Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 7/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Anayewaongoza Watu wa Mungu Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Baraza Linaloongoza Hufanyaje Kazi Leo?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 7/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, Mungu alikuwa akionyesha upendeleo kwa kuchagua kwa ajili ya baraza linaloongoza la mapema watu waliotoka katika jamii na taifa lilelile—wote wakiwa Wayahudi?

La hasha, hakuwa akionyesha upendeleo. Wote wale ambao Yesu aliita kwanza kuwa wanafunzi walikuwa Wayahudi. Halafu, kwenye Pentekoste 33 W.K., Wayahudi na wageuzwa-imani wa Kiyahudi walikuwa wa kwanza kutiwa mafuta ili kustahili kutawala na Kristo mbinguni. Ni baadaye tu Wasamaria na watu wasio Wayahudi wasiotahiriwa walipotiwa ndani. Kwa hiyo, ni jambo linaloeleweka kwamba baraza linaloongoza la wakati huo lilifanyizwa na Wayahudi, “mitume na wazee [katika Yerusalemu],” kama inavyotajwa kwenye Matendo 15:2. Hawa walikuwa wanaume waliokuwa na ujuzi mpana zaidi wa Kimaandiko na miaka mingi ya uzoefu katika ibada ya kweli, nao walikuwa wamekuwa na wakati mwingi zaidi wa kukua na kuwa wazee wa Kikristo waliokomaa.—Linganisha Warumi 3:1, 2.

Kufikia wakati wa mkutano wa baraza linaloongoza unaorejezewa katika Matendo sura ya 15, watu wengi wasio Wayahudi walikuwa wamekuwa Wakristo. Hao walikuwa ni pamoja na Waafrika, Wazungu, na watu kutoka sehemu nyinginezo. Hata hivyo, hakuna rekodi ionyeshayo kwamba yeyote kati ya hao wasio Wayahudi walikuwa wameongezwa wakati huo kwenye baraza linaloongoza ili kuufanya Ukristo uvutie watu wasio Wayahudi. Ingawa Wakristo hao wasio Wayahudi waliotoka tu kugeuzwa imani walikuwa washiriki walio sawa katika “Israeli wa Mungu,” wangestahi ukomavu na uzoefu mkubwa zaidi wa Wakristo Wayahudi, kama vile mitume, waliokuwa sehemu ya baraza linaloongoza wakati huo. (Wagalatia 6:16) Ona katika Matendo 1:21, 22 jinsi uzoefu kama huo ulivyothaminiwa sana.—Waebrania 2:3; 2 Petro 1:18; 1 Yohana 1:1-3.

Kwa karne nyingi Mungu alikuwa ameshughulika kwa njia ya kipekee na taifa la Israeli, ambalo kutoka hilo Yesu aliteua mitume wake. Halikuwa kosa wala ukosefu wa haki kwamba hakuna mitume waliotoka sehemu zile ambazo sasa ni Amerika Kusini au Afrika au Mashariki ya Mbali. Baada ya muda wanaume na wanawake kutoka sehemu hizo wangekuwa na fursa ya kupata mapendeleo matukufu zaidi kuliko kuwa mtume duniani, kuwa mshiriki wa baraza linaloongoza la karne ya kwanza, au cheo cha kuwekwa rasmi kokote miongoni mwa watu wa Mungu leo.—Wagalatia 3:27-29.

Mtume mmoja alisukumwa na moyo kusema kwamba “Mungu hana upendeleo, bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.” (Matendo 10:34, 35) Ndiyo, manufaa za fidia ya Kristo zapatikana kwa wote, bila upendeleo. Na watu mmoja-mmoja kutoka kila kabila na lugha na taifa watatiwa katika Ufalme wa kimbingu na katika umati mkubwa utakaoishi milele duniani.

Wanadamu wengi huwa na unyeti juu ya malezi ya kijamii, kilugha, au kitaifa. Jambo hili laonyeshwa na yale tusomayo katika Matendo 6:1 juu ya suala lililosababisha manung’uniko kati ya Wakristo wenye kusema Kigiriki na wale wenye kusema Kiebrania. Huenda tumelelewa na hisia hizo au kuzisitawisha hisia nyetivu za sasa juu ya lugha, jamii, malezi ya kikabila, au kijinsia. Kwa sababu ya uwezekano huo ulio halisi, itakuwa vizuri kufanya bidii sana ili tuache hisia zetu na maitikio yetu yaundwe na maoni ya Mungu, ambayo ni kwamba wanadamu wote ni sawa mbele yake, bila kujali sura yetu ya nje. Mungu alipofanya sifa za kustahili za wazee na watumishi wa huduma zirekodiwe, yeye hakutaja jamii na malezi ya kitaifa. La, yeye alikazia fikira juu ya sifa za kustahili za kiroho za wale ambao wangeweza kupatikana ili kutumikia. Ndivyo ilivyo kuhusu wazee wa kwetu, waangalizi wasafirio, na wafanyakazi wa matawi leo, kama baraza linaloongoza katika karne ya kwanza lilivyokuwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki