Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w05 4/1 kur. 30-31
  • Kuwatafuta Wanaostahili Katika Sehemu ya Mashambani ya Australia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuwatafuta Wanaostahili Katika Sehemu ya Mashambani ya Australia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Wenyeji wa Australia—Watu wa Kipekee
    Amkeni!—1994
  • “Nitaketi na Kukisoma Kando ya Moto Leo Usiku”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Upendo Wangu kwa Dunia Utatoshelezwa Milele
    Amkeni!—1998
  • Tasmania—Kisiwa Kidogo, Simulizi la Kipekee
    Amkeni!—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
w05 4/1 kur. 30-31

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Kuwatafuta Wanaostahili Katika Sehemu ya Mashambani ya Australia

KUNA eneo kubwa la mashambani nchini Australia. Sehemu fulani ya eneo hilo kubwa haikuwa imehubiriwa kwa muda wa miaka 12. Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova huko Darwin, jiji kuu la Jimbo la Northern Territory, walipanga kampeni kubwa ya kuhubiri eneo lote kwa siku tisa ili kuwatafuta wanaostahili.—Mathayo 10:11.

Walianza kufanya mipango miezi 12 mapema, kutia ndani kuchora ramani ya eneo hilo lenye ukubwa wa kilometa 800,000 za mraba—eneo lenye ukubwa mara tatu ya ukubwa wa New Zealand. Ili kuelewa ukubwa wa eneo hilo, hebu wazia kwamba barabara kwenye shamba la mifugo ina urefu wa kilometa 30 toka langoni hadi kwenye makao ya mkulima! Isitoshe, kuna umbali wa kilometa 300 au zaidi kati ya mashamba fulani.

Jumla ya Mashahidi 145 walijitolea kushiriki kampeni hiyo. Baadhi yao walitoka sehemu za mbali sana kama huko Tasmania. Baadhi yao walikuja kwa magari makubwa yaliyopakiwa vifaa vya kupiga kambi, spea, na petroli. Wengine walibeba vifaa vyao kwa trela. Pia, ili kuwabeba wale ambao hawakuwa na magari yanayofaa safari hiyo, walikodi mabasi mawili yenye viti 22 kila moja. Waliosafiri kwa mabasi waliwahubiria wakaaji wa miji midogo katika maeneo kadhaa.

Kabla ya kuanza safari, akina ndugu walipanga hotuba na maonyesho ya kuhubiri habari njema katika eneo hilo lisilo la kawaida. Kwa mfano, ili kuwahubiria wenyeji wa Australia, walihitaji kufuata utaratibu fulani na desturi za makabila hayo. Walizungumzia pia masuala ya mazingira ili kuwalinda wanyama-pori.

Wahubiri walipata mambo mengi yaliyoonwa. Kwa mfano, katika kijiji kimoja, akina ndugu walipanga kutoa hotuba ya watu wote inayotegemea Biblia. Mwanamke aliyesimamia kijiji hicho aliwajulisha watu kuhusu hotuba hiyo. Baadaye, wale wote waliohudhuria waliachiwa vitabu 5 na broshua 41. Katika kijiji kingine walimpata mwenyeji mmoja aliyekuwa na Biblia yake mwenyewe, tafsiri ya King James Version, iliyokuwa nzee na iliyoraruka-raruka. Alipoulizwa iwapo anajua jina la Mungu, alisema ndiyo na kuchomoa gazeti la zamani la Mnara wa Mlinzi kutoka katika koti lake. Alisoma gazeti hilo, akinukuu Marko 12:30 linalosema “lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote.” Akasema, “Ninapenda sana andiko hilo.” Baada ya mazungumzo marefu ya Biblia, alikubali Biblia mpya na vichapo vingine vya Biblia.

Karibu na Ghuba ya Carpentaria, msimamizi wa shamba la mifugo lenye ukubwa wa ekari milioni moja alipendezwa kwa kiasi fulani na ujumbe wa Ufalme. Alipoonyeshwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele,a aliuliza ikiwa kuna kichapo chochote katika lugha ya Kriol. Hilo halikuwa jambo la kawaida kwa sababu ingawa wenyeji walizungumza lugha ya Kriol, ni wachache waliyoisoma. Baadaye wahubiri hao waligundua kwamba wafanyakazi wote 50 wa shamba hilo walijua kusoma lugha ya Kriol. Msimamizi huyo alifurahi kupata vichapo vya Biblia katika lugha ya Kriol, na kuwapa namba yake ya simu ili wawasiliane naye.

Katika kampeni hiyo ya siku tisa, watu waliachiwa jumla ya Biblia 120, vitabu 770, magazeti 705, na broshua 1,965. Pia, walifanya ziara za kurudia 720, na mafunzo ya Biblia 215 yakaanzishwa.

Kwa kweli, njaa ya kiroho ya watu wengi wanaostahili katika eneo hilo kubwa ilianza kutoshelezwa hatimaye.—Mathayo 5:6.

[Maelezo ya Chini]

a Vilivyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Ramani katika ukurasa wa 30]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

AUSTRALIA

NORTHERN TERRITORY

Darwin

Ghuba ya Carpentaria

Sydney

TASMANIA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki