Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 6/1 kur. 24-27
  • Tukio Lenye Furaha Kuhitimu kwa Darasa la 104 la Gileadi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tukio Lenye Furaha Kuhitimu kwa Darasa la 104 la Gileadi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Shauri Lenye Kutumika la Kuendelea Kuwa na Furaha
  • Kupendezwa na Watu Hutokeza Furaha
  • Funguo za Kupata Furaha Katika Shamba la Ugenini
  • Watu Huenda Gileadi kwa Kuchochewa na Moyo wa Kupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kutoka Kuwa Wanafunzi Wenye Mafanikio Hadi Kuwa Wamishonari Wenye Mafanikio
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Wanafunzi Wenye Kuhitimu wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Gileadi Yatuma Mishonari “Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 6/1 kur. 24-27

Tukio Lenye Furaha Kuhitimu kwa Darasa la 104 la Gileadi

“HII ni siku yenye furaha, na sisi sote tunafurahi.” Kwa maneno hayo Carey Barber, mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, alifungua programu ya kuhitimu ya darasa la 104 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower katika Machi 14, 1998. Wasikilizaji 4,945 walialikwa kuanza hiyo pindi kwa kuimba wimbo wa Ufalme namba 208, wenye kichwa “Wimbo wa Kushangilia.”

Shauri Lenye Kutumika la Kuendelea Kuwa na Furaha

Sehemu ya kwanza ya programu, iliyokuwa mfululizo wa hotuba fupi zenye kutegemea Biblia, iliandaa shauri lenye kutumika juu ya jinsi ya kudumisha roho ya furaha iliyokuwa imeenea katika siku hiyo ya kuhitimu.

Hotuba ya kwanza ilitolewa na Joseph Eames wa Idara ya Uandikaji. Yeye alizungumzia kichwa “Igeni Roho ya Watu Waaminifu-Washikamanifu,” iliyotegemea simulizi la Biblia kwenye 2 Samweli sura ya 15 na 17, ambapo Absalomu, mwana wa Daudi, alikula njama ya kunyakua ufalme wa baba yake ambao alipewa na Mungu, kwa kuchochea uasi. Hata hivyo, kuna watu walioendelea kuwa waaminifu-washikamanifu kwa Mfalme Daudi, aliyekuwa mtiwa-mafuta wa Yehova. Wamishonari wapya wangeweza kujifunza nini kutokana na hotuba hiyo? “Kokote mwendako katika migawo yenu ya umishonari, kuzeni kwa uaminifu-mshikamanifu roho ya ushirikiano. Saidieni wengine kufanya hivyohivyo,” akamalizia Ndugu Eames.

Mwenye kufuata kwenye programu alikuwa David Sinclair, aliyeonyesha matakwa kumi ya kuwa wageni katika ‘hema la Yehova,’ ambayo yametajwa katika Zaburi 15. Hotuba yake yenye kichwa “Endeleeni Kuwa Wageni Katika Hema Lenu la Umishonari,” iliwatia moyo wanafunzi wenye kuhitimu watumie zaburi hiyo katika migawo yao ya umishonari, ambako watakuwa wageni. Ndugu Sinclair alikazia umuhimu wa kuishi kupatana na viwango vya Mungu nyakati zote. Kukiwa na matokeo gani? Andiko la Zaburi 15:5 lasema hivi: “Mtu atendaye mambo hayo hataondoshwa milele.”

Hotuba ya John Barr, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, ndiyo iliyofuata, naye alikazia fikira ile hali yenye kutia nguvu itokezwayo na kuimba katika mikutano ya Kikristo. Lakini ni wimbo gani wa furaha zaidi ambao unaimbwa duniani pote? Wimbo huo ni habari njema za Ufalme wa Mungu wa Kimesiya. Ni nini yaliyo matokeo ya kuimba huko kote, au ya kuhubiriwa kwa Ufalme? Ubeti wa pili wa wimbo namba 208 husema hivi kwa maneno machache na dhahiri: “Kwa kuhubiri na kufundisha, wengi wavutwa kwa Yehova. Nao waimba nyimbo za shangwe, kotekote wazivumisha!” Naam, kila siku wanafunzi wapya wapatao 1,000 wanabatizwa. Ndugu Barr alimalizia hivi: “Akina ndugu, je, si jambo lenye kupendeza kufikiria kwamba mnatumwa katika maeneo mkakutane na aina ya watu ambao watakuwa wanawangoja tu ili wasikie wimbo wenu wa sifa?”

Hotuba ya James Mantz wa Halmashauri ya Uandikaji yenye kichwa “Wasikilizeni Wenye Uzoefu” ndiyo iliyofuata. Alitaja kwamba mambo mengine hujulikana tu kupitia yale ambayo mtu binafsi amejionea. (Waebrania 5:8) Hata hivyo, andiko la Mithali 22:17 latutia moyo ‘tutege sikio letu tuyasikie maneno ya wenye hekima,’ au wale ambao wamejipatia uzoefu. Wanafunzi wanaohitimu wanaweza kujifunza mengi kutokana na wale waliowatangulia. “Wanajua jinsi ya kujadiliana bei na wenye maduka wa huko. Wanajua maeneo ya jiji ya kuepukwa kwa sababu ya hatari za kimwili au kiadili. Wanajua hisia nyepesi za watu wa huko. Wale ambao wamekuwa wamishonari kwa muda mrefu wanajua unachohitaji ili kuwa na furaha na kufaulu katika mgawo wako,” akasema Ndugu Mantz.

Alipozungumzia kichwa “Thamini Mgawo Wako wa Kitheokrasi,” Wallace Liverance, msajili wa Shule ya Gileadi, alieleza kwamba ingawa wamishonari fulani kama mtume Paulo, Timotheo, na Barnaba, walipokea migawo yao kutoka kwa Mungu kupitia roho takatifu au udhihirisho fulani wa kimuujiza, wamishonari waliozoezwa Gileadi hupewa mgawo wao katika shamba la ulimwenguni pote na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mathayo 24:45-47) Alilinganisha migawo ya wamishonari na sehemu ambazo Gideoni aliwagawia wanaume wake ambao wangepigana na Wamidiani. (Waamuzi 7:16-21) “Thamini mgawo wako wa Kitheokrasi wa umishonari. Kama vile ambavyo askari wa Gideoni ‘walisimama kila mtu mahali pake,’ uoneni mgawo wenu kuwa mahali mpaswapo kuwa. Iweni na imani kwamba Yehova anaweza kuwatumia kama vile alivyowatumia wanaume mia tatu wa Gideoni,” akahimiza Ndugu Liverance.

Kupendezwa na Watu Hutokeza Furaha

Wakati mmoja gazeti la Mnara wa Mlinzi lilieleza hivi: “Kuliko kujenga kupendezwa na maisha zetu juu ya vitu vinavyotengenezwa na vifaa vya taratibu hii, vitu ambavyo havina uhakika kama vitaendelea, ni heri na ni jambo la hekima kupendezwa sana na watu na kujifunza namna ya kupata furaha ya kweli katika kuwatumikia wengine.” Kwa kupatana na hayo, Ndugu Mark Noumair, mmoja wa wafunzi wa Shule ya Gileadi, alizungumza pamoja na kikundi cha wanafunzi juu ya mambo waliyoona shambani na kueleza hivi: “Kupendezwa kibinafsi na wengine ndiko kutakakowafanya mwe wamishonari wazuri.”

Funguo za Kupata Furaha Katika Shamba la Ugenini

Ni zipi baadhi ya funguo za kupata mafanikio na furaha katika kazi ya umishonari? Ndugu Charles Woody wa Idara ya Utumishi na Ndugu Harold Jackson, mishonari wa zamani wa Amerika ya Latini aliye msaidizi wa Halmashauri ya Kufundisha, waliwahoji washiriki wa Halmashauri ya Ofisi za Tawi mbalimbali waliokuwa wakihudhuria darasa la tisa la shule ya wafanyakazi wa ofisi za tawi. Hapa pana vielelezo vya mashauri ambayo ndugu hao waliwatolea:

Albert Musonda kutoka Zambia alisema hivi: “Mishonari achukuapo hatua ya kwanza kwenda kuwasalimu ndugu, hilo hutokeza roho nzuri sana kwa sababu ndugu watakuwa na ukaribu na huyo mishonari, naye pia atakuwa na ukaribu nao.”

Rolando Morales kutoka Guatemala alidokeza kwamba mishonari wapya wanapopewa kinywaji na watu wenye urafiki, wanaweza kujibu hivi kwa fadhili na busara: “Mimi ni mgeni nchini. Ninatamani ningeweza kunywa, lakini mwili wangu hauna kinga ambazo mwili wako unazo. Ninatumaini siku moja nitaweza kunywa, na nitafurahia kufanya hivyo.” Ni zipi baadhi ya manufaa za jibu la aina hiyo? “Watu hawataudhika, nao wamishonari watakuwa wameonyesha wengine fadhili.”

Ni nini kiwezacho kuwasaidia wamishonari wavumilie katika migawo yao? Ndugu Paul Crudass, mhitimu wa darasa la 79 la Gileadi, ambaye amekuwa akitumikia huko Liberia kwa miaka 12 iliyopita, alisema hivi: “Ninajua ni kweli kwamba wazazi huwakosa watoto wao. Lakini kuna nyakati ambapo mishonari anajaribu kuzoeleana na nchi, mazingira, utamaduni, na watu. Huenda akawa na hisia za kutaka kuacha mgawo wake. Akipata barua kutoka nyumbani ikisema, ‘Tunakukosa sana; hatujui tutafanyaje bila wewe,’ huenda maneno hayo tu yakamsababisha kufunga safari ya kurudi nyumbani. Ni muhimu sana kwa watu wa ukoo walio hapa leo kukumbuka jambo hilo.”

Baada ya mahojiano, hotuba ya mwisho ya programu ilitolewa na Theodore Jaracz, mshiriki wa Baraza Linaloongoza. Kichwa cha hotuba yake kilikuwa: “Weka Ufalme Mahali pa Kwanza Maishani Mwako.” Wamishonari wanawezaje kuendelea kukazia kazi yao fikira bila kukengeushwa? Aliwatia moyo wawe na ratiba ya funzo la kibinafsi la Biblia, litakalowasaidia kutanguliza masilahi ya Ufalme maishani mwao. Na kulikuwa na kikumbusha hiki cha wakati ufaao: “Wamishonari wengine wamepuuza funzo la kibinafsi kwa sababu walijishughulisha sana na vifaa vya elektroni, kuwasiliana kwa kutumia kompyuta, na matumizi mengine ya kompyuta. Lazima tuwe na busara ya kusawazisha matumizi ya kifaa chochote kile na kutotumia wakati mwingi kupita kiasi kuhusiana na jambo ambalo lingeweza kuingilia funzo letu la kibinafsi la Neno la Mungu.”

Baada ya hotuba ya Ndugu Jaracz, diploma zilitolewa na barua ya uthamini ya darasa hilo ikasomwa. Mwakilishi wa darasa alieleza hisia za kila mtu kwa kusema hivi: “Tuliona uthibitisho hakika wa upendo ambao Yesu alisema ungetambulisha wanafunzi wake, na jambo hilo limetuhakikishia kwamba, hata tuwe wapi, kuna tengenezo changamfu, lenye upendo, na lililo kama mama ambalo linatutegemeza. Tukiwa na tegemezo kama hilo, tuko tayari kwenda mpaka kwenye miisho ya dunia.” Huo ulikuwa umalizio wenye kuchochea wa siku yenye furaha ya kuhitimu kwa darasa la 104 la Gileadi.

[Sanduku katika ukurasa wa 24]

Takwimu za Darasa:

Idadi ya nchi zilizowakilishwa: 9

Idadi ya nchi walikogawiwa: 16

Idadi ya wanafunzi: 48

Idadi ya wenzi wa ndoa: 24

Wastani wa umri: 33

Wastani wa miaka katika kweli: 16

Wastani wa miaka katika huduma ya wakati wote: 12

[Picha katika ukurasa wa 25]

Darasa la 104 Lililohitimu la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower

Katika orodha iliyo chini, safu zimepewa nambari kutoka mbele kuelekea nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto kuelekea kulia katika kila safu

(1) Romero, M.; Howarth, J.; Blackburne-Kane, D.; Hohengasser, E.; West, S.; Thom, S. (2) Colon, W.; Glancy, J.; Kono, Y.; Drews, P.; Tam, S.; Kono, T. (3) Tam, D.; Zechmeister, S.; Gerdel, S.; Elwell, J.; Dunec, P.; Tibaudo, H. (4) Taylor, E.; Hildred, L.; Sanches, M.; Anderson, C.; Bucknor, T.; Hohengasser, E. (5) Howarth, D.; Ward, C.; Hinch, P.; McDonald, Y.; Sanches, T.; Thom, O. (6) Drews, T.; Tibaudo, E.; Elwell, D.; Dunec, W.; Blackburne-Kane, D.; Ward, W. (7) Anderson, M.; Zechmeister, R.; McDonald, R.; Bucknor, R.; Glancy, S.; Gerdel, G. (8) Romero, D.; Hinch, R.; Hildred, S.; Taylor, J.; Colon, A.; West, W.

[Picha katika ukurasa wa 26]

Ndugu walioshiriki katika kufunza darasa la 104: (kutoka kushoto) W. Liverance, U. Glass, K. Adams, M. Noumair

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki