Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 9/15 kur. 20-23
  • Familia za Kimungu za Wakati Uliopita—Kigezo cha Siku Zetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Familia za Kimungu za Wakati Uliopita—Kigezo cha Siku Zetu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ukichwa—Jambo Gumu?
  • Kuchukua Hatua ya Mara Moja
  • Agizo la Kibaba Chini ya Sheria ya Kimusa
  • Mama na Watoto Katika Jamii ya Kiyahudi
  • Kigezo cha Leo
  • Mpango wa Yehova wa Familia Wenye Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kutumia Neno la Mungu Katika Jamaa Zetu Wenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Jitahidi kwa Ajili ya Wokovu wa Nyumba Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kufanikisha Maisha ya Jamaa
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 9/15 kur. 20-23

Familia za Kimungu za Wakati Uliopita—Kigezo cha Siku Zetu

FAMILIA—Umoja wa Mataifa ulijaribu kuielekezea fikira ya ulimwengu. Jinsi gani? Kwa kutangaza 1994 kuwa “Mwaka wa Familia wa Kimataifa.” Ingawa viongozi wa ulimwengu, wanasosholojia, na washauri wa familia wameharakisha kuombolezea mambo kama vile kuongezeka kwa watoto haramu na kuongezeka kwa talaka, wameshindwa kupata suluhisho halisi lenye kutumika la matatizo kama hayo.

Je, inawezekana kwamba Biblia ina suluhisho la matatizo ya familia? Kwa watu fulani huenda likaonekana kuwa jambo la upumbavu kudokeza kwamba Biblia yaweza kuwa yenye msaada kwa familia za leo. Kwani, iliandikwa karne nyingi zilizopita katika hali na desturi ya Mashariki ya Kati. Katika sehemu nyingi za ulimwengu, maisha yamebadilika sana tangu nyakati za Biblia. Hata hivyo, Biblia ilipuliziwa na Yehova Mungu, ambaye kwake kila familia hupata jina layo. (Waefeso 3:14, 15; 2 Timotheo 3:16) Biblia inasema nini juu ya matatizo ya familia?

Yehova anajua vizuri sana kinachohitajiwa ili kufanya maisha ya familia yawe yenye furaha na yenye uradhi. Hivyo, Neno lake, Biblia, lina mengi ya kusema juu ya maisha ya familia, mengine yakiwa namna ya onyo la upole. Biblia pia ina vielelezo vya familia ambazo zilitumia kanuni za Biblia. Tokeo likawa kwamba walifurahia ukaribu na uradhi mwingi. Ebu tuchunguze maisha ya familia katika nyakati za Biblia na tuone ni masomo gani yanayoweza kupatikana.

Ukichwa—Jambo Gumu?

Kwa mfano, fikiria habari ya ukichwa wa familia. Katika nyakati za wazee wa ukoo, wanaume kama vile Abrahamu, Isaka, na Yakobo walikuwa “vichwa vya familia,” bila kupingwa. (Matendo 7:8, 9, NW; Waebrania 7:4) The New Manners and Customs of Bible Times, cha Ralph Gower, chasema: “Familia ilikuwa . . . ‘ufalme mdogo’ uliotawalwa na baba. Alitawala juu ya mke, watoto, wajukuu, na watumishi—kila mmoja katika nyumba hiyo.” Kwa kweli wazee wa ukoo mara nyingi walikuwa na mamlaka juu ya familia za wana wao vilevile.—Linganisha Mwanzo 42:37.

Je, hilo halikuwapa wanaume haki ya kuonea wake zao na watoto wao? Hasha. Ni kweli, Mungu alimwambia mwanamke wa kwanza, Hawa hivi: “Tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.” (Mwanzo 3:16) Maneno hayo yalionyesha jinsi wanawake walioolewa wangeishi kwa ujumla, lakini hayakuonyesha jinsi mambo yangekuwa miongoni mwa waabudu wa kweli wa Mungu. Waume wenye kumhofu Mungu walipaswa kukumbuka kusudi la Yehova la awali. Yehova alimuumba mwanamke awe ‘msaidizi wa kufanana na mume,’ bali si mtumwa wake. (Mwanzo 2:20) Kwa sababu wanaume wenye kumcha Mungu wa nyakati za mapema walitambua ujitiisho na wajibu wao wenyewe kwa Mungu, hawakutumia vibaya mamlaka yao. Mbali na kutendea wake zao na watoto wao kama watumwa, wazee wa ukoo wenye kumhofu Mungu waliwaonyesha upendo na shauku ya kweli.

Mtazamo mdogo wa shauku ambayo watoto kwa kawaida walipokea unaonyeshwa kwenye Mwanzo 50:23. Hapo inasema hivi juu ya vitukuu wa Yusufu: “Walizaliwa magotini mwa Yusufu.” Ingawa jambo hilo lingemaanisha kwamba Yusufu alitambua watoto kuwa wa ukoo wake, lingeweza pia kuonyesha kwamba alicheza nao kwa shauku nyingi, akiwachezesha kati ya magoti yake. Kina baba leo wanafanya vema kuonyesha watoto wao shauku kama hiyo.

Wakiwa vichwa vya familia, wazee wa ukoo wenye kumhofu Mungu pia walitunza mahitaji ya kiroho ya familia zao. Baada ya kutoka kwenye safina baada ya Gharika ya ulimwenguni pote, ‘Nuhu akamjengea BWANA madhabahu; akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.’ (Mwanzo 8:20; linganisha Ayubu 1:5.) Abrahamu mzee wa ukoo aliye mwaminifu aliweka kielelezo kizuri kwa kuwapa washiriki wa familia mwongozo wa kibinafsi. Yeye ‘aliwaamuru wanawe, na nyumba yake baada yake waishike njia ya BWANA, wafanye haki na hukumu.’ (Mwanzo 18:19) Hivyo, ukichwa wenye upendo ulichangia hali njema ya hisia-moyo na ya kiroho ya familia mbalimbali.

Wanaume Wakristo leo hufuata kigezo hicho. Wao huonyesha ukichwa katika mambo ya ibada kwa kusaidia familia zao kuishi kulingana na matakwa ya Mungu na kuweka kielelezo kizuri wao wenyewe. (Mathayo 28:19, 20; Waebrania 10:24, 25) Kama vile wazee wa ukoo, waume na baba Wakristo pia wanachukua nafasi kutoa mwongozo wa kibinafsi kwa washiriki wa familia zao.

Kuchukua Hatua ya Mara Moja

Hatimaye alipomaliza kumlipa baba-mkwe wake deni kubwa, mzee wa ukoo Yakobo aliuliza: “Nitaangalia lini mambo ya nyumba yangu mwenyewe?” (Mwanzo 30:30) Kama vile baba wengine wote, Yakobo alihisi mkazo wa kugharimia mahitaji ya kimwili ya familia yake, naye alifanya bidii kutimiza hilo. Mwanzo 30:43 lasema hivi: “Mtu huyo akazidi mno, akawa na wanyama wengi, na vijakazi, na watumwa, na ngamia, na punda.”

Hata hivyo, miaka kadhaa baadaye, baada ya Yakobo kuhamia nchi ya Kanaani, yaonekana hakujua kwamba binti yake Dina alikuwa ameanza tabia iliyokuwa hatari ya kushirikiana na Wakanaani wapagani.a (Mwanzo 34:1) Pia alikosa kuchukua hatua alipojua kwamba kulikuwa na vinyago vya kidini nyumbani mwake. Hata hivyo, baada ya msiba wa kulalwa kinguvu kwa Dina na Mkanaani, Yakobo akachukua hatua ya mara moja. “Ondoeni miungu migeni iliyoko kwenu, mjisafishe,” akaagiza.—Mwanzo 35:2-4.

Ni lazima baba Wakristo wawe waangalifu kuhusu hali ya kiroho ya familia zao. Ikiwa kuna matisho makali kwa hali-njema ya kiroho ya familia, kama vile kuwapo kwa fasihi zisizo za adili au muziki wenye kuvunja heshima nyumbani, ni lazima wachukue hatua ya mara moja.

Kwa kupendeza, wanawake wenye imani kama Sara, Rebeka, na Raheli pia walionyesha uvutano kama huo katika familia. Ingawa walikuwa wanyenyekevu kwa waume zao, hawakuzuiwa kuchukua hatua ya kwanza ilipofaa na kuhitajiwa. Kwa mfano, Kutoka 4:24-26 hutuambia kwamba Musa na familia yake walipokuwa wakienda Misri, “BWANA [“malaika wa Yehova,” Septuagint] akakutana naye akataka kumwua [mwana wa Musa].” Inaonekana kwamba mwana wa Musa alikuwa kwenye hatari ya kuuawa kwa sababu Musa hakuwa amemtahiri. Sipora alichukua hatua ya haraka na kumtahiri mwanaye. Basi, malaika akamwacha aende zake. Wanawake Wakristo leo pia waweza kuchukua hatua ya kwanza ifaapo.

Agizo la Kibaba Chini ya Sheria ya Kimusa

Katika 1513 K.W.K., kipindi cha wazee wa ukoo kilikwisha Israeli lilipokuja kuwa taifa. (Kutoka 24:3-8) Baba waliendelea kutumika wakiwa vichwa vya familia. Hata hivyo, sheria ya familia ikawa chini ya Sheria ya taifa iliyotolewa na Mungu kwa Musa na kutekelezwa na waamuzi waliowekwa rasmi. (Kutoka 18:13-26) Ukuhani wa Kilawi ukachukua mahali pa mambo ya ibada ya kutoa dhabihu. Na bado, baba aliendelea kuwa na fungu la maana. Musa alisihi hivi: “Maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.”—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.

Sheria iliandaa pindi kama vile Sikukuu ya Kupitwa, ambapo mwongozo ungetolewa kirasmi na kwa njia zisizo rasmi. Tarehe ya Sikukuu ya Kupitwa, Nisani 14, ilipofika, familia za Kiyahudi zingeanza kujitayarisha kwa ajili ya safari yao ya kwenda Yerusalemu. (Kumbukumbu 16:16; linganisha Luka 2:41.) Ni mtoto yupi angekosa kusisimukia matayarisho hayo? Safari yenyewe ingependeza. Kufikia wakati huo msimu wa mvua ulikuwa umekwisha, na jua lilianza kuondoa baridi ya kipupwe hewani. Barafu za Mlima Harmoni zilipoyeyuka, Mto Yordani ungefurika fuo zake.

Njiani, baba wangefundisha watoto wao jiografia ya nchi na pia historia nyingi zinazohusu sehemu ambazo wangepitia. Hizo huenda zilitia ndani Milima Ebali na Gerizimu, ambapo laana na baraka za Sheria zilisomwa. Huenda pia wangepitia Betheli, ambapo Yakobo alipata ono la ngazi ya kimbingu. Hayo yangekuwa mazungumzo yenye kusisimua kama nini! Walipoendelea na safari na vikundi vya familia vikiungana na wasafiri kutoka sehemu nyingine za nchi, wote walifurahia ushirika wenye kujenga.

Mwishowe familia ingeingia Yerusalemu, “ukamilifu wa uzuri.” (Zaburi 50:2) Asema msomi Alfred Edersheim: “Wengi wa wapilgrimu hawa lazima wawe walipiga kambi nje ya kuta za jiji hilo. Wale waliokaa ndani ya jiji walipewa mahali pa kulala bila malipo.” Ndiyo, vijana Waebrania walipata somo la kujionea wenyewe upendo na ukaribishaji wa kidugu. Mikusanyiko ya Mashahidi wa Yehova ya kila mwaka inatumikia kusudi lilo hilo leo.

Mwishowe Nisani 14 ingefika. Mnyama wa Sikukuu ya Kupitwa angechinjwa na kuchomwa kwa muda wa saa kadhaa. Karibu na katikati ya usiku familia hiyo ingekula nyama ya kondoo huyo, mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu. Kulingana na desturi mtoto wa kiume angeuliza hivi: “N’nini maana yake utumishi huu kwenu?” Basi baba wangefundisha kirasmi, wakisema: “Ni dhabihu ya pasaka ya BWANA, kwa kuwa alipita juu ya nyumba za wana wa Israeli huko Misri, hapo alipowapiga Wamisri, akaziokoa nyumba zetu.”—Kutoka 12:26, 27; 13:8.

Mfalme Sulemani wa Israeli alisema: ‘Kuna wakati wa kucheka na wakati wa kucheza.’ (Mhubiri 3:4) Watoto Waisraeli walipewa nafasi ya tafrija. Ni dhahiri kwamba Yesu Kristo alitazama watoto wakicheza sokoni. (Zekaria 8:5; Mathayo 11:16) Na ilikuwa kawaida kwa wazazi wa hali ya chini kufanya mpango familia ikutane kwenye vikusanyiko vya kufurahisha vilivyokuwa na nyimbo, kucheza dansi, na mlo. (Luka 15:25) Vilevile wazazi Wakristo leo huchukua hatua ya kwanza katika kuandaa tafrija na ushirika wenye kujenga kwa ajili ya watoto wao.

Mama na Watoto Katika Jamii ya Kiyahudi

Mama walikuwa na fungu gani chini ya Sheria ya Kimusa? Mithali 1:8 liliamuru hivi: “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako.” Chini ya mwongozo wa mamlaka ya mumeye, mke Myahudi angetumia matakwa aliyopewa na Mungu katika maisha ya familia. Iliwapasa watoto wake wamheshimu, hata alipozeeka.—Mithali 23:22.

Mama pia alikuwa na fungu kubwa katika kuzoeza watoto wake. Alitunza kitoto karibu peke yake hadi kilipokuwa kikubwa vya kutosha kuachishwa kunyonya, bila shaka ikitokeza muungano wenye uhusiano wa karibu wa mama na mtoto. (Isaya 49:15) Baba walipokuwa wakifundisha wana wao ustadi fulani, mama walifundisha binti zao ustadi wa kinyumbani. Mama pia walikuwa na uvutano mkubwa kwa wana wao. Kwa kielelezo, mfalme Lemueli alinufaika na “mausia aliyofundishwa na mama yake.”—Mithali 31:1.

Mke Myahudi mwenye uwezo pia alifurahia uhuru mwingi wa ‘kuangalia njia za watu wa nyumbani mwake.’ Kulingana na Mithali 31:10-31, huenda akanunua vitu vya nyumbani, akanunua nyumba, na hata kusimamia biashara ndogo. Kwa mume mwenye uthamini, thamani ya mke huyo ‘ilipita kima cha marijani’!

Kigezo cha Leo

Katika nyakati za Biblia mpango wa familia ulitumika katika ukuzi wa hisia-moyo na hali ya kiroho ya washiriki wote. Baba walikuwa watumie mamlaka yao kwa upendo ili kufaidi familia zao. Walipaswa waongoze katika ibada. Baba na mama pia walionyesha kupendezwa na watoto wao—wakiwafundisha na kuwazoeza, wakiabudu pamoja nao, na kuwaandalia tafrija. Mama wenye kumcha Mungu walithibitika kuwa wasaidizi wa maana, kwa kuheshimu ukichwa wa waume zao huku wakichukua hatua ya kwanza kwa niaba ya familia zao. Watoto watiifu waliletea wazazi wao na Yehova Mungu shangwe. Kwa kweli, familia yenye kumhofu Mungu ya nyakati za Biblia ilikuwa kigezo kizuri sana cha siku zetu.

[Maelezo ya Chini]

a Yafaa kuona kwamba kabla ya hilo, Yakobo alikuwa amechukua hatua thabiti ya kulinda familia yake kutoka kwenye uvutano wa Wakanaani. Alijenga madhabahu, bila shaka ya muundo uliofanya awe tofauti na majirani wake Wakanaani. (Mwanzo 33:20; Kutoka 20:24, 25) Zaidi ya hayo, alipiga hema lake nje ya mji wa Shekemu naye akawa na chanzo chake mwenyewe cha maji. (Mwanzo 33:18; Yohana 4:6, 12) Hivyo Dina angaliweza kujua vizuri sana juu ya tamaa ya Yakobo kwamba asishirikiane na Wakanaani.

[Picha katika ukurasa wa23]

Familia yako yaweza kuwa yenye furaha kama zile familia zilizomwabudu Yehova katika nyakati za Biblia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki