Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 2/15 uku. 29
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Yohana Alikosa Imani?
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Yohana Anataka Kusikia Kutoka kwa Yesu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Je! Yohana Alikuwa na Ukosefu wa Imani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Alikuwa Mtangulizi wa Mesiya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 2/15 uku. 29

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je! tufikie mkataa kutokana na Mathayo 11:11 kwamba Yesu alijua kimbele kwamba Yohana Mbatizaji angekufa kabla ya Yesu?

Ndiyo, Yesu yaonekana alijua kwamba Yohana asingeendelea kuishi kupata kuwa Mkristo mpakwa-mafuta, kwani Yesu alieleza hivi: “Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.”—Mathayo 11:11.

Malaika Gabrieli alipotangaza kuzaliwa kwa Yohana, alitabiri kwamba Yohana ‘katika roho ya Eliya, angemwekea Yehova tayari watu waliotengenezwa.’ Yohana angekuwa mtangulizi, akiwatayarisha watu kwa ajili ya Mesiya wa Yehova. Lakini hakuna jambo lolote katika tangazo hilo la kimungu lililoonyesha kwamba Yohana mwenyewe angepata kuwa mwanafunzi wa Mesiya huyo ambaye angekuja, wala hakukuwa dokezo lolote kuhusu hilo katika taarifa ya kiunabii iliyotolewa na baba ya Yohana, Zekaria.—Luka 1:17, 67-79.

Hivyo, baada ya kumbatiza Yesu, Yohana aliendelea kuhubiri na kubatiza, akishikamana na mgawo wake wa kutayarisha watu. Yohana alijua kimuujiza kwamba Yesu angeandaa batizo kwa roho takatifu, lakini Yohana hakusema kwamba yeye mwenyewe angepokea roho takatifu, kuwa Mkristo mpakwa-mafuta. (Mathayo 3:11) Yohana alitambua pia kwamba angeendelea kupungua, hali Yesu angeendelea kuongezeka.—Yohana 3:22-30.

Yesu aliposema yale tunayosoma kwenye Mathayo 11:11, Yohana tayari alikuwa kifungoni. Yesu alijulisha kimbele kwamba nabii huyo aliyekuwa kifungoni alikuwa mdogo kuliko yule aliye mdogo zaidi ambaye katika wakati ujao angetumikia akiwa mfalme-kuhani mbinguni. Hata hivyo, yaonekana Yesu alijua pia kwamba Yohana angekufa karibuni, akiondoka katika mambo ya kidunia kabla ya njia “mpya” ya maisha ya kimbingu kufunguliwa. (Waebrania 10:19, 20) Hilo lilimaanisha kwamba Yohana asingeendelea kuishi hadi Pentekoste 33 W.K., wakati kupakwa-mafuta kwa roho kwa wanafunzi wa Yesu kulianza. Kwa hiyo, maelezo ya Yesu kwenye Mathayo 11:11 yaweza kuchukuliwa vile vile kuwa onyesho kwamba yeye alijua kwamba Yohana asingeenda mbinguni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki