Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 8/1 kur. 25-29
  • Thawabu za Udumifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thawabu za Udumifu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Vielelezo vya Udumifu
  • Kudumu Katika Sala Kunathawabisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Sala Katika hizi “Siku za Mwisho”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kukimbia Shindano La Mbio Kwa Uvumilivu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 8/1 kur. 25-29

Thawabu za Udumifu

ALIKUWA mwanamke Mgiriki aliyekuwa akiishi Foinike katika mwaka wa 32 W.K. Binti yake alikuwa mgonjwa sana, na mwanamke huyo alikuwa akimtafutia sana bintiye matibabu. Aliposikia juu ya mgeni aliyetembelea eneo lao—mgeni aliyekuwa amejulikana kuwa na uwezo wa kuponya wagonjwa—mwanamke huyo aliazimia kumwona na kumwomba msaada.

Alipokutana naye, alipiga magoti, akisihi hivi: “Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.” Kwa njia hiyo, mwanamke huyo Mgiriki akamwomba Yesu amponye binti yake.

Je, unaweza kuwazia moyo mkuu na unyenyekevu aliohitaji mwanamke huyo ili kufanya jambo hilo? Yesu alikuwa mwenye mamlaka aliye na uwezo na sifa kwa kiasi fulani, na mapema alikuwa amejulisha kwamba hakutaka yeyote ajue alipokuwa. Alikuwa amewapeleka wafuasi wake Foinike kupata pumziko walilohitaji sana, wala si kufanya kazi miongoni mwa wasio Wayahudi wasioamini. Zaidi ya hayo, Yesu alikuwa Myahudi na mwanamke huyo hakuwa Myahudi, na bila shaka alijua jinsi Wayahudi walivyochukia kushirikiana na wasio Wayahudi. Walakini, alikuwa ameazimia kabisa mtoto wake apate ponyo.

Yesu na mitume wake walijaribu kumshauri mwanamke huyo aache kutafuta msaada wakati huo. Kwanza, Yesu hakuzungumza naye. Kisha, kwa sababu ya kilio chake cha daima, mitume kwa kuudhika wakamwambia Yesu hivi: “Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.”

Lakini mwanamke huyo alikataa. Badala ya hilo, alimsujudia Yesu, akisema: “Bwana, unisaidie!”

Akitaja daraka lake la msingi kwa wana wa Israeli na, wakati huo huo, akijaribu imani na azimio la mwanamke huyo, kwa huruma Yesu alimweleza hivi: “Si vema kukitwaa chakula cha watoto [cha Waisraeli] na kuwatupia mbwa [wasio Wayahudi].”

Badala ya kuudhiwa na rejezo hilo lisilofaa kuelekea jamii yake, kwa unyenyekevu mwanamke huyo alidumisha ombi lake kwa kujibu hivi: “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.”

Yesu alithawabisha udumifu wa mwanamke huyo Mgiriki kwa kupongeza imani yake na kutenda kulingana na ombi lake. Wazia shangwe ya mwanamke huyo aliporudi nyumbani na kupata bintiye amepona kabisa!—Mathayo 15:21-28; Marko 7:24-30.

Kama mwanamke huyo wa karne ya kwanza, twahitaji kuwa wadumifu katika jitihada zetu za kumpendeza Yehova na kupata kibali chake. Kama kwa habari ya mwanamke huyo Mgiriki, Biblia hutuhakikishia kwamba udumifu wetu “katika kutenda mema” utathawabishwa sana.—Wagalatia 6:9.

Udumifu ni nini? Kwa nini wahitajiwa? Ni mambo gani yaweza kutufanya tupoteze sifa hii, tuiache au tushindwe? Ni thawabu zipi tuwezazo kutazamia kupokea ikiwa tutadhihirisha udumifu sasa katika kutumikia Muumba na Baba yetu, Yehova?

Kamusi moja hufafanua kitenzi “dumu” kuwa “kushika kwa nguvu na kwa imara kusudi fulani, hali, au juhudi, vijapokuwa vipingamizi, maonyo, au vizuizi. . . . kuendelea kuwapo; endelea.”

Biblia kwa kurudia-rudia husihi watumishi wa Yehova wadumu katika kufanya mapenzi yake. Kwa kielelezo, tunaambiwa ‘tufulize kutafuta sana kwanza ufalme,’ ‘tushike sana lililo bora,’ ‘tudumu katika sala,’ na “tusichoke” katika kutenda mema.—Mathayo 6:33, NW; 1 Wathesalonike 5:21, NW; Warumi 12:12, NW; Wagalatia 6:9.

Katika shughuli za kila siku za maisha, udumifu ni sifa ambayo lazima sisi sote tuwe nayo na kuisitawisha ili tuokoke. Bila hiyo hatuwezi kupata chochote cha thamani ya kweli, ya kudumu. Fikiria kielelezo cha mtoto akijaribu kusimama na kuchukua hatua zake za kwanza zisizo imara. Hakuna kitoto kiwezacho kujifunza kusimama na kutembea kwa urahisi kwa siku moja. Tukiwa watoto, sisi sote huenda tulijaribu mara nyingi na kushindwa kabla mwishowe kufanikiwa kiasi fulani katika kutembea. Ni nini kingalitokea ikiwa tulipoanguka kwa mara ya kwanza, tungeamua kuacha kujaribu? Labda bado tungekuwa tukitambaa huku na huku kwa mikono na magoti yetu! Udumifu ni muhimu ili kufikia miradi inayostahili na kupata ukuzi katika ustadi na kujistahi kunakostahili. Kama usemi ujulikanao usemavyo, “Washindi hawaachi kamwe, nao waachao hawashindi kamwe.”

Mapainia wa muda mrefu hutambua kwamba fanaka haiji kwa kuwa na uwezo au vipawa vya pekee. Inahitaji udumifu wa kuendelea, azimio la kufanya mapenzi ya Yehova kikamili, na moyo mkuu mbele ya vizuizi vya muda, hata mshuko-moyo. Mradi wa kushiriki baraka za Mungu milele lazima uwekwe wazi akilini.

Ndiyo, sisi sote tutafutao kupata kibali cha Yehova na tutafutao kushinda katika mbio ya uzima twahitaji udumifu na uvumilivu. Bila sifa hizi, tungeweza kupoteza kibali cha Yehova na thawabu ya uhai ulio kwelikweli.—Zaburi 18:20; Mathayo 24:13; 1 Timotheo 6:18, 19.

Mara nyingi ni vigumu zaidi kwa Mkristo kuwa mwenye udumifu katika utendaji wake wa kiroho kuliko katika madaraka yake mengine. Mtu anaweza kuendelea kufanya kazi kwa bidii katika kazi ya kuajiriwa ili atunze mahitaji ya kimwili ya familia yake, lakini huenda akawa ‘mchovu mno’ kuongoza funzo la Biblia kwa ukawaida pamoja na mke na watoto wake. Ni mambo gani hufanya udumifu katika kazi za Kikristo uwe mgumu sana kwa wengi?

Jambo moja ni kuvunjika moyo, ambako huletwa na mapungukio yetu na udhaifu wetu wenyewe. Tukifikiria sana makosa yetu isivyofaa, twaweza kushindwa na kuacha, tukihisi kwamba Yehova hataweza kamwe kutusamehe makosa yetu yote.

Jambo jingine ni hali ya kilimwengu ya ukosefu wa adili, ufisadi, na chuki. (1 Yohana 2:15, 16) Moja ya “tabia njema” ambayo uvutano wa kilimwengu waweza kuharibu au kudhuru ni udumifu wa Kikristo.—1 Wakorintho 15:33.

Udumifu wetu katika kazi ya kuhubiri waweza kudhoofishwa na upinzani au ubaridi wa watu kuelekea utumishi wetu mtakatifu. Kwa kushindwa la kufanya, huenda tukafikia mkataa wa kwamba watu katika eneo letu hawataki kweli. Hili laweza kutufanya tuulize, ‘Kuna haja gani?’ na kuacha pendeleo letu la pekee la utumishi wa kihuduma.

Twaweza pia kuathiriwa na roho ya ulimwengu ya kujiendekeza. Kwa nini tujikakamue na kujidhabihu sana na huku wengine wote wanaonekana kuwa wakijifurahisha au kutokujikaza?—Linganisha Mathayo 16:23, 24.

Ili tudumu katika kufanya mapenzi ya Yehova, tunahitaji kuvaa utu wa Kikristo na kuishi kwa roho, wala si kwa mwili. (Warumi 8:4-8; Wakolosai 3:10, 12, 14) Kuwa na maoni ya Yehova juu ya mambo kutatusaidia kuendelea na utendaji wetu wa maana wa kiroho.—1 Wakorintho 16:13.

Vielelezo vya Udumifu

Yehova ametuandalia vielelezo vingi vyenye kuchochea vya watumishi waliobaki wakiwa waaminifu-washikamanifu na waaminifu kwake chini ya majaribu mengi magumu. Kwa kuwafikiria, twaona jinsi tuwezavyo kusitawisha na kudhihirisha udumifu wa Kikristo na kwa nini huo ni wa maana sana.

Kielelezo kikubwa zaidi ya vyote ni Yesu, aliyeteseka sana ili atukuze jina la Yehova. Biblia hututia moyo tujifunze kwa makini matendo yake ya ujitoaji mdumifu: “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha [“shangwe,” NW] iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba [“mti wa mateso,” NW] na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.”—Waebrania 12:1-3.

Mbio ya uhai ni ya mwendo mrefu, sio mbio kasi iliyo fupi. Ndiyo sababu twahitaji udumifu kama wa Kristo. Mradi, ule mstari wa kumalizia, huenda usionekane katika sehemu iliyo kubwa ya mbio hiyo. Mradi lazima uwe wazi akilini mwetu ili tuweze kuufuatia kiakili mwendo huu wote wenye kudai mno. Yesu alikuwa na picha kama hiyo mbele yake, yaani, “shangwe iliyowekwa mbele yake.”

Ni nini hutiwa ndani ya shangwe hii ya Wakristo leo? Kwanza, ni thawabu ya uhai usioweza kufa katika mbingu kwa wachache na uhai udumuo milele duniani kwa wengi. Pia, ni hisia ya uradhi iletwayo na kujua kwamba umefurahisha moyo wa Yehova na kuwa na sehemu katika utakaso wa jina la Mungu.—Mithali 27:11; Yohana 17:4.

Unaotiwa ndani ya shangwe hii ni uhusiano wa karibu, unaopendeza pamoja na Yehova. (Zaburi 40:8; Yohana 4:34) Uhusiano kama huo unaimarisha na kutegemeza uhai, ukimpa mtu nguvu za kukimbia mbio kwa uvumilivu na kutoacha. Zaidi ya hilo, Yehova hubariki uhusiano huo kwa kuwamwagia watumishi wake roho takatifu, tokeo likiwa shangwe na utendaji wenye shangwe ulioongezeka.—Warumi 12:11; Wagalatia 5:22.

Kufikiria kielelezo cha Ayubu cha imani-dumifu kunanufaisha. Alikuwa asiyekamilika naye alikuwa na ujuzi mdogo juu ya hali yake. Kwa hiyo mara kwa mara alikuwa na mwelekeo wa kujiona mwenye haki na kukosa tumaini. Hata hivyo, aliendelea bila kuacha kuonyesha azimio imara la kudumisha uaminifu-maadili kwa Yehova na kutomwacha Yeye kamwe. (Ayubu 1:20-22; 2:9, 10; 27:2-6) Yehova alimthawabisha Ayubu kwa ajili ya ujitoaji wake mdumifu, akimpa baraka za kiroho na za kimwili na tumaini la uhai udumuo milele. (Ayubu 42:10-17; Yakobo 5:10, 11) Kama Ayubu, huenda tukapatwa na mateseko mengi na kupoteza wakati mwingi wa maisha yetu ya sasa, lakini twaweza pia kuwa na hakika juu ya baraka za Yehova kuelekea uvumilivu wetu mwaminifu.—Waebrania 6:10-12.

Katika nyakati za kisasa, Mashahidi wa Yehova kwa ujumla wameonyesha udumifu wa Kikristo katika kufanya mapenzi ya Yehova. Kwa kielelezo, udumifu wao katika kazi ya nyumba kwa nyumba na mahubiri mengine ya hadharani umewafanya na kufanya ujumbe wao ujulikane ulimwenguni pote. Vyombo vya habari vimerejezea mara nyingi bidii na azimio lao la kuhubiri habari njema wajapopatwa na upinzani na majaribu. Moja la marejezo hayo hata lilikazia hivi “Hakuna mtu awezaye kuepuka Mashahidi wa Yehova!”—Mathayo 5:16.

Yehova amebariki jitihada dumifu za Mashahidi wake kwa matokeo yaliyoongezeka katika huduma. Ona maono ya Mashahidi wenye busara katika Italia huko nyuma katika miaka ya 1960 kulipokuwa na Mashahidi 10,000 wakihubiri kwa taifa la watu zaidi ya 53,000,000. Katika mji mmoja wa wakaaji 6,000, hakukuwa na Mashahidi. Ndugu wenye kuwatembelea walipata uhasama kuelekea huduma yao.

Kila wakati ndugu walipoenda huko kuhubiri, wanawake wengi, na hata wanaume, wa mji huo wangekusanya wavulana, na kuwatia moyo wafuate Mashahidi wakiwapigia mbinja na kufanya kelele nyingi. Baada ya dakika chache, ndugu walilazimika kuondoka na kwenda mji mwingine. Katika jitihada za kutoa angaa ushahidi kikamilifu kwa wakaaji wote wa mji huo, ndugu waliamua kuhubiri huko siku za mvua nyingi pekee, wakitumaini kwamba hawangesumbuliwa na wavulana hao. Waligundua kwamba watu wa mji huo hawakutaka kujilowesha ili tu wawasumbue wahubiri hao. Kwa njia hii ushahidi mzuri ulitolewa. Watu wenye kupendezwa walipatikana. Mafunzo mapya ya Biblia yalianzishwa. Kama tokeo, kutaniko lenye kukua lilianzishwa katika mji huo mdogo na kazi ya kuhubiri ikaanza kufanywa hata siku za jua. Yehova ameendelea kubariki udumifu wa Mashahidi wake katika eneo hilo na katika Italia yote. Sasa kuna Mashahidi wa Yehova zaidi ya 200,000 katika nchi hiyo.

Thawabu za udumifu katika kufanya yaliyo mema ni nyingi sana. Kwa uwezo wa roho ya Mungu, Mashahidi wa Yehova wameweza kukamilisha tendo lisilo na kifani katika historia ya kibinadamu, lile la kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa mamilioni ya watu milangoni na penginepo. (Zekaria 4:6) Kwa shangwe wameona unabii wa Biblia ukitimizwa katika ukuzi wa ajabu na kuendelea kwa tengenezo la Yehova la kidunia. (Isaya 54:2; 60:22) Wao wana dhamiri safi kuelekea Mungu, nao wanafurahia tumaini la uhai udumuo milele. Zaidi ya yote, wao wana uhusiano wa ndani pamoja na Muumba, Yehova Mungu.—Zaburi 11:7.

[Picha katika ukurasa wa25]

Yesu alithawabisha udumifu mnyenyekevu wa mwanamke huyu Mgiriki

[Picha katika ukurasa wa26]

Uhai katika Paradiso unatiwa ndani ya shangwe iliyowekwa mbele ya Wakristo leo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki