Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 2/1 kur. 4-7
  • Kuwekwa Huru na Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuwekwa Huru na Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uhuru Kutoka Katika Hali ya Kuwahofu Wafu
  • Uhuru Kutoka Katika Hali ya Kuhofu Wakati Ujao
  • Uhuru Kutoka Katika Hali ya Kumhofu Mwanadamu
  • Waweza Kuwekwa Huru na Kweli
  • “Kweli Itawaweka Ninyi Huru”—Jinsi Gani?
    Amkeni!—2012
  • Kweli Kuhusu Nafsi Ni Jambo la Maana
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
  • “Kifo Kimemezwa Milele”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Wapendwa Wako Waliokufa—Je! Utawaona Tena?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 2/1 kur. 4-7

Kuwekwa Huru na Kweli

KATIKA Marekani, watu zaidi ya milioni moja wamefungwa magerezani. Miongoni mwao, karibu elfu tatu wamehukumiwa kifo. Ebu jiwazie ukiwa katika hali hiyo. Ungehisije? Wazo la kuwa na tazamio hilo lahofisha kwelikweli. Hata hivyo, kwa maana fulani, wanadamu wote wamo katika hali hiyohiyo. Biblia husema hivi: “Wote wamefanya dhambi na hupungukiwa na utukufu wa Mungu.” (Waroma 3:23) Ndiyo, tukiwa wazao wa Adamu, hali yenye dhambi ‘imetufunga gerezani.’ (Waroma 5:12) Kila siku twahisi matokeo ya kufungwa kwetu, sawa na alivyohisi yule mtume Mkristo Paulo, aliyeandika hivi: “Naona katika viungo vyangu sheria nyingine ikifanya vita dhidi ya sheria ya akili yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu.”—Waroma 7:23.

Kwa sababu ya asili yetu yenye dhambi, kila mmoja wetu yuko chini ya hukumu ya kifo, kwa kusema kitamathali, kwa maana Biblia hutaarifu hivi: “Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo.” (Waroma 6:23) Mtunga-zaburi Musa alifafanua hali yetu vizuri hivi: “Tuna miaka sabini tu—miaka themanini, ikiwa sisi ni wenye nguvu; hata hivyo inatuletea usumbufu na majonzi tu; uhai unaisha upesi, nasi tunatoweka.”—Zaburi 90:10, Today’s English Version; linganisha Yakobo 4:14.

Yesu alikuwa akifikiria utumwa wa wanadamu katika dhambi na kifo alipowaambia wafuasi wake hivi: “Kweli itawaweka nyinyi huru.” (Yohana 8:32) Kwa maneno hayo, Yesu alikuwa akiwapa wafuasi wake tumaini la jambo kubwa kuliko uhuru kutoka katika utawala wa Kiroma—alikuwa akiwatolea msamaha wa dhambi na ondoleo katika kifo! Wangepewaje hali hiyo? “Mwana akiwaweka nyinyi huru,” Yesu akawaambia, “mtakuwa huru kikweli.” (Yohana 8:36) Ndiyo, kwa kutoa uhai wake, “Mwana,” Yesu, alikuwa dhabihu ya kufunika ili kununua tena alichopoteza Adamu. (1 Yohana 4:10) Hilo liliwafungulia wanadamu watiifu wote njia ya kuondolewa katika utumwa wa dhambi na kifo. Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu alikufa “ili kila mtu anayedhihirisha imani katika yeye asipate kuangamizwa bali awe na uhai udumuo milele.”—Yohana 3:16.

Kwa hiyo, kweli iwezayo kutuweka huru yamkazia fikira Yesu Kristo. Wale wanaokuwa wafuasi wafuatao hatua zake za miguu wana tumaini la kuwekwa huru kutoka katika dhambi na kifo Ufalme wa Mungu uanzapo kudhibiti kikamili mambo ya dunia. Hata sasa, wale wanaoikubali kweli ya Neno la Mungu hupata uhuru wa kweli. Katika njia zipi?

Uhuru Kutoka Katika Hali ya Kuwahofu Wafu

Mamilioni leo huishi katika hali ya kuwahofu wafu. Kwa nini? Kwa sababu dini zao zimewafundisha kwamba nafsi huuacha mwili wakati wa kifo na kwenda kwenye makao ya kiroho. Hiyo ndiyo sababu, ni jambo la kidesturi katika nchi fulani kwa jamaa za mfu kukesha siku kadhaa mchana na usiku. Mara nyingi hilo latia ndani kuimba kwa sauti kubwa na upigaji wa ngoma. Waombolezi huamini kwamba hilo litampendeza mfu na kuizuia roho yake isirudi kuwazuru mara nyingi. Mafundisho yasiyo ya kweli ya Jumuiya ya Wakristo kuhusu wafu yamesaidia tu kuendeleza mapokeo hayo.

Hata hivyo, Biblia hufunua kweli kuhusu hali ya wafu. Hiyo hutaarifu kwa wazi kwamba nafsi yako ndiyo wewe, si sehemu yako fulani ya kifumbo inayoishi baada ya kifo. (Mwanzo 2:7; Ezekieli 18:4) Zaidi ya hayo, wafu hawateswi katika helo yenye moto, wala wao si sehemu ya makao ya roho iwezayo kuwaathiri walio hai. “Wafu,” Biblia husema, “hawajui neno lo lote . . . hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu [kaburini] uendako wewe.”—Mhubiri 9:5, 10.

Kweli hizo za Biblia zimewaweka watu wengi huru kutoka katika hali ya kuwahofu wafu. Hawatoi tena dhabihu zenye gharama ya juu ili kuwaridhisha wazazi wao wa kale waliokufa, wala hawana wasiwasi kwamba wapendwa wao wanateswa bila huruma kwa ajili ya dhambi zao. Wamejifunza kwamba Biblia huwatolea tumaini la ajabu wale ambao wamekufa, kwa kuwa hiyo hutuambia kwamba kwa wakati uliowekwa na Mungu, kutakuwa na “ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.” (Matendo 24:15; Yohana 5:28, 29) Hivyo, sasa wafu wanapumzika tu, kana kwamba wamo katika usingizi mzito.—Linganisha Yohana 11:11-14.

Ukweli kuhusu hali ya wafu na tumaini la ufufuo waweza kutuweka huru kutoka katika hali ya kukata tumaini iwezayo kuletwa na kifo. Tumaini hilo lilitegemeza wenzi wa ndoa katika Marekani wakati mwana wao mwenye umri wa miaka minne alipokufa katika aksidenti. “Kuna utupu maishani mwetu usioweza kujazwa hadi tutakapomwona mwana wetu tena kupitia ufufuo,” akiri mamaye. “Lakini twajua kwamba umivu letu ni la muda tu, kwa kuwa Yehova aahidi kufutilia mbali machozi yetu ya majonzi.”—Ufunuo 21:3, 4.

Uhuru Kutoka Katika Hali ya Kuhofu Wakati Ujao

Wakati ujao una nini? Je, dunia yetu itachomeka katika maangamizi makubwa ya nyuklia? Uangamizo wa mazingira ya dunia utafanya sayari yetu isikalike? Je, mvunjiko wa adili utaongoza kwenye ukosefu wa utaratibu na machafuko? Hizo ni hali halisi ambazo huhofiwa na watu wengi leo.

Hata hivyo, Biblia hutoa uhuru kutoka katika hali hizo mbaya zinazohofiwa. Biblia hutuhakikishia kwamba “dunia hudumu daima.” (Mhubiri 1:4) Yehova hakuumba sayari yetu ili tu aione ikiharibiwa na wanadamu wasiojali madaraka. (Isaya 45:18) Badala ya hivyo, Yehova aliiumba dunia iwe makao ya paradiso kwa familia ya kibinadamu yenye muungano. (Mwanzo 1:27, 28) Kusudi lake halikubadilika. Biblia hutuambia kwamba Mungu “[ata]waleta kwenye uangamizi wale wanaoiangamiza dunia.” (Ufunuo 11:18) Baada ya kufanya hivyo, “wenye upole watairithi nchi,” Biblia husema, “watajifurahisha kwa wingi wa amani.”—Zaburi 37:11.

Ahadi hiyo ni yenye kutumainika, kwa maana Mungu hasemi uwongo. Yehova alitaarifu hivi kupitia nabii wake Isaya: “Neno langu, litokalo katika kinywa changu . . . halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.” (Isaya 55:11; Tito 1:2) Kwa hiyo, twaweza kutazamia kwa uhakika utimizo wa ahadi ya Mungu iliyorekodiwa katika Biblia kwenye 2 Petro 3:13: “Ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizo uadilifu utakaa.”

Uhuru Kutoka Katika Hali ya Kumhofu Mwanadamu

Biblia hutuandalia vielelezo vyema vya wanaume na wanawake walioonyesha hali ya kutohofu katika ujitoaji wao kwa Mungu. Miongoni mwao walikuwa Gideoni, Baraka, Debora, Danieli, Esta, Yeremia, Abigaili, na Yaeli—kwa kutaja wachache tu. Wanaume na wanawake hao waaminifu walidhihirisha mtazamo wa mtunga-zaburi aliyeandika hivi: “Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; mwanadamu atanitenda nini?”—Zaburi 56:11.

Katika karne ya kwanza, mitume Petro na Yohana walidhihirisha ujasiri uo huo wakati wenye mamlaka ya kidini walipowaamuru waache kuhubiri. “Kwa habari yetu,” wakajibu, “sisi hatuwezi kukoma kusema juu ya mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.” Kwa sababu ya msimamo wao imara, Petro na Yohana walifungwa gerezani baadaye. Baada ya kuachiliwa kwao kimuujiza, walirudia utendaji wao, wakaendelea “[ku]sema neno la Mungu kwa ujasiri.” Upesi Petro na wale mitume wengine wakaletwa mbele ya Sanhedrini ya Kiyahudi. “Tuliwaagiza hakika nyinyi msifulize kufundisha juu ya msingi wa jina hili,” kuhani wa cheo cha juu akawaambia, “na bado, tazameni! mmejaza Yerusalemu fundisho lenu.” Petro na wale mitume wengine wakajibu: “Lazima sisi tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”—Matendo 4:16, 17, 19, 20, 31; 5:18-20, 27-29.

Katika kazi yao ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu, Mashahidi wa Yehova leo hujitahidi kuiga ile bidii ya Wakristo wa karne ya kwanza. Mara nyingi hata vijana miongoni mwao hujithibitisha kuwa wasio na hofu kwa kusema na wengine juu ya imani yao. Fikiria baadhi ya vielezi.

Stacie, aliye tineja, ni mwenye kuona haya kiasili. Kwa sababu hiyo, kuzungumza na wengine kuhusu imani yake kulikuwa jambo gumu mwanzoni. Alifanya nini ili kushinda hali yake ya kuona haya? “Nilijifunza Biblia, nikahakikisha kwamba nilielewa yale niliyokuwa nikizungumza,” asema. “Hilo lilifanya liwe rahisi zaidi, nikawa na hali ya kujiamini zaidi.” Sifa nzuri ya Stacie iliripotiwa katika gazeti la habari la mahali hapo. Makala hiyo, iliyoandikwa na mwalimu fulani shuleni mwake, ilieleza hivi: “Imani ya [Stacie] yaonekana imempa nguvu za kupigana dhidi ya misongo mingi ambayo matineja walio wengi huhisi. . . . Yeye ahisi kwamba utumishi kwa Mungu wapasa kutangulizwa akilini mwake.”

Tommy alianza kujifunza juu ya Biblia kutoka kwa wazazi wake alipokuwa na miaka mitano tu. Hata tangu umri wa mapema, alichukua msimamo wenye ujasiri kwa ajili ya ibada ya kweli. Wakati wanafunzi wenzake wachanga walipokuwa wakichora picha za sikukuu, Tommy alichora mandhari za Paradiso iliyoahidiwa na Mungu. Akiwa tineja, Tommy aliona kwamba itikadi za Mashahidi wa Yehova ziliwakoroweza wanafunzi wengi. Badala ya kukaa kimya kwa sababu ya hofu, alimwomba mmoja wa walimu wake kama angeweza kuongoza mazungumzo ya maswali na majibu pamoja na darasa lake ili aweze kujibu maswali yalo yote kwa wakati mmoja. Alipewa ruhusa, na ushahidi mzuri ukatolewa.

Alipokuwa na umri wa miaka 17, Markietta alipata fursa bora kabisa ya kuzungumza na wengine darasani mwake juu ya imani yake. “Tulipewa mgawo wa kutoa hotuba,” yeye asema. “Nilichagua habari yangu iwe juu ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.a Nilichagua sura tano kutoka hicho kitabu, nikaandika vichwa vyazo kwenye ubao wa kuandikia. Niliomba darasa liorodheshe vichwa hivyo kulingana na umaana wavyo.” Mazungumzo ya maswali na majibu pamoja na darasa yakafuata. “Nililionyesha darasa hicho kitabu,” Markietta amalizia, “na wanafunzi kadhaa wakaomba kupata nakala. Hata mwalimu wangu alisema kuwa alitaka nakala moja.”

Waweza Kuwekwa Huru na Kweli

Kama vile tumeona, kweli iliyomo katika Biblia inaweza kuweka huru watu wa umri mbalimbali wanaojifunza kweli hiyo na kuzingatia moyoni ujumbe wayo. Inawaweka huru kutoka katika hali ya kuwahofu wafu, hali ya kuhofu wakati ujao, na hali ya kuhofu binadamu. Hatimaye, fidia ya Yesu itawaweka huru wanadamu watiifu kutoka katika dhambi na kifo. Itakuwa shangwe iliyoje kuishi milele juu ya dunia iliyo paradiso, bila kuzuiwa tena na hali yetu yenye dhambi iliyorithiwa!—Zaburi 37:29.

Je, ungependa kujifunza zaidi juu ya baraka ambazo Mungu ameahidi? Ikiwa ndivyo, wapaswa kufanya nini? Yesu alisema hivi: ‘Hii yamaanisha uhai udumuo milele, wao kuendelea kutwaa ujuzi juu yako wewe, Mungu pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.’ (Yohana 17:3) Basi ikiwa wataka kuuona uhuru ambao Yesu aliwaahidi wanafunzi wake, lazima ujifunze kuhusu Yehova Mungu na Mwana wake. Wahitaji kujua mapenzi ya Mungu ni nini kisha uyafanye, kwa maana Biblia husema hivi: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hudumu milele.”—1 Yohana 2:17.

[Maelezo ya Chini]

a Kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Chini ya Ufalme wa Mungu, wanadamu watawekwa huru hatimaye kutoka katika dhambi na kifo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki