Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w05 11/1 uku. 14
  • Mwenendo Mwema Huleta Matokeo Mazuri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwenendo Mwema Huleta Matokeo Mazuri
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Nguvu za Salamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Kuonyesha Adabu Tukiwa Wahudumu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kutumia Neno la Mungu Katika Jamaa Zetu Wenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kuwalea Watoto Wako Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
w05 11/1 uku. 14

Mwenendo Mwema Huleta Matokeo Mazuri

KATIKA kisiwa kidogo kwenye pwani ya kusini ya Japani, mama mmoja na watoto wake watatu walianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Majirani katika kisiwa hicho chenye kufuatia utamaduni sana, walipojua hivyo, walianza kumpuuza mama huyo walipokutana naye. Anaeleza hivi: “Kilichoniudhi hata zaidi ni kwamba walimdharau mume wangu na watoto wangu.” Hata hivyo, aliwaambia watoto wake: “Tutaendelea kuwasalimu majirani wetu,  kwa ajili ya jina la Yehova.”—Mathayo 5:47, 48.

Akiwa nyumbani, aliwafundisha watoto wake kuwa wenye adabu licha ya kukataliwa na watu. Wakiwa njiani kutembelea chemchemi za maji ya moto, watoto hao walifanya mazoezi ya kusalimiana ndani ya gari. Walipoingia kwenye jengo hilo, sikuzote watoto hao walisema hivi kwa shauku “Konnichiwa!” yaani, “Siku njema!” Kwa subira, familia hiyo iliendelea kuwasalimu watu wote waliokutana nao hata ingawa majirani hawakuwachangamkia. Lakini watu hawakukosa kutambua adabu nzuri ya watoto hao.

Hatimaye, majirani mbalimbali walijibu kwa kusema “Konnichiwa.” Baada ya miaka miwili, karibu kila mtu mjini alikuwa akijibu aliposalimiwa na familia hiyo. Pia, majirani walianza kusalimiana na kuonyeshana shauku. Msaidizi wa meya alitaka kuwapa tuzo watoto hao kwa sababu ya kuchangia badiliko hilo. Lakini mama yao alimweleza kwamba walifanya tu kile ambacho Wakristo wanapaswa kufanya. Baadaye, katika mashindano ya kuzungumza mbele ya watu yaliyofanywa katika kisiwa hicho, mwana mmoja wa mama huyo alieleza jinsi mama yao alivyokuwa amewazoeza kuwasalimu wengine kwa heshima bila kujali itikio lao. Alipata tuzo la kwanza na hotuba yake ikachapishwa katika gazeti la mji. Leo, familia hiyo inafurahi sana kwa sababu walipata matokeo mazuri kwa kufuata kanuni za Kikristo. Ni rahisi kuwahubiria wengine habari njema ikiwa wana urafiki.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki