Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 2/15 kur. 4-6
  • Kung’olea Mbali Uchafuzi—Kutoka Moyoni na Akilini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kung’olea Mbali Uchafuzi—Kutoka Moyoni na Akilini
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kukubali Maoni ya Mungu
  • Je! Tuushiriki kwa Bidii?
  • Usafishaji wa Kiroho
  • Shangilia Katika Dunia Safi Iliyoko Mbele!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Paradiso au Mahali pa Kutupia Takataka—Wewe Wapendelea Jambo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kupata Suluhisho Lifaalo
    Amkeni!—1996
  • Uchafuzi—Nani Huusababisha?
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 2/15 kur. 4-6

Kung’olea Mbali Uchafuzi—Kutoka Moyoni na Akilini

YEHOVA hakuwapa wanadamu tamaa ya kuwa na uchafu au ukosefu wa utaratibu. Makao yao ya sayari yalikusudiwa yawe paradiso yenye usafi, utaratibu, na uzuri. Mungu hakukusudia yaharibike yawe mahali pa kutupia takataka pasipopendeza macho.—Mwanzo 2:8, 9.

Hata hivyo, baada ya wanadamu kukatalia mbali mwongozo wa kimungu, walianza kujenga aina yao wenyewe ya utaratibu wa ulimwengu. Wakikosa hekima ya kimungu na ujuzi, walilazimika wajifunze kwa kujaribu-jaribu mambo. Historia ya ulimwengu huthibitisha ukweli wa Biblia kwamba wanadamu hawawezi kujitawala wenyewe kwa mafanikio; kwa maelfu ya miaka “mwanadamu ametawala mwanadamu kwa kumwumiza.” (Mhubiri 8:9, New World Translation; Yeremia 10:23) Tatizo la ki-siku-hizi la uchafuzi, katika namna zao zote, ni tokeo la kutawala vibaya kwa mwanadamu.

Kukubali Maoni ya Mungu

Watu wanaotamani kumpendeza Mungu hujitahidi sana kuishi kulingana na viwango vya usafi vya Muumba. Hivyo, Mashahidi wa Yehova walikabiliwa na tatizo fulani wakati mkusanyiko wa kimataifa ulipopangwa kufanywa katika Prague, Chekoslovakia, katikati mwa 1991.a Watu karibu 75,000 wangehudhuria, umati ambao ungeenea kwa ustarehe katika Stediamu ya Strahov. Lakini stediamu hiyo haikuwa imetumiwa kwa miaka mitano. Haikuwa imerekebishwa, ilikuwa imeharibiwa na hali za anga. Mashahidi wa Yehova 1,500 hivi walitumia zaidi ya muda wa saa 65,000 ili kuitengeneza na kuipaka rangi upya. Kufikia wakati wa mkusanyiko kampeni hiyo ya usafishaji ilikuwa imeifanya stediamu hiyo kuwa mahali palipostahili pa kumwabudu Mungu wa kweli, Yehova.

Ni nini kinachowachochea Mashahidi wa Yehova wawe tofauti, hali ulimwengu kwa ujumla huonyesha uthamini mdogo sana kwa usafi na utaratibu? Uthamini kwa lile shauri la Biblia kwamba Wakristo wanapaswa wang’olee mbali vitabia visivyofaa, kama vile ubinafsi, kutokufikiria wengine, pupa, na ukosefu wa upendo. ‘Uvue kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake,’ Biblia husema. Weka mahali pao “utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.” Utu wenye sifa za upendo wa usafi, utaratibu, na uzuri hauna nafasi ya mielekeo yenye kuchafua.—Wakolosai 3:9, 10; 2 Wakorintho 7:1; Wafilipi 4:8; Tito 2:14.

Utu mpya hutaka kwamba Wakristo wahangaikie uchafuzi, wasichafue kimakusudi au kupuuza sheria dhidi ya uchafuzi ambazo serikali hufanyiza. Huo unawafanya waepuke ule mtazamo wa kutojali, wenye ubinafsi, na wenye uvivu unaoongoza kwenye kutupa-tupa takataka. Kwa kuonyesha staha kwa mali za wengine, unaondolea mbali kule kutumia michoro kwenye sehemu za umma kuwa njia ya kuonyesha mawazo na hisia, likiwa jambo la kujifurahisha lisilo na hatia, au likiwa namna nyingineyo ya usanii. Huo unataka kwamba nyumba, magari, mavazi, na miili iwekwe ikiwa safi.—Linganisha Yakobo 1:21.

Kwa habari ya watu wasio na nia ya kujivika utu huo mpya, je, Mungu ni wa kulaumiwa kwa ajili ya kuwazuia wasipate uhai katika Paradiso yake inayokuja? Sivyo. Yeyote ambaye angali na mielekeo ya kuchafua iliyofichika moyoni au akilini mwake angetisha ule uzuri wa kiparadiso uliorudishwa wa Dunia sayari, akisababisha huzuni nyingi kwa wale wanaotamani kuudumisha. Uamuzi wa Mungu wa “kuwaharibu hao waiharibuo nchi” ni wenye uadilifu na upendo pia.—Ufunuo 11:18; 21:8.

Je! Tuushiriki kwa Bidii?

Hata hivyo, je! hiyo inamaanisha kwamba Wakristo wanatakwa waendeleze hatua dhidi ya uchafuzi au za usafishaji?

Kwa wazi uchafuzi ni wenye kudhuru afya na usalama wa umma. Yehova ana hangaiko lifaalo juu ya mambo hayo, kama tuwezavyo kuona kutokana na sheria alizowapa Waisraeli. (Kutoka 21:28-34; Kumbukumbu la Torati 22:8; 23:12-14) Lakini yeye hakuwaelekeza wakati wowote wajaribu kuongoza watu wengineo juu ya mambo kuhusu usalama wa umma; wala Wakristo wa karne ya kwanza hawakuambiwa wafanye hivyo.

Leo, mambo ya kimazingira yaweza kwa urahisi kuwa masuala ya kisiasa. Kwa kweli, baadhi ya vyama vya kisiasa vimefanyizwa hasa kwa kusudi la kusuluhisha matatizo ya kimazingira. Mkristo anayejiruhusu kuvutwa kuunga mkono upande mmoja wa kisiasa si mwenye kutokuwamo tena kwa habari za kisiasa. Yesu aliwawekea wanafunzi wake kanuni hii: “Wao si wa [si sehemu ya, NW] ulimwengu, kama mimi nisivyo wa [sehemu ya, NW] ulimwengu.” Mkristo anayepuuza takwa hilo hujiweka katika hatari ya kuunga mkono upande wa “hao wanaoitawala dunia hii, wanaobatilika.”—Yohana 17:16; 1 Wakorintho 2:6.

Yesu hakujaribu kusuluhisha matatizo yote ya kijamii ya siku yake; wala hakuwaambia wanafunzi wake wafanye hivyo. Amri yake kwao ilikuwa: “Enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza . . . , na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi.” Yeye hakuwaamuru kuhusu sera za kimazingira.—Mathayo 28:19, 20.

Akieleza jambo lililopasa kutangulizwa katika maisha ya Mkristo, Kristo alisema hivi: “Utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake.” (Mathayo 6:33) Wakati Yehova anapofikiliza kanuni zake zenye uadilifu duniani pote, kupitia Ufalme wa Kimesiya, matatizo ya kimazingira yatasuluhishwa kwa kudumu na kwa uradhi wa wote.

Hivyo, Mashahidi wa Yehova huchukua msimamo wenye usawaziko. Kulingana na Warumi 13:1-7, ni lazima watii kwa kudhamiria sheria za kiserikali zinazoongoza mazingira. Kwa kuongezea, upendo wa kimungu kwa jirani huwasukuma waonyeshe staha kwa mali za wengine—za umma au za faragha—kwa kutoziharibu sura na kwa kutotupa-tupa takataka. Lakini kwa wazi hawaelekezwi kuongoza katika hatua za usafishaji za kilimwengu. Wanaweka kwanza ifaavyo kuhubiri ujumbe wa Ufalme wa Mungu, wakitambua kwamba hiyo ndiyo njia ya kufanya mema yenye kudumu zaidi.

Usafishaji wa Kiroho

Waisraeli wa kale walionywa tena na tena juu ya matokeo ikiwa wangechafua dunia kwa kumwaga damu, kwa kukubali mtindo-maisha wenye kukosa adili, au kwa kutoonyesha staha kwa mambo matakatifu. (Hesabu 35:33; Yeremia 3:1, 2; Malaki 1:7, 8) Jambo la maana ni kwamba, walihukumiwa kwa ajili ya uchafuzi huo wa kiroho, si kwa ajili ya uchafuzi wowote wa kimwili ambao huenda pia walikuwa na hatia.b

Kwa hiyo, uchafuzi au uchafu wa kiroho ndilo jambo ambalo Mkristo hujitahidi hasa kuepuka leo. Yeye anafanya hivyo kwa kujivika “utu mpya,” unaong’olea mbali mielekeo yenye kuchafua kutoka moyoni na akilini. Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni nne hunufaika kutokana na usafishaji huo wa kiroho, wakitimiza kati yao usafi wa kidini na wa kiadili, pamoja na usafi wa kimwili wenye kutokeza.—Waefeso 4:22-24.

Leo ndio wakati wa kampeni ya usafishaji wa kiroho. Kampeni ya usafishaji wa kimwili duniani pote itafuata kwa wakati uliowekwa na itaokoa makao yetu yasiwe mahali pa kutupia takataka pa duniani pote kwa kuyapa mazingira yasiyo na uchafuzi yanayostahili.—Mhubiri 3:1.

[Maelezo ya Chini]

a Ili kupata ripoti yenye maelezo zaidi juu ya mfululizo huo wa mikusanyiko ya Ulaya ya Mashariki, ona Amkeni! la Desemba 8, 1992.

b Waisraeli walifahamu ule utaratibu wa kuyeyusha. Masalio yamepatikana ya baadhi ya migodi ya shaba nyekundu, na shaba nyekundu iliyeyushwa ili kutayarisha vyombo vya hekalu. (Linganisha 1 Wafalme 7:14-46.) Yaonekana kwamba utaratibu huo wa kuyeyusha usingaliweza kufanywa bila kutokeza kadiri fulani ya uchafuzi kwa namna ya mioshi, mavi ya madini, na povu, kukiwa pia na athari nyinginezo. Hata hivyo, yaonekana Yehova alikuwa na nia ya kuvumilia kadiri ndogo ya uchafu wa mahali fulani katika mkoa huo usio na wakaaji wengi na ulio mbali.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki