Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 1/15 kur. 13-18
  • Fulizeni Kutembea na Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fulizeni Kutembea na Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mwendo wa Maisha Wenye Upatano
  • Epuka Mtego wa Kujitumaini
  • Usiache Hali ya Kuhofu Mwanadamu Ikuongoze
  • Epuka Kupunguza Umaana wa Shauri
  • Kukabiliana kwa Mafanikio na Mahangaiko ya Maisha
  • Tembea Kwa Imani, Si Kwa Kuona!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Enenda kwa Imani!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Manufaa za Kumhofu Mungu wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Unaweza Kutembea Pamoja na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 1/15 kur. 13-18

Fulizeni Kutembea na Mungu

“Fulizeni kutembea kwa roho na hamtatekeleza tamaa ya kimwili hata kidogo.”—WAGALATIA 5:16.

1. (a) Enoki alitembea na Mungu katikati ya hali gani na kwa muda gani? (b) Noa alitembea na Mungu kwa muda gani, na ni daraka gani zito alilokuwa nalo?

BIBLIA hutuambia kwamba Enoki “alifuliza kutembea na Mungu wa kweli.” Ujapokuwa usemi wa kushtua na mwenendo wa watu waliomzunguka wa kutomwogopa Mungu, alidumu katika kutembea na Mungu hadi mwisho wa uhai wake akiwa na umri wa miaka 365. (Mwanzo 5:23, 24, NW; Yuda 14, 15) Noa pia “alitembea na Mungu wa kweli.” Alifanya hivyo huku akiitunza familia yake, akikabiliana na uvutano wa malaika waasi na wazao wao wenye jeuri, na wakati uleule akishughulikia mambo yote yaliyohusika katika kujenga safina kubwa iliyokuwa kubwa kuliko chombo chochote cha baharini cha nyakati za kale. Alifuliza kutembea na Mungu baada ya Gharika, hata wakati ambapo uasi dhidi ya Yehova ulipozuka tena Babeli. Kwa kweli, Noa alifuliza kutembea na Mungu hadi kifo chake akiwa na umri wa miaka 950.—Mwanzo 6:9, NW; 9:29.

2. ‘Kutembea na Mungu’ kwamaanisha nini?

2 Isemapo kwamba wanaume hao wa imani “walitembea” na Mungu, Biblia inatumia mtajo huo katika maana ya kisitiari. Yamaanisha kwamba Enoki na Noa walijiongoza katika njia iliyotoa uthibitisho wa imani yenye nguvu katika Mungu. Walifanya yale ambayo Yehova aliwaamuru na walipatanisha maisha zao na yale waliyojua juu yake kutokana na shughuli zake na wanadamu. (Linganisha 2 Mambo ya Nyakati 7:17.) Hawakukubaliana kiakili tu na yale ambayo Mungu alisema na kufanya bali walitenda yote aliyowataka watende—si baadhi yake tu bali yote kwa kadiri ilivyowezekana kwao wakiwa wanadamu wasio wakamilifu. Hivyo Noa, kwa kielelezo, alifanya sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu. (Mwanzo 6:22) Noa hakufanya mambo kupita mielekezo aliyopewa, wala hakubaki nyuma kwa uzembe. Akiwa mmoja aliyeonea shangwe ukaribu na Yehova, akihisi kuwa huru kusali kwa Mungu na kuthamini sana mwelekezo wa kimungu, alikuwa akitembea na Mungu. Je, wewe wafanya hivyo?

Mwendo wa Maisha Wenye Upatano

3. Ni jambo gani lililo la maana sana kwa watumishi wote wa Mungu waliojiweka wakfu na kubatizwa?

3 Yasisimua kuona watu wakianza kutembea na Mungu. Wachukuapo hatua chanya kupatana na mapenzi ya Yehova, wao watoa uthibitisho wa imani, ambayo bila hiyo hakuna awezaye kumpendeza Mungu. (Waebrania 11:6) Jinsi tushangiliavyo kwamba kila mwaka, kwa wastani kwa miaka mitano iliyopita, watu zaidi ya 330,000 wamejiweka wakfu kwa Yehova na kujitoa wabatizwe kwa maji! Lakini ni jambo la maana pia kwao na kwetu sote tufulize kutembea na Mungu.—Mathayo 24:13; Ufunuo 2:10.

4. Ingawa walionyesha imani fulani, kwa nini Waisraeli walio wengi ambao walitoka Misri hawakuingia Bara Lililoahidiwa?

4 Katika siku ya Musa, imani ilihitajika ili familia ya Israeli isherehekee Sikukuu ya Kupitwa katika Misri na kunyunyiza damu kwenye miimo ya milango na kwenye sehemu ya juu ya mlango wa nyumba yao. (Kutoka 12:1-28) Hata hivyo, imani ya wengi ilisitasita walipoona jeshi la Farao nyuma karibu nao kwenye Bahari Nyekundu. (Kutoka 14:9-12) Andiko la Zaburi 106:12 laonyesha kwamba walipokuwa wamepita salama kwenye bahari kavu na walipokuwa wameona maji yenye kubingirika yakiliangamiza jeshi la Misri, ‘waliyaamini tena maneno ya [Yehova].’ Hata hivyo, muda mfupi baadaye wakiwa nyikani, Waisraeli walianza kulalamika juu ya maji ya kunywa, chakula, na usimamizi. Ripoti hasi ya wapelelezi 10 kati ya 12 waliorudi kutoka katika Bara Lililoahidiwa iliwafanya wahofu. Chini ya hali hizo, kama vile andiko la Zaburi 106:24 lisemavyo, ‘hawakuliamini neno la [Mungu].’ Walitaka kurudi Misri. (Hesabu 14:1-4) Imani yoyote ile waliyokuwa nayo ilidhihirika tu walipoona mawonyesho yasiyo ya kawaida ya nguvu za Mungu. Hawakufuliza kutembea na Mungu. Tokeo ni kwamba, Waisraeli hao hawakuingia Bara Lililoahidiwa.—Zaburi 95:10, 11.

5. Andiko la 2 Wakorintho 13:5 na la Mithali 3:5, 6 yahusikaje katika kutembea na Mungu?

5 Biblia hutuonya kwa upole hivi: “Fulizeni kujijaribu kama nyinyi mumo katika imani, fulizeni kujithibitisha wenyewe nyinyi ni nini.” (2 Wakorintho 13:5) Kuwa “katika imani” humaanisha kushikamana na itikadi zote za Kikristo. Kufanya hivyo ni muhimu ikiwa tutafanikiwa katika kutembea na Mungu sikuzote za maisha yetu. Ili kutembea na Mungu, lazima pia tudhihirishe sifa ya imani, kumtumaini Yehova kikamili. (Mithali 3:5, 6) Kuna mitego mingi iwezayo kunasa wakosao kufanya hivyo. Baadhi yake ni ipi?

Epuka Mtego wa Kujitumaini

6. Wakristo wote wajua nini juu ya uasherati na uzinzi, nao huhisije juu ya dhambi hizo?

6 Kila mtu ambaye amejifunza Biblia, akaweka maisha yake wakfu kwa Yehova, na amebatizwa ajua kwamba Neno la Mungu hulaumu uasherati na uzinzi. (1 Wathesalonike 4:1-3; Waebrania 13:4) Hao hukubali kwamba hilo ni sawa. Hunuia kuishi kupatana nalo. Lakini, ukosefu wa adili katika ngono waendelea kuwa mojawapo ya mitego yenye matokeo zaidi ya Shetani. Kwa nini?

7. Kwenye Nyanda za Moabu, wanaume Waisraeli walihusikaje katika mwenendo ambao walijua ulikuwa wenye kosa?

7 Mwanzoni, huenda wahusikao katika mwenendo huo wa ukosefu wa adili wasiwe wakipanga kufanya hivyo. Labda hilo lilikuwa kweli pia kuhusu Waisraeli kwenye Nyanda za Moabu. Kwa wanaume Waisraeli waliokuwa wanyong’onyevu kuhusu maisha wakiwa nyikani, huenda mwanzoni wanawake Wamoabi na Wamidiani waliowashawishi wakawa walionekana kuwa wenye urafiki na wenye kukaribisha wageni. Lakini ni nini lililotukia wakati ambapo Waisraeli walikubali mialiko ya kushirikiana na watu waliotumikia Baali wala si Yehova, watu walioruhusu wasichana wao (hata kutoka katika familia mashuhuri) wafanye ngono na wanaume ambao hawakuwa wameolewa nao? Wanaume kutoka katika kambi ya Israeli walipoanza kuona ushirika huo kuwa kitu cha kutamanika, walishawishiwa kufanya mambo waliyojua kuwa yalikuwa kosa, na hilo liliwagharimu uhai wao.—Hesabu 22:1; 25:1-15; 31:16; Ufunuo 2:14.

8. Katika siku yetu, ni nini kiwezacho kumwongoza Mkristo katika ukosefu wa adili katika ngono?

8 Ni nini kiwezacho kumfanya mtu aangukie mtego kama huo leo? Ingawa huenda akajua uzito wa ukosefu wa adili katika ngono, ikiwa hang’amui pia hatari ya kujitumaini, aweza kujiruhusu kuingia katika hali ambamo kishawishi cha kufanya kosa chazidi kusababu kwake.—Mithali 7:6-9, 21, 22; 14:16.

9. Ni maonyo gani ya Kimaandiko yawezayo kutulinda dhidi ya ukosefu wa adili?

9 Kwa lugha sahili Neno la Mungu hutuonya tusipotoshwe kufikiri kwamba tu wenye nguvu sana hivi kwamba ushirika mbaya hauwezi kutufisidi. Hilo latia ndani kutazama programu za televisheni zionyeshazo maisha ya watu wasio na adili na kutazama magazeti yachocheayo tamaa zisizo za adili. (1 Wakorintho 10:11, 12; 15:33) Hata ushirika pamoja na waamini wenzetu chini ya hali mbaya waweza kuongoza kwenye matatizo mazito. Uvutano kati ya watu wa jinsia tofauti ni wenye nguvu. Kwa hiyo, likiwa na hangaiko lenye upendo, tengenezo la Yehova limetahadharisha dhidi ya kuwa peke yetu na faraghani pamoja na mtu wa jinsia tofauti ambaye hatujafunga ndoa naye au asiye mshiriki wa familia. Ili kuendelea kutembea na Mungu, twahitaji kuepuka mtego wa kujitumaini na kutii shauri lenye kuonya atupatialo.—Zaburi 85:8.

Usiache Hali ya Kuhofu Mwanadamu Ikuongoze

10. “Kuwaogopa wanadamu” huletaje mtego?

10 Hatari nyingine yatambulishwa kwenye andiko la Mithali 29:25, lisemalo hivi: “Kuwaogopa wanadamu huleta mtego.” Mtego wa mwindaji mara nyingi hutia ndani tanzi ivutayo kwa nguvu shingoni au kamba zitegazo miguu ya mnyama. (Ayubu 18:8-11) Vivyo hivyo, kuwaogopa wanadamu kwaweza kuzuia uwezo wa mtu kusema kwa uhuru au kujiendesha katika njia impendezayo Mungu. Tamaa ya kuwapendeza wengine ni ya kawaida, na kuwapuuza wengine kwa kutojali mambo ambayo wengine wafikiri si Ukristo. Lakini usawaziko wahitajiwa. Wakati ambapo hangaiko juu ya maitikio yawezekanayo ya vile huenda wanadamu wengine wakaitikia limfanyapo mtu afanye mambo ambayo Mungu hukataza au kumfanya ajiepushe na kufanya mambo ambayo Neno la Mungu huamuru, mtu huyo amenaswa.

11. (a) Ulinzi dhidi ya kuruhusu hali ya kuhofu wanadamu iongoze mtu ni nini? (b) Yehova amewasaidiaje watumishi wake ambao walikuwa wakipambana na hali ya kuhofu wanadamu?

11 Ulinzi dhidi ya mtego huo wapatikana katika ‘kumtumaini Yehova’ wala si katika mwelekeo wa asili wa mtu mwenyewe. (Mithali 29:25b) Akimtumaini Mungu, hata mtu aonaye haya kiasili aweza kuthibitika kuwa mjasiri na imara. Maadamu tumezingirwa na misongo ya mfumo wa mambo wa Shetani, tutahitaji kuwa wenye kulinda dhidi ya hali ya kuhofu mwanadamu yenye kuleta mtego. Ingawa nabii Eliya alikuwa na rekodi nzuri ya utumishi wa ujasiri, Yezebeli alipotisha kumfanya auawe, alitoroka kwa kuhofu. (1 Wafalme 19:2-18) Chini ya mkazo, mtume Petro alikana kwa kuhofu kwamba hakumjua Yesu Kristo, na miaka kadhaa baadaye aliruhusu hali ya kuhofu imfanye ajiendeshe katika njia iliyopinga imani. (Marko 14:66-71; Wagalatia 2:11, 12) Hata hivyo, Eliya na Petro walikubali msaada wa kiroho na wakiwa na uhakika katika Yehova, waliendelea kumtumikia Mungu kwa kukubalika.

12. Ni vielelezo gani vya siku ya kisasa vionyeshavyo jinsi ambavyo watu wamesaidiwa kuepuka kuacha hofu iwafanye wasite kumpendeza Mungu?

12 Wengi wa watumishi wa Yehova katika siku yetu wamejifunza pia jinsi ya kushinda hali ya kuhofu yenye kuleta mtego. Tineja mmoja Shahidi katika Guyana alikiri hivi: “Shuleni pigano la kukinza msongo wa marika ni lenye nguvu.” Lakini aliongeza kusema hivi: “Ndivyo na imani yangu katika Yehova.” Mwalimu wake alipomdhihaki mbele ya darasa lote kwa sababu ya imani yake, alisali kwa Yehova kimya-kimya. Baadaye faraghani alimtolea huyo mwalimu ushahidi wa busara. Alipokuwa akizuru Benin, kijana mmoja aliyekuwa akijifunza matakwa ya Yehova alitaka kuondolea mbali sanamu ambayo baba yake alikuwa amemchongea. Huyo kijana alijua kwamba mfano huo haukuwa na uhai, naye hakuuogopa, lakini alijua pia kwamba huenda wanakijiji wenye hasira wakajaribu kumwua. Alisali kwa Yehova, kisha usiku akaichukua sanamu hiyo hadi kichakani na kuitupa. (Linganisha Waamuzi 6:27-31.) Wakati ambapo mwanamke mmoja katika Jamhuri ya Dominika alianza kumtumikia Yehova, mume wake alidai kwamba achague kati yake na Yehova. Mwanamume huyo alitisha kumtaliki. Je, hali ya kuhofu ingemfanya aache imani yake? Alijibu hivi: “Ikiwa ukosefu wa uaminifu ungehusika, ningeaibika, lakini siaibiki kwa sababu ya kumtumikia Yehova Mungu!” Aliendelea kutembea na Mungu, na baada ya muda mume wake alijiunga naye katika kufanya mapenzi ya Yehova. Tukimtumaini kikamili Baba yetu wa kimbingu, sisi pia twaweza kuepuka kuruhusu hali ya kuhofu mwanadamu ituzuie tusifanye mambo tujuayo yatakuwa yenye kumpendeza Yehova.

Epuka Kupunguza Umaana wa Shauri

13. Twaonywa dhidi ya mtego gani kwenye 1 Timotheo 6:9?

13 Ingawa mitego fulani itumiwayo na wawindaji imekusudiwa kunasa mnyama yeyote atukiaye kupita mahali fulani, mitego mingine hushawishi wanyama kwa kutumia chambo chenye kuvutia kwa udanganyo. Kwa wanadamu wengi, mali ziko hivyo. (Mathayo 13:22) Kwenye 1 Timotheo 6:8, 9, Biblia yatutia moyo turidhike na riziki na cha kujifunika. Kisha yaonya hivi: “Wale waazimiao kuwa matajiri huanguka ndani ya kishawishi na mtego na tamaa nyingi zisizo za akili na zenye kuumiza, ambazo hutumbukiza watu ndani ya uharibifu na uangamizo.”

14. (a) Ni nini huenda kikamzuia mtu asizingatie moyoni shauri la kuridhika na riziki na cha kujifunika? (b) Fasili yenye kosa ya mali yaweza kupunguzaje uzito wa onyo lililorekodiwa kwenye 1 Timotheo 6:9? (c) Ni katika njia gani “tamaa ya macho” yaweza kuwapofusha watu fulani wasione mtego uwasubirio?

14 Lijapokuwa onyo hilo, wengi hunaswa kwa sababu hawatumii shauri hilo wao wenyewe. Kwa nini? Je, ingeweza kuwa kwamba kuwa na fahari huwasukuma wasisitize kushikilia mtindo-maisha uhitajio mengi zaidi ya “riziki na cha kujifunika” mambo ambayo Biblia hutuhimiza turidhike nayo? Je, labda wao hupunguza uzito wa onyo la Biblia kwa sababu wao hufasili mali kuwa vitu walivyo navyo watu wenye mali nyingi sana? Biblia hutaja tu lile azimio la watu la kuwa wenye mali kwa kulitofautisha na kuridhika na riziki na cha kujifunika. (Linganisha Waebrania 13:5.) Je, “tamaa ya macho”—tamaa ya kuwa na vitu waonavyo, hata wakidhabihu miradi ya kiroho—yawafanya wasukume masilahi ya ibada ya kweli mahali pa pili? (1 Yohana 2:15-17; Hagai 1:2-8) Jinsi walivyo wenye furaha wazingatiao moyoni shauri la Biblia na kutembea na Mungu kwa kufanya utumishi wa Yehova uwe jambo kuu maishani mwao!

Kukabiliana kwa Mafanikio na Mahangaiko ya Maisha

15. Ni hali zipi ambazo kwa kueleweka husababisha hangaiko kwa wengi wa watu wa Yehova, na ni mtego gani tupaswao kuwa chonjo kuuona tunapokuwa chini ya mkazo huo?

15 Jambo la kawaida zaidi kuliko azimio la kupata mali ni hangaiko la kupata mahitaji ya lazima ya maisha. Watumishi wa Yehova walio wengi huishi wakiwa na mali chache sana. Wao hufanya kazi kwa bidii kwa saa nyingi ili wapate mavazi ya lazima, mahali pa familia yao kulala usiku, na angalau kiasi fulani cha chakula cha siku. Wengine hushindana na matatizo kwa sababu ya ugonjwa au kuzeeka kwao wenyewe au kwa washiriki wa familia. Ingekuwa rahisi kama nini kuacha hali hizo zisonge masilahi ya kiroho kutoka maishani mwao!—Mathayo 13:22.

16. Yehova hutusaidiaje kukabiliana na misongo ya maisha?

16 Kwa upendo, Yehova hutuambia juu ya kitulizo kitakachopatikana chini ya Ufalme wa Kimesiya. (Zaburi 72:1-4, 16; Isaya 25:7, 8) Pia atusaidia kukabiliana na misongo ya maisha sasa kwa kutupatia shauri juu ya jinsi ya kupanga mambo ya kutangulizwa. (Mathayo 4:4; 6:25-34) Kupitia rekodi ya jinsi alivyowasaidia watumishi wake katika nyakati zilizopita, Yehova hututumainisha. (Yeremia 37:21; Yakobo 5:11) Yeye hututia nguvu kupitia ule ujuzi wa kwamba, bila kujali janga lolote lile ambalo hutupata, upendo wake kwa watumishi wake waaminifu wadumu daima. (Waroma 8:35-39) Kwa wale wawekao tumaini lao katika Yehova, yeye atangaza hivi: “Hakika sitakuacha kwa vyovyote wala kukuachilia mbali kwa vyovyote.”—Waebrania 13:5.

17. Toa vielelezo vya jinsi ambavyo watu mmoja-mmoja wapatwao na janga kali wameweza kuendelea kutembea na Mungu.

17 Wakiwa wametiwa nguvu na ujuzi huo, Wakristo wa kweli huendelea kutembea na Mungu badala ya kugeukia njia za kilimwengu. Falsafa ya kawaida ulimwenguni miongoni mwa maskini katika nchi nyingi ni kwamba kuchukua kitu kutoka kwa mtu aliye na vingi ili uweze kulisha familia yako si wizi. Lakini wale watembeao kwa imani hukataa maoni hayo. Wao huthamini kibali cha Mungu kuliko kitu kinginecho chote na humtegemea athawabishe mwenendo wao wenye kufuatia haki. (Mithali 30:8, 9; 1 Wakorintho 10:13; Waebrania 13:18) Mjane katika India alipata kwamba nia ya kufanya kazi pamoja na ubunifu ni mambo yaliyomsaidia kukabiliana na hali. Badala ya kuona uchungu kwa sababu ya hali yake maishani, alijua kwamba, akitanguliza maishani mwake Ufalme wa Mungu na uadilifu wake, Yehova angebariki jitihada zake za kupata mahitaji yake na ya mwana wake. (Mathayo 6:33, 34) Maelfu mengi ulimwenguni huonyesha kwamba, bila kujali janga ambalo huenda wakakabili, Yehova ni kimbilio na ngome yao. (Zaburi 91:2) Je, hilo ni kweli kukuhusu?

18. Ufunguo wa kuepuka mitego ya ulimwengu wa Shetani ni nini?

18 Maadamu twaishi katika mfumo wa mambo uliopo, kutakuwa na mitego ya kuepuka. (1 Yohana 5:19) Biblia huitambulisha hiyo na kutuonyesha jinsi ya kuiepuka. Wampendao Yehova kwelikweli na wana hofu ifaayo ya kutomchukiza waweza kushughulika na mitego hiyo kwa mafanikio. ‘Wakifuliza kutembea kwa roho,’ hawatashindwa na njia za kilimwengu. (Wagalatia 5:16-25) Kwa wote ambao kwa kweli hujenga maisha zao juu ya uhusiano wao na Yehova, wana tazamio tukufu la kutembea na Mungu, wakifurahia ukaribu naye milele.—Zaburi 25:14.

Elezo Lako Ni Nini?

◻ Kujitumaini kwaweza kuwaje mtego?

◻ Ni nini kiwezacho kutulinda salama dhidi ya kuongozwa na hali ya kuhofu wanadamu?

◻ Ni nini huenda kikatufanya tushindwe kutumia shauri juu ya hatari ya kufuatia mali?

◻ Ni nini kiwezacho kutuwezesha kuepuka kunaswa na mahangaiko ya maisha?

[Picha katika ukurasa wa 16, 17]

Watu wengi hufuliza kutembea na Mungu katika maisha yao yote

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki