Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 3/15 kur. 10-11
  • Watumwa wa Wanadamu au Watumishi wa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watumwa wa Wanadamu au Watumishi wa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hatari za Kuwafuata Wanadamu
  • Je! Mashahidi wa Yehova Ni Kidhehebu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Wakristo na Jamii ya Kibinadamu Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Je, Mashahidi wa Yehova Ni Dhehebu la Marekani?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 3/15 kur. 10-11

Watumwa wa Wanadamu au Watumishi wa Mungu?

“MASHAHIDI WA YEHOVA wapasa kustahiwa kwa njia fulani.” Ndivyo kitaarifuvyo kitabu Kijerumani Seher, Grübler, Enthusiasten (Wenye Kuona Maono, Wenye Kufikiri kwa Uzito, Wenye Shauku). Ingawa kwa njia fulani ni chenye kuchambua Mashahidi, kitabu hicho chakubali hivi: “Kwa ujumla, wao huishi bila lawama, maisha ya tabaka la kati. Wao ni wenye bidii yenye kuendelea na wenye kudhamiria katika kazi yao, ni raia watulivu na walipaji kodi wenye kufuatia haki. Wao hujiepusha na kufuatia mali. . . . Nidhamu yao kwenye mikusanyiko yastahili sifa. Roho yao ya kujidhabihu ni sawa na ya kikundi kingine chochote cha kidini; kwa habari ya huduma, wao huwazidi ubora wale wengine wote. Lakini jambo ambalo huwainua juu ya kila kanisa na kila kikundi kingine cha Kikristo cha siku yetu ni azimio lisilovunjika kabisa ambalo kwalo wengi wao hupiga mbiu juu ya mafundisho yao chini ya hali zote na katika hatari zote zenye kuwakabili.”a

Kujapokuwa na tathmini hiyo chanya, kauli fulani hujaribu kuwakilisha Mashahidi wa Yehova katika njia tofauti kabisa. Katika nchi zilizo nyingi ulimwenguni pote, Mashahidi wamefanya utumishi wao wa kidini waziwazi kwa miongo mingi bila kuingiliwa. Mamilioni ya watu wanawajua, wanawastahi, na kukubali kwamba wana haki ya kuzoea imani yao. Kwa nini basi, kuna ukosefu wowote wa uhakika juu ya Mashahidi wa Yehova ni nani?

Labda sababu moja ya kuwa na huo ukosefu wa uhakika ni kwamba nyakati za juzi idadi fulani ya vikundi vingine vya kidini imejihusisha na kutenda watoto vibaya, ujiuaji kimakusudi wa watu wengi, na mashambulio ya kigaidi. Bila shaka, tabia kama hiyo yenye upotovu iko kila mahali, si katika watu wa kidini tu. Hata hivyo, kwa habari ya dini, watu wengi wamekuwa wenye kutia shaka, wengine wakiwa hata wenye uhasama.

Hatari za Kuwafuata Wanadamu

“Farakano” limefasiliwa kuwa “kikundi chenye kushikamana sana na fundisho fulani dhahiri au na kiongozi fulani.” Vivyo hivyo, washiriki wa “madhehebu” wana “ujitoaji mkubwa kwa mtu fulani, wazo, au kitu.” Kwa hakika, washiriki wa kikundi chochote cha kidini ambao wanashikamana kwa nguvu na viongozi wa kibinadamu na mawazo yao wamo hatarini mwa kuwa watumwa wa watu. Uhusiano wenye kukazia kiongozi fikira kwa nguvu waweza kuongoza kwenye tegemeo la kihisia-moyo na la kiroho lililo hatari. Huenda hatari hiyo ikaongezeka mtu alelewapo katika mazingira ya kifarakano tangu utoto.

Wale walio na mahangaiko kama hayo kuhusu dini wahitaji habari yenye kutegemeka. Huenda wengine wakawa wameambiwa kwamba Mashahidi wa Yehova ni washiriki wa tengenezo la kidini lifanyalo washiriki wake watumwa, lizoealo udhibiti wa kimabavu juu yao, lenye kuzuia uhuru wao kupita kiasi, na kuwafanya wawe watu wasiofuata desturi za jamii kwa ujumla.

Mashahidi wa Yehova wajua kwamba mahangaiko hayo hayana msingi. Kwa hiyo, wanakualika ujichunguzie. Baada ya uchunguzi wa uangalifu, fikia mkataa wako mwenyewe. Je, Mashahidi ni watumishi wa Mungu, kama wadaivyo, au kwa kweli ni watumwa wa wanadamu? Chanzo cha nguvu yao ni nini? Makala mbili kwenye ukurasa wa 12 hadi 23 zitaandaa majibu yenye kutosheleza kwa maswali hayo.

[Maelezo ya Chini]

a Ile chapa ya awali ya mwaka wa 1950 haikuwa na hiyo taarifa iliyopo juu. Hivyo kuonekana kwake katika chapa iliyofanyiwa marekebisho ya mwaka wa 1982 hufunua mwelekeo fulani wa kuwaelewa Mashahidi wa Yehova kwa njia bora.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki