Je! Wakumbuka?
Je! wewe umethamini kusoma matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya hivi karibuni? Basi, ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:
▫ Ni nini kiwezacho kwa kufaa kufananishwa na yale mapendeleo ya utumishi yaliyoongezeka ambayo walipewa Wanethini na wana wa watumishi wa Sulemani waliporudi kutoka uhamishoni katika Babuloni?
Leo, mabaki ya Israeli wa kiroho walio duniani wanapoendelea kupungua, kondoo wengine wanaendelea kuongezeka. Baadhi ya hao wenye mfano wa kondoo, sawa na Wanethini na wana wa watumishi wa Sulemani, sasa wamepewa madaraka mazito chini ya uangalizi wa mabaki. (Isaya 61:5)—4/15, kurasa 16-17.
▫ Nabii Sefania alimaanisha nini aliposema: “Huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya BWANA [Yehova, NW]”? (Sefania 2:2, 3)
Ili mtu aweze kulindwa wakati wa ile “dhiki kubwa” inayokuja, si jambo la kwamba mtu akiisha kuokolewa ameokolewa sikuzote. (Mathayo 24:13, 21) Kufichwa katika siku hiyo kutategemea kuendelea kwa mtu akifanya mambo matatu: Ni lazima amtafute Yehova, autafute uadilifu, na autafute upole.—5/1, kurasa 15-16.
▫ Mikaeli “atasimama” kwa maana gani katika “wakati wa Mwisho”? (Danieli 12:1, 4)
Tangu kuwekwa kwake kuwa Mfalme katika 1914, Mikaeli amekuwa ‘akisimama’ kwa ajili ya watu wa Yehova. Lakini hivi karibuni Mikaeli “atasimama” kwa maana ya pekee sana—akiwa Wakili wa Yehova wa kuondoa uovu wote kutoka duniani na akiwa Mkombozi wa watu wa Mungu.—5/1, ukurasa 17.
▫ Furaha ya kweli hutegemea nini?
Furaha ya kweli hutegemea uhusiano wetu na Yehova wenye thamani kubwa, kibali chake, na baraka yake. (Mithali 10:22) Kwa hiyo, furaha ya kweli haiwezi kutimizwa pasipo utii kwa Yehova na ujitiisho wenye shangwe kwa mapenzi yake. (Luka 11:28)—5/15, kurasa 16, 19.
▫ Yesu alipofanya miujiza yake ya uponyaji, je, imani ilihitajiwa kwa upande wa yule aliyeponywa?
Kadiri fulani ya imani ilihitajiwa kwa upande wa wengi ili wamjie Yesu wapate kuponywa. (Mathayo 8:13) Hata hivyo, hakuna ungamo lolote la imani lililohitajiwa ili Yesu afanye miujiza yake, kama vile alipomponya mwanamume mmoja kilema ambaye hakumjua Yesu. (Yohana 5:5-13) Yesu hata alirudisha sikio lililokatwa la mtumishi wa kuhani mkuu aliyekuwa miongoni mwa kile kikundi cha maadui wa Yesu. (Luka 22:50, 51) Miujiza hiyo ilifanywa kwa uwezo wa roho takatifu ya Mungu, si kwa sababu ya imani ya mtu aliyekuwa mgonjwa.—6/1, ukurasa 3.
▫ Ni nini kinachowakilishwa na lile “juya [wavu, NW]” lililozungumziwa katika kielezi cha Yesu kwenye Mathayo 13:47-50?
Hilo “juya” huwakilisha chombo cha kidunia kinachodai kuwa kundi la Mungu na ambacho hukusanya “samaki.” Kimetia ndani Jumuiya ya Wakristo na pia lile kundi la Wakristo wapakwa-mafuta, lile la pili likiwa limeendelea kukusanya ‘samaki wema,’ chini ya mwongozo wa malaika, kulingana na Mathayo 13:49.—6/15, ukurasa 20.
▫ Ni baadhi gani ya kanuni ambazo waamuzi katika Israeli walipaswa watumie katika kutekeleza migawo yao?
Haki sawa kwa matajiri na maskini, kutokuwa na upendeleo hata kidogo, na kutokubali rushwa. (Mambo ya Walawi 19:15; Kumbukumbu la Torati 16:19)—7/1, ukurasa 13.
▫ Wazee wanapaswa wajaribu kutimiza nini kupitia vikao vya hukumu?
Lengo moja ni kupata kujua mambo ya hakika ya kesi, wakifanya hivyo kwa upendo. Mambo hayo yanapojulikana, ni lazima wazee wafanye lolote linalohitajiwa ili kulinda kundi na kudumisha ndani yalo viwango vya juu vya Yehova na mtiririko usiozuiwa wa roho ya Mungu. Kikao hicho ni cha kumwokoa, ikiwezekana kwa vyovyote, mtenda dhambi aliye hatarini. (Linganisha Luka 15:8-10.)—7/1, kurasa 18-19.
▫ Ni kwa nini fantasia zinazohusu ngono ya haramu ni zenye kudhuru sana?
Kulingana na maneno ya Yesu kwenye Mathayo 5:27, 28, wote wanaoendelea kujifurahisha katika fantasia za ngono ya haramu wana hatia ya kufanya uzinzi mioyoni mwao. Na kuna hatari halisi kwamba fantasia za jinsi hizo zaweza kuongoza kwenye ukosefu wa maadili.—7/15, ukurasa 15.
▫ Yehova aweza kutusaidia katika njia zipi ili tuyaone majaribu yetu ifaavyo na kuyavumilia?
Huenda fikira zetu zikaelekezwa kwenye Maandiko na waamini wenzetu au wakati wa funzo la Biblia. Matukio yaliyoongozwa na Mungu huenda yakatusaidia tuone jambo la kufanya. Malaika huenda wakashiriki katika kutuelekeza, au huenda tukapokea mwongozo kupitia roho takatifu. (Waebrania 1:14)—7/15, ukurasa 21.
▫ Je! Baraza la Nisea katika 325 W.K. lilithibitisha au kuyakinisha fundisho la Utatu?
La, Baraza la Nisea lilimsawazisha tu Mwana na Baba kwa kuwa “wa asili moja.” Wazo la kwamba Baba, Mwana, na roho takatifu walikuwa wote Mungu wa kweli—watatu katika Mungu mmoja—halikusitawishwa na baraza hilo wala na Mababa wa Kanisa wa mapema zaidi.—8/1, ukurasa 20.
▫ Je! Ayubu alikuwa binadamu wa pekee aliyekuwa mwaminifu kwa Yehova katika kipindi ambacho aliishi? (Ayubu 1:8)
La, Kitabu cha Ayubu chenyewe huonyesha kwamba Elihu alikubaliwa na Mungu. Pia, katika wakati ambapo Ayubu aliishi, kulikuwako Waisraeli wengi walioishi Misri, na hakuna sababu yoyote ya kufikiri kwamba wao wote hawakuwa waaminifu na hawakukubaliwa na Mungu.—8/1, ukurasa 31.