Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 1/15 kur. 8-9
  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Puerto Riko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Puerto Riko
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Eneo Jipya
  • Wahamia Puerto Riko
    Amkeni!—1993
  • Wathamini Ndugu na Dada Zako Viziwi!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Puerto Riko—Nchi Yenye Utajiri
    Amkeni!—2008
  • Kusikiliza kwa Macho Yako
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 1/15 kur. 8-9

Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Puerto Riko

KATI ya Bahari ya Karibea na Bahari ya Atlantiki hujibana kisiwa cha Puerto Riko, chenye usitawi wa kitropiki. Christopher Columbus alikidai kuwa cha Hispania katika 1493 na kukiita San Juan Bautista katika ukumbuko wa Yohana Mbatizaji. Jiji lake kubwa zaidi liliitwa kwa muda mrefu Puerto Riko, au “Bandari Yenye Utajiri.” Baada ya muda, jina hilo lilikuja kutumika kwa kisiwa chote, huku jiji kuu likija kuitwa San Juan.

Puerto Riko imethibitika kuwa bandari yenye utajiri katika mambo mengi. Dhahabu nyingi ilisafirishwa kutoka hapa katika miaka ya mapema ya utawala wa Kihispania. Kisiwa hicho sasa hupeleka nje miwa, kahawa, ndizi, na matunda ya jamii ya machungwa, ijapokuwa viwanda vya utengenezaji bidhaa na huduma hufanyiza sehemu kubwa ya mfumo wa kiuchumi. Hata hivyo, Puerto Riko imethibitika kuwa bandari yenye utajiri katika namna yenye umaana zaidi.

Habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu zilianza kuhubiriwa hapa katika ile miaka ya 1930. Leo, kuna wahubiri wa habari njema zaidi ya 25,000 katika Puerto Riko. Katika 1993 wafanyakazi kwenye tawi hili la Watch Tower Society waliongezeka kutoka 23 hadi zaidi ya 100. Ongezeko hili lilihitajika ili tawi hilo liweze kusimamia utafsiri wa fasihi ya Biblia katika Kihispania, ikiwezesha vichapo hivyo kupatikana kwa wasemao Kihispania wapatao 350,000,000 ulimwenguni pote.

Eneo Jipya

Ofisi ya tawi yaripoti hivi pia: “Eneo jipya limefunguka katika Puerto Riko kwa sababu tumekuwa tukifanya jitihada ya kupeleka ujumbe wa Ufalme kwa viziwi. Dada mmoja asimulia ono lifuatalo: ‘Nilikuwa nikifanya kazi miongoni mwa viziwi nikamzuru mwanamke mmoja mwenye watoto wadogo wawili. Alipong’amua kwamba nilikuwa Shahidi, alinikataa mara moja kwa sababu mume wake, ambaye pia ni kiziwi, hakupendelea Mashahidi wa Yehova.

“‘Miezi michache baadaye mwanamke huyu huyu alizuru rafiki aliyekuwa akijifunza Biblia pamoja na Mashahidi. Alijiunga katika funzo na kulifurahia sana. Nilimzuru mwanamke huyo tena, naye akarudia kwamba mume wake hakupendelea hawa Mashahidi. Hata hivyo, alitaka kuifahamu Biblia na alichoshwa na kanisa lake kwa sababu hawakuwa wakifundisha chochote. Tulianza kujifunza, kwa kutumia trakti. Siku moja aliniambia nirudi Jumamosi kwa kuwa mume wake angekuwapo. “Lakini yeye hatupendi, sivyo?” nikauliza. Naye alijibu: “Yeye ataka kuhakiki kile mfundishacho.”

“‘Siku iliyofuata wote wawili walikuwa wakibisha mlango wangu! Kwa kuwa mume huyo alikuwa na maswali mengi, niliwaalika kwenye mikutano yetu kwa viziwi. Alikuwapo pale kabla ya mimi na hajakosa mkutano wowote tangu wakati huo. Anawahubiria viziwi wengine, amehudhuria kusanyiko, na anatazamia sana ubatizo.’”

Ripoti ya tawi yaendelea hivi: “Katika mkusanyiko wetu wa wilaya mwaka huu, programu yote ilitolewa kwa lugha ya ishara, kwa hiyo viziwi wengi walihudhuria na familia zao. Pindi yenye hisia sana ilifika wakati wa hotuba ya mwisho, wakati msemaji alitaja kazi inayofanywa miongoni mwa viziwi na kusema kuwa 70 walikuwapo wakati huo. Makofi yalipigwa sana, lakini kama alivyotaja msemaji, viziwi hawakuweza kuyasikia. Kwa hiyo akiuliza viziwi wawaangalie wasikilizaji, msemaji alirudia lile swali, ‘Je! mnafurahia kuwa na ndugu zenu walio viziwi pamoja nanyi hapa?’ halafu akauliza wasikilizaji wapige makofi kwa kupunga mikono yote miwili. Ilikuwa tamasha yenye kuvutia kuona ndugu na dada 11,000 wakipiga makofi kwa kupunga mikono yao. Ndugu na dada zetu walio viziwi walifurika kwa shangwe na kuhisi kuwa sehemu ya ule udugu mkuu. Wengi walitokwa na machozi ya shangwe.”

Mashahidi wa Yehova washirikipo katika kazi ya mavuno katika Puerto Riko, hakuna shaka kwamba itaendelea kuwa bandari yenye utajiri. “Kondoo” wa Mungu, ambao yeye huwaita “vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote,” wataendelea kuja ndani ili nyumba ya Yehova ijawe na utukufu.—Yohana 10:16; Hagai 2:7.

[Sanduku katika ukurasa wa 9]

HABARI ZA NCHI

Mwaka wa Utumishi wa 1994

KILELE CHA WANAOTOA USHAHIDI: 25,428

UWIANO: Shahidi 1 kwa watu 139

HUDHURIO LA UKUMBUSHO: 60,252

WASTANI WA WAHUBIRI WALIO MAPAINIA: 2,329

WASTANI WA MAFUNZO YA BIBLIA: 19,012

IDADI YA WALIOBATIZWA: 919

IDADI YA MAKUTANIKO: 312

OFISI YA TAWI: GUAYNABO

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki