Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 2/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Kuokoka Katika Upande Wenye Kushinda Katika Har–Magedoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • “Mwana-Mfalme wa Amani” Akabili Har–Magedoni
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Faida za Wanadamu Kutokana na Ushindi Katika Har–Magedoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Har–Magedoni
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 2/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

“Vita vya . . . Mungu Mweza-Yote” kwenye Har–Magedoni ni nini, na matokeo yatakuwa nini?—Ufunuo 16:14, 16.

Kwa ufupi, vita vya Har–Magedoni ni vita vitakavyotukia duniani pote wakati ujao. Katika vita hivyo, Yesu Kristo, Mfalme aliyewekwa rasmi na Yehova, atawaharibu maadui wa Mungu. Biblia inaeleza kwamba maadui hao, “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa,” wanakusanywa pamoja “kwa vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote . . . mahali panapoitwa katika Kiebrania Har–Magedoni.”—Ufunuo 16:14, 16.

Mahali ambapo wanakusanywa ili kupigana si mahali halisi. Neno Har–Magedoni, au “Armagedoni” katika tafsiri nyingine za Biblia, linamaanisha “Mlima wa Megido.” (Ufunuo 16:16) Hakuna mlima wowote ambao umewahi kuitwa kwa jina hilo. Zaidi ya hilo, “wafalme wa dunia na majeshi yao” hawawezi kamwe kukusanyika kihalisi mahali pamoja. (Ufunuo 19:19) Badala yake, “mahali” hapo panawakilisha hali ambamo watawala wa kisiasa wa dunia pamoja na wale ambao wanawaunga mkono wanaongozwa kuingia. Hiyo ni hali ya kumpinga Yehova na “majeshi yaliyokuwa mbinguni” chini ya amri ya kijeshi ya Yesu Kristo, ambaye ni “Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.”—Ufunuo 19:14, 16.

Inapendeza kujua kwamba neno “Har–Magedoni” linahusiana na jiji la kale la Megido huko Israeli. Likiwa mahali pazuri sana upande wa mashariki wa Mlima Karmeli, Megido lilisimamia njia kuu za kibiashara na za kijeshi siku hizo. Pia, vita vya kukata maneno vilipiganwa huko. Kwa mfano, ni “kando ya maji ya Megido” ndipo Mwamuzi wa Israeli anayeitwa Baraka aliposhinda jeshi kubwa la Wakanaani ambalo liliongozwa na Jenerali Sisera. (Waamuzi 4:12-24; 5:19, 20) Pia, katika eneo hilo, Mwamuzi Gideoni aliwashinda kabisa Wamidiani. (Waamuzi 7:1-22) Kwa kuhusianisha Megido na vita vinavyokuja, Biblia inatuhakikishia kwamba Mungu, kupitia Mwana wake, atayashinda kabisa majeshi yote yanayompinga.

Matokeo yatakuwa nini? Vita vya Har–Magedoni vitaondoa ufisadi na uovu wote duniani. Vitaleta enzi bora kabisa katika historia yote ya wanadamu. (Ufunuo 21:1-4) Chini ya utawala wenye upendo wa Ufalme wa Mungu, dunia itageuzwa kuwa paradiso ambamo waadilifu wataishi milele.—Zaburi 37:29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki