Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 4/15 kur. 178-184
  • Faida za Wanadamu Kutokana na Ushindi Katika Har–Magedoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Faida za Wanadamu Kutokana na Ushindi Katika Har–Magedoni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UFALME ULISIMAMISHWA KATIKA WAKATI WAKE
  • FAIDA ZA BAADA YA VITA KWA WAOKOKAJI
  • Chanzo cha Taabu ya Wanadamu Chakaribia Kuondolewa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Kuokoka Katika Upande Wenye Kushinda Katika Har–Magedoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Huu Ndio Wakati wa Kumkaribisha Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 4/15 kur. 178-184

Faida za Wanadamu Kutokana na Ushindi Katika Har–​Magedoni

1. Kwa sababu gani wanadamu watafaidika milele kutokana na ushindi utakaopatikana katika Har–​Magedoni?

WANADAMU watafaidika milele kutokana na ushindi utakaopatikana katika Har–​Magedoni. Ushindi huo utakuwa kwa ajili ya wanadamu, zaidi waokokaji wa vita katika Har–​Magedoni, wakaukumbuke milele. Ni ushindi utakaoonyesha ‘siku kuu.’ Mpaka sasa hakujapata kuwa na siku kama hiyo, kwa maana itakuwa ‘siku kuu ya Mungu Mwenye Nguvu Zote.’ Ataifanya ‘siku kuu’ yake Mwenyewe kwa ushindi atakaoupata katika vita ya ulimwengu wote ya siku hiyo. Wanadamu watafaidika kutokana na ushindi wa Mungu Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Yeye ni Rafiki bora wa wanadamu.

2. (a) Ufalme ambao umo katika ulizo watia nini ndani kama makao yake, na kwa sababu gani? (b) Ulizo ni utawala hali gani ikiwapo duniani?

2 Katika Har–​Magedoni Mungu Mwenye Nguvu Zote atashindana na “wafalme wa dunia yote inayokaliwa na watu.” Ni kwa sababu UFALME ndilo ulizo litakaloamuliwa katika Har–​Magedoni. Ufalme huo lazima uwe na dunia kama makao yake, kwa maana ndipo “wafalme wa dunia yote inayokaliwa na watu” wanapotawala na wanapoamua kuendelea kutawala. Ulizo ni Ufalme, lakini si juu ya dunia iliyogawanyika kama ilivyo sasa kati ya jamii ya mataifa ya kidemokrasi na jamii ya mataifa ya Kikomunisti, jamii zote mbili zikiwapo wakati mmoja kwa kuvumiliana, au kati ya Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) na upagani. Bali, ulizo ni Ufalme juu ya dunia moja isiyogawanyika, Ufalme mmoja wa dunia yote. Je! huo hautakuwa wenye faida kwa wanadamu wote?

3. Je! pigano katika Har–​Magedoni juu ya ulizo la Ufalme latokea kwa bahati, na kwa sababu gani twaweza kushukuru kwamba badiliko litaletwa na Mungu?

3 Ulizo la Ufalme halipiganiwi katika uwanja wa vita wa Har–​Magedoni kwa sababu ya tukio lisilotazamiwa katika mambo ya kibinadamu wala halipiganiwi kwa bahati. Shauri lote limewekewa wakati kwa ajili ya Mungu na mwanadamu. Mungu Mwenye Nguvu Zote, aliyetoa jua, mwezi na nyota na mizunguko ya dunia ili mwanadamu aweke wakati, ameimarisha wakati wake wa Ufalme wa dunia yote. Je! yeye hakuchukuliana na utawala wa kibinadamu juu ya dunia yote kwa wakati wa kutosha sasa? Je! watawala wa kibinadamu ndio watakaoamua ni wakati gani na ni kwa njia gani Mungu Mwenye Nguvu Zote atauchukua ufalme wa dunia, uumbaji wake mwenyewe? Je! atawaacha wanadamu walio hoi watatanike-tatanike kwa wakati usiojulikana katika taabu yote ya ulimwengu na huzuni kuu ya mataifa iliyoanza na Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ya mwaka wa 1914 bila kuwasaidia? Kwa furaha, Sivyo! Ufalme wake unaohitajiwa peke yake juu ya dunia yote utaleta maendeleo makubwa juu ya cho chote ambacho watawala wa kibinadamu wasiokamilika na wenye kufa wameweza kuwapa wanadamu mpaka sasa. Bila shaka badiliko lo lote litakalofanywa Naye katika utawala wa viumbe vyake vya kibinadamu haliwezi kamwe kuleta mabaya zaidi. Twaweza kushukuru kwamba Mungu Mwenye Nguvu Zote ndiye atakayetufanyia badiliko, na kwamba wakati wake wa kufanya hivi aliouchagua kwa hekima umefika.

4, 5. Mungu amesikiliza sala gani juu ya utawala wake Yeye kwa muda mrefu, na mwalimu wa sala hiyo alisema na akafanya nini kuendeleza faida za utawala huo?

4 Kwa zaidi ya karne kumi na tisa sasa Mungu Mwenye Nguvu Zote ameisikiliza sala iliyotolewa kwake mara nyingi na wale wafuatao fundisho la Mahubiri juu ya Mlima, “Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mt. 6:9, 10) Mungu Mwenye Nguvu Zote hakujibu sala hiyo aliyoiongoza mwenyewe kabla ya sasa kwa kuwa wakati wake mwenyewe uliowekwa haukuwa umefika. Sala hiyo ilifundishwa na mtu aliyeuamini ufalme wa Mungu kufikia hatua ya kutoa uhai wake mwenyewe aendeleze faida za ufalme huo. Masihi wa uongo asingeweza kufanya jambo hilo. Si kwamba tu aliwafundisha wasikiaji wake wauombee ufalme wa kimbinguni wa Baba katika Mahubiri yake juu ya Mlima, bali pia aliwaambia hivi: “Basi endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na haki yake.” Kichwa chake cha kuanzia kilikuwa hiki alipokuwa akifanya kazi yake ya kufundisha kati ya wakaaji wa Palestina: “Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.” (Mt. 4:17; 6:33, NW) Na katika unabii wake wenye kueleza taabu ambazo zingetokea kwa sababu ya kusimamishwa kwa ufalme wa Mungu wa Kimasihi, alisema hivi:

5 “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mt. 24:14, NW.

6, 7. (a) Wale ambao kupitia kwao unabii huo unatimizwa wanaamini nini juu ya msemaji wa unabii huo? (b) Simoni Petro alisema nini juu yake kwa Wayahudi katika sikukuu ya Juma?

6 Unabii huo wa maana umetimizwa sana, nao ungali waendelea kutimizwa, si kupitia kwa Kristendomu pamoja na wafalme wake wote wa kidunia, vita zake na mizozo yake ya kisiasa, bali kupitia kwa waamini wa kweli wa Mungu Mwenye Nguvu Zote na wa ufalme wa kimbinguni wa Masihi wake. Hawa wanajua ni nani aliyetimiza unabii mbalimbali ulioongozwa na Mungu katika Maandiko Matakatifu ya Kiebrania kwa habari ya Masihi wa Mungu aliyeahidiwa. Wao wanajua kwamba huyu ndiye aliyekuwa mteteaji mkuu zaidi wa ufalme wa Mungu wa Kimasihi aliyepata kuwapo duniani. Wakiwa na matumaini na hakika wanaweza kuhakikisha kutokana na Maandiko yaliyopewa na Mungu kwamba Masihi huyu ndiye aliyeitwa na ndiye anayeitwa na aliyekuwa mtoza kodi aitwaye Mathayo Lawi, “Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.” (Mt. 1:1) Huyu ndiye ambaye Mgalilayo jina lake Simoni Petro alimtolea ushuhuda katika sikukuu ya Shavuoth (Juma) katika Yerusalemu wa kale, kwa zaidi ya waadhimishaji elfu tatu, akiwaambia hivi Wayahudi hawa wenye kuuliza:

7 “Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, [Yehova] alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume. Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako. Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo [mliyemtundika mtini] kuwa Bwana na Kristo.”​—Matendo 2:34-36.

8. (a) Kwa sababu gani Kristendomu na Wayahudi wanaotazamia Masihi mwenye damu na nyama wanatazamia kisichofaa? (b) Ufalme wa Masihi wa kweli utaweza kufanyia wanadamu nini?

8 Daudi alikuwa mfalme wa kwanza wa Kiyahudi wa Yerusalemu, naye mzao wake Yesu ‘wa kabila la Yuda’ ndiye Bwana wa Daudi wa kimbinguni na pia Masihi au Mtiwa Mafuta, Kristo. Watu wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) na pia Wayahudi waliotahiriwa wanaotazamia Masihi karibuni akiwa katika mwili wenye nyama na damu wanatazamia jambo lisilofaa. Masihi wa kweli, ambaye Daudi aliyeongozwa na Mungu alisema Yehova angemkaribisha aketi mkono wake wa kuume mbinguni na ambaye angekuwa Mfalme-Kuhani kama Melkizedeki wa kale, sasa yeye ni Masihi wa kimbinguni naye atakuwa hivyo sikuzote, Mwana wa Mungu wa kiroho wa kimbinguni. (Zab. 110:1-4) Ufalme wake wa Kimasihi utakuwa bora kuliko ule wa mwanadamu mwenye kufa duniani. Utakuwa wenye uwezo upitao wa mwanadamu na kwa hiyo utaweza kufanyia wanadamu lisiloweza kufanywa kamwe na ufalme wa kidunia wa mtawala wa kibinadamu tu. Ufalme wa kweli wa Kimasihi ni wa kimbinguni na unaweza kuvunja uwezo wa Shetani Ibilisi, ambaye ni malaika wa kimbinguni asiyetii, mkuu wa malaika wa kishetani. Wanadamu, ambao ni mateka wastahilio kuhurumiwa wa Shetani Ibilisi na mashetani zake, wanaweza kupata ukombozi wa faida ya milele kutokana na ufalme huo wa Kimasihi.

UFALME ULISIMAMISHWA KATIKA WAKATI WAKE

9. (a) Ni wakati gani ufalme wa kidunia wa Daudi ulipopinduliwa, uendelee kuwa hivyo kwa kipindi gani cha wakati? (b) Ni wakati gani lazima utawala wa Mataifa uondoke na utawala wa Masihi uingie?

9 Ufalme wa kidunia wa jamaa ya Daudi katika Yerusalemu ulipinduliwa na majeshi ya Babeli mwaka wa 607 kabla ya Wakati wetu wa Kawaida. Muda mfupi kabla ya msiba huo mkuu Yehova Mungu alimtumia nabii wake Ezekieli kutangaza kwamba Masihi aliyeahidiwa angekuja katika wakati wake Mungu na kwamba Yeye angempa Masihi huyu Ufalme kwa sababu ni haki yake. (Eze. 21:25-27) Kutokana na historia, Wayahudi na Mataifa pia wanajua lililotukia baada ya uharibifu wa kiti cha enzi cha Daudi huko nyuma ulioletwa na Wababeli wasio Wayahudi. Wakati usiokatizwa wa utawala wa Mataifa juu ya dunia ulifuata bila ya ufalme wo wote wa nyumba ya kifalme kuwakatiza watawala hao wa Kitaifa. Yameitwa “Majira ya Mataifa.” (Luka 21:24, Authorized Version Bible) Lakini Mungu Mwenye Nguvu Zote angeacha Majira ya Mataifa ya utawala wa ulimwengu yaendelee kwa kipindi hicho tu. Aliweka wakati usiobadilika wa mwisho wa Majira ya Mataifa hayo. Aliuonyesha uhakika huo kwa mfalme wa Babeli, aliyeuharibu Yerusalemu. (Dan. 4:16, 23, 25, 31) Kwa hiyo lazima utawala wa Mataifa uondoke; lazima utawala wa Masihi uje!

10. Ni mamlaka gani yenye nguvu zaidi kupita zote aliyoitaja Danieli kwa unabii, nayo imeshindwaje kubadili wakati na sheria ya Mungu kwa habari ya utawala?

10 Kupitia kwa nabii wake Danieli, Mungu alisema kwa unabii kwamba mamlaka ya kisiasa ya Kitaifa ingetokea ambayo ingejaribu kuubadili wakati wa Mungu na sheria yake juu ya utawala wa dunia. (Dan. 7:25) Walakini, historia ya ulimwengu ya karne hii ya 20 yaonyesha kwamba mamlaka hii ya kisiasa iliyotajwa kwa unabii, mamlaka ya ulimwengu yenye uwezo kupita zote katika historia yote ya kibinadamu, haikuweza kubadili tarehe ya Mungu ya mwisho wa Majira ya Mataifa isiwe mwaka wa 1914 na kuipeleka kwenye tarehe nyingine ya baadaye katika wakati ujao usiojulikana. Kweli, Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilitokea mwaka wa 1914; lakini kilichoonyesha hasa mwisho wa Majira ya Mataifa mwaka huo kilikuwa kuzaliwa kwa ufalme wa Mungu wa Kimasihi mbinguni kwa kutawazwa kwa Mwanawe Yesu Kristo kama Mfalme Mtiwa Mafuta. Wakati wa miaka yote yenye taabu iliyofuata Mamlaka ya Ulimwengu ya Saba yenye nguvu (Mamlaka ya Mwungano wa Waingereza na Waamerika) imeshindwa kuubadili uhakika huo wa maana katika ulimwengu wote. Hasira kuu ambayo mataifa yote ya kilimwengu yameonyesha kwa kuwatesa mashahidi wa Yehova wa Kikristo ambao wamezihubiri “habari njema hizi za ufalme” katika dunia yote inayokaliwa na watu imeshindwa kufuta wakati wa Mungu wa ufalme Wake.

11. (a) Wakati wa kutolewa kwa shukrani kwa sababu ya Mungu kuchukua mamlaka yake kutawala ulifika lini? (b) Ni nini linaloonyesha kama mataifa ya kidunia yalikuwa kati ya wenye kushukuru?

11 Mwishoni mwa Majira ya Mataifa katika vuli ya mapema ya mwaka wa 1914 saa ya tangazo la kimbinguni ilifika, kama ilivyosemwa kwa unabii katika Ufunuo 11:15: “Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele.” Haya, sasa, je! mataifa ya Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu) yalishukuru kwa tukio hili katika historia ya ulimwengu wote? Je! mataifa yaitwayo ya Kikristo yalikuwamo kati ya wale walioshukuru kwa kuzaliwa kwa ufalme wa Bwana Mungu mikononi mwa Kristo wake? Hata kidogo! Kwa maana unabii wa Ufunuo 11:17, 18 ulisema kwamba watu wenye shukrani wangesema: “Tunakushukuru wewe, [Yehova] Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa sababu umeutwaa uweza wako ulio mkuu, na kumiliki. Na mataifa walikasirika, hasira yako nayo ikaja.” Historia yashuhudia uhakika wa kwamba mataifa hayo yenye hasira kuu yakawa watesi wakali wa wahubiri wa Ufalme.

12, 13. Shetani alifurahia kuzaliwa kwa Ufalme, na Ufunuo 12:7-12 waonyeshaje kama alifurahia?

12 Haikupaswa itazamiwe vingine, Shetani Ibilisi na malaika zake wa kishetani hawakufurahia kuzaliwa kwa ufalme wa Mungu wa Kimasihi mbinguni katika mwaka wa 1914. Sura ifuatayo ya Ufunuo, sura ya kumi na mbili, mstari wa saba mpaka wa kumi na mbili, yatuambia kilichofuata kuzaliwa kwa Ufalme:

13 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa. chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. . . . Ole wa nchi na bahari! kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.”

14. (a) Wafalme wa kidunia wanajiacha wakusanywe wapi, kwa sababu gani na chini ya uongozi gani? (b) Mwishowe itakuwa na maana gani kwetu kukusanywa huko pamoja na wafalme hao?

14 Hivyo Shetani Ibilisi na malaika zake wa kishetani na mataifa ya dunia waliona uchungu pia ufalme wa Mungu wa Kimasihi ulipozaliwa mwishoni mwa Majira ya Mataifa katika mwaka wa 1914. Kwa hiyo, haishangazi kwamba roho itokayo kinywani mwa joka mkuu, Shetani Ibilisi, ingewakusanya wafalme wa dunia yote inayokaliwa na watu kwenye vita itakayopigwa juu ya ulizo la Ufalme katika Har–​Magedoni. Wala haishangazi kwamba wafalme wa mataifa haya yenye hasira kuu wangejiacha wakusanywe chini ya maongozi hayo ya kishetani. Lakini ulizo la kipekee listahililo tulichunguze sana ni, Je! sisi kama watu mmoja mmoja tunajiacha tukusanywe huko katika upande wa hao “wafalme wa dunia yote inayokaliwa na watu” waliopotoshwa? Tukifanya hivyo, basi tutaonyesha bila shaka kwamba tunaunga mkono ufalme wao, si ufalme wa Mungu wa Kimasihi. Halafu tena, itatulazimu kupata kile watakachokipata ‘wafalme hao wa dunia yote inayokaliwa na watu’ katika Har–​Magedoni. Hicho ni nini? Ufunuo 19:19-21 watuambia hivi:

15. Kwa njia ya mfano Ufunuo 19:19-21 waonyeshaje kinachowapata wafalme wa dunia na wenye kuwaunga mkono?

15 “Kisha [mtume Yohana] nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana [yaani, katika Har–​Magedoni] kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake. [Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA. (Mstari wa 16)] Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti; na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.”

16. (a) Kwa hiyo ni nani atokeaye kama mshindi katika Har–​Magedoni, na kwa sababu gani aitwa Mfalme wa wafalme? (b) Adui wanauawa na nani, na mizoga ya washinde itaondolewaje mbali?

16 Kutokana na mfano huo wa unabii haipaswi iwe vigumu kwa ye yote kuamua ni nani atokeaye akiwa mshindi katika hiyo “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenye Nguvu Zote” katika Har–​Magedoni. Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana anayefananishwa kama akiwa amekalia farasi mweupe wa vita ndiye atokeaye akiwa mshindi. (Ufu. 19:11) Kana kwamba upanga mrefu ulikuwa ukitoka kinywani mwake, Shujaa huyu wa kimbinguni apaza sauti akitoa amri za kuuawa kwa wafalme wa dunia na wale waliojipanga upande wao katika Har–​Magedoni. Jeshi la kimbinguni la malaika linatimiza amri hizi za Mfalme wa wafalme. Kwa njia hii yahakikishwa kwamba yeye ni Mfalme wa wafalme, yaani, Mfalme aliye mkuu kupita wafalme hao wote wa dunia. Wote wale wawafuatao na kuwaunga mkono wafalme hao wa dunia kwa njia ya siasa watauawa pamoja na wafalme hao wa kibinadamu. Wafuasi wa Mfalme wa wafalme, ambao wanaiokoka vita hiyo ya ulimwengu wote katika Har–​Magedoni, hawafananishwi hapa kama wakiamriwa kuzika mizoga ya wafalme hao wa kidunia na majeshi yao. Basi, ni nani atakayeiondolea mbali mizoga hiyo iliyoachwa peupe na yenye kunuka? Mawakili wa kuiondolea mbali wanaonyeshwa kuwa ndege wenye kula mizoga.

17. Kifo hicho na kuondolewa mbali kwa masalio ya miili kutamaanisha nini kwa hao watakaouawa, na kwa sababu gani?

17 Kifo hicho chenye kuchukiza na kuondolewa mbali kwa masalio ya nyama chamaanisha kifo kisicho na tumaini la ufufuo. Hii ni kwa sababu wanauawa na Mungu Mwenye Nguvu Zote kwa kuyatumia majeshi yake ya kimbinguni chini ya Kristo katika uwanja wa vita wa Har–​Magedoni. Wanajionyesha kuwa wapinzani wasiobadilika wa Yehova Mungu na ufalme wake wa Kimasihi. Hawataishi tena, kama vile “mnyama” wa mfano na “nabii wa uongo” wa mfano, matengenezo ya kisiasa ya kibinadamu, hayatakuwapo tena yakiharibiwa milele kana kwamba kwa kutupwa yangali hai ndani ya “ziwa liwakalo moto na kiberiti.” Ufunuo 20:14 na 21:8 waliita “ziwa” hili lenye kiberiti kuwa mfano wa “mauti ya pili,” maangamizi ya milele!

FAIDA ZA BAADA YA VITA KWA WAOKOKAJI

18. Wapendao serikali yenye haki watampenda nani na kumchukia nani, nao watajipanga katika upande gani bila kukawia?

18 Kwa kuwa hili ni jambo zito hivyo kwa watu wote wa kizazi hiki, Biblia yaonyesha wazi sana juu ya kinachowangoja wale wanaojipanga sasa katika upande unaoelekea kushindwa katika vita ya ulimwengu wote katika Har–​Magedoni. Wapenda kweli wa serikali kamilifu yenye haki kwa wanadamu wote wanahofu sana waonapo litukialo kwa wale watakaopigana kwa makusudi na Mfalme wa wafalme na ambao kwa njia hiyo wanaukataa ufalme wa Mungu wa Kimasihi. Wao wanampenda Mungu mwenye rehema ambaye Ufalme huu wenye haki, amani na ufanisi ulioahidiwa zamani unatokana naye. Wao wanamchukia adui ya Mungu, Shetani Ibilisi, ambaye utawala wote mbaya juu ya wanadamu pamoja na udhalimu wake wote, hatari na maisha magumu yametokana naye. Wao wanatamani kuona haki ya Yehova Mungu ya enzi kuu ya ulimwengu wote juu ya viumbe vyote vyenye akili ikishuhudiwa na ushindi wake mtukufu kupitia kwa Mwanawe Yesu Kristo katika Har–​Magedoni. Hao wapendao Enzi Kuu ya haki ya Ulimwengu Wote ni watu watakaojipanga sasa, bila ya kukawia zaidi, katika upande wa Masihi Wake, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Ni katika upande huo peke yake wawezao kuokoka.

19. Kwa sababu gani ushindi wa Yehova katika Har–​Magedoni utakuwa wakati wa furaha isiyoelezeka kwa upande wa waokokaji wa kidunia?

19 Ushindi wa Kimungu katika uwanja wa vita wa Har–​Magedoni utakuwa wakati wa furaha isiyoelezeka kwa waokokaji wote duniani, ambapo ndipo “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenye Nguvu Zote” itatokea. Nyimbo zao za shangwe kwa kushuhudiwa kwa enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote zitakuwa jambo lisilopata kuwa na kifani kamwe katika dunia yote. Loo! ni vema namna gani kufikiria kuona hasa dunia yote ikiachwa bila taratibu ya kinyama na ya kisiasa ambayo adui mkuu wa Yehova ameitumia tangu Babeli ya ufalme wa Nimrodi! Ndiyo, kuona dunia yote ikisafishwa ili ufalme mwema wa Mtiwa Mafuta wa Yehova utoe uongozi wenye upendo kwa utukufu wa Mungu na baraka ya milele ya wanadamu ni vema namna gani!

20. Kuongezea furaha hiyo kutakuwa na furaha juu ya ushindi gani ulio mkubwa zaidi?

20 Furaha itakayoletwa na ushindi mkubwa hata zaidi kwa upande wa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova itaongeza furaha hiyo isiyolinganika. Huu utafuata mara baada ya mwisho wa vita katika Har–​Magedoni. Kutakuwa ni kufungwa kwa Aliye Mwovu ambaye ameiongoza taratibu ionekanayo ya kisiasa duniani ikaumiza wanadamu, yaani, Shetani Ibilisi, pamoja na malaika zake wa kishetani. Wataondolewa katika ujirani wa dunia na kutiwa katika kifungo chenye muhuri katika shimo refu lisilopimika la mbali, wakawe hoi wasiweze kupinga ufalme wa Mungu wa Kimasihi.

21. (a) Waokokaji watashuhudiaje kutiwa kwa mashetani katika shimo refu lisilopimika, lakini hili litafanywa liwe jambo halisi kwa waokokaji hawa kwa njia gani? (b) Kwa sababu gani waokokaji watajiona salama ndani ya ulinzi wa ufalme wa Mungu wa Kimasihi?

21 Waokokaji wa kidunia wa Har–​Magedoni wataona mashetani wakitiwa katika shimo refu lisilopimika kwa macho yao ya imani tu, kulingana na masimulizi ya unabii yatolewayo katika Ufunuo 20:1-3, lakini bila shaka watayaona matokeo yake yenye kupendeza kwa njia ya hakika sana. Hawatalazimika tena kuendelea kuwa na “silaha zote” zitokazo kwa Mungu ili kupigana na kuzipinga kwa imara hila za Ibilisi. Haitawapasa tena kupigana mweleka na serikali zisizoonekana zenye uwezo upitao wa mwanadamu na “majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” Adui, Ibilisi, hataendelea tena kutembea kama simba anayenguruma akitafuta mtu ammeze. (Efe. 6:11-18; 1 Pet. 5:8) Hakutakuwa na woga juu ya wapinzani hao wakorofi wasioonekana, na waokokaji wa dhiki iliyo kubwa zaidi ya zote za dunia watafarijika kuwa salama ndani ya ulinzi wa “mbingu mpya” za Kimasihi. Serikali hiyo ya kimbinguni itakuwa na huruma ya mchungaji wa Mashariki alindaye kondoo zake kwa upendo. Mchungaji Mwema, Yesu Kristo, aliyetoa uhai wake kwa ajili ya “kondoo” zake wa kibinadamu, atakuwa Mchungaji wa kifalme juu ya wanadamu wote aliowafia.​—Ufu. 21:1; 7:9-17; Yohana 10:10-16.

22. (a) Kupitisha kwa Yehova waabudu wake wakiwa hai katika “dhiki kubwa” kutakuwa na maana gani kwake, kama wonyesho wa Zaburi 145:20? (b) Ni nani duniani watakaokuwa wa kwanza kuingia katika mambo mazuri sana yaliyosemwa kwa unabii kwa makao ya Ufalme?

22 Hatusahau kwamba kusudi ovu la Shetani na mashetani zake baada ya kutupwa nje ya mbingu takatifu kuja chini duniani lilikuwa kuleta “ole” huo duniani na baharini ili kuleta uharibifu wa wanadamu wote, zaidi waabudu wa kweli wa Yehova Mungu. Kulingana na uhakika huu kupitishwa kwa waabudu hao katika “dhiki kubwa” na upeo wake wa Har–​Magedoni kutakuwa tendo kubwa la ushindi kwa upande wa Mungu Mwenye Nguvu Zote na Mfalme wake wa Kimasihi. (Mt. 24:21, 22; Marko 13:19, 20) Ni wonyesho mwingine wa uhakikisho wa Biblia: “[Yehova] huwahifadhi wote wampendao, na wote wasio haki atawaangamiza.” (Zab. 145:20) Alitoa unabii wa mambo mazuri mno kwa dunia hii chini ya ufalme wa miaka elfu wa Masihi Yesu, na waokokaji wa “dhiki kubwa” ndio watakaokuwa wa kwanza duniani kuingia katika utimizo wa unabii huo mbalimbali ulio mzuri sana.

23. (a) Ndipo dunia itakapokuwa mahali pa uhusiano gani kati ya wakaaji wa dunia? (b) Kwa sababu gani wakati huo hakutakuwa na kumtolea Kaisari mambo ya Kaisari?

23 Mwishowe dunia yote itakuwa mahali pa udugu wa kibinadamu​—kati ya waokokaji hao ambao wamejipanga kwa uaminifu katika upande wa Mungu Mwenye Nguvu Zote na Mwanawe Yesu Kristo. Hakutakuwa na haja ya Mkutano wa Amani kufanya Mkataba wa Amani na kuponya majeraha na kuondoa kutopatana kati ya washindi na washinde. Hakutakuwa na washinde walio hai duniani. Walio hai, washirikio katika ushindi wa kimungu wa Yehova, hawatagawanya tena fikira zao kati ya kumtolea Kaisari vitu vilivyo vya Kaisari na Mungu vitu vilivyo vya Mungu, kwa maana “Kaisari” na serikali yake ya kisiasa atakuwa ametoweka milele. (Mt. 22:21) Vitu vyote sasa lazima viwe vya Mungu, na wakaaji wa dunia lazima wamtolee Mungu vitu vyote hivi.​—Zab. 103:19; 1 Nya. (Sik.) 29:11.

24. Chini ya utawala wa Shetani dunia imekuwa mahali ambapo nini kimetawala, lakini ni nini kitakachotawala badala yake chini ya ufalme wa Mungu?

24 Chini ya utawala wa Ibilisi juu ya wanadamu wakati wa miaka elfu sita iliyopita dunia imekuwa makao ambamo dhambi na adhabu yake mauti vimetawala. Chini ya serikali moja duniani pote itakayoongozwa na Mungu kupitia kwa Mwokozi Yesu Kristo dunia itakuwa makao ambamo haki na thawabu yake, uzima, vitatawala. Waokokaji wa dhiki watajisikia wakirudiwa kweli na nguvu za ujana mwilini na akilini wanapotimiza mapenzi ya Serikali ya Kimungu.

25. (a) Waokokaji wa kidunia watafurahia kuona faida za Ufalme zikitolewa kwa nani wengine, kwa njia gani? (b) Ni hali gani ya kidunia watakayofurahi kuiona hao watakaorudi? (c) Macho na mioyo ya waokokaji itabarikiwaje kwa sababu ya kusimama sasa katika upande wenye kushinda?

25 Mioyo yenye upendo ya waokokaji itafurahi faida za uzima zitakapotolewa kwa uongozi wa Serikali kamilifu ya kimbinguni kwa wale walalao katika shimo la dunia, jambo la kimwujiza litakalotukia ufufuo wa wafu uanzapo kwa amri ya Yesu Kristo. (Yohana 5:28, 29) Lo! ni badiliko gani la hali za dunia litakuwa limetokea wafu waliokombolewa waanzapo kurudi! Watafurahia kuona Paradiso ikitengenezwa upya warudipo! Furaha za kuishi wakati huo na kutumikia chini ya ufalme wa Mungu wa Kimasihi zaweza kuwaziwa tu zitakavyokuwa. Lakini yaliyobarikiwa yatakuwa macho na mioyo ya wale watakaookoka katika upande wenye kushinda katika Har–​Magedoni, kwa maana wataishi na kujitayarisha kuyaona mambo haya yakitukia!

​—Kutoka The Watchtower, April 15, 1975.

[Chati katika ukurasa wa 181]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

1914

Majira ya Mataifa Yalikwisha

Ufalme wa Kimasihi Wazaliwa Mbinguni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki