Hudhuria “Wapendao Uhuru” Mkusanyiko Wa Wilaya!
SIKU tatu zenye kuthawabisha za maagizo ya Biblia zakungoja wewe. Uwepo saa 4:20 Ijumaa asubuhi wakati mkusanyiko uanzapo kwa muziki. Onea shangwe hotuba ya kufungua, “Kwa Nini Uichungulie Sheria Kamilifu ya Uhuru?,” na sehemu ya kumalizia ya pindi ya asubuhi, ile hotuba ya msingi: “Kusudi na Utumizi wa Uhuru Wetu Wenye Kutolewa na Mungu.”
Alasiri ya Ijumaa, onyo la upole litaandaliwa Wakristo ili watimize agizo lao wakiwa wahudumu wa Mungu. “Una Shughuli—Katika Kazi Zisizo na Uhai au Katika Utumishi wa Yehova?” na “Watu Walio Huru Lakini Watatoa Hesabu” ni viwili vya vichwa vitakavyokuzwa. Kitia moyo ili mtu atumie uhuru wake kumtumikia Yehova kitaandaliwa katika drama ya mavazi kamili. Itachota habari kutokana na maono ya Ezra na washirika wake waliorudi Yerusalemu kutoka Babuloni katika 468 K.W.K. ili kurembesha hekalu la Mungu.
Jambo kuu la pindi ya Jumamosi asubuhi litakuwa mfululizo wa sehemu tatu, “Uhuru Pamoja na Daraka Katika Familia.” Itakayofuata hotuba ya kujichunguza nafsi “Endelea Kuwa Huru Umtumikie Yehova” ni hotuba juu ya wakfu na ubatizo wa Kikristo. Alasiri wengi watangoja kwa hamu sehemu “Je! Ndoa Ndio Ufunguo wa Kupata Furaha?” Pindi hiyo itamalizia kwa jambo kuu ambalo bila shaka litawaletea wapendao uhuru wote shangwe kubwa.
Utataka kuwapo Jumapili asubuhi usikie mfululizo wa sehemu tatu “Kutumika Tukiwa Wavuvi wa Watu.” Huo utazungumza kielezi cha Yesu cha wavu na samaki na utaonyesha sehemu tulio nao katika utimizo wao. Pindi ya asubuhi itamalizia kwa hotuba muhimu “Kuendelea Kukesha Katika ‘Wakati wa Mwisho’” na “Nani Atauponyoka ‘Wakati wa Dhiki’?” Halafu, alasiri, hutataka kuikosa hotuba ya watu wote, “Kukaribisha kwa Shangwe Ulimwengu Mpya wa Mungu wa Uhuru.” Kabla ya hotuba ya kumalizia yenye kusisimua, kutakuwa na mazungumzo ya somo la makala ya Mnara wa Mlinzi la juma hiyo. Lete nakala yako ya gazeti hilo litakalosomwa juma hiyo.
Wakati wa Novemba na Desemba mikusanyiko imeratibiwa kotekote katika Afrika Mashariki, kwa hiyo kutakuwa na mmoja si mbali kutoka nyumbani kwako. Omba habari kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu ili ujue wakati na mahali pa ule ulio karibu kabisa na wewe.