Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 6/8 kur. 8-9
  • Kupata Suluhisho Lifaalo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupata Suluhisho Lifaalo
  • Amkeni!—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Usawaziko wa Kikristo
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kutafuta Masuluhisho Yanayokubalika
    Amkeni!—1996
  • Kung’olea Mbali Uchafuzi—Kutoka Moyoni na Akilini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Uchafuzi—Nani Huusababisha?
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 6/8 kur. 8-9

Kupata Suluhisho Lifaalo

NENO LA MUNGU, Biblia, husema juu ya wakati ambapo serikali ya kimbingu ya Mungu itakapokuwa imesuluhisha matatizo yote ya wanadamu, ambayo sasa hutia ndani tatizo la uchafuzi usababishwao na magari. Je, Ufalme huu wa Kimesiya, ambao wengi wamefunzwa kuuomba, utaandaa suluhisho lifaalo kwa kutokeza magari yasiyotokeza uchafuzi kabisa? Au suluhisho lifaalo litapatikana kwa kuondoa magari yote duniani? Kwa kuwa Biblia haitupatii jibu hususa, hatuwezi kufanya lolote ila kungojea na kuona tu.—Mathayo 6:9, 10.

Lakini twaweza kuwa na uhakika juu ya hili: Serikali ya Mungu haitaruhusu uchafuzi uharibu urembo wa uumbaji katika Paradiso iliyorudishwa itakayoletwa na huo Ufalme.—Isaya 35:1, 2, 7; 65:17-25.

Kwa kuwa wale wanaotii Neno la Mungu tayari wanazoezwa kwa ajili ya maisha katika ulimwengu mpya usio na uchafuzi, wanapaswa kuhisije juu ya utumizi wa magari leo? Amkeni! la Juni 22, 1987 (la Kiingereza), lilishughulikia habari “Ni Nini Kinachoipata Misitu Yetu?” Hilo liliripoti kwamba wanasayansi fulani hufikiri kwamba kuna uhusiano kati ya vichafuzi vya hewa vilivyo katika michemuo ya magari na kufa kwa misitu. Hilo lilifanya msomaji mmoja aliyehangaishwa kuandikia Watchtower Society akiuliza ikiwa kwa sababu ya jambo hilo ingefaa Wakristo kuendesha magari. Aliuliza ikiwa kufanya hivyo kungeonyesha ukosefu wa staha kwa uumbaji wa Yehova.

Barua yake ilijibiwa hivi, kwa sehemu: “Mashahidi wa Yehova hutii kwa ushikamanifu sheria za kimazingira zilizowekwa na mamlaka za serikali ili kupunguza uchafuzi. (Warumi 13:1, 7; Tito 3:1) Kuchukua hatua zaidi ya kile ambacho serikali huamuru ni uamuzi wa mtu mmoja-mmoja. Ikiwa mtu aamua kutotumia tena gari, hilo ni jambo lake la kibinafsi. Hata hivyo, makala hiyo ya Amkeni! ilionyesha kile ambacho watu fulani huhisi, kwa kusema hivi kwenye ukurasa 8: ‘Wengi wanachukua hatua zifaazo za kupunguza uchafuzi wa hewa kwa kadiri wawezavyo. Wanaendesha polepole zaidi, hawasafiri sana, wanajiunga na mipango ya kusafiri kwa kikundi cha wenye magari katika gari moja, wanatumia petroli zisizo na madini ya risasi, na kutii maagizo yaliyo dhidi ya uchafuzi yaliyowekwa na serikali.’”

Usawaziko wa Kikristo

Jibu hilo lilidhihirisha usawaziko wa Kikristo. Ni lazima ikumbukwe kwamba si magari pekee yanayoleta uchafuzi. Ndege na magari-moshi—kwa hakika, aina nyingi za kisasa za usafiri—hufanya hivyo. Lakini namna hizi za usafiri hazikutokezwa kwa kusudi la moja kwa moja la kusababisha uchafuzi. Kwa kusikitisha, uchafuzi unaotokea ni athari mbaya inayosababishwa na ujuzi haba na mitazamo isiyokamilika.

Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1993, ukurasa 31, lilizungumzia jambo hili, likisema hivi: “Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tunahangaikia sana yale matatizo mengi ya kiekolojia (mazingira) yanayoathiri makao yetu ya kidunia. Zaidi ya watu wengi, sisi tunathamini kwamba dunia iliumbwa iwe makao safi, yenye afya kwa ajili ya familia kamilifu ya kibinadamu. (Mwanzo 1:31; 2:15-17; Isaya 45:18) . . . Kwa hiyo inafaa kufanya jitihada zenye usawaziko, zinazofaa ili kuepuka kuongezea ule uharibifu wa mwanadamu wa dunia yetu unaoendelea sasa. Lakini, angalia lile neno ‘zinazofaa.’ . . . Watu wa Mungu hawapaswi wawe wasahaulifu kuhusu mambo ya kiekolojia. Yehova aliwataka watu wake wa kale wachukue hatua za kuondolea mbali takataka, hatua zilizokuwa za muhimu kwa kiekolojia na kwa kiafya pia. (Kumbukumbu la Torati 23:9-14) Na kwa kuwa tunajua maoni yake juu ya wale wanaoiharibu dunia, kwa hakika hatupaswi kupuuza mambo tunayoweza kufanya ili kudumisha mazingira yakiwa safi. . . . Hata hivyo, kadiri ambayo Mkristo angejitahidi katika hayo ni jambo la kibinafsi isipokuwa ikiwa inahitajiwa na sheria. . . . Wanadamu wasiokamilika hutumbukia kwa urahisi katika mtego wa kuwa bila kiasi. . . . Jitihada za kibinadamu za kuiondolea dunia matatizo yayo makubwa ya kiekolojia, kutia na uchafuzi, hazitafanikiwa kikamili. Huenda yakawa maendeleo huko na huko, lakini suluhisho pekee la kudumu lataka mwingilio wa Mungu. Kwa sababu hiyo tunakaza jitihada na nyenzo zetu kwenye suluhisho la kimungu, kuliko kujaribu kusuluhisha dalili za kijuujuu tu.”

Wakristo ni wenye usawaziko wanapofuata kanuni za Biblia, wakikumbuka utume wa kimungu ambao wamepokea wa kuhubiri ujumbe wa Ufalme wa Mungu kotekote ulimwenguni. (Mathayo 24:14) Hakuna jambo lililo muhimu au lenye uharaka mkubwa kuliko hilo! Ikiwa namna ya kisasa ya usafiri na mawasiliano yaweza kuwasaidia Wakristo kutimiza wajibu huu, wana sababu nzuri ya kuitumia. Wakati huohuo, wao huepuka kutokeza uchafuzi bila sababu au kwa kusudi. Hivyo wanadumisha dhamiri njema mbele ya mwanadamu na Mungu.

Kwa hiyo ingawa sisi leo hatujui hasa jinsi tatizo la uchafuzi wa magari litakavyosuluhishwa hatimaye, twajua kwamba litatatuliwa. Kwa hakika, suluhisho lifaalo liko karibu sana.

[Sanduku katika ukurasa wa9]

Kupambana na Uchafuzi

• Kutembea au kuendesha baiskeli inapowezekana

• Kushiriki katika mipango ya kusafiri kwa kikundi cha wenye magari katika gari moja

• Kuhakikisha magari yanarekebishwa na kudumishwa kwa ukawaida

• Kuhakikisha natumia fueli isiyoleta uchafuzi sana

• Kuepuka usafiri usio wa lazima

• Kuendesha kwa mwendo wa kiasi lakini ufaao

• Kutumia usafiri wa umma iwezekanapo na ifaapo

• Kuzima injini badala ya kuiacha ikinguruma gari linaposimama kwa kipindi chochote cha wakati

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki