Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 8/15 kur. 4-7
  • Afya Na Furaha—Waweza Kuzipataje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Afya Na Furaha—Waweza Kuzipataje?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Afya na Furaha—kwa Ufupi
  • Ufalme, au Serikali, ya Mungu
  • Twaweza Kuonea Shangwe Afya na Furaha Sasa?
  • Afya Yako, Furaha Yako
  • Afya Na Furaha—Waweza Kuwa Nazo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Jinsi ya Kupata Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Jitihada ya Kutafuta Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 8/15 kur. 4-7

Afya Na Furaha—Waweza Kuzipataje?

MWANADAMU ametambua tangu zamani uhusiano wa karibu kati ya afya na furaha. Hippocrates, aliyefikiriwa kuwa “baba wa dawa,” alitaarifu hivi: “Mtu mwenye hekima apaswa aone kwamba afya ndiyo mojawapo ya mibaraka ya kibinadamu iliyo kubwa zaidi.” Arthur Schopenhauer (Artur Shopenhaur) mwanafalsafa Mjerumani alisema hivi: “Adui wawili wa furaha ya kibindamu ni maumivu na uchovu.”

Katika kitabu Anatomy of an Illness as Perceived by the Patient, Norman Cousins alisimulia mambo aliyoyaona katika kutumia kicheko kushindana na ugonjwa wake uliokuwa wenye uwezo wa kutisha uhai. Alionyesha sababu ya kupona kwake kuwa angalau kwa sehemu ni kile kicheko cha kutoka moyoni alichoonea shangwe alipokuwa akitazama sinema za ucheshi. Madaktari wenye sifa wameanza kuchunguza faida ambayo huenda ikapatikana kutokana na kemikali fulani ziitwazo endofini, zinazotolewa mwilini tunapocheka. Kwa hiyo twaweza kuona hekima ya mithali hii iliyopuliziwa roho: “Moyo uliochangamka ni dawa nzuri.”—Mithali 17:22.

Hata hivyo, jambo la kinyume ni kwamba, watafiti wamepata kuona kwamba afya nzuri haihakikishi furaha kwa lazima, kwa sababu watu wengi wenye afya nzuri hawana furaha. Utafiti wenye msingi wa maitikio ya orodha ya maswali na kuhojiwa kwa watu zaidi ya 100,000, ulimwongoza Jonathan Freed-man kwenye mkataa usiotazamiwa wa kwamba, zaidi ya asilimia 50 ya watu ambao hawakufurahia maisha yao ni wale ambao kwa msingi walikuwa na afya nzuri.

Afya na Furaha—kwa Ufupi

Kwa hiyo, basi, je, tunapaswa kutafuta ule mchanganyo wa afya na furaha usioweza kupatikana? Mwono-ndani wenye kupendeza ulitolewa na Konfusho karne nyingi zilizopita: “Serikali nzuri hufanikiwa wakati wale walio karibu wanapofurahishwa, na wale walio mbali sana wanapovutwa.” Karibu sana na wakati wetu, mwanasiasa Thomas Jefferson alitangaza kwamba mradi wa pekee wa serikali ni “kupatia umati wa raia wale wanaoishi chini yayo kadiri kubwa zaidi ya furaha wanayoweza kuwa nayo.”

Kwa hakika, uchunguzi wa ukaribu unafunua kwamba jibu la mwisho kabisa la utafutaji wa ainabinadamu afya na furaha kwa kweli hukazia fikira jambo moja—serikali.

Katika enzi zote zilizopita, wanadamu wametegemea hapo—serikali—kwa ajili ya furaha yao. Kwa mfano, Tangazo la Kujitawala la United States lina maneno haya yenye kujulikana sana: “Sisi tunashikilia hizi kweli kuwa wazi, kwamba watu wote waumbwa wakiwa sawa, wapewa na Muumba wao Haki fulani zisizoweza kupingwa, kwamba miongoni mwazo ni Uhai, Uhuru na ufuatiaji wa Furaha.” Angalia kwamba serikali ambayo ilitazamiwa na waandishi hao iliwaahidi raia zayo haki tu ya kufuatia furaha. Kwa habari ya afya, serikali nyingi kwa kustahili sifa zimeeneza programu ili kukuza hali ya afya ya wananchi wazo. Bado, afya nzuri ya ujumla kwa walio wengi imethibitika kutoweza kupatikana.

Hata hivyo hali ikoje kuhusu serikali inayoahidi kuandaa hata zaidi? Vipi kama inaahidi si ufuatiaji wa furaha tu bali pia furaha yenyewe? Na vipi kama inaahidi, si bima ya afya, lakini afya nzuri yenyewe? Je! hungeshangilia kwamba katika serikali hiyo kuna ule ufunguo wa mwisho wa utafutaji wa ainabinadamu afya na furaha?

Huenda wengi leo wakaona hii kuwa ndoto isiyowezekana, hata hivyo kwa kweli serikali kama hiyo imetabiriwa na kuelezwa kwa kadiri fulani. Twaweza kupata habari hiyo inayotegemeka katika Biblia Takatifu, na serikali hiyo ni Ufalme wa Mungu wa Kimesiya.

Ufalme, au Serikali, ya Mungu

Biblia inasema mara nyingi juu ya “ufalme wa Mungu.” Hiyo ni nini hasa? Websters New World Dictionary of the American Language hufasili “ufalme” kuwa “serikali au nchi yenye kuongozwa na mfalme au malkia.” Kwa usahili, Ufalme wa Mungu ni serikali, serikali ya kifalme yenye kuongozwa na Yesu Kristo, Mwana na Mfalme wa Mungu aliyepakwa mafuta. Serikali hiyo ni yenye umaana gani hasa katika kusudi la Mungu? Acha maneno ya Yesu yajibu: “Utafuteni [Endeleeni kuutafuta, NW] kwanza ufalme wake . . . Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote . . . Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu . . . maana kwa sababu hiyo nilitumwa. . . . Habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu [anasonga mbele kuuelekea, NW].”—Mathayo 6:33; 24:14; Luka 4:43; 16:16.

Neno “ufalme” linatumiwa zaidi ya mara mia moja katika masimulizi ya Gospeli ya maisha ya Yesu, nyakati nyingine kwa uwazi sana kuhusiana na afya na furaha. Angalia Mathayo 9:35: “Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.” Ingawa Yesu aliunganisha kuletwa kwa afya njema na kufundisha kwake juu ya Ufalme, twapaswa kuona kwamba kuponya kwake magonjwa kulikuwa jambo la umaana mdogo kukilinganishwa na kazi yake ya kuhubiri na kufunza. Alijulikana kuwa “Mwalimu,” si “Mponyaji.” (Mathayo 26:18; Marko 14:14; Yohana 1:38) Hakukazia fikira hasa juu ya kuwaponya watu au kuwaandalia wagonjwa utunzi. Ufikirio wake wa kwanza ulikuwa Ufalme sikuzote. Kwa kuponya maradhi ya watu, alionyesha huruma yake kubwa tena akadhihirisha kwamba alikuwa na utegemezo wa kimungu.

Maponyo ya Yesu yalitumika pia kuwa wonyesho wa kimbele wa kurudishwa kwa afya ya kibinadamu atakakotimiza wakati Ufalme wa Mungu unapotawala dunia kikamili. Kurudishwa huko kwa afya kunatiwa nguvu na njozi inayoelezwa kwenye Ufunuo 22:1, 2: “Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo, katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni kuwaponya mataifa.”

Lakini itawezekana kwetu tuonee shangwe wapi yote hayo? Huenda likaonekana kuwa jambo zuri mno kuwa la kweli kutazamia mponyo wa ajabu kama huo kutukia duniani. Hata hivyo, kumbuka maneno ya Yesu ambayo huenda wewe mwenyewe umeyasema katika sala: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.”—Mathayo 6:10.

Kwa hiyo, katika utawala wa Ufalme wa Mungu wa Kimesiya, ndipo mahali ambapo tungepata tumaini letu lililo kweli, lenye kutegemeka la afya na furaha katika wakati ujao. Lakini, swali labaki.

Twaweza Kuonea Shangwe Afya na Furaha Sasa?

Hata sasa, kufuata kwetu kanuni za Biblia huenda kukatuwezesha tuonee shangwe kadiri kubwa zaidi ya afya, pamoja na furaha iliyoongezeka. Kama ambavyo imeonyeshwa mara nyingi katika kurasa za jarida hili, wale wanaotumia Biblia maishani mwao kila siku kwa kawaida hulindwa dhidi ya matatizo ya afya yanayotokana na ngono haramu, kuvuta sigareti, kunywa vileo kupindukia, na matumizi mabaya ya dawa za kulevya. Wao huona pia manufaa za maisha matulivu zaidi na mahusiano yaliyo bora zaidi pamoja na watu wa ukoo na wengineo.

Lakini, tumeona tayari kwamba kuwa na afya nzuri hakutokezi kwa lazima furaha ya kudumu. Ungehitaji ufanye nini ili uonee shangwe kadiri kubwa zaidi ya furaha?

Katika utafiti uliotajwa mapema, Jonathan Freedman alifikiria swali hilo kwa kina kirefu. Alichunguza mambo kama vile “Upendo na Ngono,” Ujana na Uzee,” “Chumo na Elimu,” hata “Mji na Nchi.” Huenda ikakushangaza kujua kwamba alipata kwamba mambo hayo hayangemletea mtu furaha nyingi ya msingi. Kwa mfano, akitaja mifano ya watu waliokuwa na vitu vingi vya kimwili lakini ambao hawakuwa na furaha bado, alifikia mkataa huu: “Kwa kushangaza kidogo, tumeona kwamba wala chumo wala elimu havionekani kuwa vyaleta furaha nyingi.”

Mikataa yake ilirudisha maneno ya mtume Paulo mwandishi wa Biblia mwenye hekima aliyesema hivi: “Nimejifunza, katika hali yoyote nilimo, kuridhika nayo.” (Wafilipi 4:11, King James Version) Kumbuka pia maneno ya Yesu: “Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.”—Luka 12:15.

Kwa kweli, Profesa Freedman alipata jambo hilo: “Wakati baada ya wakati, tunapoyatazama maneno ya watu wasio na furaha wanaoonekana kuwa na kila kitu, tunawapata wakieleza kwamba maisha zao zinakosa maana na mwelekezo.” Aliongeza hivi: “Nasita kusisitizia jambo hili, lakini inaonekana kwamba thamani za kiroho huongoza maoni ya mtu juu ya uhalisi, hali kutokuwa nazo hutia sumu au huondoa kwa kadiri fulani sehemu kutoka kila kitu kinginecho.”

Katika siku yetu tunaona ushuhuda wa ukweli wa uchunguzi huo. Tazama karibu nawe. Je! huoni karibu kila mtu—wengine wenye vitu vichache na wengi wenye vitu vingi—akitafuta furaha lakini bila kuionea shangwe nyingi? Ni kweli, wengine wamechoka na hali iliyopo nao waishi maisha yenye kukata tamaa kabisa, hata hivyo wengine huishi maisha yenye namna ile ile yenye kuchosha, wakifuatia-fuatia, lakini wasipate kamwe wanachofuatia. Watu fulani huoa au huolewa ili kupata furaha, hata wakati jirani yao anapotaliki kwa sababu iyo hiyo. Wengine hujichosha kabisa kwa kazi, na wengine bado huacha kazi zao kwenda malikizo marefu na labda yenye bei kubwa. Wote hutafuta mradi ule ule usioweza kupatikana, kuwa na afya na furaha. Je! wao huupata? Je! wewe umeupata?

Afya Yako, Furaha Yako

Uhakika ni kwamba, waweza kuwa na kadiri kubwa ya afya na furaha sasa. Jinsi gani hivyo?

Bila shaka ni jambo la hekima kujaribu kutunza afya yako katika njia ya usawaziko, kama vile kwa kutumia shauri la Biblia linalofaa. Kuwa mwenye akili inasaidia pia. Hilo latia ndani kutambua kwamba ugonjwa waweza kuipata miili yetu isiyo mikamilifu, hata hivyo hatutalemewa wakati jambo hilo linapotukia. Hiyo huenda ikahitaji jitihada zaidi ili kudumisha mtazamo wenye matumaini mazuri tunapokazia fikira ahadi ya kuwa na afya iliyo kamilifu katika ulimwengu mpya unaokuja.

Ili uone kama una kadiri nzuri ya furaha sasa, jiulize maswali haya: 1. Je! mimi nina usimamizi wa kutosha wa maisha yangu mwenyewe? 2. Je! mimi kwa msingi niko katika hali ya amani pamoja na mimi mwenyewe na pamoja na wale walio karibu yangu? 3. Je! ninapendezwa kwa ujumla na yale ambayo nimetimiza maishani yanapolinganishwa na Biblia? 4. Je! familia yangu na mimi tunaonea shangwe kuwa na uwezo wa kumtumikia Mungu?

Kwa kadiri kubwa, chaguo ni letu. Kwa msingi huenda wengi wetu tukawa wenye afya, nasi tuna hiari pia ya kuwa wenye furaha. Lakini ni lazima tuwe na miradi ya kiroho na kufanya bidii kuitimiza. Kumbuka maneno ya Yesu: “Hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.” (Mathayo 6:21) Na sisi tuna sababu yenye msingi wa Biblia kutazamia afya na furaha iliyo bora hata zaidi chini ya utawala mkamilifu wa Ufalme wa Kimesiya. Wakati huo twaweza kuwa na afya na furaha za kikamili.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Watu wenye furaha wanaterema kushiriki pamoja na wengine tumaini lao la afya iliyo kamilifu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki