Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 2/15 uku. 7
  • Shangilia Katika Dunia Safi Iliyoko Mbele!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shangilia Katika Dunia Safi Iliyoko Mbele!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Paradiso au Mahali pa Kutupia Takataka—Wewe Wapendelea Jambo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kung’olea Mbali Uchafuzi—Kutoka Moyoni na Akilini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Yehova Anawapenda Watu Safi
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Usafi Unamaanisha Nini Hasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 2/15 uku. 7

Shangilia Katika Dunia Safi Iliyoko Mbele!

TWAWEZA kufurahi kama nini kwamba Yehova, Mungu wa utaratibu na usafi, atatimiza kusudi lake la kwanza la kufanya dunia kuwa paradiso ya duniani pote! (Isaya 11:6-9) Yeye anaahidi hivi: “Neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu.” “Mungu hawezi kusema uongo,” kwa hiyo hayo si maneno matupu tu.—Isaya 55:11; Waebrania 6:18.

Twaweza kuwa na kitulizo kwamba Yehova ataingilia mambo kwa upendo kabla ya wanadamu kusababisha uchafuzi mwingi sana, hivi kwamba uharibifu kamili wa kimazingira usiweze kukomeshwa!—Ufunuo 11:18.

Yehova ataondolea mbali wachafuzi wa kimakusudi wasiotubu na watu wanaopuuza kanuni zake za utaratibu na usafi. Hakuna atakayeruhusiwa ahatarishe Paradiso itakayorudishwa.—Mithali 2:20-22.

Wakati wa utawala wa Ufalme wa Mungu, chini ya mwelekezo wa Kristo Yesu, wanadamu watafundishwa jinsi ya kung’olea mbali visababishi vyovyote vinavyobaki vya uchafuzi wa kimwili. Wakati huo—si sasa—ndipo itakapokuwa lazima watumishi wote wa Mungu wahusike kwa bidii katika hatua za binafsi na za pamoja zitakazochangia usafishaji wa duniani pote usio na kifani.—Linganisha Ezekieli 39:8-16.

Waokokaji wa mwisho wa mfumo mbovu wa mambo uliopo wataunga mkono programu hiyo ya usafishaji wa kimwili kwa ujitoaji na idili ileile waliyonayo wanaposhiriki katika kampeni ya leo ya usafishaji wa kiroho.—Zaburi 110:3.

Kwa hakika dunia safi itakuja, ikitanguliwa na kampeni kubwa zaidi ya usafishaji ya wakati wote, yenye kutimizwa na Ufalme wa Mungu. Alama zote za uchafuzi zitaondolewa mbali. Hakutakuwa tena mahali popote pa umma palipochorwa-chorwa. Hakutakuwa tena chupa, mikebe, mifuko ya plastiki, vikaratasi vya kufungia peremende, magazeti ya habari, na magazeti mengine yaliyotupwa yakichafua ufuko au mahali popote pa kiparadiso.

Shangilia katika dunia safi iliyoko mbele!

[Picha katika ukurasa wa 7]

Je! wewe utashiriki katika usafishaji wa duniani pote unaokuja?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki