Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 4/15 kur. 3-4
  • Matukio Yenye Kuongezeka ya Habari Mbaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matukio Yenye Kuongezeka ya Habari Mbaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Nyingi Katika Historia Yote
  • Ongezeko Katika Miaka ya Majuzi
  • Kuna Habari Njema Mbele!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • ‘Habari Njema Zenye Utukufu Kutoka kwa Mungu Aliye na Furaha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • “Habari Njema”!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Habari Njema kwa Wanadamu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 4/15 kur. 3-4

Matukio Yenye Kuongezeka ya Habari Mbaya

JE, UMEPATA kugundua kwamba vichwa vikuu vinavyotangaza habari mbaya huamsha upendezi mwingi zaidi wa wasomaji kuliko vile vinavyotoa habari njema? Iwe ni kichwa kikuu cha gazeti la habari cha msiba wa asili au porojo yenye kupendeza sana iliyoonyeshwa kwa maandishi makubwa kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti lenye kuvutia, yaonekana kwamba habari mbaya huuza vichapo vingi zaidi kuliko habari njema.

Leo hakuna uhaba wa habari mbaya. Lakini nyakati fulani mtu hujiuliza ikiwa maripota na waandishi wanazoezwa kutafuta na kutokeza habari mbaya—wakiacha kando habari zozote njema.

Nyingi Katika Historia Yote

Kwa kweli, habari mbaya zimekuwa nyingi katika karne zote, zikishinda habari zozote njema. Katika rekodi za kihistoria, mizani zimelala sana upande wa kuteseka kwa wanadamu, mafadhaiko, na kukata tamaa, ambako kumekuwa sehemu ya maisha ya wanadamu.

Ebu tufikirie vielelezo vichache tu. Kitabu Chronicle of the World, kilichotungwa na Jacques Legrand, hutoa masimulizi kadhaa, kila simulizi likiwa limeandikwa kwa tarehe hususa ambayo tukio lilitendeka lakini kana kwamba lilikuwa likielezwa na mwandishi wa habari wa kisasa akiripoti tukio hilo. Kutokana na ripoti hizi zilizofanyiwa utafiti mzuri, twaona kwa njia yenye manufaa kuenea kwa habari mbaya ambazo mwanadamu amesikia katika kuwapo kwake kote kulikojaa taabu hapa kwenye sayari Dunia.

Kwanza, fikiria ripoti hii ya mapema kutoka Ugiriki katika 429 K.W.K. Inaripoti juu ya vita iliyokuwa ikipiganwa wakati huo kati ya Athene na Sparta: “Jiji lenye kujitawala la Potidaea limelazimika kusalimu amri kwa Waathene wenye kulizingira baada ya kukumbwa na njaa hivi kwamba watu walo wamekuwa wakila miili ya wafu wao.” Habari mbaya kwelikweli!

Tukisonga mbele kwenye karne ya kwanza kabla ya Wakati wa Kawaida wetu, twapata ripoti iliyofafanuliwa wazi ya kifo cha Kaisari Yuliasi, yenye tarehe Roma, Machi 15, 44 W.K. “Kaisari Yuliasi ameuawa kihila. Yeye aliuawa kwa kudungwa kisu na kikundi cha wahaini, wengine wao wakiwa marafiki wake wa karibu zaidi, alipokuwa akiketi Bungeni leo, tarehe 15, Machi.”

Katika karne zilizofuata, habari mbaya ziliendelea kuongezeka. Kielelezo kimoja chenye kushtua ni habari hizi kutoka Mexico katika 1487: “Katika wonyesho wenye kutazamisha zaidi uliopata kuonwa katika jiji kuu la Aztec, Tenochtitlan, mioyo ya watu 20,000 ilitolewa dhabihu kwa Huitzilopochtli, mungu wa vita.”

Ukatili wa mwanadamu haujatoa tu habari mbaya bali uzembe wake umeongezwa katika orodha ndefu ya matukio yaletayo habari mbaya. Moto mkubwa wa London yaonekana ulikuwa msiba mmoja kama huo. Ripoti kutoka London, Uingereza, yenye tarehe Septemba 5, 1666, yasomeka hivi: “Hatimaye, baada ya siku nne mchana na usiku, moto wa London umesimamishwa na Dyuki wa York, ambaye alileta vikundi vya meli za kivita vyenye baruti ili kulipua majengo yaliyokuwa njiani mwa miale ya moto. Hektare zipatazo 160 zimeharibiwa kabisa pamoja na makanisa 87 na zaidi ya nyumba 13,000. Kimuujiza, ni watu tisa tu waliokufa.”

Katika vielelezo hivi vya habari mbaya lazima tuongeze maradhi yenye kuenea sana ambayo yameenea bila kudhibitiwa kotekote katika kontinenti nyingi—kwa kielelezo, maradhi yenye kuenea ya kipindupindu ya mapema katika miaka ya 1830. Kichwa kilichochapishwa kilichoripoti hilo chasomeka: “Madhila ya kipindupindu yahangaisha Ulaya.” Ripoti yenye uhalisi ifuatayo yaonyesha habari mbaya katika hali mbaya zaidi yenye kutisha: “Kipindupindu, ambacho hakikujulikana katika Ulaya hadi 1817, kinaenea kuelekea magharibi kutoka Asia. Tayari idadi za watu katika majiji ya Urusi kama vile Moscow na St. Petersburg zimepunguzwa kwa kifo—wengi wa majeruhi wakiwa maskini wa majijini.”

Ongezeko Katika Miaka ya Majuzi

Kwa hiyo ingawa ni kweli kwamba habari mbaya zimekuwa uhalisi wa maisha katika rekodi yote ya historia, miongo ya majuzi ya karne ya 20 hutoa uthibitisho kwamba habari mbaya zinaongezeka, kwa hakika zinaongezeka kwa haraka.

Hakuna shaka kwamba habari za vita zimekuwa aina mbaya kupita zote ya habari mbaya ambazo zimesikiwa katika karne yetu ya sasa. Vita viwili vikuu zaidi katika historia—vikiitwa kwa kufaa Vita ya Ulimwengu 1 na Vita ya Ulimwengu 2—vilikuwa na ripoti za habari mbaya kwa kiwango chenye kuogofya. Lakini hilo limekuwa kiasi kidogo tu cha habari mbaya ambazo zimetolewa na karne hii isiyo na furaha.

Fikiria vichwa vikuu vichache tu vilivyochaguliwa hapa na pale:

Septemba 1, 1923: Tetemeko laharibu Tokyo Vibaya—300,000 wafa; Septemba 20, 1931: Tatizo—Uingereza yapunguza thamani ya pauni; Juni 25, 1950: Korea Kaskazini yaingilia kivita Korea Kusini; Oktoba 26, 1956: Wahungaria waasi dhidi ya utawala wa Sovieti; Novemba 22, 1963: John Kennedy auawa kwa kupigwa risasi Dallas; Agosti 21, 1968: Vifaru vya Urusi vyawasili kuvunja-vunja waasi wa Prague; Septemba 12, 1970: Ndege zilizotekwa nyara zalipuliwa jangwani; Desemba 25, 1974: Kimbunga Tracy chatandaza jiji la Darwin—66 wafa; Aprili 17, 1975: Kambodia yashindwa na majeshi ya Kikomunisti; Novemba 18, 1978: Ujiuaji wa kimakusudi wa watu wengi katika Guyana; Oktoba 31, 1984: Bi. Gandhi auawa kwa kupigwa risasi; Januari 28, 1986: Chombo cha angani chalipuka kinapoanza kuondoka; Aprili 26, 1986: Kitendanishio cha Sovieti chashika moto; Oktoba 19, 1987: Soko la hisa laporomoka; Machi 25, 1989: Alaska yaathiriwa vibaya na mmwagiko wa mafuta ghafi; Juni 4, 1989: Majeshi yachinja waandamanaji katika Uwanja wa Tiananmen.

Ndiyo, historia yaonyesha kwamba sikuzote habari mbaya zimekuwa nyingi, huku habari njema zikiwa chache kwa kulinganishwa. Kadiri ambavyo habari mbaya zimezidi katika miongo ya majuzi, ndivyo habari njema zimedidimia kila mwaka ukipita.

Kwa nini iwe hivyo? Je, sikuzote itakuwa hivyo?

Makala ifuatayo itashughulikia maswali haya mawili.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

WHO/Shirika la Msalaba Mwekundu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki