Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 4/15 kur. 4-6
  • Je! Mungu Husikiliza Usalipo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Mungu Husikiliza Usalipo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sala Zilizosikizwa
  • Majibu kwa Sala
  • Uwe na Uhakika Kwamba Mungu Husikiliza
  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Sala Ambazo Zinajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 4/15 kur. 4-6

Je! Mungu Husikiliza Usalipo?

MKURUGENZI mkuu huamua kama ataagiza mtu mwingine ashughulikie jambo fulani au kama atalishughulikia yeye binafsi. Vivyo hivyo, Mtawala Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima ana uchaguzi wa kuamua kadiri ya kuhusika kwake kibinafsi katika jambo lolote. Maandiko hufundisha kwamba Mungu amechagua kujihusisha mwenyewe kibinafsi katika sala zetu na kwa hiyo yanatuagiza tuzielekeze kwake.—Zaburi 66:19; 69:13.

Uchaguzi wa Mungu katika jambo hilo hufunua upendezi wake binafsi katika sala za watumishi wake wa kibinadamu. Badala ya kuwavunja moyo watu wake wasimkaribie na kila wazo na hangaiko, awahimiza hivi: “Ombeni bila kukoma,” “katika kusali, mkidumu,” “umtwike BWANA [Yehova, NW] mzigo wako naye atakutegemeza,” “mkimtwika yeye [Mungu] fadhaa zenu zote.”—1 Wathesalonike 5:17; Warumi 12:12; Zaburi 55:22; 1 Petro 5:7.

Ikiwa Mungu asingetaka kuelekeza fikira zake kwenye sala za watumishi wake, yeye asingepanga kamwe kuwe na njia ya kumkaribia na kutia moyo itumiwe kwa uhuru. Huko, basi, kuchagua kwa Mungu kujifanya mwenyewe akaribike kwa watu wake, ni sababu moja ya kuwa na uhakika kwamba yeye husikiliza kwa kweli. Naam, yeye hutoa ufikirio kwenye kila moja ya sala za watumishi wake.

Jambo lisilopasa kupuuzwa ni uhakika wa kwamba Biblia hutaarifu kwa wazi kwamba Mungu husikiliza sala. Kwa mfano, mtume Yohana aandika hivi: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.” (1 Yohana 5:14) Mfalme Daudi alimrejezea Yehova Mungu kuwa ndiye “Msikiaji wa sala” na akasema kwa uthabiti: “Atasikia sauti yangu.”—Zaburi 55:17; 65:2, NW.

Kwa hiyo ingawa tendo la kusali bila shaka lina manufaa lenyewe, Maandiko huonyesha kwamba mengi zaidi huhusika wakati mtu mwadilifu anaposali. Mtu fulani anamsikiliza. Msikilizaji huyo ni Mungu.—Yakobo 5:16-18.

Sala Zilizosikizwa

Biblia ina masimulizi mengi ya watu ambao sala zao, kwa kweli, zilisikizwa na kujibiwa na Mungu. Waliyoyaona huhakikisha kwa wazi kwamba manufaa za sala hupita ile hali ya kutuliza inayotokana na kuelewesha wazi na kutokeza mawazo ya mtu. Zinapita jitihada za kibinafsi za mtu kwa kupatana na sala zake.

Kwa mfano, alipokabiliwa na njama ya Absalomu ya kunyang’anya umaliki wa Israeli, Mfalme Daudi alisali hivi: “Ee BWANA [Yehova, NW], nakusihi, uligeuze shauri la Ahithofeli [mshauri wa Absalomu] liwe ubatili.” Jambo aliloomba halikuwa dogo, kwani “shauri lake Ahithofeli . . . lilikuwa kama mtu aulizapo kwa neno la Mungu; ndivyo yalivyokuwa mashauri yote ya Ahithofeli.” Baadaye Absalomu alikatalia mbali hila ambayo Ahithofeli alikuwa amedokeza ya kumpindua Mfalme Daudi. Kwa nini? “BWANA [Yehova, NW] alikuwa amekusudia kulivunja shauri jema la Ahithofeli, ili BWANA [Yehova, NW] alete mabaya juu ya Absalomu.” Kwa wazi, sala ya Daudi ilisikiwa.—2 Samweli 15:31; 16:23; 17:14.

Vivyo hivyo, baada ya Hezekia kumwomba Mungu amkomboe na ugonjwa wake wa kusababisha kifo, alipona. Je! hiyo ilikuwa kwa sababu tu ya manufaa ya kisaikolojia kwa Hezekia likiwa tokeo la kusali? Bila shaka, la! Ujumbe wa Yehova kwa Hezekia, kama ulivyoletwa na nabii Isaya, ulikuwa: “Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama nitakuponya.”—2 Wafalme 20:1-6.

Danieli, ambaye sala yake ilijibiwa baadaye zaidi ya vile ambavyo huenda akawa alikuwa ametarajia, alihakikishiwa na malaika wa Yehova: “Maneno yako yalisikiwa.” Sala za wengine, kama vile Hana, wanafunzi wa Yesu, na ofisa wa jeshi Kornelio, zilijibiwa katika njia zisizoweza kuhesabiwa kuwa za uwezo wa kibinadamu peke yake. Basi, Biblia hufundisha kwa wazi kwamba sala zinazopatana na mapenzi ya kimungu hupokewa, husikiwa, na kujibiwa na Mungu.—Danieli 10:2-14; 1 Samweli 1:1-20; Matendo 4:24-31; 10: 1-7.

Lakini Mungu hujibuje sala za watumishi wake waaminifu leo?

Majibu kwa Sala

Sala zilizotajwa juu zilijibiwa katika njia za kutazamisha, za kimuujiza. Lakini, tafadhali kumbuka kwamba hata katika nyakati za Biblia, yaliyo mengi ya majibu kwa sala hayakutambulika kwa urahisi. Hiyo ilikuwa kwa sababu yalihusu kutoa imara ya kiadili na mwangazio, ili kuwezesha watumishi wa Mungu washikilie mwendo wa uadilifu. Hasa kwa Wakristo, majibu kwa sala yalihusisha mambo yaliyokuwa ya kiroho hasa, si vitendo vya kustaabisha au vya nguvu.—Wakolosai 1:9.

Kwa hiyo, usitamaushwe ikiwa sikuzote sala zako hazijibiwi katika njia ambayo unatazamia au kupendelea. Kwa mfano, badala ya kuondoa jaribu, Mungu aweza kuchagua kukupa “nguvu ipitayo iliyo ya kawaida” ili kulivumilia. (2 Wakorintho 4:7, NW; 2 Timotheo 4:17) Tusidharau kamwe thamani ya nguvu hiyo, wala tusikate maneno kwamba kwa kweli Yehova hakujibu sala yetu hata kidogo.

Fikiria kisa cha Mwana wa Mungu mwenyewe, Yesu Kristo. Akihangaika kwamba asife akiwa kana kwamba ni mkufuru, Yesu alisali: “Ee Baba ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki.” Je! sala hiyo ilisikilizwa na Mungu kwa upendeleo? Ndiyo, kama inavyothibitishwa kwenye Waebrania 5:7. Yehova hakumwondolea Mwana wake ule uhitaji wa kufa penye mti wa mateso. Badala ya hiyo, “malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.”—Luka 22:42, 43.

Je! hilo lilikuwa jibu la kutazamisha, la kimuujiza? Kwa yeyote kati yetu, lingekuwa hivyo! Lakini kwa Yehova Mungu, chanzo cha nguvu hiyo, huo haukuwa muujiza. Na Yesu, kutokana na maisha yake ya mapema mbinguni, alikuwa anafahamu pindi za zamani wakati malaika walijitokeza kwa wanadamu. Kwa hiyo kutokea kwa malaika kusingekuwa jambo la kumtazamisha jinsi ambavyo kungekuwa kwetu. Hata hivyo, malaika huyo, ambaye Yesu kwa wazi alimjua binafsi kutokana na kuwako kwake kabla ya kuwa mwanadamu, alisaidia kumwimarisha Yeye kwa ajili ya jaribu lililokuwa mbele tu.

Katika kujibu sala za watumishi wake waaminifu leo, Yehova mara nyingi hutoa imara inayohitajika ili kuvumilia. Utegemezo huo huenda ukawa kwa namna ya kitia-moyo kutoka kwa waabudu wenzetu tunaoshirikiana nao kibinafsi. Je! yeyote kati yetu angetaka kukatalia mbali kitia-moyo hicho, labda akikata maneno kwamba kwa kuwa watumishi wenzetu hawajapatwa na majaribu yaliyo sawa na yetu, hawawezi kutuimarisha? Yesu angeweza kuwa na maoni kama hayo kuelekea yule malaika aliyejitokeza kwake. Badala ya hiyo, yeye alikubali kile kitia-moyo kuwa ndilo jibu la Yehova kwa sala yake na kwa hiyo aliweza kutimiza kwa uaminifu mapenzi ya Baba yake. Sisi pia tutataka kukubali kwa neema ile imara ambayo Mungu hutoa katika kujibu sala zetu. Kumbuka pia, kwamba vipindi kama hivyo vya uvumilivu wenye saburi hufuatana mara nyingi na mibaraka isiyohesabika.—Mhubiri 11:6; Yakobo 5:11.

Uwe na Uhakika Kwamba Mungu Husikiliza

Usikose kuwa na uhakika kamwe katika matokeo mazuri ya sala ikiwa haujibiwi papo hapo. Majibu kwa sala nyinginezo, kama vile zile kuhusu kupata kitulizo cha kibinafsi kutoka katika taabu au kupata kwa mtu madaraka zaidi katika utumishi wa Yehova, huenda yakahitaji kungojea wakati ambao Mungu ajua unafaa na ni ule ulio bora zaidi. (Luka 18:7, 8; 1 Petro 5:6) Ikiwa unasali kuhusu jambo linalokuhangaisha sana kibinafsi, mwonyeshe Mungu kwa udumifu wako kwamba tamaa yako ni nyingi sana, kusudi lako ni safi na la kweli. Yakobo alionyesha roho hiyo, baada ya kushindana mweleka pamoja na malaika mmoja kwa muda mrefu na kwa bidii sana, alisema hivi: “Sikuachi, usiponibariki.” (Mwanzo 32:24-32) Ni lazima tuwe na uhakika huo huo kwamba tukiendelea kuomba, tutapokea baraka hatimaye.—Luka 11:9.

Wazo moja la mwisho. Kusikiwa na Bwana Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima ni pendeleo la thamani kubwa. Kwa hiyo, je, sisi husikiliza kwa makini wakati Yehova Mungu, kupitia Neno lake, anaposema nasi juu ya matakwa yake? Kwa kuwa sala zetu hutufanya tumkaribie zaidi Muumba wetu, tutataka kuelekeza uangalifu wetu kwa uzito kwenye kila jambo ambalo anatuambia.

[Picha katika ukurasa wa 6]

Mungu husikiliza sala. Je! wewe humsikiliza yeye kupitia Neno lake?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki