Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 5/15 kur. 24-25
  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Thailand

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Thailand
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakimbizi Wasikia Habari Njema
  • Vidio Yaamsha Kupendezwa
  • Kuwasaidia “Wakaaji Wageni” ‘Wamtumikie Yehova kwa Kushangilia’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Suluhisho Ni Nini?
    Amkeni!—1996
  • Idadi Yenye Kuongezeka ya Wakimbizi
    Amkeni!—1996
  • Ulimwengu Ambao Kila Mtu Atafurahia
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 5/15 kur. 24-25

Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Thailand

“NCHI ya walio huru.” Hiyo ndiyo maana ya jina Thailand. Wakazi wayo wapatao zaidi ya 57,000,000 walio wapole, na wenye bidii kazini, wana mawazo mbalimbali ya kidini. Ingawa Ubuddha ndiyo dini kubwa, dini za Jumuiya ya Wakristo zimo pia katika nchi hii ya kusini-mashariki mwa Asia. Watu hao wote wahitaji kusikia habari njema za Ufalme wa Mungu.—Mathayo 24:14.a

Wakimbizi Wasikia Habari Njema

Katika kambi zilizotapakaa kotekote katika vilima vya Thailand kandokando ya mpaka wa Myanmar, kweli ya Biblia inazidi kuenezwa miongoni mwa wakimbizi wa Karen zaidi ya 10,000. Washiriki wa familia moja ya Karen wanaoishi katika eneo hilo ni Mashahidi wa Yehova. Wamekuwa wakieneza habari njema miongoni mwa wakimbizi. Kazi yao ilianzaje?

Miaka kadhaa iliyopita kijana mmoja aliacha kushirikiana na Kanisa la Anglikana akawa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Wakisukumwa na mhubiri wao, watu wake wa ukoo walimpinga. Hata hivyo, yeye alivumilia kwa saburi, na hatua kwa hatua upinzani wa familia yake ukakwisha. Makasisi wa Kanisa Anglikana waliendelea na dhihaka yao hadi karibu miaka miwili iliyopita walipofukuzwa kutoka vyeo vyao kwa sababu ya ukosefu wa adili. Kwa kuwa wakati huo kanisa halikuwa na mchungaji, watu wa familia ya karibu na watu wengine wa ukoo wa Shahidi huyo walishtuka na kuwa hoi. Kumi na mmoja kati yao walijiuzulu kanisani na kuomba Mashahidi wajifunze Biblia pamoja nao.

Funzo hilo liliendelea vizuri, wakimbizi wengine wakishiriki. Kweli ilienea upesi, ikitokeza kubatizwa kwa Mashahidi wapya 17 katika mto unaotiririka kupitia kambi hiyo ya wakimbizi. Ilikuwa vizuri kama nini kumwona nyanya wa miaka 88 akibatizwa pamoja nao!

Vidio Yaamsha Kupendezwa

Uwezekano wa ukuzi miongoni mwa wakimbizi ni mkubwa. Katika 1993 kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho, watu 57 walihudhuria. Wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko katika Mei ya mwaka huo, watu 67 walikusanyika kusikiliza mojapo hotuba zake. Na karibu 250 walikusanyika ili kutazama vidio Sosaiti ya Watchtower Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name.

Mke wa pasta wa Baptisti katika kambi hiyo ya wakimbizi alihudhuria hotuba ya Biblia ya watu wote iliyoandaliwa na Mashahidi naye akaandika maandiko ya Biblia yaliyozungumzwa. Yeye alimwambia mume wake jinsi hakuridhika na hotuba za kurudia-rudia alizosikia kanisani mwao. Yeye alipinga, akisema kwamba ikiwa mke wake angeenda kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova, wale waenda-kanisa wengine wote wangemfuata. Alipohudhuria tena mikutano hiyo, mume wake alimkimbiza kwa kisu na kuteketeza maandishi yake ya habari za mkutano na fasihi za Biblia. Ingawa hivyo, vidio hiyo ilipoonyeshwa, mke huyo alihudhuria tena. Baadaye mwanamke huyo alimwambia mume wake yale aliyokuwa ameona. Akiwa na moyo tofauti, mume wake alitaka kuona vidio hiyo na aliomba radhi kwamba alikuwa ameteketeza maandishi yake na fasihi za Biblia.

Kwa hiyo watu wanasikia habari njema katika Thailand. Hivyo wanapata uhuru wa kiroho katika “nchi ya walio huru.”—Yohana 8:32.

[Maelezo ya Chini]

a Ili kupata habari zaidi, ona 1994 Calendar of Jehovah’s Witnesses.

[Sanduku katika ukurasa wa 24]

HABARI ZA NCHI Mwaka wa Utumishi wa 1993

KILELE CHA WANAOTOA USHAHIDI: 1,434

UWIANO: Shahidi 1 kwa watu 40,299

HUDHURIO LA UKUMBUSHO: 3,342

WASTANI WA WAHUBIRI WALIO MAPAINIA: 232

WASTANI A MAFUNZO YA BIBLIA: 1,489

IDADI YA WALIOBATIZWA: 92

IDADI YA MAKUTANIKO: 39

OFISI YA TAWI: BANGKOK

[Picha katika ukurasa wa 25]

Wapiga-mbiu ya Ufalme wakihubiri habari njema kwa bidii

[Picha katika ukurasa wa 25]

Ofisi ya tawi ya kwanza, 1947

[Picha katika ukurasa wa 25]

Familia ya Betheli mbele ya ofisi mpya ya tawi katika Bangkok, iliyowekwa wakfu Februari 8, 1992

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki