Nehemia pia walikuwa watumishi wa serikali za kigeni ambazo zilikuwa na mamlaka juu ya watu wa Mungu. (Nehemia 1:1, 11; 2:1, 2; Danieli 1:19; 2:49; 6:1-3) Vitabu viwili vya Biblia ni vyenye majina ya wanaume wawili hao.

Makuhani: Manabii wawili wa Mungu ambao walitumiwa kuandika vitabu vya Biblia walikuwa makuhani. Walikuwa Yeremia na Ezekieli. (Yeremia 1:1; Ezekieli 1:1-3) Zaidi ya hayo, Ezra alikuwa kuhani wa Kiharuni aliyekuwa “mwandishi mwepesi katika sheria ya Musa.” “Alikuwa ameuelekeza moyo wake kuitafuta sheria ya BWANA [Yehova, NW], na kuitenda, na kufundisha maagizo na hukumu katika Israeli.”—Ezra 7:1-6, 10, 11.

Jemadari: Daraka la Yoshua katika kuliongoza jeshi wakati Waisraeli walipohamia Bara Lililoahidiwa na kupigana vita dhidi ya watu wengi maadui linamstahilisha kuwa jemadari. (Yoshua 1:1-3; 11:5, 6) Alipendelewa kuandika kitabu cha Yoshua. Halafu, pia, wasomaji wengine wa Biblia huenda wakamwona Daudi kuwa mtu ambaye alitumika akiwa jenerali kabla ya kuwa mfalme.—1 Samweli 19:8; 23:1-5.

Tabibu: Mwishowe, Wakolosai 4:14 inataja “Luka, yule tabibu mpendwa.” Luka aliandika Gospeli iliyo na jina lake, na kwa wazi Matendo ya Mitume pia.

[Maelezo ya Chini]

a Kilichochapishwa katika 1989 na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki