Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 3/1 kur. 6-7
  • Njia Bora

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njia Bora
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ulimwengu Wenye Kanuni Imara
  • Harakati ya Kufuata Kanuni za Msingi za Kidini—Hiyo ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Serikali Itakayoleta Maadili ya Kimungu
    Amkeni!—2003
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?
    Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 3/1 kur. 6-7

Njia Bora

MASHAHIDI WA YEHOVA wanahangaikia mmomonyoko wa hali ya kiroho ulimwenguni na ukosefu wa adili na ugeugeu wa kidini unaoenea katika jamii. Tokeo ni kwamba, nyakati nyingine wao huitwa washiriki wa harakati ya kufuata kanuni za msingi. Lakini je, wao ni washiriki wa harakati ya aina hiyo? La. Ingawa wana masadikisho thabiti ya kidini, wao si washiriki wa harakati ya kufuata kanuni za msingi katika maana ambayo usemi huo umekuja kutumiwa. Wao hawasongi viongozi wa kisiasa ili waendeleze maoni fulani, nao hawafanyi maandamano na vitendo vya jeuri dhidi ya wale ambao hawakubaliani nao. Wamepata njia bora. Wanamwiga Kiongozi wao, Yesu Kristo.

Mashahidi wa Yehova wanasadiki kwamba kuna kweli ya kidini, inayopatikana katika Biblia. (Yohana 8:32; 17:17) Lakini Biblia hufundisha Wakristo wawe wenye fadhili, wema, wapole, na wenye kukubali sababu—sifa zisizoruhusu ushupavu. (Wagalatia 5:22, 23; Wafilipi 4:5) Katika kitabu cha Biblia cha Yakobo, Wakristo wanatiwa moyo kusitawisha “hekima ya kutoka juu,” inayofafanuliwa kuwa ‘kwanza kabisa safi kiadili, kisha yenye kufanya amani, yenye kukubali sababu, tayari kutii, yenye kujaa rehema na matunda mema.’ Yakobo aliongeza hivi: “Tunda la uadilifu hupandwa mbegu yalo chini ya hali zenye amani kwa ajili ya wale wanaofanya amani.”—Yakobo 3:17, 18.

Mashahidi wa Yehova wanakumbuka kwamba Yesu alihangaikia sana ile kweli. Alimwambia Pontio Pilato hivi: “Kwa ajili ya hili mimi nimezaliwa, na kwa ajili ya hili nimekuja kuingia ulimwenguni, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli.” (Yohana 18:37) Ingawa alikuwa mteteaji hodari wa ile kweli, hakujaribu kulazimisha wengine wafuate masadikisho yake. Badala ya hivyo, alivuta akili na mioyo yao. Alijua ya kwamba Babaye wa kimbingu, aliye Mungu “mwema, [na] mwenye adili,” angeamua jinsi ya kuondolea mbali mambo yasiyo ya kweli na udhalimu kutoka usoni pa dunia na wakati wa kufanya hivyo. (Zaburi 25:8) Kwa sababu hiyo, hakujaribu kuwanyamazisha wale ambao hawakukubaliana naye. Kinyume cha hilo, ni viongozi wa kidini wenye imani ya kidesturi wa siku yake waliojaribu kumnyamazisha Yesu.—Yohana 19:5, 6.

Mashahidi wa Yehova wana masadikisho thabiti juu ya mafundisho ya kidini, nao wanadhihirisha kanuni imara kwa habari ya maadili. Sawa na mtume Paulo, wanasadiki kwamba kuna “Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,” tu. (Waefeso 4:5) Wana habari pia juu ya maneno haya ya Yesu: “Lango ni jembamba na barabara ni yenye kufinyana inayoongoza kuingia katika uhai, na wachache ndio wanaoipata.” (Mathayo 7:13, 14) Hata hivyo, hawajaribu kuwalazimisha wengine wafuate itikadi zao. Badala ya hivyo, wanamwiga Paulo na ‘kuwaomba’ wote wanaotamani ‘wawe wenye kupatanishwa na Mungu.’ (2 Wakorintho 5:20) Hiyo ndiyo njia bora. Ndiyo njia ya Mungu.

Harakati ya kufuata kanuni za msingi katika dini ni tofauti sana, kulingana na jinsi ambavyo usemi huo hutumiwa leo. Washiriki wa harakati ya kufuata kanuni za msingi hutumia mbinu nyingi—kutia ndani jeuri—ili kulazimisha jamii ifuate kanuni zao. Katika kufanya hivyo, wanakuwa sehemu muhimu ya mfumo wa kisiasa. Lakini, Yesu alisema kwamba wafuasi wake hawapaswi kuwa “sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19; 17:16; Yakobo 4:4) Kwa kupatana na maneno hayo, Mashahidi wa Yehova hudumisha hali ya kutokuwamo kabisa katika ubishi mbalimbali wa kisiasa. Na, sawa na vile gazeti la habari la Kiitalia Fuoripagina lilivyokiri, “hawamlazimishi mtu yeyote afuate jambo lolote lile; kila mtu yuko huru kukubali au kukataa yale wasemayo.” Tokeo ni nini? Ujumbe wa Biblia wenye amani wa Mashahidi huvuta watu wa aina zote, hata wale ambao wakati mmoja walikuwa washiriki wa harakati ya kufuata kanuni za msingi.—Isaya 2:2, 3.

Ulimwengu Wenye Kanuni Imara

Mashahidi hutambua kwamba wanadamu hawawezi kusuluhisha matatizo yanayowahangaisha washiriki wa harakati ya kufuata kanuni za msingi. Huwezi kumlazimisha mtu amwamini Mungu au akubali itikadi zako binafsi. Kuamini kwamba jambo hilo lawezekana kuliongoza kwenye baadhi ya mambo yenye kuchukiza sana katika historia, kama zile Krusedi, yale Mabaraza ya Kuhukumu Wazushi ya enzi za kati, na kule “kugeuzwa imani” kwa Wahindi wa Amerika. Hata hivyo, ikiwa una itibari katika Mungu, utakuwa tayari kumwacha ashughulikie mambo.

Kulingana na Biblia, Mungu amewekea mpaka ule wakati ambao awaruhusu wanadamu wavunje sheria zake na hivyo kusababisha kuteseka na umivu. Wakati huo karibu umeisha. Tayari, Yesu anatawala akiwa Mfalme katika Ufalme wa Mungu wa kimbingu, na upesi Ufalme huo utatenda ili kuondoa serikali za kibinadamu na kutwaa uongozi wa kila siku juu ya wanadamu. (Mathayo 24:3-14; Ufunuo 11:15, 18) Tokeo litakuwa paradiso ya ulimwenguni pote ambamo amani na uadilifu utakuwa kwa wingi. Wakati huo hakutakuwa na ugeugeu juu ya jinsi Mungu wa kweli apasavyo kuabudiwa. “Wenye haki watairithi nchi, nao watakaa humo milele.” (Zaburi 37:29) Kanuni za milele kama vile fadhili-upendo, kweli, haki, na wema zitashinda kwa faida ya wanadamu watiifu wote.

Akitazamia wakati huo, mtunga-zaburi asema hivi katika njia ya kishairi: “Fadhili na kweli zimekutana, haki na amani zimehusiana. Kweli imechipuka katika nchi, haki imechungulia kutoka mbinguni. Naam, BWANA atatoa kilicho chema, na nchi yetu itatoa mazao yake. Haki itakwenda mbele zake, nayo itazifanya hatua zake kuwa njia.”—Zaburi 85:10-13.

Ingawa hatuwezi kuubadili ulimwengu, sisi tukiwa mtu mmoja-mmoja twaweza kusitawisha kanuni za kimungu hata leo. Hivyo, twaweza kujaribu kuwa aina ya watu ambao Mungu atataka wawe waabudu wake katika ulimwengu huo mpya. Ndipo tutakapokuwa miongoni mwa wale wasikivu wanaorejezewa na mtunga-zaburi hivi: “Wenye upole [“wasikivu,” NW] watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.” (Zaburi 37:11) Mungu hutegemeza na kuwabariki wale wafanyao mapenzi yake, naye aahidi mambo ya ajabu kwa wakati ujao wao. Mtume Yohana alisema hivi: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hudumu milele.”—1 Yohana 2:17.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Mashahidi wa Yehova huwaalika wote wapate kufahamu habari njema ya Ufalme wa Mungu

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 6]

Taa kwenye kurasa 3, 4, 5, na 6: Printer’s Ornaments/na Carol Belanger Grafton/Dover Publications, Inc.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki