Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 11/1 uku. 4
  • Hadithi ya Kwanza ya Uwongo: Nafsi Haifi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hadithi ya Kwanza ya Uwongo: Nafsi Haifi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Nafsi Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Maoni Yako Juu ya Nafsi Huathiri Uhai Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Nafsi Kulingana na Biblia
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
  • Nafsi Yako Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 11/1 uku. 4

Hadithi ya Kwanza ya Uwongo: Nafsi Haifi

Ni nini chanzo cha hadithi hiyo? “Wanafalsafa wa mapema ambao walikuwa Wakristo walikubali fundisho la Wagiriki la kwamba nafsi haiwezi kufa na walifikiri kwamba nafsi inaumbwa na Mungu na kutiwa ndani ya mwili wakati wa kuzaliwa.”—The New Encyclopædia Britannica (1988), Buku la 11, ukurasa wa 25.

Biblia inasema nini? “Nafsi inayofanya zambi, itakufa.”—Ezekieli 18:4, Zaire Swahili Bible.

Kuhusu kuumbwa kwa nafsi ya kwanza ya mwanadamu, Biblia inasema hivi: “Yehova Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya nchi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai, naye mtu akawa nafsi hai [Kiebrania, neʹphesh].”—Mwanzo 2:7.

Neno la Kiebrania neʹphesh, linalotafsiriwa “nafsi,” linamaanisha ‘kiumbe kinachopumua.’ Mungu alipomuumba mwanadamu wa kwanza Adamu, hakutia ndani ya mwanadamu huyo nafsi isiyoweza kufa lakini alitia ndani yake nguvu ya uhai ambayo inaendelezwa kwa kupumua. Kwa hiyo, neno “nafsi” katika Biblia linamaanisha kwa ujumla kiumbe hai. Nafsi ikitenganishwa na nguvu ya uhai ambayo ilitoka kwa Mungu, nafsi hiyo inakufa.—Mwanzo 3:19; Ezekieli 18:20.

Fundisho la kwamba nafsi haifi linatokeza maswali: Nafsi zinaenda wapi baada ya kifo? Nafsi za waovu zinapatwa na nini? Wakati watu waliodai kuwa Wakristo walipokubali hadithi ya uwongo ya kwamba nafsi haifi, hilo liliwafanya wakubali hadithi nyingine ya uwongo, yaani, fundisho la moto wa mateso.

Linganisha mistari hii ya Biblia: Mhubiri 3:19; Mathayo 10:28; Matendo 3:23

UKWELI:

Baada ya kifo mtu haendelei kuishi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki