Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 9/1 uku. 26
  • “Mpingeni Shetani, Naye Atawakimbia”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mpingeni Shetani, Naye Atawakimbia”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Hujibu Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Niliacha Vitu Vyote Ili Kumfuata Bwana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Mwishowe Mbegu Ilichipuka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 9/1 uku. 26

Wapiga-Mbiu wa Ufalme Waripoti

“Mpingeni Shetani, Naye Atawakimbia”

KATIKA karne ya kwanza, kikundi cha watu waliofuata “mambo ya uganga” katika Efeso waliitikia ujumbe wa Kikristo kwa kuchoma hadharani vitabu vyao vya uganga. (Matendo 19:19) Thamani iliyokadiriwa ya vitabu hivyo ilikuwa vipande 50,000 vya fedha. Ikiwa masimulizi hayo ya Biblia yanarejezea dinari, sarafu ya fedha ya Warumi, basi thamani hiyo ingejumlika kuwa angalau dola 37,000!

Leo kuna wengi ambao wakati mmoja walikuwa na fasihi zinazohusu mafumbo ya kipepo lakini walioonyesha azimio kama lile la Waefeso wa kale. Ebu fikiria ono hili kutoka Kanada.

Karibu miaka mitano iliyopita, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuwa akihubiri nyumba kwa nyumba wakati ambapo kwenye mlango mmoja mwanamke mmoja aliyeitwa Nora alimvuta kihalisi ndani ya nyumba. Kwa miaka mingi sana ya utafutaji wa kiroho, Nora alikuwa amekusanya mamia ya vitabu vya mambo ya dini na ya roho, lakini alitaka kujua jambo ambalo Biblia inasema juu ya tumaini kwa watu waliokufa. Shahidi huyo alimpa trakti Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa? Maswali ya Nora yalijibiwa, naye akakubali kuandikisha magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

Baadaye alihama na kupoteza uwasiliano na Mashahidi wa Yehova. Lakini, yeye aliendelea kuyapokea magazeti kupitia posta katika anwani yake mpya. Aliagiza vilevile baadhi ya vichapo vyenye msingi wa Biblia vilivyotajwa katika magazeti. Baada ya muda, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuja mlangoni pake. Akivutiwa kwamba Shahidi huyo alifungua Biblia moja kwa moja alipokuwa akijibu maswali, Nora alimkaribisha arudi kwa mazungumzo zaidi.

Lakini, Shahidi huyo akapata ugumu wa kuwasiliana na Nora tena. Alifanya ziara za mara kwa mara saa tofauti-tofauti katika siku na nyakati tofauti-tofauti katika juma bila kufanikiwa. Hata hivyo, bidii yake ilithawabishwa, naye akapata matokeo mazuri. Funzo la kawaida la Biblia lilianzishwa, ambalo lilifanywa mara tatu kwa juma kwa kusisitizwa na Nora. Mambo aliyokuwa akijifunza yalimchochea aseme na marafiki na washiriki wa familia, jambo lililotokeza watatu kati yao kuomba kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova.

Kupitia funzo lake Nora alikuja kutambua kwamba kuna dini nyingi za bandia na manabii wengi bandia lakini njia moja tu ielekezeayo kwenye uhai. Kwa miaka mingi alikuwa amekuwa akitafuta majibu ya maswali yake katika dini za bandia, lakini baada ya kujifunza yale ambayo Biblia inasema juu ya roho waovu, alitenda kama Waefeso wa kale waliotajwa kwenye Matendo 19:19. Yeye aliondoa vitabu visivyofaa katika maktaba yake na, kwa muda wa siku kadhaa, akaharibu zaidi ya vitabu elfu moja vinavyohusu mafumbo ya kishetani na mafundisho ya dini bandia. Miongoni mwa vichapo vilivyoharibiwa, seti moja ya vitabu zilikuwa na thamani ya zaidi ya dola 800!

Kwa wazi roho waovu walikasirika na hatua ya Nora, nao walimsumbua-sumbua kwa karibu majuma mawili. Hata hivyo, roho waovu hao hawakuweza kumzuia asiendelee na funzo lake la Biblia na vilevile ushirika wake na tengenezo la kisasa la Yehova.

Maono kama haya huonyesha vema ukweli wa maneno ya Biblia: “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.”—Yakobo 4:7.y

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki